World English Bible

Swahili: New Testament

Luke

4

1Jesus, full of the Holy Spirit, returned from the Jordan, and was led by the Spirit into the wilderness
1Yesu alitoka katika mto Yordani akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akaongozwa na Roho mpaka jangwani.
2for forty days, being tempted by the devil. He ate nothing in those days. Afterward, when they were completed, he was hungry.
2Huko alijaribiwa na Ibilisi kwa muda wa siku arubaini. Wakati huo wote hakula chochote, na baada ya siku hizo akasikia njaa.
3The devil said to him, “If you are the Son of God, command this stone to become bread.”
3Ndipo Ibilisi akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate."
4Jesus answered him, saying, “It is written, ‘Man shall not live by bread alone, but by every word of God.’”
4Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Mtu haishi kwa mkate tu."
5The devil, leading him up on a high mountain, showed him all the kingdoms of the world in a moment of time.
5Kisha Ibilisi akamchukua hadi mahali pa juu, akamwonyesha kwa mara moja falme zote za ulimwengu. Huyo Shetani akamwambia,
6The devil said to him, “I will give you all this authority, and their glory, for it has been delivered to me; and I give it to whomever I want.
6"Nitakupa uwezo juu ya falme zote hizi na fahari zake, kwa maana nimepewa hivi vyote; nikitaka kumpa mtu ninaweza.
7If you therefore will worship before me, it will all be yours.”
7Hivi vyote vitakuwa mali yako wewe, kama ukiniabudu."
8Jesus answered him, “Get behind me Satan! For it is written, ‘You shall worship the Lord your God, and you shall serve him only.’”
8Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Utamwabudu Bwana Mungu wako, na utamtumikia yeye peke yake."
9He led him to Jerusalem, and set him on the pinnacle of the temple, and said to him, “If you are the Son of God, cast yourself down from here,
9Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, kwenye mnara wa Hekalu, akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu,
10for it is written, ‘He will put his angels in charge of you, to guard you;’
10kwa maana imeandikwa: Atawaamuru malaika wake wakulinde,
11and, ‘On their hands they will bear you up, lest perhaps you dash your foot against a stone.’”
11na tena, Watakuchukua mikononi mwao usije ukajikwaa mguu wako kwenye jiwe."
12Jesus answering, said to him, “It has been said, ‘You shall not tempt the Lord your God.’”
12Lakini Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Usimjaribu Bwana Mungu wako."
13When the devil had completed every temptation, he departed from him until another time.
13Ibilisi alipokwishamjaribu kwa kila njia, akamwacha kwa muda.
14Jesus returned in the power of the Spirit into Galilee, and news about him spread through all the surrounding area.
14Yesu alirudi Galilaya akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, na habari zake zikaenea katika sehemu zote za jirani.
15He taught in their synagogues, being glorified by all.
15Naye akawa anawafundisha watu katika masunagogi yao, akasifiwa na wote.
16He came to Nazareth, where he had been brought up. He entered, as was his custom, into the synagogue on the Sabbath day, and stood up to read.
16Basi, Yesu alikwenda Nazareti, mahali alipolelewa, na siku ya Sabato, aliingia katika sunagogi, kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome Maandiko Matakatifu kwa sauti.
17The book of the prophet Isaiah was handed to him. He opened the book, and found the place where it was written,
17Akapokea kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na akakuta mahali palipoandikwa:
18 “The Spirit of the Lord is on me, because he has anointed me to preach good news to the poor. He has sent me to heal the brokenhearted, to proclaim release to the captives, recovering of sight to the blind, to deliver those who are crushed,
18"Roho wa Bwana yu juu yangu, kwani amenipaka mafuta niwahubirie maskini Habari Njema. Amenituma niwatangazie mateka watapata uhuru, vipofu watapata kuona tena; amenituma niwakomboe wanaoonewa,
19 and to proclaim the acceptable year of the Lord.”
19na kutangaza mwaka wa neema ya Bwana."
20He closed the book, gave it back to the attendant, and sat down. The eyes of all in the synagogue were fastened on him.
20Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.
21He began to tell them, “Today, this Scripture has been fulfilled in your hearing.”
21Naye akaanza kuwaambia, "Andiko hili mlilosikia likisomwa, limetimia leo."
22All testified about him, and wondered at the gracious words which proceeded out of his mouth, and they said, “Isn’t this Joseph’s son?”
22Wote wakavutiwa sana naye, wakastaajabia maneno mazuri aliyosema. Wakanena, "Je, huyu si mwana wa Yosefu?"
23He said to them, “Doubtless you will tell me this parable, ‘Physician, heal yourself! Whatever we have heard done at Capernaum, do also here in your hometown.’”
23Naye akawaambia, "Bila shaka mtaniambia msemo huu: Mganga jiponye mwenyewe, na pia mtasema: Yote tuliyosikia umeyafanya kule Kafarnaumu, yafanye hapa pia katika kijiji chako."
