Swahili: New Testament

World English Bible

Luke

20

1Siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuwahubiria juu ya Habari Njema, makuhani wakuu na walimu wa Sheria pamoja na wazee walifika,
1It happened on one of those days, as he was teaching the people in the temple and preaching the Good News, that the priests and scribes came to him with the elders.
2wakasema, "Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?"
2They asked him, “Tell us: by what authority do you do these things? Or who is giving you this authority?”
3Yesu akawaambia, "Na mimi nitawaulizeni swali:
3He answered them, “I also will ask you one question. Tell me:
4mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?"
4 the baptism of John, was it from heaven, or from men?”
5Lakini wao wakajadiliana hivi: "Tukisema yalitoka mbinguni, yeye atatuuliza: Mbona hamkumsadiki?
5They reasoned with themselves, saying, “If we say, ‘From heaven,’ he will say, ‘Why didn’t you believe him?’
6Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii."
6But if we say, ‘From men,’ all the people will stone us, for they are persuaded that John was a prophet.”
7Basi, wakamwambia, "Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi."
7They answered that they didn’t know where it was from.
8Yesu akawaambia, "Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani."
8Jesus said to them, “Neither will I tell you by what authority I do these things.”
9Yesu akaendelea kuwaambia watu mfano huu: "Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima; kisha akasafiri hadi nchi ya mbali, akakaa huko kwa muda mrefu.
9He began to tell the people this parable. “A man planted a vineyard, and rented it out to some farmers, and went into another country for a long time.
10Wakati wa mavuno, mtu huyo alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akachukue sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga mtumishi huyo wakamrudisha mikono mitupu.
10 At the proper season, he sent a servant to the farmers to collect his share of the fruit of the vineyard. But the farmers beat him, and sent him away empty.
11Yule bwana akamtuma tena mtumishi mwingine; lakini wao wakampiga huyo vilevile na kumtendea vibaya, wakamrudisha mikono mitupu.
11 He sent yet another servant, and they also beat him, and treated him shamefully, and sent him away empty.
12Akamtuma tena wa tatu; huyu naye, baada ya kumwumiza, wakamfukuza.
12 He sent yet a third, and they also wounded him, and threw him out.
13Yule mwenye shamba akafikiri: Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpenzi; labda watamjali yeye.
13 The lord of the vineyard said, ‘What shall I do? I will send my beloved son. It may be that seeing him, they will respect him.’
14Wale wakulima walipomwona tu, wakasemezana: Huyu ndiye mrithi. Basi, tumwue ili urithi wake uwe wetu.
14 “But when the farmers saw him, they reasoned among themselves, saying, ‘This is the heir. Come, let’s kill him, that the inheritance may be ours.’
15Basi, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamwua." Yesu akauliza, "Yule mwenye shamba atawafanya nini hao wakulima?
15 They threw him out of the vineyard, and killed him. What therefore will the lord of the vineyard do to them?
16Atakuja kuwaangamiza wakulima hao, na atawapa wakulima wengine hilo shamba la mizabibu." Watu waliposikia maneno hayo, walisema: "Hasha! Yasitukie hata kidogo!"
16 He will come and destroy these farmers, and will give the vineyard to others.” When they heard it, they said, “May it never be!”
17Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, "Maandiko haya Matakatifu yana maana gani basi? Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi!
17But he looked at them, and said, “Then what is this that is written, ‘The stone which the builders rejected, the same was made the chief cornerstone?’
18Mtu yeyote akianguka juu ya jiwe hilo, atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamsaga kabisa."
18 Everyone who falls on that stone will be broken to pieces, but it will crush whomever it falls on to dust.”
19Walimu wa Sheria na makuhani wakuu walifahamu kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu, na hivyo walitaka kumkamata palepale, ila tu waliogopa watu.
19The chief priests and the scribes sought to lay hands on him that very hour, but they feared the people—for they knew he had spoken this parable against them.
20Basi, wakawa wanatafuta wakati wa kufaa. Wakawahonga watu fulani wajisingizie kuwa wema, wakawatuma wamnase Yesu kwa maswali, na hivyo waweze kumtia nguvuni na kumpeleka kwa wakuu wa serikali.
20They watched him, and sent out spies, who pretended to be righteous, that they might trap him in something he said, so as to deliver him up to the power and authority of the governor.
21Hao wapelelezi wakamwambia, "Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli; tunajua kwamba wewe huna ubaguzi; wewe wafundisha ukweli juu ya njia ya Mungu.
