1After these things, Jesus went away to the other side of the sea of Galilee, which is also called the Sea of Tiberias.
1Baada ya hayo, Yesu alivuka ziwa Galilaya (au Ziwa Tiberia).
2A great multitude followed him, because they saw his signs which he did on those who were sick.
2Umati mkubwa wa watu ulimfuata kwa sababu watu hao walikuwa wameona ishara alizokuwa akifanya kwa kuwaponya wagonjwa.
3Jesus went up into the mountain, and he sat there with his disciples.
3Yesu alipanda mlimani, akaketi pamoja na wanafunzi wake.
4Now the Passover, the feast of the Jews, was at hand.
4Sikukuu ya Wayahudi iitwayo Pasaka ilikuwa imekaribia.
5Jesus therefore lifting up his eyes, and seeing that a great multitude was coming to him, said to Philip, “Where are we to buy bread, that these may eat?”
5Basi, Yesu na alipotazama na kuona umati wa watu ukija kwake, alimwambia Filipo, "Tununue wapi mikate ili watu hawa wapate kula?"
6This he said to test him, for he himself knew what he would do.
6(Alisema hivyo kwa kumjaribu Filipo, kwani alijua mwenyewe atakalofanya.)
7Philip answered him, “Two hundred denarii worth of bread is not sufficient for them, that everyone of them may receive a little.”
7Filipo akamjibu, "Mikate ya denari mia mbili za fedha haiwatoshi watu hawa hata kama ila mmoja atapata kipande kidogo tu!"
8One of his disciples, Andrew, Simon Peter’s brother, said to him,
8Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, nduguye Simoni Petro, akamwambia,
9“There is a boy here who has five barley loaves and two fish, but what are these among so many?”
9"Yupo hapa mtoto mmoja aliye na mikate mitano ya shayiri na samaki wawili; lakini hivi vyatosha nini kwa watu wengi kama hawa?"
10Jesus said, “Have the people sit down.” Now there was much grass in that place. So the men sat down, in number about five thousand.
10Yesu akasema, "Waketisheni watu." Palikuwa na nyasi tele mahali hapo. Basi, watu wakaketi, jumla yapata wanaume elfu tano.
11Jesus took the loaves; and having given thanks, he distributed to the disciples, and the disciples to those who were sitting down; likewise also of the fish as much as they desired.
11Yesu akaitwaa ile mikate, akamshukuru Mungu, akawagawia watu waliokuwa wameketi; akafanya vivyo hivyo na wale samaki, kila mtu akapata kadiri alivyotaka.
12When they were filled, he said to his disciples, “Gather up the broken pieces which are left over, that nothing be lost.”
12Watu waliposhiba Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Kusanyeni vipande vilivyobaki visipotee."
13So they gathered them up, and filled twelve baskets with broken pieces from the five barley loaves, which were left over by those who had eaten.
13Basi, wakakusanya vipande vya mikate ya shayiri walivyobakiza wale watu waliokula, wakajaza vikapu kumi na viwili.
14When therefore the people saw the sign which Jesus did, they said, “This is truly the prophet who comes into the world.”
14Watu walipoiona ishara hiyo aliyoifanya Yesu, wakasema, "Hakika huyu ndiye nabii anayekuja ulimwenguni."
15Jesus therefore, perceiving that they were about to come and take him by force, to make him king, withdrew again to the mountain by himself.
15Yesu akajua ya kuwa watu walitaka kumchukua wamfanye mfalme, akaondoka tena, akaenda mlimani peke yake.
16When evening came, his disciples went down to the sea,
16Ilipokuwa jioni wanafunzi wake waliteremka hadi ziwani,
17and they entered into the boat, and were going over the sea to Capernaum. It was now dark, and Jesus had not come to them.
17wakapanda mashua ili wavuke kwenda Kafarnaumu. Giza lilikuwa limeingia, na Yesu alikuwa hajawafikia bado.
18The sea was tossed by a great wind blowing.
18Ziwa likaanza kuchafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma.
