1不法的人必要显露
1Sasa yahusu kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo na kukusanywa kwetu pamoja tukae naye. Ndugu, tunawaombeni sana
2无论有灵、有话、有冒我们的名的书信,说主的日子现在到了,你们都不要轻易动心,也不要惊慌。
2msifadhaike upesi moyoni, na wala msitiwe wasiwasi kwa sababu ya madai kwamba Siku ya Bwana imekwisha fika. Labda inadhaniwa kwamba jambo hili limetokana na uaguzi fulani, mahubiri au barua inayosemekana kuwa imetoka kwetu.
3不要让人用任何方法迷惑了你们,因为主的日子来到以前,必定有背道的事,并且那不法的人,就是那沉沦之子,必定显露出来。
3Msikubali kudanganywa na mtu yeyote kwa namna yoyote ile. Maana Siku hiyo haitakuja mpaka kwanza ule Uasi Mkuu utokee na yule Mwovu aonekane ambaye mwisho wake ni kuangamizwa kabisa.
4他抵挡 神,抬举自己,高过一切称为神和受人敬拜的,甚至坐在 神的殿中,自称为 神。
4Yeye atapinga kila kitu wanachokiona watu kuwa ni mungu, au wanachokiabudu. Naam, hata ataingia na kuketi ndani ya Hekalu la Mungu akijidai kuwa Mungu.
5我还在你们那里的时候,曾经把这些事告诉你们,你们不记得吗?
5Je, hamkumbuki kwamba niliwaambieni haya yote wakati nilipokuwa pamoja nanyi?
6现在你们也知道,那箝制他,使他到了时候才可以显露出来的是什么。
6Lakini kuna kitu kinachomzuia sasa, nanyi mwakijua kitu hicho. Basi, huyo Mwovu ataonekana wakati wake ufaao.
7因为那不法的潜力已经发动,只是现在有一个箝制他的在那里,直等到那箝制解除了,
7Hata hivyo, Mwovu huyo aliyefichika anafanya kazi sasa, lakini hataonekana mpaka yule anayemzuia aondolewe.
8那时,这不法的人必要显露出来。主耶稣要用自己口中的气除掉他,以自己再来所显现的光辉消灭他。
8Hapo ndipo Mwovu atakapotokea; lakini Bwana Yesu anapokuja atamuua kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kwa mng'ao wa kuja kwake.
9这不法的人来到,是照着撒但的行动,行各样的异能奇迹和荒诞的事,
9Huyo Mwovu atakuja na nguvu za Shetani na kufanya kila namna ya miujiza na maajabu ya uongo,
10并且在那些沉沦的人身上,行各样不义的欺诈,因为他们不领受爱真理的心,使他们得救。
10na kutumia udanganyifu wa kila namna kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea. Hao watapotea kwa sababu hawakuupokea na kuupenda ule ukweli ili waokolewe.
11因此, 神就使错谬的思想运行在他们当中,让他们相信虚谎,
11Ndiyo maana Mungu amewaweka chini ya nguvu ya upotovu, wauamini uongo.
12叫所有不信真理倒喜爱不义的人,都被定罪。
12Matokeo yake ni kwamba wote wasioamini ukweli, ila wafurahia dhambi, watahukumiwa.
13站立得稳持守信仰主所爱的弟兄们,我们应该常常为你们感谢 神,因为他从起初就拣选了你们,借着圣灵成圣的工作,和你们对真道的信心,使你们可以得救。
13Tunapaswa kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu ninyi ndugu, ninyi mnaopendwa na Bwana, kwa maana Mungu amewateua tangu mwanzo mpate kuokolewa kwa nguvu ya Roho mfanywe watu wake watakatifu kwa imani yenu katika ukweli.
14因此, 神借着我们所传的福音呼召你们,使你们得着我们主耶稣基督的荣耀。
14Mungu aliwaitieni jambo hili kwa njia ya Habari Njema tuliyowahubirieni; aliwaiteni mpate kupokea sehemu yenu katika utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.
15所以弟兄们,你们要站立得稳;你们所领受的教训,无论是我们口传的,或是信上写的,都要持守。
15Basi, ndugu, simameni imara na zingatieni yale mafundisho tuliyowafundisheni kwa mahubiri yetu na barua zetu.
16愿我们的主耶稣基督自己,和那爱我们、开恩把永远的安慰和美好的盼望赐给我们的父 神,
16Tunamwomba Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu ambaye alitupenda, na kwa neema yake akatujalia faraja ya milele na tumaini jema,
17安慰你们的心,并且在一切善行善言上,坚定你们。
17aifariji mioyo yenu na kuwaimarisheni ili mweze daima kutenda na kusema yaliyo mema.