24He said, “Most certainly I tell you, no prophet is acceptable in his hometown.
24Akaendelea kusema, "Hakika nawaambieni, nabii hatambuliwi katika kijiji chake.
25 But truly I tell you, there were many widows in Israel in the days of Elijah, when the sky was shut up three years and six months, when a great famine came over all the land.
25Lakini, sikilizeni! Kweli kulikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli nyakati za Eliya. Wakati huo mvua iliacha kunyesha kwa muda wa miaka mitatu na nusu; kukawa na njaa kubwa katika nchi yote.
26 Elijah was sent to none of them, except to Zarephath, in the land of Sidon, to a woman who was a widow.
26Hata hivyo, Eliya hakutumwa kwa mjane yeyote ila kwa mwanamke mjane wa Sarepta, Sidoni.
27 There were many lepers in Israel in the time of Elisha the prophet, yet not one of them was cleansed, except Naaman, the Syrian.”
27Tena, katika nchi ya Israeli nyakati za Elisha kulikuwa na wenye ukoma wengi. Hata hivyo, hakuna yeyote aliyetakaswa ila tu Naamani, mwenyeji wa Siria."
28They were all filled with wrath in the synagogue, as they heard these things.
28Wote waliokuwa katika lile sunagogi waliposikia hayo walikasirika sana.
29They rose up, threw him out of the city, and led him to the brow of the hill that their city was built on, that they might throw him off the cliff.
29Wakasimama, wakamtoa nje ya mji wao uliokuwa umejengwa juu ya kilima, wakampeleka mpaka kwenye ukingo wa kilima hicho ili wamtupe chini.
30But he, passing through their midst, went his way.
30Lakini Yesu akapita katikati yao, akaenda zake.
31He came down to Capernaum, a city of Galilee. He was teaching them on the Sabbath day,
31Kisha Yesu akashuka mpaka Kafarnaumu katika mkoa wa Galilaya, akawa anawafundisha watu siku ya Sabato.
32and they were astonished at his teaching, for his word was with authority.
32Wakastaajabia uwezo aliokuwa nao katika kufundisha.
33In the synagogue there was a man who had a spirit of an unclean demon, and he cried out with a loud voice,
33Na katika lile sunagogi kulikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na roho ya pepo mchafu; akapiga ukelele wa kuziba masikio:
34saying, “Ah! what have we to do with you, Jesus of Nazareth? Have you come to destroy us? I know you who you are: the Holy One of God!”
34"We! Yesu wa Nazareti! Kwa nini unatuingilia? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakufahamu wewe ni nani. Wewe ni mjumbe Mtakatifu wa Mungu!"
35Jesus rebuked him, saying, “Be silent, and come out of him!” When the demon had thrown him down in their midst, he came out of him, having done him no harm.
35Lakini Yesu akamkemea huyo pepo akisema: "Nyamaza! Mtoke mtu huyu!" Basi, huyo pepo baada ya kumwangusha yule mtu chini, akamtoka bila kumdhuru hata kidogo.
36Amazement came on all, and they spoke together, one with another, saying, “What is this word? For with authority and power he commands the unclean spirits, and they come out!”
36Watu wote wakashangaa, wakawa wanaambiana, "Hili ni jambo la ajabu, maana kwa uwezo na nguvu anawaamuru pepo wachafu watoke, nao wanatoka!"
37News about him went out into every place of the surrounding region.
37Habari zake zikaenea mahali pote katika mkoa ule.
38He rose up from the synagogue, and entered into Simon’s house. Simon’s mother-in-law was afflicted with a great fever, and they begged him for her.
38Yesu alitoka katika lile sunagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa na homa kali; wakamwomba amponye.
39He stood over her, and rebuked the fever; and it left her. Immediately she rose up and served them.
39Yesu akaenda akasimama karibu naye, akaikemea ile homa, nayo ikamwacha. Mara yule mama akainuka, akawatumikia.
40When the sun was setting, all those who had any sick with various diseases brought them to him; and he laid his hands on every one of them, and healed them.
40Jua lilipokuwa linatua, wote waliokuwa na wagonjwa wao mbalimbali waliwaleta kwake; naye akaweka mikono yake juu ya kila mmoja wao, akawaponya wote.
41Demons also came out from many, crying out, and saying, “You are the Christ, the Son of God!” Rebuking them, he didn’t allow them to speak, because they knew that he was the Christ.
41Pepo waliwatoka watu wengi, wakapiga kelele wakisema: "Wewe u Mwana wa Mungu!" Lakini Yesu akawakemea, wala hakuwaruhusu kusema, maana walimfahamu kwamba yeye ndiye Kristo.
42When it was day, he departed and went into an uninhabited place, and the multitudes looked for him, and came to him, and held on to him, so that he wouldn’t go away from them.
42Kesho yake asubuhi Yesu aliondoka akaenda mahali pa faragha. Watu wakawa wanamtafuta, na walipofika mahali alipokuwa, wakajaribu kumzuia ili asiondoke kwao.
43But he said to them, “I must preach the good news of the Kingdom of God to the other cities also. For this reason I have been sent.”
43Lakini yeye akawaambia, "Ninapaswa kuhubiri Habari Njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, maana nilitumwa kwa ajili hiyo."
44He was preaching in the synagogues of Galilee.
44Akawa anahubiri katika masunagogi ya Yudea.