1要讨 神喜悦
1Hatimaye, ndugu zangu, mmejifunza kutoka kwetu namna mnavyopaswa kuishi ili kumpendeza Mungu. Na kweli mmekuwa mnaishi hivyo. Sasa tunawaombeni na kuwasihi kwa jina la Bwana Yesu mfanye vema zaidi.
2我们凭着主耶稣传给你们的是什么命令,你们是知道的。
2Maana mnayajua yale maagizo tuliyowapeni kwa mamlaka ya Bwana Yesu.
3 神的旨意是要你们圣洁,远避淫行;
3Mungu anataka ninyi muwe watakatifu na mjiepushe kabisa na maisha ya zinaa.
4要你们各人晓得怎样用圣洁尊贵的方法保守自己的身体(“身体”原文作“器皿”);
4Kila mwanamume anapaswa kujua namna ya kuishi na mkewe kwa utakatifu na heshima,
5不要放纵邪情私欲,像那些不认识 神的外族人一样;
5na si kwa tamaa mbaya kama watu wa mataifa mengine wasiomjua Mungu.
6谁也不要在这事上越轨,占弟兄的便宜,因为这一类的事,主必报应。这是我们从前告诉过你们,又严严警戒过你们的。
6Basi, mtu yeyote asimkosee au kumpunja mwenzake kuhusu jambo hili. Tulikwisha waambieni hayo na kuwaonya kwamba Bwana atawaadhibu wanaofanya mambo hayo.
7 神呼召我们,不是要我们沾染污秽,而是要我们圣洁。
7Mungu hakutuita tuishi maisha ya zinaa, bali tuishi katika utakatifu.
8所以那弃绝这命令的,不是弃绝人,而是弃绝把他自己的圣灵赐给你们的那位 神。
8Kwa hiyo basi, anayedharau mafundisho hayo hamdharau mtu, bali amdharau Mungu mwenyewe anayewapeni Roho wake Mtakatifu.
9论到弟兄相爱,用不着人写什么给你们,因为你们自己受了 神的教导,要彼此相爱。
9Hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya kuwapenda ndugu zenu waumini. Ninyi wenyewe mmefundishwa na Mungu namna mnavyopaswa kupendana.
10其实,你们向全马其顿所有的弟兄,已经这样行了。但是,弟兄们,我们劝你们要更加彼此相爱;
10Na mmekuwa mkiwatendea hivyo ndugu zenu wote kila mahali katika Makedonia. Basi, ndugu tunawaombeni mfanye hata zaidi.
11又要立志过安静的生活,办自己的事,亲手作工,正如我们从前吩咐过你们,
11Muwe na nia ya kuishi maisha ya utulivu, kila mmoja ashughulikie mambo yake mwenyewe na afanye kazi kwa mikono yake mwenyewe kama tulivyowaagiza pale awali.
12使你们行事为人可以得到外人的尊敬,自己也不会有什么缺乏了。
12Kwa namna hiyo mtajipatia sifa nzuri kutoka kwa wale wasio Wakristo, na hamtakuwa na lazima ya kuwategemea wengine kwa mahitaji yenu.
13在主里睡了的人必先复活弟兄们,论到睡了的人,我们不愿意你们不知道,免得你们忧伤,像那些没有盼望的人一样。
13Ndugu, twataka mjue ukweli kuhusu wale ambao wamekwisha fariki dunia, ili msipatwe na huzuni kama watu wengine wasio na matumaini.
14我们若信耶稣死了,又复活了,照样,也应该相信那些靠着耶稣已经睡了的人, 神必定把他们和耶稣一同带来。
14Sisi tunaamini kwamba Yesu alikufa, akafufuka; na hivyo sisi tunaamini kwamba Mungu atawaleta pamoja na Yesu wale wote waliofariki wakiwa wanamwamini.
15我们现在照着主的话告诉你们:我们这些活着存留到主再来的人,绝不能在那些睡了的人以先。
15Hili tunalowaambieni ni fundisho la Bwana; sisi tulio hai, ambao tutakuwa tumebaki, wakati Bwana atakapokuja, hakika hatutawatangulia wale waliokwisha fariki dunia.
16因为主必亲自从天降临,那时,有发令的声音,有天使长的呼声,还有 神的号声,那些在基督里死了的人必先复活;
16Maana patatolewa amri, sauti ya malaika mkuu, sauti ya tarumbeta ya Mungu, naye Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni. Ndipo wale waliokufa wakiwa wanamwamini Kristo watafufuliwa kwanza.
17然后,我们还活着存留的人,必和他们一同被提到云里,在空中与主相会。这样,我们就要和主常常同在。
17Kisha sisi tulio hai wakati huo tutakusanywa pamoja nao katika mawingu kumlaki Bwana hewani. Na hivyo tutakuwa daima pamoja na Bwana.
18所以,你们应该用这些话彼此劝慰。
18Basi, farijianeni kwa maneno haya.