1"Mimi ni mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima.
1 “I am the true vine, and my Father is the farmer.
2Yeye huliondoa ndani yangu kila tawi lisilozaa matunda, na kila tawi lizaalo hulisafisha lipate kuzaa zaidi.
2 Every branch in me that doesn’t bear fruit, he takes away. Every branch that bears fruit, he prunes, that it may bear more fruit.
3Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya ule ujumbe niliowaambieni.
3 You are already pruned clean because of the word which I have spoken to you.
4Kaeni ndani yangu, nami nikae ndani yenu. Tawi haliwezi peke yake kuzaa matunda lisipokaa katika mzabibu hali kadhalika nanyi hamwezi kuzaa matunda msipokaa ndani yangu.
4 Remain in me, and I in you. As the branch can’t bear fruit by itself, unless it remains in the vine, so neither can you, unless you remain in me.
5"Mimi ni mzabibu, nanyi ni matawi yake. Akaaye ndani yangu, nami ndani yake, huyo atazaa matunda mengi, maana bila mimi hamwezi kufanya chochote.
5 I am the vine. You are the branches. He who remains in me, and I in him, the same bears much fruit, for apart from me you can do nothing.
6Mtu yeyote asipokaa ndani yangu hutupwa nje kama tawi litupwalo nje hata likakauka. Watu huliokota tawi la namna hiyo na kulitupa motoni liungue.
6 If a man doesn’t remain in me, he is thrown out as a branch, and is withered; and they gather them, throw them into the fire, and they are burned.
7Mkikaa ndani yangu na maneno yangu yakikaa ndani yenu, basi, ombeni chochote mtakacho nanyi mtapewa.
7 If you remain in me, and my words remain in you, you will ask whatever you desire, and it will be done for you.
8Baba yangu hutukuzwa kama mkizaa matunda mengi na kuwa wanafunzi wangu.
8 “In this is my Father glorified, that you bear much fruit; and so you will be my disciples.
9Mimi nimewapenda ninyi kama vile Baba alivyonipenda mimi. Kaeni katika pendo langu.
9 Even as the Father has loved me, I also have loved you. Remain in my love.
10Mkizishika amri zangu mtakaa katika pendo langu, kama vile nami nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake.
10 If you keep my commandments, you will remain in my love; even as I have kept my Father’s commandments, and remain in his love.
11Nimewaambieni mambo haya ili furaha yangu ikae ndani yenu, na furaha yenu ikamilike.
11 I have spoken these things to you, that my joy may remain in you, and that your joy may be made full.
12Hii ndiyo amri yangu: pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda ninyi.
12 “This is my commandment, that you love one another, even as I have loved you.
13Hakuna upendo mkuu zaidi kuliko upendo wa mtu atoaye uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.
13 Greater love has no one than this, that someone lay down his life for his friends.
14Ninyi ni rafiki zangu mkifanya ninayowaamuru.
14 You are my friends, if you do whatever I command you.
15Ninyi siwaiti tena watumishi, maana mtumishi hajui anachofanya bwana wake. Lakini mimi nimewaita ninyi rafiki, kwa sababu nimewajulisha yote ambayo nimeyasikia kutoka kwa Baba yangu.
15 No longer do I call you servants, for the servant doesn’t know what his lord does. But I have called you friends, for everything that I heard from my Father, I have made known to you.
16Ninyi hamkunichagua mimi; mimi niliwachagueni na kuwatuma mwende mkazae matunda, matunda yadumuyo, naye Baba apate kuwapa ninyi chochote mumwombacho kwa jina langu.
16 You didn’t choose me, but I chose you, and appointed you, that you should go and bear fruit, and that your fruit should remain; that whatever you will ask of the Father in my name, he may give it to you.
17Basi, amri yangu kwenu ndiyo hii: pendaneni.
17 “I command these things to you, that you may love one another.
18"Kama ulimwengu ukiwachukia ninyi, kumbukeni kwamba umenichukia mimi kabla haujawachukia ninyi.
18 If the world hates you, you know that it has hated me before it hated you.
19Kama mngalikuwa watu wa ulimwengu, ulimwengu ungaliwapenda ninyi kama watu wake. Lakini kwa vile ninyi si wa ulimwengu, ila mimi nimewachagueni kutoka ulimwenguni, kwa sababu hiyo ulimwengu unawachukieni.
19 If you were of the world, the world would love its own. But because you are not of the world, since I chose you out of the world, therefore the world hates you.
20Kumbukeni niliyowaambieni: mtumishi si mkuu zaidi kuliko bwana wake. Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa na ninyi pia; kama wameshika neno langu, watalishika na lenu pia.
20 Remember the word that I said to you: ‘A servant is not greater than his lord.’ John 13:16 If they persecuted me, they will also persecute you. If they kept my word, they will keep yours also.
21Lakini hayo yote watawatendeeni ninyi kwa sababu ya jina langu, kwani hawamjui yeye aliyenituma.
21 But all these things will they do to you for my name’s sake, because they don’t know him who sent me.
22Kama nisingalikuja na kusema nao wasingalikuwa na hatia; lakini sasa hawawezi kujitetea kwamba hawana dhambi.
22 If I had not come and spoken to them, they would not have had sin; but now they have no excuse for their sin.
23Anayenichukia mimi, anamchukia na Baba yangu pia.
23 He who hates me, hates my Father also.
24Kama nisingalifanya kwao mambo ambayo hakuna mtu mwingine amekwisha yafanya wasingalikuwa na hatia; lakini sasa wameona niliyoyafanya wakinichukia mimi, wakamchukia na Baba yangu pia.
24 If I hadn’t done among them the works which no one else did, they wouldn’t have had sin. But now have they seen and also hated both me and my Father.
25Na hivi ni lazima yatimie yale yaliyoandikwa katika Sheria yao: Wamenichukia bure!
25 But this happened so that the word may be fulfilled which was written in their law, ‘They hated me without a cause.’ Psalms 35:19; 69:4
26"Atakapokuja huyo Msaidizi nitakayemtuma kwenu kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia mimi.
26 “When the Counselor Greek Parakletos: Counselor, Helper, Advocate, Intercessor, and Comforter. has come, whom I will send to you from the Father, the Spirit of truth, who proceeds from the Father, he will testify about me.
27Nanyi pia mtanishuhudia kwa kuwa mmekuwa nami tangu mwanzo.
27 You will also testify, because you have been with me from the beginning.