1问安
1Mimi Simoni Petro, mtumishi na mtume wa Yesu Kristo, nawaandikia ninyi ambao, kwa wema wake Mungu wetu, na Mwokozi Yesu Kristo, mmejaliwa imani ileile ya thamani kuu tuliyojaliwa sisi.
2愿恩惠平安,因你们确实认识 神和我们的主耶稣,多多加给你们。
2Nawatakieni neema na amani tele katika kumjua Mungu na Yesu Bwana wetu.
3信徒应当追求长进 神以他神圣的能力,因着我们确实认识那位用自己的荣耀和美善呼召我们的,把一切有关生命和敬虔的事,都赐给了我们。
3Kwa uwezo wake wa kimungu, Mungu ametujalia mambo yote tunayohitaji, ili tuishi maisha ya kumcha Mungu kwa kumjua yeye aliyetuita tuushiriki utukufu na wema wake yeye mwenyewe.
4借着这些,他把又宝贵又极大的应许赐给了我们,好叫你们既然逃脱世上因私欲而来的败坏,就可以分享 神的本性。
4Kwa namna hiyo ametujalia zawadi kuu na za thamani ambazo alituahidia, ili kwa zawadi hizo mpate kuziepa kabisa tamaa mbaya zilizomo duniani, na mpate kuishiriki hali yake ya kimungu.
5正因这缘故,你们要多多努力:有了信心,又要增添美德;有了美德,又要增添知识;
5Kwa sababu hiyo, fanyeni bidii ya kuongeza fadhila katika imani yenu: ongezeni elimu katika fadhila yenu,
6有了知识,又要增添节制;有了节制,又要增添忍耐;有了忍耐,又要增添敬虔;
6kuwa na kiasi katika elimu yenu, uvumilivu katika kuwa na kiasi, uchaji wa Mungu katika uvumilivu wenu,
7有了敬虔,又要增添弟兄的爱;有了弟兄的爱,还要增添神圣的爱。
7udugu katika uchaji wenu, na mapendo katika udugu wenu.
8因为你们有了这几样,并且继续增长,就必叫你们在确实认识我们的主耶稣基督上,不至于闲懒不结果子。
8Mkiwa na sifa hizo zote kwa wingi, zitawawezesheni kuwa watendaji na kupata faida katika kumjua Bwana wetu Yesu Kristo.
9人若没有这几样,就是近视,简直是瞎眼的,忘记他过去的罪已经得了洁净。
9Lakini mtu asiye na sifa hizo ni kipofu, hawezi kuona na amesahau kwamba alikwisha takaswa dhambi zake za zamani.
10所以弟兄们,要更加努力,使你们所蒙的呼召和拣选坚定不移;你们若实行这几样,就决不会跌倒。
10Kwa hiyo basi, ndugu zangu, fanyeni bidii zaidi kuufanya huo wito wenu mlioitiwa na Mungu uwe jambo la kudumu katika maisha yenu; kama mkiishi namna hiyo hamtaanguka kamwe.
11这样,你们就得着充分的装备,可以进入我们的主和救主耶稣基督永远的国。
11Kwa namna hiyo mtafaulu kupewa haki kamili ya kuingia katika Utawala wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.
12因此,你们虽然已经知道这些事,又在你们已有的真道上得到坚固,我还要时常提醒你们。
12Kwa hiyo nitaendelea kuwakumbusheni daima mambo haya, ingawa mmekwisha yafahamu, na mko imara katika ukweli mlioupokea.
13趁着我还在世上(“在世上”原文作“在这帐棚”)的时候,我认为应当提醒你们,使你们常常警醒,
13Nadhani ni jambo jema kwangu, muda wote niishio hapa duniani, kuwapeni moyo na kuwakumbusheni juu ya mambo haya.
14因为我知道我离世(“离世”原文作“离开这帐棚”)的时候快到了,正如我们的主耶稣基督清楚指示我的。
14Najua kwamba karibu nitauweka kando mwili huu wenye kufa, kama Bwana alivyoniambia waziwazi.
15我也要努力,使你们在我去世以后,还时常追念这些事。
15Basi, nitajitahidi kuwapatieni njia ya kuyakumbuka mambo haya kila wakati, baada ya kufariki kwangu.
16信徒和先知都为基督作见证我们从前把我们主耶稣基督的大能和降临的事告诉你们,并不是随从巧妙捏造传奇的故事,我们却是亲眼看见过他威荣的人。
16Wakati tulipowafundisheni juu ya ukuu wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, hatukutegemea hadithi tupu zisizo na msingi. Sisi tuliuona utukufu wake kwa macho yetu wenyewe.
17因为他从父 神得着尊贵荣耀的时候,在极显赫的荣光中,有这样的声音对他说:“这是我的爱子,我所喜悦的。”
17Sisi tulikuwapo wakati alipopewa heshima na kutukuzwa na Mungu Baba, wakati sauti ilipomjia kutoka kwake yeye aliye Utukufu Mkuu, ikisema: "Huyu ni Mwanangu mpenzi, nimependezwa naye."
18这从天上发出来的声音,是我们和他同在圣山上的时候,亲自听见过的。
18Tena, sisi wenyewe tulisikia sauti hiyo kutoka mbinguni wakati tulipokuwa pamoja naye juu ya ule mlima mtakatifu.
19我们还有先知的话,是更确实的。你们要特别注意它,好像注意照在暗处的明灯,直到天将破晓,晨星在你们心里出现的时候。
19Tena, ujumbe wa manabii watuthibitishia jambo hilo; nanyi mwafanya vema kama mkiuzingatia, maana ni kama taa inayoangaza mahali penye giza mpaka Siku ile itakapopambazuka na mwanga wa nyota ya asubuhi utakapong'ara mioyoni mwenu.
20最要紧的,你们应当知道:圣经所有的预言,都不是先知自己的见解,
20Zaidi ya hayo, lakini, kumbukeni kwamba hakuna mtu yeyote awezaye kufafanua mwenyewe unabii ulio katika Maandiko Matakatifu.
21因为预言不是出于人意的,而是人受圣灵的感动,说出从 神而来的话。
21Maana hakuna ujumbe wa kinabii unaotokana na matakwa ya binadamu, bali watu walinena ujumbe wa Mungu wakiongozwa na Roho Mtakatifu.