Swahili: New Testament

World English Bible

Luke

18

1Basi, Yesu aliwasimulia mfano kuonyesha kwamba ni lazima kusali daima bila kukata tamaa.
1He also spoke a parable to them that they must always pray, and not give up,
2Alisema: "Katika mji mmoja kulikuwa na hakimu ambaye hakuwa anamcha Mungu wala kumjali binadamu.
2saying, “There was a judge in a certain city who didn’t fear God, and didn’t respect man.
3Katika mji huohuo, kulikuwa pia na mama mmoja mjane, ambaye alimwendea huyo hakimu mara nyingi akimwomba amtetee apate haki yake kutoka kwa adui yake.
3 A widow was in that city, and she often came to him, saying, ‘Defend me from my adversary!’
4Kwa muda mrefu huyo hakimu hakupenda kumtetea huyo mjane; lakini, mwishowe akajisemea: Ingawa mimi simchi Mungu wala simjali binadamu,
4 He wouldn’t for a while, but afterward he said to himself, ‘Though I neither fear God, nor respect man,
5lakini kwa vile huyu mjane ananisumbua, nitamtetea; la sivyo ataendelea kufika hapa, na mwisho atanichosha kabisa!"
5 yet because this widow bothers me, I will defend her, or else she will wear me out by her continual coming.’”
6Basi, Bwana akaendelea kusema, "Sikieni jinsi alivyosema huyo hakimu mbaya.
6The Lord said, “Listen to what the unrighteous judge says.
7Je, ndio kusema Mungu hatawatetea wale aliowachagua, ambao wanamlilia mchana na usiku? Je, atakawia kuwasikiliza?
7 Won’t God avenge his chosen ones, who are crying out to him day and night, and yet he exercises patience with them?
8Nawaambieni atawatetea upesi. Hata hivyo, je, kutakuwako na imani duniani wakati Mwana wa Mtu atakapokuja?"
8 I tell you that he will avenge them quickly. Nevertheless, when the Son of Man comes, will he find faith on the earth?”
9Halafu Yesu aliwaambia pia mfano wa wale ambao walijiona kuwa wema na kuwadharau wengine.
9He spoke also this parable to certain people who were convinced of their own righteousness, and who despised all others.
10"Watu wawili walipanda kwenda Hekaluni kusali: mmoja Mfarisayo, na mwingine mtoza ushuru.
10 “Two men went up into the temple to pray; one was a Pharisee, and the other was a tax collector.
11Huyo Mfarisayo akasimama, akasali kimoyomoyo: Ee Mungu, nakushukuru kwa vile mimi si kama watu wengine: walafi, wadanganyifu au wazinzi. Nakushukuru kwamba mimi si kama huyu mtoza ushuru.
11 The Pharisee stood and prayed to himself like this: ‘God, I thank you, that I am not like the rest of men, extortioners, unrighteous, adulterers, or even like this tax collector.
12Nafunga mara mbili kwa juma, natoa zaka sehemu ya kumi ya pato langu.
12 I fast twice a week. I give tithes of all that I get.’
13Lakini yule mtoza ushuru, akiwa amesimama kwa mbali bila hata kuinua macho yake mbinguni, ila tu akijipiga kifua kwa huzuni, alisema: Ee Mungu, unionee huruma mimi mwenye dhambi.
13 But the tax collector, standing far away, wouldn’t even lift up his eyes to heaven, but beat his breast, saying, ‘God, be merciful to me, a sinner!’
14Nawaambieni, huyu mtoza ushuru alirudi nyumbani akiwa amesamehewa. Lakini yule mwingine, sivyo. Kwa maana kila anayejikweza atashushwa, na kila anayejishusha atakwezwa."
14 I tell you, this man went down to his house justified rather than the other; for everyone who exalts himself will be humbled, but he who humbles himself will be exalted.”
15Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono yake. Wanafunzi walipowaona, wakawazuia kwa maneno makali.
15They were also bringing their babies to him, that he might touch them. But when the disciples saw it, they rebuked them.
16Lakini Yesu akawaita kwake akisema: "Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu kama hawa.
16Jesus summoned them, saying, “Allow the little children to come to me, and don’t hinder them, for the Kingdom of God belongs to such as these.
17Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hataingia katika Ufalme huo."
17 Most certainly, I tell you, whoever doesn’t receive the Kingdom of God like a little child, he will in no way enter into it.”
18Kiongozi mmoja, Myahudi, alimwuliza Yesu, "Mwalimu mwema, nifanye nini ili niweze kuupata uzima wa milele?"
18A certain ruler asked him, saying, “Good Teacher, what shall I do to inherit eternal life?”
19Yesu akamwambia, "Mbona waniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
19Jesus asked him, “Why do you call me good? No one is good, except one—God.
20Unazijua amri: Usizini; usiue; usiibe; usitoe ushahidi wa uongo; waheshimu baba yako na mama yako."
