1信心使我们胜过世界
1Kila mtu anayeamini kwamba Yesu ni Kristo, huyo ni mtoto wa Mungu; na, anayempenda mzazi humpenda pia mtoto wa huyo mzazi.
2我们若爱 神,并且遵行他的命令,就知道我们是爱 神的儿女了。
2Hivi ndivyo tunavyojua kwamba tunawapenda watoto wa Mungu: Kwa kumpenda Mungu na kuzitii amri zake;
3我们遵守 神的命令,就是爱他了;而且他的命令是不难遵守的,
3maana kumpenda Mungu ni kuzitii amri zake. Na, amri zake si ngumu,
4因为凡从 神生的就胜过世界。使我们胜过世界的,就是我们的信心。
4maana kila aliye mtoto wa Mungu anaweza kuushinda ulimwengu. Hivi ndivyo tunavyoushinda ulimwengu: kwa imani yetu.
5胜过世界的是谁呢?不就是那信耶稣是 神的儿子的吗?
5Nani, basi, awezaye kuushinda ulimwengu? Ni yule anayeamini kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.
6 神为他儿子作的见证那借着水和血来的就是耶稣基督,不是单用水,而是用水又用血;作见证的是圣灵,因为圣灵就是真理。
6Yesu Kristo ndiye aliyekuja kwa maji ya ubatizo wake na kwa damu ya kifo chake. Hakuja kwa maji tu, bali kwa maji na kwa damu. Naye Roho anashuhudia kwamba ni kweli, kwani Roho ni ukweli.
7原来作见证的有三样,
7Basi, wako mashahidi watatu:
8就是圣灵、水和血,这三样是一致的。
8Roho, maji na damu; na ushahidi wa hawa watatu waafikiana.
9我们若接受人的见证, 神的见证就更强而有力了,因为这是 神为他的儿子作的见证。
9Ikiwa twaukubali ushahidi wa binadamu, ushahidi wa Mungu una uzito zaidi; na huu ndio ushahidi alioutoa Mungu mwenyewe juu ya Mwanae.
10信 神的儿子的,就有这见证在他心里;不信 神的,就是把 神当作说谎的,因为他不信 神为他儿子所作的见证。
10Anayemwamini mwana wa Mungu anao ushahidi huo ndani yake; lakini asiyemwamini Mungu, anamfanya yeye kuwa mwongo, maana hakuamini ushahidi alioutoa Mungu juu ya Mwanae.
11这见证就是 神已经把永远的生命赐给我们,这生命是在他儿子里面的。
11Na, ushahidi wenyewe ndio huu: Mungu alitupatia uzima wa milele, na uzima huo uko kwa Bwana.
12凡有 神儿子的,就有生命;没有 神儿子的,就没有生命。
12Yeyote, aliye na Mwana wa Mungu anao uzima huo; asiye na Mwana wa Mungu, hana uzima.
13要照 神的旨意祈求我把这些事写给你们信 神的儿子之名的人,是要你们知道自己有永生。
13Nawaandikieni mpate kujua kwamba mnao uzima wa milele ninyi mnaoamini kwa jina la Mwana wa Mungu.
14如果我们照着 神的旨意祈求,他必听我们;这就是我们对 神所存的坦然无惧的心。
14Na sisi tuko thabiti mbele ya Mungu kwani tuna hakika kwamba tukimwomba chochote kadiri ya mapenzi yake, yeye hutusikiliza.
15既然他听我们的祈求,我们就知道,我们无论求什么,他必赐给我们。
15Yeye hutusikiliza kila tunapomwomba; na kwa vile tunajua kwamba yeye hutusikiliza kila tunapomwomba, twajua pia kwamba atupatia yote tunayomwomba.
16如果有人看见弟兄犯了不至于死的罪,他就要祈求, 神必因他的缘故,把生命赐给那些犯了不至于死的罪的人;有至于死的罪,我不说他应当为那罪祈求。
16Mtu akimwona ndugu yake ametenda dhambi isiyompeleka kwenye kifo anapaswa kumwombea kwa Mungu, naye Mungu atampatia uzima. Nasema jambo hili kuhusu wale waliotenda dhambi ambazo si za kifo. Lakini ipo dhambi yenye kumpeleka mtu kwenye kifo nami sisemi kwamba mnapaswa kumwomba Mungu kwa ajili ya hiyo.
17一切不义都是罪,但也有不至于死的罪。
17Kila tendo lisilo adilifu ni dhambi, lakini kuna dhambi isiyompeleka mtu kwenye kifo.
18我们知道凡从 神生的就不犯罪,而且从 神生的那一位也必保守他,连那恶者也不能碰他。
18Tunajua kwamba kila aliye mtoto wa Mungu hatendi dhambi, kwa sababu Mwana wa Mungu humlinda salama, na yule Mwovu hawezi kumdhuru.
19我们知道我们是属于 神的,而整个世界是伏在那恶者手下。
19Tunajua kwamba sisi ni wake Mungu ingawa ulimwengu wote unatawaliwa na yule Mwovu.
20我们知道 神的儿子已经来了,并且赐给我们悟性,使我们能认识那位真实者。我们也在那位真实者里面,就是在他儿子耶稣基督里面。这一位就是真神,也是永远的生命。
20Twajua pia kwamba Mwana wa Mungu amekuja, akatupa elimu ili tumjue Mungu wa kweli; tuishi katika muungano na Mungu wa kweli--katika muungano na Mwanae, Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli, na huu ndio uzima wa milele.
21孩子们,你们要保守自己远离偶像。
21Watoto wangu, epukaneni na sanamu za miungu.