1After these things, Jesus was walking in Galilee, for he wouldn’t walk in Judea, because the Jews sought to kill him.
1Baada ya hayo, Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea mkoani Yudea kwa sababu viongozi wa Wayahudi walikuwa wanataka kumwua.
2Now the feast of the Jews, the Feast of Booths, was at hand.
2Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
3His brothers therefore said to him, “Depart from here, and go into Judea, that your disciples also may see your works which you do.
3Basi ndugu zake wakamwambia, "Ondoka hapa uende Yudea ili wanafunzi wako wazione kazi unazozifanya.
4For no one does anything in secret, and himself seeks to be known openly. If you do these things, reveal yourself to the world.”
4Mtu hafanyi mambo kwa siri kama anataka kujulikana kwa watu. Maadam unafanya mambo haya, basi, jidhihirishe kwa ulimwengu."
5For even his brothers didn’t believe in him.
5(Hata ndugu zake hawakumwamini!)
6Jesus therefore said to them, “My time has not yet come, but your time is always ready.
6Basi, Yesu akawaambia, "Wakati wangu ufaao haujafika bado. Lakini kwenu ninyi kila wakati unafaa.
7 The world can’t hate you, but it hates me, because I testify about it, that its works are evil.
7Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini mimi wanichukia kwa sababu mimi nauambia wazi kwamba matendo yake ni maovu.
8 You go up to the feast. I am not yet going up to this feast, because my time is not yet fulfilled.”
8Ninyi nendeni kwenye sikukuu hiyo. Mimi siendi kwenye sikukuu hiyo, maana saa yangu ifaayo haijafika."
9Having said these things to them, he stayed in Galilee.
9Alisema hayo kisha akabaki huko Galilaya.
10But when his brothers had gone up to the feast, then he also went up, not publicly, but as it were in secret.
10Baada ya ndugu zake kwenda kwenye sikukuu, Yesu naye alikwenda, lakini hakuenda kwa hadhara bali kwa siri.
11The Jews therefore sought him at the feast, and said, “Where is he?”
11Viongozi wa Wayahudi walikuwa wanamtafuta kwenye sikukuu hiyo; Wakauliza: "Yuko wapi?"
12There was much murmuring among the multitudes concerning him. Some said, “He is a good man.” Others said, “Not so, but he leads the multitude astray.”
12Kulikuwa na minong'ono mingi katika umati wa watu. Baadhi yao walisema, "Ni mtu mwema." Wengine walisema, "La! Anawapotosha watu."
13Yet no one spoke openly of him for fear of the Jews.
13Hata hivyo hakuna mtu aliyethubutu kusema, habari zake hadharani kwa kuwaogopa viongozi wa Wayahudi.
14But when it was now the midst of the feast, Jesus went up into the temple and taught.
14Sikukuu hiyo ilipofikia katikati, Yesu naye alikwenda Hekaluni, akaanza kufundisha.
15The Jews therefore marveled, saying, “How does this man know letters, having never been educated?”
15Basi, Wayahudi wakashangaa na kusema "Mtu huyu amepataje elimu naye hakusoma shuleni?"
16Jesus therefore answered them, “My teaching is not mine, but his who sent me.
16Hapo Yesu akawajibu, "Mafundisho ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
17 If anyone desires to do his will, he will know about the teaching, whether it is from God, or if I am speaking from myself.
17Mtu anayependa kufanya yale anayotaka Mungu, atajua kama mafundisho yangu yametoka kwa Mungu, au mimi najisemea tu mwenyewe.
18 He who speaks from himself seeks his own glory, but he who seeks the glory of him who sent him is true, and no unrighteousness is in him.
18Yeye anayejisemea tu mwenyewe anatafuta sifa yake mwenyewe; lakini anayetafuta sifa ya yule aliyemtuma, huyo ni mwaminifu, na ndani yake hamna uovu wowote.
