1问安我这作长老的,写信给蒙拣选的夫人和她的儿女。你们是我在真理中所爱的;不单是我,凡认识真理的,
1Mimi Mzee nakuandikia wewe Bimkubwa mteule, pamoja na watoto wako ninaowapenda kweli. Wala si mimi tu ninayewapenda, bali pia wote wanaoujua ule ukweli wanawapenda ninyi,
2也因为真理的缘故爱你们。这真理在我们里面,也必与我们同在,直到永远。
2kwa sababu ukweli unakaa nasi milele.
3愿恩惠、怜悯、平安,从父 神和他儿子耶稣基督在真理和爱中与我们同在。
3Neema na huruma na amani zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo, Mwana wa Baba, zitakuwa pamoja nasi katika ukweli na upendo.
4要按真理凭爱心行事我看见你的儿女中,有人照着我们从父领受的命令在真理中行事,我就非常欣慰。
4Nilifurahi sana kuona kwamba baadhi ya watoto wako wanaishi katika ukweli kama Baba alivyotuamuru.
5夫人哪,我现在请求你,我们要彼此相爱。我写给你的,不是一条新命令,而是我们从起初就有的。
5Basi, Bimkubwa, ninalo ombi moja kwako: tupendane. Ombi hili si amri mpya, bali ni amri ileile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo.
6我们要照着他的命令行事,这就是爱。你们从起初所听见的那命令,就是要你们凭着爱心行事。
6Upendo maana yake ni kuishi kwa kuzitii amri zake Mungu. Amri niliyoisikia tangu mwanzo ndiyo hii: mnapaswa nyote kuishi katika upendo.
7有许多欺骗人的已经在世上出现,他们否认耶稣基督是成了肉身来的;这就是那骗人的和敌基督的。
7Wadanganyifu wengi wamezuka duniani, watu ambao hawakiri kwamba Yesu Kristo amekuja kwetu akawa binadamu. Mtu asemaye hivyo ni mdanganyifu na ni Adui wa Kristo.
8你们要小心,不要拆毁我们已经完成的工作,却要得着美满的赏赐。
8Basi, jihadharini ninyi wenyewe ili msije mkapoteza kile mlichokishugulikia, bali mpate tuzo lenu kamili.
9凡越过基督的教训又不持守的,就没有 神;持守这教训的,就有父和子了。
9Asiyezingatia na kudumu katika mafundisho ya Kristo, bali anayakiuka, hana Mungu. Lakini anayedumu katika mafundisho hayo anaye Baba na Mwana.
10如果有人到你们那里,不传这教训,你们就不要接待他到家里,也不要问候他;
10Basi, kama mtu akija kwenu bila kuwaleteeni mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani kwenu, wala msimsalimu.
11因为问候他的,就在他的恶事上有分了。
11Maana anayemsalimu mtu huyo, anashirikiana naye katika matendo yake maovu.
12问候的话我还有许多话要写给你们,可是我不想借用纸墨,只是盼望到你们那里当面谈谈,好让我们的喜乐充足。
12Ninayo mengi ya kuwaambieni lakini sipendi kufanya hivyo kwa karatasi na wino; badala yake, natumaini kuwatembeleeni na kuzungumza nanyi ana kwa ana, ili furaha yetu ikamilike.
13你那蒙拣选的姊妹的儿女都问候你。
13Watoto wa dada yako mteule wanakusalimu.