Swahili: New Testament

Turkish: New Testament

Romans

10

1Ndugu zangu, ninataka na kutazamia kwa moyo wangu wote hao wananchi wenzangu wakombolewe. Tena nawaombea kwa Mungu daima.
1Kardeşler! Yüreğimin arzusu ve İsraillilerin uğruna Tanrı'ya yalvarışım, kurtuluşları içindir.
2Maana naweza kuthibitisha kwa niaba yao kwamba wanayo bidii ya kumtafuta Mungu; lakini bidii hiyo haikujengwa juu ya ujuzi wa kweli.
2Kendilerine tanıklık ederim ki, Tanrı için gayretlidirler; ama bu bilinçli bir gayret değildir.
3Maana hawakufahamu jinsi Mungu anavyowafanya watu wawe waadilifu, na wamejaribu kuanzisha mtindo wao wenyewe, na hivyo hawakuikubali njia hiyo ya Mungu ya kuwafanya wawe waadilifu.
3Tanrı'nın öngördüğü doğruluğu anlamadıkları ve kendi doğruluklarını yerleştirmeye çalıştıkları için Tanrı'nın öngördüğü doğruluğa boyun eğmediler.
4Maana kwa kuja kwake Kristo, Sheria imefikia kikomo chake, ili kila mtu anayeamini akubaliwe kuwa mwadilifu.
4Ne var ki, her iman edenin aklanması için Mesih, Kutsal Yasa'nın sonudur.
5Kuhusu kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa kuitii Sheria, Mose aliandika hivi: "Mtu yeyote anayetimiza matakwa ya Sheria ataishi."
5Musa, Kutsal Yasa'ya dayanan doğrulukla ilgili şunları yazıyor: «Yasa'da yazılanları yerine getiren, bunlarla yaşayacaktır.»
6Lakini, kuhusu kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa njia ya imani, yasemwa hivi: "Usiseme moyoni mwako: Nani atapanda mpaka mbinguni? (yaani, kumleta Kristo chini);
6İmana dayanan doğruluk ise şöyle diyor: «Yüreğinde, `Göğe - yani Mesih'i indirmeye - kim çıkacak?' ya da, `Dipsiz derinliklere - yani Mesih'i ölüler arasından çıkarmaya - kim inecek?' deme.»
7wala usiseme: Nani atashuka mpaka Kuzimu (yaani, kumleta Kristo kutoka kwa wafu)."
8Ne deniyor? «Tanrı sözü sana yakındır, ağzında ve yüreğindedir.» İşte duyurduğumuz iman sözü budur.
8Maandiko Matakatifu yesema hivi, "Ujumbe huo wa Mungu uko karibu nawe, uko kinywani mwako na moyoni mwako" nao ndio ile imani tunayoihubiri.
9İsa'nın Rab olduğunu ağzınla açıkça söyler ve Tanrı'nın O'nu ölümden dirilttiğine yürekten iman edersen, kurtulacaksın.
9Kama ukikiri kwa kinywa chako kwamba Yesu ni Bwana na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka wafu, utaokoka.
10İnsan yürekten iman etmekle aklanır, imanını ağzıyla açıklamakla da kurtulur.
10Maana tunaamini kwa moyo na kukubaliwa kuwa waadilifu; na tunakiri kwa midomo yetu na kuokolewa.
11Kutsal Yazı, «O'na iman eden hiç kimse utandırılmayacak» der.
11Maandiko Matakatifu yasema: "Kila amwaminiye hatakuwa na sababu ya kuaibika."
12Çünkü Yahudi ve Grek ayrımı yoktur, aynı Rab hepsinin Rabbidir. Kendisine yakaranların hepsine karşı eli açıktır.
12Jambo hili ni kwa wote, kwani hakuna tofauti kati ya Wayahudi na wasio Wayahudi; Bwana wa wote ni mmoja, naye ni mkarimu sana kwao wote wamwombao.
13«Rab'be yakaran herkes kurtulacaktır.»
13Maana Maandiko Matakatifu yasema: "Kila mtu atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa."
14Ama iman etmedikleri kişiye nasıl yakaracaklar? Duymadıkları kişiye nasıl iman edecekler? Tanrı sözünü yayan olmazsa, nasıl duyacaklar?
14Basi, watamwombaje yeye ambaye hawamwamini? Tena, watamwaminije kama hawajapata kusikia habari zake? Na watasikiaje habari zake kama hakuna mhubiri?
15Sözü yaymaya gönderilmezlerse, sözü nasıl yayacaklar? Yazılmış olduğu gibi, «İyi haber müjdeleyenlerin ayakları ne güzeldir!»
15Na watu watahubirije kama hawakutumwa? Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Ni jambo la kupendeza mno kuja kwa wale wanaohubiri Habari Njema!"
16Ne var ki, herkes Müjde'ye uymadı. Yeşaya'nın dediği gibi: «Rab, verdiğimiz habere kim inandı?»
16Lakini wote hawakuipokea hiyo Habari Njema. Maana Isaya alisema: "Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu?"
17Demek ki iman, haberi duymakla, duymak da Mesih'le ilgili sözün yayılmasıyla olur.
17Hivyo basi, imani inatokana na kuusikiliza ujumbe, na huo ujumbe unatokana na neno la Kristo.
18Ama şunu soruyorum: onlar duymadılar mı? Elbette duydular. «Sesleri bütün yeryüzüne, sözleri dünyanın dört bucağına ulaştı.»
18Lakini nauliza: je, hawakuusikia huo ujumbe? Naam, waliusikia; kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Sauti yao imeenea duniani kote; maneno yao yamefika mpaka kingo za ulimwengu."
19Yine şunu soruyorum: İsrail anlamadı mı? Önce Musa, «Ben sizi ulus olmayanla kıskandıracağım, anlayışsız bir ulusla sizi kızdıracağım» diyor.
19Tena nauliza: je, yawezekana kwamba watu wa Israeli hawakufahamu? Mose mwenyewe ni kwa kwanza kujibu: "Nitawafanyeni mwaonee wivu watu ambao si taifa; nitawafanyeni muwe na hasira juu ya taifa la watu wapumbavu."
20Sonra Yeşaya cesaretle, «Beni aramayanlar beni buldu, beni sormayanlara kendimi gösterdim» diyor.
20Tena Isaya anathubutu hata kusema: "Wale ambao hawakunitafuta wamenipata; nimejionyesha kwao wasiouliza habari zangu."
21Ama İsrail'le ilgili diyor ki, «Söz dinlemeyen, asi bir halka bütün gün ellerimi uzattım.»
21Lakini kuhusu Israeli anasema: "Mchana kutwa niliwanyoshea mikono yangu watu waasi na wasiotii."