1For this cause I, Paul, am the prisoner of Christ Jesus on behalf of you Gentiles,
1Kutokana na hayo, mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu, namwomba Mungu.
2if it is so that you have heard of the administration of that grace of God which was given me toward you;
2Bila shaka mmekwisha sikia kwamba Mungu, kwa neema yake, alinikabidhi kazi hii niifanye kwa faida yenu.
3how that by revelation the mystery was made known to me, as I wrote before in few words,
3Mimi nilijulishwa kwa njia ya ufunuo mpango wake uliofichika. (Nimeandika kwa ufupi juu ya jambo hili,
4by which, when you read, you can perceive my understanding in the mystery of Christ;
4nanyi mkiyasoma maneno yangu mtaweza kujua jinsi ninavyoielewa siri hiyo ya Kristo.)
5which in other generations was not made known to the children of men, as it has now been revealed to his holy apostles and prophets in the Spirit;
5Zamani watu hawakujulishwa siri hiyo; lakini sasa Mungu amewajulisha mitume na manabii wake watakatifu kwa njia ya Roho.
6that the Gentiles are fellow heirs, and fellow members of the body, and fellow partakers of his promise in Christ Jesus through the Good News,
6Siri yenyewe ni hii: kwa njia ya Habari Njema watu wa mataifa mengine wanapata sehemu yao pamoja na Wayahudi katika zile baraka za Mungu; wao ni viungo vya mwili uleule, na wanashiriki ahadi ileile aliyofanya Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.
7of which I was made a servant, according to the gift of that grace of God which was given me according to the working of his power.
7Mimi nimefanywa kuwa mtumishi wa Habari Njema kwa neema ya pekee aliyonijalia Mungu kwa uwezo wake mkuu.
8To me, the very least of all saints, was this grace given, to preach to the Gentiles the unsearchable riches of Christ,
8Mimi ni mdogo kuliko watu wote wa Mungu; lakini amenijalia neema yake, ili niwahubirie watu wa mataifa utajiri wake Kristo usiopimika,
9and to make all men see what is the administration TR reads “fellowship” instead of “administration” of the mystery which for ages has been hidden in God, who created all things through Jesus Christ;
9tena niwaangazie watu wote waone jinsi mpango wa Mungu uliofichika unavyotekelezwa. Mungu aliye Muumba wa vitu vyote alificha siri hiyo yake tangu milele,
10to the intent that now through the assembly the manifold wisdom of God might be made known to the principalities and the powers in the heavenly places,
10kusudi, sasa kwa njia ya kanisa, wakuu na wenye enzi wa mbinguni wapate kuitambua hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi.
11according to the eternal purpose which he purposed in Christ Jesus our Lord;
11Mungu alifanya jambo hilo kufuatana na azimio lake la milele ambalo amelifanya kwa njia ya Kristo Bwana wetu.
12in whom we have boldness and access in confidence through our faith in him.
12Basi, katika kuungana na Kristo, na kwa njia ya imani katika Kristo, sisi tunathubutu kumkaribia Mungu kwa uhodari.
13Therefore I ask that you may not lose heart at my troubles for you, which are your glory.
13Kwa hiyo, nawaombeni msife moyo kwa sababu ya mateso ninayopata kwa ajili yenu, maana hayo ni kwa ajili ya utukufu wenu.
14For this cause, I bow my knees to the Father of our Lord Jesus Christ,
14Kwa sababu hiyo, nampigia magoti Baba,
15from whom every family in heaven and on earth is named,
15aliye asili ya jamaa zote duniani na mbinguni.
16that he would grant you, according to the riches of his glory, that you may be strengthened with power through his Spirit in the inward man;
16Namwomba Mungu, kadiri ya utajiri wa utukufu wake, awajalieni kwa uwezo wa Roho wake, nguvu ya kuwa imara ndani yenu,
17that Christ may dwell in your hearts through faith; to the end that you, being rooted and grounded in love,
17naye Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani. Namwomba mpate kuwa na mzizi na msingi katika mapendo
18may be strengthened to comprehend with all the saints what is the breadth and length and height and depth,
18kusudi muweze kufahamu pamoja na watu wote wa Mungu jinsi upendo wa Kristo ueneavyo kwa mapana na marefu, kwa kimo na kina.
19and to know Christ’s love which surpasses knowledge, that you may be filled with all the fullness of God.
19Naam, mpate kujua upendo wa Kristo upitao elimu yote, mjazwe kabisa utimilifu wote wa Mungu.
20Now to him who is able to do exceedingly abundantly above all that we ask or think, according to the power that works in us,
20Kwake yeye ambaye kwa nguvu yake ifanyayo kazi ndani yetu, aweza kufanya mambo makuu zaidi ya yale tuwezayo kuomba au kufikiria;
21to him be the glory in the assembly and in Christ Jesus to all generations forever and ever. Amen.
21kwake Mungu uwe utukufu katika kanisa na katika Kristo Yesu, nyakati zote, milele na milele! Amina.