19When therefore they had rowed about twenty-five or thirty stadia, 25 to 30 stadia is about 5 to 6 kilometers or about 3 to 4 miles they saw Jesus walking on the sea, see Job 9:8 and drawing near to the boat; and they were afraid.
19Wanafunzi walipokuwa wamekwenda umbali wa kilomita tano au sita, walimwona Yesu akitembea juu ya maji, anakaribia mashua; wakaogopa sana.
20But he said to them, “It is I or, I AM . Don’t be afraid.”
20Yesu akawaambia, "Ni mimi, msiogope!"
21They were willing therefore to receive him into the boat. Immediately the boat was at the land where they were going.
21Walifurahi kumchukua Yesu katika mashua; na mara mashua ikawasili nchi kavu walipokuwa wanakwenda.
22On the next day, the multitude that stood on the other side of the sea saw that there was no other boat there, except the one in which his disciples had embarked, and that Jesus hadn’t entered with his disciples into the boat, but his disciples had gone away alone.
22Kesho yake umati wa watu wale waliobaki upande wa pili wa ziwa walitambua kwamba kulikuwa na mashua moja tu pale, na Yesu hakuingia katika mashua pamoja na wanafunzi wake, ila wanafunzi hao walikuwa wamekwenda zao peke yao.
23However boats from Tiberias came near to the place where they ate the bread after the Lord had given thanks.
23Mashua nyingine kutoka Tiberia zilifika mahali hapo watu walipokula ile mikate, Bwana alipokwisha mshukuru Mungu.
24When the multitude therefore saw that Jesus wasn’t there, nor his disciples, they themselves got into the boats, and came to Capernaum, seeking Jesus.
24Basi, hao watu walipogundua kwamba Yesu na wanafunzi wake hawakuwapo mahali hapo, walipanda mashua, wakaenda Kafarnaumu wakimtafuta.
25When they found him on the other side of the sea, they asked him, “Rabbi, when did you come here?”
25Wale watu walipomkuta Yesu ng'ambo ya pili wa ziwa walimwuliza, "Mwalimu, ulifika lini hapa?"
26Jesus answered them, “Most certainly I tell you, you seek me, not because you saw signs, but because you ate of the loaves, and were filled.
26Yesu akawajibu, "Kweli nawaambieni, mnanitafuta si kwa kuwa mmeona ishara, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba.
27 Don’t work for the food which perishes, but for the food which remains to eternal life, which the Son of Man will give to you. For God the Father has sealed him.”
27Msikishughulikie chakula kiharibikacho; kishugulikieni chakula kidumucho kwa ajili ya uzima wa milele. Mwana wa Mtu ambaye Baba amemthibitisha atawapeni chakula hicho."
28They said therefore to him, “What must we do, that we may work the works of God?”
28Wao wakamwuliza, "Tufanye nini ili tuweze kuzitenda kazi za Mungu?"
29Jesus answered them, “This is the work of God, that you believe in him whom he has sent.”
29Yesu akawajibu, "Hii ndiyo kazi anayotaka Mungu muifanye: kumwamini yule aliyemtuma."
30They said therefore to him, “What then do you do for a sign, that we may see, and believe you? What work do you do?
30Hapo wakamwambia, "Utafanya ishara gani ili tuione tupate kukuamini? Utafanya kitu gani?
31Our fathers ate the manna in the wilderness. As it is written, ‘He gave them bread out of heaven Greek and Hebrew use the same word for “heaven”, “the heavens”, “the sky”, and “the air”. to eat.’” Exodus 16:4; Nehemiah 9:15; Psalm 78:24-25
31Wazee wetu walikula mana kule jangwani, kama yasemavyo Maandiko: Aliwalisha mkate kutoka mbinguni."
32Jesus therefore said to them, “Most certainly, I tell you, it wasn’t Moses who gave you the bread out of heaven, but my Father gives you the true bread out of heaven.
32Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, Mose hakuwapeni mkate kutoka mbinguni; Baba yangu ndiye awapaye ninyi mkate halisi kutoka mbinguni.
33 For the bread of God is that which comes down out of heaven, and gives life to the world.”
33Maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na aupaye ulimwengu uzima."
