聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

2 Corinthians

11

1提防诡诈的假使徒
1Laiti mngenivumilia kidogo, hata kama mimi ni mjinga kiasi fulani! Naam, nivumilieni kidogo.
2我以 神的热爱爱你们,因为我把你们献给基督,好像把贞洁的童女许配给一个丈夫。
2Ninawaoneeni wivu lakini ni wivu wa Mungu; maana ninyi ni kama bikira safi niliyemposa kwa mwanamume mmoja tu ambaye ndiye Kristo.
3我只怕你们的心受到引诱,失去对基督的单纯和贞洁,好像蛇用诡计骗了夏娃一样。
3Lakini naogopa kwamba, kama vile yule nyoka kwa hila zake za uongo alimdanganya Hawa, fikira zenu zaweza kupotoshwa, mkauacha uaminifu wenu wa kweli kwa Kristo.
4如果有人来传讲另一位耶稣,不是我们传过的,或者你们接受另一个不同的灵,不是你们领受过的,又或者接受另一个不同的福音,不是你们接受过的,你们倒可以容忍得下!
4Maana mtu yeyote ajaye na kumhubiri Yesu aliye tofauti na yule tuliyemhubiri, ninyi mwampokea kwa mikono miwili; au mnakubali roho au habari njema tofauti kabisa na ile mliyopokea kutoka kwetu!
5但我认为自己没有一点比不上那些“超等使徒”;
5Sidhani kwamba mimi ni mdogo kuliko hao "mitume wakuu."
6虽然我不善于辞令,却是有学问的,我们在各方面,已经向你们清楚显明了。
6Labda sina ufasaha wa lugha, lakini elimu ninayo; jambo hili tumelionyesha wazi kwenu, kila mahali na kila wakati.
7我贬低自己,使你们高升,把 神的福音白白地传给你们,我这样是犯罪吗?
7Mimi niliihubiri kwenu Habari Njema ya Mungu bila kudai mshahara; nilijinyenyekeza ili nipate kuwakweza ninyi. Je, nilifanya vibaya?
8我为了服事你们,就接受了别的教会的供应,也可以说是剥削了他们。
8Nilipofanya kazi kati yenu, mahitaji yangu yaligharimiwa na makanisa mengine. Kwa namna moja au nyingine niliwapokonya wao mali yao nipate kuwatumikia ninyi.
9我在你们那里有缺乏的时候,并没有连累任何人,因为从马其顿来的弟兄们,补足了我的缺乏。我在各方面都不让自己成为你们的重担,将来也是一样。
9Nilipokuwa nanyi sikumsumbua mtu yeyote nilipohitaji fedha; ndugu waliotoka Makedonia waliniletea kila kitu nilichohitaji. Nilikuwa mwangalifu sana nisiwe mzigo kwa namna yoyote ile, na nitaendelea kufanya hivyo.
10我有基督的真理在我里面,在亚该亚一带没有人能阻止我这样夸口。
10Naahidi kwa ule ukweli wa Kristo ulio ndani yangu, kwamba hakuna kitakachoweza kunizuia kujivunia jambo hilo popote katika Akaya.
11为什么呢?是我不爱你们吗? 神是知道的。
11Kwa nini nasema hivyo? Kwa sababu eti siwapendi ninyi? Mungu anajua kwamba nawapenda!
12我现在所作的,将来还要作,为了要断绝那些投机分子的机会,不让他们在所夸的事上,被人认为是跟我们一样的。
12Nitaendelea kufanya kama ninavyofanya sasa, ili nisiwape nafasi wale wanaotafuta nafasi, nafasi ya kujivuna kwamba eti wanafanya kazi kama sisi.
13这样的人是假使徒,是诡诈的工人,装成基督的使徒。
13Maana, hao ni mitume wa uongo, wafanyakazi wadanganyifu wanojisingizia kuwa mitume wa Kristo.
14这并不希奇,因为撒但自己也装作光明的天使,
14Wala si ajabu, maana hata Shetani mwenyewe hujisingizia kuwa malaika wa mwanga!
15所以,撒但的仆役装成公义的仆役,也不必大惊小怪。他们的结局必按他们所作的而定。
15Kwa hiyo si jambo la kushangaza ikiwa na hao watumishi wake wanajisingizia kuwa watumishi wa haki. Mwisho wao watapata kile wanachostahili kufuatana na matendo yao.
16保罗可夸的受苦经历我再说,谁也不要以为我是愚昧的;就算这样,也要接纳我这个愚昧的人,使我可以稍微地夸口。
