1喜欢夸自己的软弱
1Nitajivuna basi, ingawa haifai! Lakini sasa nitasema juu ya maono na ufunuo alivyonijalia Bwana.
2我认识一个在基督里的人,他十四年前被提到第三层天上去。(是带着身体被提的呢?我不知道,是离开了身体呢?我也不知道,只有 神知道。)
2Namjua mtu mmoja Mkristo, ambaye miaka kumi na minne iliyopita alinyakuliwa mpaka katika mbingu ya tatu. (Sijui kama alikuwa huko kwa mwili au kwa roho; Mungu ajua.)
3我认识这个人,(是带着身体被提,还是在身体以外被提,我都不知道,只有 神知道。)
3Narudia: najua kwamba mtu huyo alinyakuliwa mpaka peponi. (Lakini sijui kama alikuwa huko kwa mwili au kwa roho; Mungu ajua.)
4他被提到乐园里去,听见了难以言喻的话,那是人不可以说的。
4Huko akasikia mambo ya siri ambayo binadamu hastahili kuyatamka.
5为了这个人,我要夸口,但为了我自己,除了我的软弱以外,我没有可夸的。
5Basi, nitajivunia juu ya mtu wa namna hiyo, na si juu yangu mimi binafsi, isipokuwa tu juu ya udhaifu wangu.
6即使我想夸口,也不算愚妄,因为我要说的是真话。但我闭口不提,免得有人把我看得太高,过于他在我身上所见所闻的。
6Kama ningetaka kujivuna singekuwa mpumbavu hata kidogo, maana ningekuwa nasema ukweli mtupu. Lakini sitajivuna; sipendi mtu anifikirie zaidi ya vile anavyoona na kusikia kutoka kwangu.
7又因为我所得的启示太大,恐怕会高抬自己,所以就有一根刺加在我的身上,就是撒但的差役来攻击我,免得我高抬自己。
7Lakini, kusudi mambo haya makuu niliyofunuliwa yasinifanye nilewe majivuno, nilipewa maumivu mwilini kama mwiba, mjumbe wa Shetani mwenye kunipiga nisijivune kupita kiasi.
8为了这事,我曾经三次求主,使这根刺离开我。
8Nilimsihi Bwana mara tatu kuhusu jambo hili ili linitoke.
9他却对我说:“我的恩典是够你用的,因为我的能力在人的软弱上显得完全。”所以,我更喜欢夸自己的软弱,好让基督的能力临到我的身上。
9Lakini akaniambia: "Neema yangu inatosha kwa ajili yako; maana uwezo wangu hukamilishwa zaidi katika udhaifu." Basi, ni radhi kabisa kujivunia udhaifu wangu ili uwezo wake Kristo ukae juu yangu.
10因此,我为基督的缘故,就以软弱、凌辱、艰难、迫害、困苦为喜乐,因为我什么时候软弱,什么时候就刚强了。
10Kwa hiyo nakubali kwa radhi udhaifu, madharau, taabu, udhalimu na mateso, kwa ajili ya Kristo; maana ninapokuwa dhaifu, ndipo ninapokuwa na nguvu.
11表明爱哥林多教会的心我成了愚妄的人,是你们逼成的。其实你们应该称赞我,因为我虽然算不得什么,却没有一点比不上那些“超等使徒”。
11Nimekuwa kama mpumbavu, lakini, ninyi mmenilazimisha kuwa hivyo. Ninyi ndio mngalipaswa kunisifu. Maana, ingawa mimi si kitu, kwa vyovyote, mimi si mdogo zaidi kuliko hao "mitume wakuu."
12我在你们中间,以各种忍耐,用神迹、奇事和大能,作为使徒的凭据。
12Miujiza na maajabu yaonyeshayo wazi kwamba mimi ni mtume yalifanyika miongoni mwenu kwa uvumilivu wote.
13除了我自己没有成为你们的重担以外,你们还有什么比不上别的教会呢?这一点委屈,请原谅我吧!
13Je, mlipungukiwa nini zaidi kuliko makanisa mengine, isipokuwa tu kwamba mimi kwa upande wangu sikuwasumbueni kupata msaada wenu? Samahani kwa kuwakoseeni haki hiyo!
14好了,我打算第三次到你们那里去,这一次也不会成为你们的重担,因为我所要的不是你们的东西,而是你们自己。儿女不需要为父母积财,父母却应该为儿女积财。
14Sasa niko tayari kabisa kuja kwenu mara ya tatu, na sitawasumbua. Maana ninachotafuta si mali zenu, bali ni ninyi wenyewe. Ni kawaida ya wazazi kuwawekea watoto wao akiba, na si watoto kuwawekea wazazi wao.
15至于我,我甘心乐意为你们的灵魂付上一切,鞠躬尽瘁。难道我越爱你们,就越得不到你们的爱吗?
15Mimi ni radhi kabisa kutumia nilicho nacho, na hata kujitolea mimi mwenyewe kabisa, kwa faida ya roho zenu. Je, mtanipenda kidogo ati kwa kuwa mimi nawapenda ninyi mno?
16算了!我没有成为你们的重担,却是个狡猾的人,用诡计牢笼你们。
16Basi, mtakubali kwamba sikuwa mzigo kwenu. Lakini labda mtu mwingine atasema: "Kwa vile Paulo ni mwerevu, amewafanyieni ulaghai."
17我派到你们那里去的人,我借着谁占过你们的便宜?
17Je, mimi niliwanyonyeni kwa njia ya mjumbe yeyote niliyemtuma kwenu?
18我劝提多到你们那里去,又派了那位弟兄一同去。提多占过你们的便宜吗?我们行事,不是同一个心灵吗?不是同样的步伐吗?
18Mimi nilimwita Tito, nikamtuma kwenu na ndugu yetu mwingine. Je, Tito aliwanyonyeni? Je, hamjui kwamba sisi tumekuwa tukiongozwa na roho yuleyule, na mwenendo wetu ni mmoja?
19你们一直以为我们是在向你们申辩吗?我们是在基督里,当着 神面前说话的。亲爱的,一切事都是为了建立你们。
19Labda mnafikiri kwamba mpaka sasa tumekuwa tukijitetea wenyewe mbele yenu! Lakini, tunasema mambo haya mbele ya Mungu, tukiwa tumeungana na Kristo. Mambo hayo, yote, wapenzi wangu, ni kwa ajili ya kuwajenga ninyi.
20我怕我来的时候,见你们不如我所想的,你们见我也不如你们所想的。又怕有纷争、嫉妒、恼怒、自私、毁谤、谗言、狂傲、混乱的事。
20Naogopa, huenda nitakapokuja kwenu nitawakuta katika hali nisiyopenda, nami itanilazimu kuwa katika hali msiyoipenda. Naogopa huenda kukawa na ugomvi, wivu, uhasama, ubishi, masengenyano, kunong'ona, majivuno na fujo kati yenu.
21又怕我再来的时候,我的 神使我在你们面前羞愧;并且我要为许多从前犯罪的人哀痛,因为他们行了污秽、奸淫、邪荡的事,却不肯悔改。
21Naogopa huenda hapo nitakapokuja safari ijayo Mungu wangu atanifanya niaibike mbele yenu, nami nitaomboleza kwa ajili ya wengi wa wale waliotenda dhambi lakini hawakujutia huo uchafu, tamaa zao mbaya na uzinzi waliokuwa wamefanya.