21They asked him, “Teacher, we know that you say and teach what is right, and aren’t partial to anyone, but truly teach the way of God.
22Basi, twambie kama ni halali, au la, kulipa kodi kwa Kaisari!"
22Is it lawful for us to pay taxes to Caesar, or not?”
23Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
23But he perceived their craftiness, and said to them, “Why do you test me?
24"Nionyesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?"
24 Show me a denarius. Whose image and inscription are on it?” They answered, “Caesar’s.”
25Nao wakamjibu, "Ni vya Kaisari." Yesu akawaambia, "Basi, mpeni Kaisari vilivyo vyake Kaisari, na Mungu vilivyo vyake Mungu."
25He said to them, “Then give to Caesar the things that are Caesar’s, and to God the things that are God’s.”
26Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.
26They weren’t able to trap him in his words before the people. They marveled at his answer, and were silent.
27Kisha Masadukayo, ambao husema kwamba wafu hawafufuki, wakamjia Yesu, wakasema:
27Some of the Sadducees came to him, those who deny that there is a resurrection.
28"Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu ya mtu fulani akifa na kumwacha mjane wake bila watoto, ni lazima ndugu yake amchukue huyo mama mjane, amzalie watoto ndugu yake marehemu.
28They asked him, “Teacher, Moses wrote to us that if a man’s brother dies having a wife, and he is childless, his brother should take the wife, and raise up children for his brother.
29Sasa, wakati mmoja kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza alioa na baadaye akafa bila kuacha mtoto.
29There were therefore seven brothers. The first took a wife, and died childless.
30Yule ndugu wa pili akamwoa yule mjane, naye pia, akafa;
30The second took her as wife, and he died childless.
31na ndugu wa tatu vilevile. Mambo yakawa yaleyale kwa wote saba--wote walikufa bila kuacha watoto.
31The third took her, and likewise the seven all left no children, and died.
32Mwishowe akafa pia yule mwanamke.
32Afterward the woman also died.
33Je, siku wafu watakapofufuliwa, mwanamke huyo atakuwa mke wa nani? Alikuwa ameolewa na wote saba."
33Therefore in the resurrection whose wife of them will she be? For the seven had her as a wife.”
34Yesu akawaambia, "Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa;
34Jesus said to them, “The children of this age marry, and are given in marriage.
35lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa.
35 But those who are considered worthy to attain to that age and the resurrection from the dead, neither marry, nor are given in marriage.
36Ama hakika, hawawezi kufa tena, kwa sababu watakuwa kama malaika, na ni watoto wa Mungu kwa vile wamefufuliwa katika wafu.
36 For they can’t die any more, for they are like the angels, and are children of God, being children of the resurrection.
37Lakini, kwamba kuna kufufuka kutoka wafu, hata Mose alithibitisha jambo hilo katika Maandiko Matakatifu. Katika sehemu ya Maandiko Matakatifu juu ya kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto, anamtaja Bwana kama Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.
37 But that the dead are raised, even Moses showed at the bush, when he called the Lord ‘The God of Abraham, the God of Isaac, and the God of Jacob.’
38Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa wale walio hai; maana wale aliowaita kwake, wanaishi naye."
38 Now he is not the God of the dead, but of the living, for all are alive to him.”
39Baadhi ya wale walimu wa Sheria wakasema, "Mwalimu, umejibu vema kabisa."
39Some of the scribes answered, “Teacher, you speak well.”
40Walisema hivyo kwa sababu hawakuthubutu kumwuliza tena maswali mengine.
40They didn’t dare to ask him any more questions.
41Yesu akawauliza, "Yasemekanaje kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
41He said to them, “Why do they say that the Christ is David’s son?
42Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia
42 David himself says in the book of Psalms, ‘The Lord said to my Lord, “Sit at my right hand,
43mpaka niwafanye adui zako kama kiti cha kuwekea miguu yako.
43 until I make your enemies the footstool of your feet.”’
44Ikiwa Daudi anamwita yeye, Bwana, basi atakuwaje mwanawe?"
44 “David therefore calls him Lord, so how is he his son?”
45Yesu aliwaambia wanafunzi wake mbele ya watu wote,
45In the hearing of all the people, he said to his disciples,
46"Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamevalia kanzu. Hupenda kusalimiwa na watu kwa heshima masokoni, huketi mahali pa heshima katika masunagogi na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
46 “Beware of the scribes, who like to walk in long robes, and love greetings in the marketplaces, the best seats in the synagogues, and the best places at feasts;
47Huwadhulumu wajane huku wakisingizia kuwa wema kwa kusali sala ndefu. Hao watapata hukumu kali zaidi!"
47 who devour widows’ houses, and for a pretense make long prayers: these will receive greater condemnation.”