Swahili: New Testament

World English Bible

1 Thessalonians

5

1Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
1But concerning the times and the seasons, brothers, you have no need that anything be written to you.
2Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
2For you yourselves know well that the day of the Lord comes like a thief in the night.
3Watu watakapokuwa wanasema: "Kila kitu ni shwari na salama" ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
3For when they are saying, “Peace and safety,” then sudden destruction will come on them, like birth pains on a pregnant woman; and they will in no way escape.
4Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
4But you, brothers, aren’t in darkness, that the day should overtake you like a thief.
5Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
5You are all children of light, and children of the day. We don’t belong to the night, nor to darkness,
6Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
6so then let’s not sleep, as the rest do, but let’s watch and be sober.
7Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
7For those who sleep, sleep in the night, and those who are drunk are drunk in the night.
8Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
8But let us, since we belong to the day, be sober, putting on the breastplate of faith and love, and, for a helmet, the hope of salvation.
9Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
9For God didn’t appoint us to wrath, but to the obtaining of salvation through our Lord Jesus Christ,
10ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
10who died for us, that, whether we wake or sleep, we should live together with him.
11Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
11Therefore exhort one another, and build each other up, even as you also do.
12Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
12But we beg you, brothers, to know those who labor among you, and are over you in the Lord, and admonish you,
13Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
13and to respect and honor them in love for their work’s sake. Be at peace among yourselves.
14Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
14We exhort you, brothers, admonish the disorderly, encourage the fainthearted, support the weak, be patient toward all.
15Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
15See that no one returns evil for evil to anyone, but always follow after that which is good, for one another, and for all.
16Furahini daima,
16Rejoice always.
17salini kila wakati
17Pray without ceasing.
18na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
18In everything give thanks, for this is the will of God in Christ Jesus toward you.
19Msimpinge Roho Mtakatifu;
19Don’t quench the Spirit.
20msidharau unabii.
20Don’t despise prophesies.
21Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
21Test all things, and hold firmly that which is good.
22na epukeni kila aina ya uovu.
22Abstain from every form of evil.
23Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu--roho, mioyo na miili yenu--mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
23May the God of peace himself sanctify you completely. May your whole spirit, soul, and body be preserved blameless at the coming of our Lord Jesus Christ.
24Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
24He who calls you is faithful, who will also do it.
25Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
25Brothers, pray for us.
26Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
26Greet all the brothers with a holy kiss.
27Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
27I solemnly command you by the Lord that this letter be read to all the holy brothers.
28Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.
28The grace of our Lord Jesus Christ be with you. Amen.