19 Didn’t Moses give you the law, and yet none of you keeps the law? Why do you seek to kill me?”
19Je, Mose hakuwapeni Sheria? Hata hivyo, hakuna hata mmoja wenu anayeishika Sheria. Kwa nini mnataka kuniua?"
20The multitude answered, “You have a demon! Who seeks to kill you?”
20Hapo watu wakamjibu, "Una wazimu wewe! Nani anataka kukuua?"
21Jesus answered them, “I did one work, and you all marvel because of it.
21Yesu akawajibu, "Kuna jambo moja nililofanya, nanyi mnalistaajabia.
22 Moses has given you circumcision (not that it is of Moses, but of the fathers), and on the Sabbath you circumcise a boy.
22Mose aliwapeni ile desturi ya kutahiri. (Si kwamba desturi hiyo ilitoka kwa Mose, bali ilitoka kwa mababu). Sasa ninyi humtahiri mtu hata siku ya Sabato.
23 If a boy receives circumcision on the Sabbath, that the law of Moses may not be broken, are you angry with me, because I made a man completely healthy on the Sabbath?
23Ikiwa basi, mtu hutahiriwa hata siku ya Sabato kusudi Sheria ya Mose isivunjwe, mbona mnanikasirikia kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya Sabato?
24 Don’t judge according to appearance, but judge righteous judgment.”
24Msihukumu mambo kwa nje tu; toeni hukumu ya haki."
25Therefore some of them of Jerusalem said, “Isn’t this he whom they seek to kill?
25Baadhi ya watu wa Yerusalemu walisema, "Je, yule mtu wanayemtafuta wamuue si huyu?
26Behold, he speaks openly, and they say nothing to him. Can it be that the rulers indeed know that this is truly the Christ?
26Tazameni sasa! Anawaonya hadharani, wala hakuna mtu anayemwambia hata neno. Je, yawezekana kuwa viongozi wametambua kweli kwamba huyu ndiye Kristo?
27However we know where this man comes from, but when the Christ comes, no one will know where he comes from.”
27Kristo atakapokuja hakuna mtu atakayejua mahali alikotoka, lakini sisi tunajua alikotoka mtu huyu!"
28Jesus therefore cried out in the temple, teaching and saying, “You both know me, and know where I am from. I have not come of myself, but he who sent me is true, whom you don’t know.
28Basi, Yesu alipokuwa anafundisha Hekaluni alipaaza sauti na kusema, "Ati mnanijua; hata nilikotoka mnakujua! Hata hivyo, sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe; ila yeye aliyenituma mimi ni wa kweli, nanyi hamumjui.
29 I know him, because I am from him, and he sent me.”
29Lakini mimi namjua kwa sababu nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma."
30They sought therefore to take him; but no one laid a hand on him, because his hour had not yet come.
30Basi, watu wakataka kumtia nguvuni, lakini hakuna mtu aliyethubutu kumkamata kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
31But of the multitude, many believed in him. They said, “When the Christ comes, he won’t do more signs than those which this man has done, will he?”
31Wengi katika ule umati wa watu walimwamini, wakasema, "Je, Kristo akija atafanya ishara kubwa zaidi kuliko alizozifanya huyu?"
32The Pharisees heard the multitude murmuring these things concerning him, and the chief priests and the Pharisees sent officers to arrest him.
32Mafarisayo waliwasikia watu wakinong'ona maneno hayo juu ya Yesu. Basi, wao pamoja na makuhani wakuu wakawatuma walinzi wamtie nguvuni.
33Then Jesus said, “I will be with you a little while longer, then I go to him who sent me.
33Yesu akasema, "Bado niko nanyi kwa muda mfupi, kisha nitamwendea yule aliyenituma.
34 You will seek me, and won’t find me; and where I am, you can’t come.”
34Mtanitafuta lakini hamtaniona, maana pale nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika."
35The Jews therefore said among themselves, “Where will this man go that we won’t find him? Will he go to the Dispersion among the Greeks, and teach the Greeks?
