聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

1 Thessalonians

5

1警醒谨慎等候主再来
1Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
2因为你们自己清楚知道,主的日子来到,就像夜间的贼来到一样。
2Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
3人正在说平安稳妥的时候,毁灭性的灾祸就突然临到他们,好像生产的痛苦临到怀胎的妇人一样,他们绝不能逃脱。
3Watu watakapokuwa wanasema: "Kila kitu ni shwari na salama" ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
4但是弟兄们,你们不在黑暗里,以致那日子会临到你们像贼来到一样。
4Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
5你们都是光明之子、白昼之子;我们不是属于黑夜的,也不是属于黑暗的。
5Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
6所以,我们不要沉睡像别人一样,总要警醒谨慎。
6Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
7因为睡觉的人是在晚上睡,醉酒的人是在晚上醉;
7Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
8但我们既然属于白昼,就应当谨慎,披上信和爱的胸甲,戴上救恩的盼望作头盔。
8Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
9因为 神不是定意要我们受刑罚(“刑罚”原文作“忿怒”),而是要我们借着我们的主耶稣基督得着救恩。
9Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
10基督替我们死,使我们无论是醒着或睡着,都和他一同活着。
10ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
11所以,你们应该彼此劝慰,互相造就,正如你们一向所行的。
11Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
12训勉和祝福弟兄们,我们求你们要敬重那些在你们中间劳苦的人,就是在主里面治理你们、劝戒你们的人。
12Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
13又因为他们的工作,你们要用爱心格外尊重他们。你们应当彼此和睦。
13Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
14弟兄们,我们劝你们,要警戒游手好闲的人,勉励灰心丧志的人,扶助软弱无力的人,也要容忍所有的人。
14Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
15你们要注意,不管是谁都不要以恶报恶,却要在彼此相处和对待众人这方面,常常追求良善。
15Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
16要常常喜乐,
16Furahini daima,
17不住祷告,
17salini kila wakati
18凡事谢恩;这就是 神在基督耶稣里给你们的旨意。
18na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
19不要熄灭圣灵的感动。
19Msimpinge Roho Mtakatifu;
20不要藐视先知的话语。
20msidharau unabii.
21凡事都要察验,好的要持守,
21Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
22各样的恶事要远离。
22na epukeni kila aina ya uovu.
23愿赐平安的 神亲自使你们完全成圣,又愿你们整个人:灵、魂和身体都得蒙保守,在我们的主耶稣基督再来的时候,无可指摘。
23Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu--roho, mioyo na miili yenu--mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
24那呼召你们的是信实的,他必成就这事。
24Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
25弟兄们,请为我们祷告。
25Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
26要用圣洁的亲嘴问候众弟兄。
26Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
27我凭着主吩咐你们,要把这封信读给众弟兄听。
27Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
28愿我们主耶稣基督的恩惠与你们同在。
28Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.