聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

2 Peter

2

1提防假先知和假教师
1Palitokea manabii wa uongo kati ya watu, na vivyo hivyo walimu wa uongo watatokea kati yenu. Watu hao wataingiza mafundisho maharibifu na kumkana Bwana aliyewakomboa, na kwa njia hiyo watasababisha ghafla maangamizi yao wenyewe.
2许多人会随从他们的淫行,因此真理的道,就因他们的缘故被人毁谤。
2Tena watu wengi watazifuata hizo njia zao mbaya, kwa sababu yao, wengine wataipuuza Njia ya ukweli.
3他们因为有贪心,就用捏造的话,想在你们身上图利;惩罚他们的,自古以来就没有松懈;毁灭他们的,也不会打盹。
3Kwa tamaa yao mbaya watajipatia faida kwa kuwaambieni hadithi za uongo. Lakini kwa muda mrefu sasa Hakimu wao yu tayari, na Mwangamizi wao yu macho!
4 神没有姑息犯罪的天使,反而把他们丢入地狱,囚禁在幽暗的坑里,等候审判。
4Malaika walipotenda dhambi, Mungu hakuwahurumia, bali aliwatupa katika moto wa Jehanamu ambako wamefungwa wakingojea Siku ile ya Hukumu.
5 神也没有姑息上古的世界,反而使洪水临到那不敬虔的世人,只保存了传义道的挪亚一家八口。
5Mungu hakuihurumia dunia ya hapo kale, bali alileta gharika kuu juu ya nchi ile ya watu wasiomcha Mungu; lakini Noa ambaye alihubiri uadilifu, Mungu alimwokoa pamoja na watu wengine saba.
6 神判定了所多玛、蛾摩拉二城的罪,把它们倾覆,烧成灰烬,作为后世不敬虔的人的鉴戒;
6Mungu aliadhibu miji ya Sodoma na Gomora, akaiteketeza kwa moto, akaifanya iwe mfano wa mambo yatakayowapata watu wasiomcha Mungu.
7只救了那因恶人的淫行而常受委屈的义人罗得;
7Alimwokoa Loti, mtu mwema, ambaye alisikitishwa sana na mwenendo mbaya wa watu hao waasi.
8(因为这义人住在他们中间,天天看见和听见他们不法的事,他正直的心就感到伤痛。)
8Loti aliishi miongoni mwa watu hao, na kwa siku nyingi moyo wake ulikuwa katika wasiwasi mkuu aliposikia matendo yao maovu.
9主知道怎样搭救敬虔的人脱离试探,又把不义的人留下来,等候在审判的日子受刑罚,
9Kwa hiyo, basi, Bwana anajua jinsi ya kuwaokoa katika majaribu watu wanaomcha Mungu, na jinsi ya kuwaweka waovu katika adhabu hadi Siku ile ya hukumu,
10尤其是那些随从肉体,生活在污秽的私欲中,和轻蔑当权的,更是这样。他们胆大任性,毫无畏惧地毁谤在尊位的。
10hasa wale wanaofuata tamaa mbaya za mwili na kupuuza mamlaka. Watu hao ni washupavu na wenye majivuno, huvitukana na hawaviheshimu viumbe vitukufu vya juu.
11就是天使,虽有更大的力量与权能,尚且不用毁谤的话在主面前控告他们。
11Lakini malaika, ambao wana uwezo na nguvu zaidi kuliko hao walimu wa uongo, hawawashtaki na kuwatukana hao mbele ya Bwana.
12但这些人,好像没有理性的牲畜,生下来就是给人捉去宰杀的;他们毁谤自己所不知道的事,必在自己的败坏中灭亡。
12Watu hao ambao hutukana chochote kile wasichoelewa, ni sawa na wanyama wasio na akili, ambao huzaliwa na baadaye hukamatwa na kuchinjwa! Wataangamizwa kutokana na uharibifu wao wenyewe,
13他们行不义,就得了不义的工价。他们在白昼纵情作乐,满了污点与瑕疵,和你们一同吃饭的时候,就因自己的诡诈而沾沾自喜。
13na watalipwa mateso kwa mateso ambayo wameyasababisha. Furaha yao ni kufanya, tena mchana kabisa, chochote kinachotosheleza anasa zao za mwili. Hao ni fedheha na aibu tupu kwa jumuiya yenu wakati wanapojiunga nanyi katika karamu zenu, bali wakifurahia njia zao za udanganyifu.
14他们满眼淫色,而且不住地犯罪。他们引诱心志不坚固的人。他们的心习惯了贪婪,是应当受咒诅的族类。
14Macho yao yamejaa uzinzi na uwezo wao wa kutenda dhambi hauna kikomo. Huwaongoza watu walio dhaifu mpaka mitegoni. Mioyo yao imezoea kuwa na tamaa ya mali. Wapo chini ya laana ya Mungu!
15他们离弃正路,走入歧途,跟从了比珥的儿子巴兰的道路。这巴兰贪爱不义的工价,
15Wameiacha njia iliyonyoka, wakapotoka na kuifuata njia aliyofuata Balaamu, mwana wa Beori, ambaye alipendelea kupata faida kwa kufanya udanganyifu,
16他曾经因着自己的过犯受了责备:不能说话的驴,竟用人的声音说出话来,制止了这先知的狂妄。
16akakaripiwa kwa ajili ya uovu wake. Punda ambaye hasemi alinena kwa sauti ya binadamu, akaukomesha wazimu wa huyo nabii.
17这些人是无水的泉源,是暴风催逼的雾气,有漆黑的幽暗为他们存留。
17Watu hao ni kama chemchemi zilizokauka, kama mawingu yanayopeperushwa na tufani; makao yao waliyowekewa ni mahali pa giza kuu.
18因为他们说虚妄夸大的话,用肉体的私欲和邪荡的事,引诱那些刚刚逃脱了错谬生活的人。
18Husema maneno ya majivuno na yasiyo na maana, na kutumia tamaa zao mbaya za kimwili kuwatega wale ambao wamejitenga hivi karibuni na watu waishio katika udanganyifu.
19他们应许给人自由,自己却作了败坏的奴仆;因为人给谁制伏了,就作谁的奴仆。
19Huwaahidi watu wengine eti watakuwa huru, kumbe wao wenyewe ni watumwa wa upotovu--maana mtu ni mtumwa wa chochote kile kinachomtawala.
20如果他们因为认识我们的主、救主耶稣基督,可以脱离世上的污秽,后来又在其中被缠住、受制伏,他们末了的景况,就比先前的更不好了。
20Watu waliokwisha ponyoka katika upotovu wa ulimwengu kwa kupata kumjua Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, kisha wakakubali kunaswa na kutawaliwa tena na upotovu huo, hali yao itakuwa mbaya zaidi kuliko awali.
21既然认识了义路,竟又背弃传给他们的圣诫命,对他们来说,倒不如不认识好得多了。
21Ingalikuwa afadhali kwao kama wasingalijua kamwe njia hiyo ya uadilifu kuliko kujua na kisha kuiacha na kupoteza amri takatifu waliyopokea.
22他们的情形,正像俗语所说的:“狗转过来,又吃自己所吐的;猪洗净了,又到污泥中去打滚。”
22Ipo mithali isemayo: "Mbwa huyarudia matapishi yake mwenyewe," na nyingine isemayo: "Nguruwe aliyekwisha oshwa hugaagaa tena katika matope!" Ndivyo ilivyo kwao sasa.