20 You know the commandments: ‘Don’t commit adultery,’ ‘Don’t murder,’ ‘Don’t steal,’ ‘Don’t give false testimony,’ ‘Honor your father and your mother.’”
21Yeye akasema, "Hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu."
21He said, “I have observed all these things from my youth up.”
22Yesu aliposikia hayo akamwambia, "Unatakiwa bado kufanya kitu kimoja: uza kila ulicho nacho, wagawie maskini, na hivyo utakuwa na hazina yako mbinguni; halafu njoo unifuate."
22When Jesus heard these things, he said to him, “You still lack one thing. Sell all that you have, and distribute it to the poor. You will have treasure in heaven. Come, follow me.”
23Lakini huyo mtu aliposikia hayo, alihuzunika sana kwa sababu alikuwa tajiri sana.
23But when he heard these things, he became very sad, for he was very rich.
24Yesu alipoona akihuzunika hivyo, akasema, "Jinsi gani ilivyo vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!
24Jesus, seeing that he became very sad, said, “How hard it is for those who have riches to enter into the Kingdom of God!
25Naam, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu."
25 For it is easier for a camel to enter in through a needle’s eye, than for a rich man to enter into the Kingdom of God.”
26Wale watu waliposikia hayo, wakasema, "Nani basi, atakayeokolewa?"
26Those who heard it said, “Then who can be saved?”
27Yesu akajibu, "Yasiyowezekana kwa binadamu, yanawezekana kwa Mungu."
27But he said, “The things which are impossible with men are possible with God.”
28Naye Petro akamwuliza, "Na sisi je? Tumeacha vitu vyote tukakufuata!"
28Peter said, “Look, we have left everything, and followed you.”
29Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, mtu yeyote aliyeacha nyumba au mke au kaka au wazazi au watoto kwa ajili ya Ufalme wa Mungu,
29He said to them, “Most certainly I tell you, there is no one who has left house, or wife, or brothers, or parents, or children, for the Kingdom of God’s sake,
30atapokea mengi zaidi wakati huu wa sasa, na kupokea uzima wa milele wakati ujao."
30 who will not receive many times more in this time, and in the world to come, eternal life.”
31Yesu aliwachukua kando wale kumi na wawili, akawaambia, "Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu na huko kila kitu kilichoandikwa na manabii kuhusu Mwana wa Mtu kitakamilishwa.
31He took the twelve aside, and said to them, “Behold, we are going up to Jerusalem, and all the things that are written through the prophets concerning the Son of Man will be completed.
32Kwa maana atakabidhiwa kwa watu wa mataifa nao watamtendea vibaya na kumtemea mate.
32 For he will be delivered up to the Gentiles, will be mocked, treated shamefully, and spit on.
33Watampiga mijeledi, watamuua; lakini siku ya tatu atafufuka."
33 They will scourge and kill him. On the third day, he will rise again.”
34Lakini wao hawakuelewa hata kidogo jambo hilo; walikuwa wamefichwa maana ya maneno hayo, na hawakutambua yaliyosemwa.
34They understood none of these things. This saying was hidden from them, and they didn’t understand the things that were said.
35Wakati Yesu alipokaribia Yeriko, kulikuwa na mtu mmoja kipofu ameketi njiani akiomba.
35It happened, as he came near Jericho, a certain blind man sat by the road, begging.
36Aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza, "Kuna nini?"
36Hearing a multitude going by, he asked what this meant.
37Wakamwambia, "Yesu wa Nazareti anapita."
37They told him that Jesus of Nazareth was passing by.
38Naye akapaza sauti akisema, "Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!"
38He cried out, “Jesus, you son of David, have mercy on me!”
39Wale watu waliotangulia wakamkemea wakimwambia anyamaze; lakini yeye akazidi kupaza sauti: "Mwana wa Daudi, nihurumie;"
39Those who led the way rebuked him, that he should be quiet; but he cried out all the more, “You son of David, have mercy on me!”
40Yesu alisimama, akaamuru wamlete mbele yake. Yule kipofu alipofika karibu, Yesu akamwuliza,
40Standing still, Jesus commanded him to be brought to him. When he had come near, he asked him,
41"Unataka nikufanyie nini?" Naye akamjibu, "Bwana, naomba nipate kuona tena."
41 “What do you want me to do?” He said, “Lord, that I may see again.”
42Yesu akamwambia, "Ona! Imani yako imekuponya."
42Jesus said to him, “Receive your sight. Your faith has healed you.”
43Na mara yule aliyekuwa kipofu akapata kuona, akamfuata Yesu akimtukuza Mungu. Watu wote walipoona hayo, wakamsifu Mungu.
43Immediately he received his sight, and followed him, glorifying God. All the people, when they saw it, praised God.