16Tena nasema: Mtu asinifikirie kuwa mpumbavu. Lakini kama mkifikiri hivyo, basi, nichukueni kama mpumbavu ili nami nipate kuwa na cha kujivunia angaa kidogo.
17我这样满有自信地夸口,不是照着主所吩咐的,而是好像愚昧人在说话。
17Ninachosema sasa si kile alichoniagiza Bwana; kuhusu jambo hili la kujivuna, nasema tu kama mtu mpumbavu.
18既然有许多人按着世俗的标准夸口,我也要夸口。
18Maadam wengi hujivuna kwa sababu za kidunia, nami pia nitajivuna.
19你们那么精明,竟然乐意容忍愚昧的人。
19Ninyi ni wenye busara, ndiyo maana hata mnawavumilia wapumbavu!
20如果有人奴役你们,侵吞、榨取你们,向你们趾高气扬,打你们的脸,你们就容忍吧!
20Mnamvumilia hata mtu anayewafanya ninyi watumwa, mtu mwenye kuwanyonya, mwenye kuwakandamiza, mwenye kuwadharau na kuwapiga usoni!
21说来惭愧,我们太软弱了。说句愚昧的话,如果有人在什么事上是勇敢的,我也是勇敢的。
21Kwa aibu nakubali kwamba sisi tulikuwa dhaifu. Iwe iwavyo, lakini kama kuna mtu yeyote anayethubutu kujivunia kitu--nasema kama mtu mpumbavu--mimi nathubutu pia.
22他们是希伯来人吗?我也是。他们是以色列人吗?我也是。他们是亚伯拉罕的后裔吗?我也是。
22Je, wao ni Waebrania? Hata mimi. Je, wao ni Waisraeli? Hata mimi. Wao ni wazawa wa Abrahamu? Hata mimi.
23他们是基督的仆人吗?说句狂话,我更是。我受更多的劳苦,更多的坐监,受了过量的鞭打,常常有生命的危险。
23Wao ni watumishi wa Kristo? Hata mimi--nanena hayo kiwazimu--ni mtumishi wa Kristo zaidi kuliko wao. Mimi nimefanya kazi ngumu zaidi, nimekaa gerezani mara nyingi zaidi, nimepigwa mara nyingi zaidi na nimekaribia kifo mara nyingi.
24我被犹太人打过五次,每次四十下减去一下,
24Mara tano nilichapwa vile viboko thelathini na tisa vya Wayahudi.
25被棍打过三次,被石头打过一次,三次遇着船坏,在深海里飘了一昼一夜;
25Nilipigwa viboko mara tatu, nilipigwa mawe mara moja; mara tatu nilivunjikiwa meli baharini, na humo nikakesha usiku kucha na kushinda mchana kutwa.
26多次行远路,遇着江河的危险、强盗的危险、同族的危险、外族的危险、城中的危险、旷野的危险、海上的危险、假弟兄的危险;
26Kila mara safarini nimekabiliwa na hatari za mafuriko ya mito, na hatari za wanyama; hatari kutoka kwa wananchi wenzangu na kutoka kwa watu wa mataifa mengine; hatari za mjini, hatari za porini, hatari za baharini, hatari kutoka kwa ndugu wa uongo
27劳碌辛苦,多次不得睡觉,又饥又渴,多次缺粮,赤身挨冷。
27Nimefanya kazi na kutaabika, nimekesha bila usingizi mara nyingi; nimekuwa na njaa na kiu; mara nyingi nimefunga na kukaa katika baridi bila nguo.
28除了这些外面的事,还有为各教会挂心的事,天天压在我的身上。
28Na, licha ya mengine mengi, kila siku nakabiliwa na shughuli za makanisa yote.
29有谁软弱,我不软弱呢?有谁陷在罪里,我不焦急呢?
29Kama mtu yeyote ni dhaifu, nami pia ni dhaifu; mtu yeyote akikwazwa, nami pia huwa na wasiwasi.
30如果必须夸口,我就夸自己的弱点。
30Ikinilazimu kujivuna, basi, nitajivunia udhaifu wangu.
31主耶稣的父 神是应当永远受称颂的,他知道我没有说谎。
31Mungu na Baba wa Bwana Yesu--jina lake litukuzwe milele--yeye anajua kwamba sisemi uongo.
32在大马士革,亚里达王手下的总督把守着大马士革城,要拘捕我,
32Nilipokuwa Damasko, mkuu wa mkoa, aliyekuwa chini ya mfalme Areta, alikuwa akiulinda mji wa Damasko ili apate kunikamata.
33我就被人放在一个大篮子里,从城墙的窗户缒下来,逃脱了他的手。
33Lakini, ndani ya kapu kubwa, niliteremshwa nje kupitia katika nafasi ukutani, nikachopoka mikononi mwake.