1问安
1Mimi Paulo, mtume wa Yesu Kristo kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na Yesu Kristo tumaini letu,
2写信给因信主而作我真儿子的提摩太。愿恩惠、怜悯、平安从父 神和我们的主基督耶稣临到你。
2nakuandikia Timotheo mwanangu halisi katika imani. Nakutakia neema, huruma na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Kristo Yesu Bwana wetu.
3提防别的教义我往马其顿去的时候,曾经劝你留在以弗所,为要嘱咐某些人,不可传别的教义,
3Napenda ukae huko Efeso, kama nilivyokuomba nilipokuwa ninakwenda Makedonia. Wako watu fulani huko wanaofundisha mafundisho ya uongo. Wakomeshe watu hao.
4也不可沉迷于无稽之谈和无穷的家谱;这些事只能引起争论,对于 神在信仰上所定的计划是毫无帮助的。
4Waambie waachane na zile hadithi tupu na orodha ndefu za mababu, ambazo huleta tu ubishi, wala haviwajengi watu katika mpango ujulikanao kwa imani.
5这嘱咐的目的是出于爱;这爱是发自纯洁的心、无愧的良心和无伪的信心。
5Shabaha ya amri hii ni kuhimiza mapendo yatokayo katika moyo safi, dhamiri njema, na imani ya kweli.
6有些人偏离了这些,就转向无意义的辩论,
6Watu wengine wamepotoka na kugeukia majadiliano yasiyo na maana.
7想要作律法教师,却不明白自己讲的是什么,主张的又是什么。
7Wanapenda kuwa walimu wa Sheria, lakini hawaelewi maneno yao wenyewe au mambo wanayosisitiza.
8我们知道律法是好的,只要应用得恰当。
8Twajua kwamba Sheria ni njema, kama ikitumiwa ipasavyo.
9要知道律法本来不是为义人设立的,而是为那些无法无天和放荡不羁的、不敬虔和犯罪的、不圣洁和世俗的、弒父母和杀人的、
9Lakini tunapaswa kukumbuka kwamba sheria haziwekwi kwa ajili ya watu wema, bali kwa ajili ya wahalifu na wasiotii, wasiomcha Mungu na wenye dhambi, watu wasio na dini na wa kidunia. Watu wanaowaua baba na mama zao, au wauaji wowote wale;
10淫乱的、亲男色的、拐带人口的、说谎话的、发假誓的,以及为其他抵挡纯正教训的人设立的。
10sheria imewekwa kwa ajili ya waasherati, wafiraji, wanaowaiba watu, waongo, na wanaoapa uongo au wanaofanya chochote ambacho ni kinyume cha mafundisho ya kweli.
11这是照着可称颂的、荣耀的 神所交托我的福音说的。
11Mafundisho hayo hupatikana katika Habari Njema ambayo mimi nimekabidhiwa niihubiri, Habari Njema ya Mungu mtukufu na mwenye heri.
12基督耶稣降世为要拯救罪人我感谢那赐我能力的、我们的主基督耶稣,因为他认为我有忠心,派我服事他。
12Namshukuru Bwana wetu Yesu Kristo aliyenipa nguvu kwa ajili ya kazi yangu. Namshukuru kwa kuniona mimi kuwa ni mwaminifu, akaniteua nimtumikie,
13我从前是亵渎 神的、迫害人的、凌辱人的,然而我还蒙了怜悯,因为我是在不信的时候,由于无知而作的。
13ingawa pale awali mimi nilimtukana na kumtesa na kumdhulumu. Lakini Mungu alinionea huruma, kwa sababu sikuwa na imani bado, na hivyo sikujua nilichokuwa ninafanya.
14我们主的恩典,随着在基督耶稣里的信心和爱心,在我身上越发增加。
14Lakini Bwana wetu alinijalia neema yake kwa wingi, akanipa imani na upendo katika kuungana na Kristo Yesu.
15“基督耶稣降世,为要拯救罪人。”这话是可信的,是值得完全接纳的。在罪人中我是个罪魁。
15Usemi huu ni wa kuaminika, na tena unafaa kukubaliwa kabisa: Kristo Yesu alikuja ulimwenguni kuwaokoa wenye dhambi. Nami ni mkosefu zaidi kuliko hao wote,
16可是,我竟然蒙了怜悯,好让基督耶稣在我这个罪魁身上,显明他完全的忍耐,给后来信他得永生的人作榜样。
16lakini Mungu alinionea huruma, ili Kristo aonyeshe uvumilivu wake wote kwangu mimi, kama mfano kwa wale wote ambao baadaye watamwamini na kupokea uzima wa milele.
17但愿尊贵荣耀归给万世的君王,就是那不朽坏、人不能见、独一的 神,直到永永远远。阿们。
17Kwake yeye aliye Mfalme wa milele na asiyekufa, yeye aliye Mungu pekee--kwake viwe heshima na utukufu milele na milele! Amina.
18我儿提摩太啊!我照着从前关于你的预言,把这命令交托你,为的是要叫你借着这些预言打那美好的仗。
18Mwanangu Timotheo, nakukabidhi amri hii kufuatana na maneno ya unabii yaliyosemwa zamani juu yako. Yatumie maneno hayo yawe silaha yako katika kupigana vita vizuri,
19常常存着信心和无愧的良心。有些人丢弃良心,就在信仰上失落了。
19na ushike imani yako na dhamiri njema. Watu wengine hawakusikiliza dhamiri zao na hivyo wakaiharibu imani yao.
20他们当中有许米乃和亚历山大,我已经把他们交给撒但,使他们受管教不再亵渎。
20Miongoni mwao ni Humenayo na Aleksanda ambao nimewakabidhi kwa Shetani, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.