聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

2 Thessalonians

3

1祈求主的道快快传开
1Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili ujumbe wa Bwana uzidi kuenea upesi na kupokelewa kwa heshima kama vile ulivyo kati yenu.
2也使我们能够脱离那些不讲理的恶人,因为不是人人都有信心。
2Ombeni pia ili Mungu atuokoe na watu wapotovu na waovu, maana si wote wanaoamini ujumbe huu.
3主是信实的,他必坚定你们,保护你们脱离那恶者。
3Lakini Bwana ni mwaminifu. Yeye atawaimarisheni na kuwalinda salama na yule Mwovu.
4我们靠着主深深相信,你们现在以及将来都会遵行我们所吩咐的,
4Naye Bwana anatupatia tumaini kubwa juu yenu, na hatuna shaka kwamba mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaambieni.
5愿主引导你们的心,使你们有 神的爱和基督的坚忍。
5Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.
6不可游手好闲弟兄们,我们奉主耶稣基督的名吩咐你们,凡是游手好闲的弟兄,不按着你们从我们所领受的教训去行,就应当远离他。
6Ndugu, tunawaamuru kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, mjiepushe na ndugu wote walio wavivu na ambao hawafuati maagizo tuliyowapa.
7你们自己本来就知道应当怎样效法我们,因为我们在你们中间并没有游手好闲,
7Ninyi wenyewe mnajua kwamba mnapaswa kufuata mfano wetu. Sisi tulipokuwa nanyi hatukuwa wavivu;
8也没有白吃过谁的饭,反而辛苦劳碌,昼夜作工,免得加重你们任何一人的负担。
8hatukula chakula kwa mtu yeyote bila ya kumlipa. Tulifanya kazi kwa bidii na taabu mchana na usiku ili tusiwe mzigo kwa mtu yeyote kati yenu.
9这不是因为我们没有权利,而是要给你们作榜样,好让你们效法我们。
9Tulifanya hivyo si kwa kuwa hatuna haki ya kutaka msaada wenu, ila kwa sababu tunataka kuwapeni mfano.
10我们在你们那里的时候,曾经吩咐过你们,如果有人不肯作工,就不可吃饭。
10Tulipokuwa pamoja nanyi tulikuwa tukiwaambieni, "Mtu asiyefanya kazi, asile."
11因为我们听说,你们中间有人游手好闲,什么工也不作,反倒专管闲事。
11Tunasema mambo hayo kwa sababu tumesikia kwamba wako baadhi yenu ambao ni wavivu na ambao hawafanyi chochote, isipokuwa tu kujiingiza katika mambo ya watu wengine.
12我们靠着主耶稣基督,吩咐劝戒这样的人,要安静作工,自食其力。
12Kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo tunawaamuru na kuwaonya watu hao wawe na nidhamu na kufanya kazi ili wajipatie maslahi yao wenyewe.
13弟兄们,你们行善不可灰心。
13Lakini ninyi ndugu, msichoke kutenda mema.
14如果有人不听从我们这封信上的训勉,要把这个人记下来,不可和他来往,好叫他自己觉得惭愧。
14Huenda kwamba huko kuna mtu ambaye hatautii huu ujumbe tunaowapelekeeni katika barua hii. Ikiwa hivyo, basi, mfichueni mtu huyo na msiwe na uhusiano wowote naye kusudi aone aibu.
15但不要把他看作仇敌,却要劝他好像劝弟兄一样。
15Lakini msimtendee mtu huyo kama adui, bali mwonyeni kama ndugu.
16祝福愿赐平安的主亲自随时随地赐平安给你们。愿主与你们众人同在。
16Bwana mwenyewe ndiye chanzo cha amani, awajalieni amani siku zote kwa kila namna. Bwana awe nanyi nyote.
17我保罗亲笔问候你们。这是我每一封信的记号;我的笔迹就是这样。
17Kwa mkono wangu mwenyewe naandika hivi: Salamu kutoka kwa Paulo! Hivi ndivyo ninavyotia sahihi kila barua; ndivyo ninavyoandika.
18愿我们主耶稣基督的恩惠与你们众人同在。
18Tunawatakieni nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.