34They said therefore to him, “Lord, always give us this bread.”
34Basi, wakamwambia, "Mheshimiwa, tupe daima mkate huo."
35Jesus said to them, “I am the bread of life. He who comes to me will not be hungry, and he who believes in me will never be thirsty.
35Yesu akawaambia, "Mimi ndimi mkate wa uzima. Anayekuja kwangu hataona njaa; anayeniamini hataona kiu kamwe.
36 But I told you that you have seen me, and yet you don’t believe.
36Lakini niliwaambieni kwamba ingawa mmeniona hamniamini.
37 All those whom the Father gives me will come to me. He who comes to me I will in no way throw out.
37Wote anaonipa Baba watakuja kwangu; nami sitamtupa nje yeyote anayekuja kwangu,
38 For I have come down from heaven, not to do my own will, but the will of him who sent me.
38kwani nimeshuka kutoka mbinguni si kwa ajili ya kufanya matakwa yangu, ila kutimiza matakwa ya yule aliyenituma.
39 This is the will of my Father who sent me, that of all he has given to me I should lose nothing, but should raise him up at the last day.
39Na matakwa ya yule aliyenituma ndiyo haya: nisimpoteze hata mmoja kati ya wale alionipa, ila niwafufue wote Siku ya mwisho.
40 This is the will of the one who sent me, that everyone who sees the Son, and believes in him, should have eternal life; and I will raise him up at the last day.”
40Maana anachotaka Baba yangu ndicho hiki: kila amwonaye Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele; nami nitamfufua Siku ya mwisho."
41The Jews therefore murmured concerning him, because he said, “I am the bread which came down out of heaven.”
41Basi, Wayahudi wakaanza kunung'unika kwa kuwa alisema: "Mimi ni mkate ulioshuka kutoka mbinguni."
42They said, “Isn’t this Jesus, the son of Joseph, whose father and mother we know? How then does he say, ‘I have come down out of heaven?’”
42Wakasema, "Je, huyu si mwana wa Yosefu? Tunawajua baba yake na mama yake! Basi, anawezaje kusema kwamba ameshuka kutoka mbinguni?"
43Therefore Jesus answered them, “Don’t murmur among yourselves.
43Yesu akawaambia, "Acheni kunung'unika ninyi kwa ninyi.
44 No one can come to me unless the Father who sent me draws him, and I will raise him up in the last day.
44Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, Baba aliyenituma asipomvuta kwangu; nami nitamfufua mtu huyo Siku ya mwisho.
45 It is written in the prophets, ‘They will all be taught by God.’ Isaiah 54:13 Therefore everyone who hears from the Father, and has learned, comes to me.
45Manabii wameandika: Watu wote watafundishwa na Mungu. Kila mtu anayemsikia Baba na kujifunza kutoka kwake, huja kwangu.
46 Not that anyone has seen the Father, except he who is from God. He has seen the Father.
46Hii haina maana kwamba yupo mtu aliyemwona Baba, isipokuwa yule aliyetoka kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba.
47 Most certainly, I tell you, he who believes in me has eternal life.
47Kweli, nawaambieni, anayeamini anao uzima wa milele.
48 I am the bread of life.
48Mimi ni mkate wa uzima.
49 Your fathers ate the manna in the wilderness, and they died.
49Wazee wenu walikula mana kule jangwani, lakini walikufa.
50 This is the bread which comes down out of heaven, that anyone may eat of it and not die.
50Huu ndio mkate kutoka mbinguni; mkate ambao anayekula hatakufa.
51 I am the living bread which came down out of heaven. If anyone eats of this bread, he will live forever. Yes, the bread which I will give for the life of the world is my flesh.”
51Mimi ni mkate hai ulioshuka kutoka mbinguni. Mtu yeyote akila mkate huu ataishi milele. Na mkate nitakaompa ni mwili wangu ninaoutoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu."
52The Jews therefore contended with one another, saying, “How can this man give us his flesh to eat?”