35Viongozi wa Wayahudi wakasema wao kwa wao, "Mtu huyu atakwenda wapi ambapo hatutaweza kumpata? Atakwenda kwa Wayahudi waliotawanyika kati ya Wagiriki, na kuwafundisha Wagiriki?
36What is this word that he said, ‘You will seek me, and won’t find me; and where I am, you can’t come’? ”
36Ana maana gani anaposema: Mtanitafuta lakini hamtanipata, na mahali nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika?"
37Now on the last and greatest day of the feast, Jesus stood and cried out, “If anyone is thirsty, let him come to me and drink!
37Siku ya mwisho ya sikukuu hiyo ilikuwa siku maalum. Yesu alisimama, akasema kwa sauti kubwa, "Aliye na kiu na aje kwangu anywe.
38 He who believes in me, as the Scripture has said, from within him will flow rivers of living water.”
38Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: Anayeniamini mimi, mito ya maji yenye uzima itatiririka kutoka moyoni mwake!"
39But he said this about the Spirit, which those believing in him were to receive. For the Holy Spirit was not yet given, because Jesus wasn’t yet glorified.
39(Alisema hayo kumhusu Roho ambaye wale waliomwamini yeye watampokea. Wakati huo Roho alikuwa hajafika kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.)
40Many of the multitude therefore, when they heard these words, said, “This is truly the prophet.”
40Baadhi ya watu katika ule umati walisikia maneno hayo, wakasema, "Kweli mtu huyu ndiye yule nabii!"
41Others said, “This is the Christ.” But some said, “What, does the Christ come out of Galilee?
41Wengine wakasema, "Huyu ndiye Kristo!" Lakini wengine walisema, "Je, yawezekana Kristo akatoka Galilaya?
42Hasn’t the Scripture said that the Christ comes of the seed of David, 2 Samuel 7:12 and from Bethlehem, Micah 5:2 the village where David was?”
42Maandiko Matakatifu yasemaje? Yanasema: Kristo atatoka katika ukoo wa Daudi, na atazaliwa Bethlehemu, mji wa Daudi!"
43So there arose a division in the multitude because of him.
43Basi, kukatokea mafarakano juu yake katika ule umati wa watu.
44Some of them would have arrested him, but no one laid hands on him.
44Baadhi ya watu walitaka kumtia nguvuni lakini hakuna aliyejaribu kumkamata.
45The officers therefore came to the chief priests and Pharisees, and they said to them, “Why didn’t you bring him?”
45Kisha wale walinzi wakarudi kwa makuhani wakuu na Mafarisayo; nao wakawauliza, "Kwa nini hamkumleta?"
46The officers answered, “No man ever spoke like this man!”
46Walinzi wakawajibu, "Hakuna mtu aliyepata kamwe kusema kama asemavyo mtu huyu!"
47The Pharisees therefore answered them, “You aren’t also led astray, are you?
47Mafarisayo wakawauliza, "Je, nanyi pia mmedanganyika?
48Have any of the rulers believed in him, or of the Pharisees?
48Je, mmekwisha mwona hata mmoja wa viongozi wa watu, au mmoja wa Mafarisayo aliyemwamini?
49But this multitude that doesn’t know the law is accursed.”
49Lakini umati huu haujui Sheria ya Mose; umelaaniwa!"
50Nicodemus (he who came to him by night, being one of them) said to them,
50Mmoja wao alikuwa Nikodemo ambaye hapo awali alikuwa amemwendea Yesu. Basi, yeye akawaambia,
51“Does our law judge a man, unless it first hears from him personally and knows what he does?”
51"Je, Sheria yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza na kujua anafanya nini?"
52They answered him, “Are you also from Galilee? Search, and see that no prophet has arisen out of Galilee. See Isaiah 9:1 and Matthew 4:13-16. ”
52Nao wakamjibu, "Je, wewe pia umetoka Galilaya? Haya, kayachunguze Maandiko Matakatifu nawe utaona kwamba Galilaya hakutoki kamwe nabii!"
53Everyone went to his own house,
53Basi, wote wakaondoka, kila mtu akaenda zake;