52Ndipo Wayahudi wakaanza kubishana kati yao:
53Jesus therefore said to them, “Most certainly I tell you, unless you eat the flesh of the Son of Man and drink his blood, you don’t have life in yourselves.
53Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, msipokula mwili wa Mwana wa Mtu na kunywa damu yake, hamtakuwa na uzima ndani yenu.
54 He who eats my flesh and drinks my blood has eternal life, and I will raise him up at the last day.
54Anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu anao uzima wa milele nami nitamfufua siku ya mwisho.
55 For my flesh is food indeed, and my blood is drink indeed.
55Maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
56 He who eats my flesh and drinks my blood lives in me, and I in him.
56Aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, akaa ndani yangu, nami nakaa ndani yake.
57 As the living Father sent me, and I live because of the Father; so he who feeds on me, he will also live because of me.
57Baba aliye hai alinituma, nami naishi kwa sababu yake; vivyo hivyo anilaye mimi ataishi pia kwa sababu yangu.
58 This is the bread which came down out of heaven—not as our fathers ate the manna, and died. He who eats this bread will live forever.”
58Basi, huu ndio mkate ulioshuka kutoka mbinguni; si kama mana waliyokula babu zetu, wakafa. Aulaye mkate huu ataishi milele."
59He said these things in the synagogue, as he taught in Capernaum.
59Yesu alisema hayo alipokuwa akifundisha katika sunagogi kule Kafarnaumu.
60Therefore many of his disciples, when they heard this, said, “This is a hard saying! Who can listen to it?”
60Basi, wengi wa wafuasi wake waliposikia hayo, wakasema, "Haya ni mambo magumu! Nani awezaye kuyasikiliza?"
61But Jesus knowing in himself that his disciples murmured at this, said to them, “Does this cause you to stumble?
61Yesu alijua bila kuambiwa na mtu kwamba wanafunzi wake walikuwa wananung'unika juu ya jambo hilo, akawauliza, "Je, jambo hili linawafanya muwe na mashaka?
62 Then what if you would see the Son of Man ascending to where he was before?
62Itakuwaje basi, mtakapomwona Mwana wa Mtu akipanda kwenda kule alikokuwa kwanza?
63 It is the spirit who gives life. The flesh profits nothing. The words that I speak to you are spirit, and are life.
63Roho ndiye atiaye uzima; binadamu peke yake hawezi. Maneno niliyowaambieni ni Roho, ni uzima.
64 But there are some of you who don’t believe.” For Jesus knew from the beginning who they were who didn’t believe, and who it was who would betray him.
64Hata hivyo, wako baadhi yenu wasioamini." (Yesu alisema hivyo kwani alijua tangu mwanzo ni kina nani wasioamini, na pia ni nani atakayemsaliti.)
65He said, “For this cause have I said to you that no one can come to me, unless it is given to him by my Father.”
65Kisha akasema, "Ndiyo maana niliwaambieni kwamba hakuna awezaye kuja kwangu asipowezeshwa na Baba yangu."
66At this, many of his disciples went back, and walked no more with him.
66Kutokana na hayo, wengi wa wafuasi wake walirudi nyuma wasiandamane naye tena.
67Jesus said therefore to the twelve, “You don’t also want to go away, do you?”
67Basi, Yesu akawauliza wale kumi na wawili, "Je, nanyi pia mwataka kwenda zenu?"
68Simon Peter answered him, “Lord, to whom would we go? You have the words of eternal life.
68Simoni Petro akamjibu, "Bwana, tutakwenda kwa nani? Wewe unayo maneno yaletayo uzima wa milele.
69We have come to believe and know that you are the Christ, the Son of the living God.”
69Sisi tunaamini, na tunajua kwamba wewe ndiwe yule Mtakatifu wa Mungu."
70Jesus answered them, “Didn’t I choose you, the twelve, and one of you is a devil?”
70Yesu akawaambia, "Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Hata hivyo, mmoja wenu ni Ibilisi!"
71Now he spoke of Judas, the son of Simon Iscariot, for it was he who would betray him, being one of the twelve.
71Yesu alisema hayo juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti; maana huyu alikuwa ndiye atakayemsaliti, ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili.