1忽略伟大的救恩不能逃罪
1Kwa sababu hiyo tunapaswa kuzingatia kwa makini zaidi yote tuliyosikia, ili tusije tukapotoshwa.
2那透过天使所传讲的信息既然是确定的,所有干犯和不听从的,都受了应得的报应。
2Ujumbe ule waliopewa wazee wetu na malaika ulionyeshwa kuwa kweli, hata mtu yeyote ambaye hakuufuata au hakuutii aliadhibiwa kama alivyostahili.
3如果我们忽略了这么大的救恩,怎么能逃罪呢?这救恩起初是由主亲自宣讲的,后来听见的人给我们证实了。
3Basi, sisi tutaokokaje kama hatuujali wokovu mkuu kama huu? Kwanza Bwana mwenyewe aliutangaza wokovu huu, na wale waliomsikia walituthibitishia kwamba ni kweli.
4 神又照着自己的旨意,用神迹、奇事和各样异能,以及圣灵的恩赐,与他们一同作见证。
4Mungu pia aliongeza hapo ushahidi wake kwa kufanya kila namna ya miujiza na maajabu, na kwa kuwagawia watu vipaji vya Roho Mtakatifu kadiri ya mapenzi yake.
5耶稣因受死得了荣耀尊贵 神并没有把我们所说的“将来的世界”,交给天使管辖;
5Mungu hakuwaweka malaika wautawale ulimwengu ujao, yaani ulimwengu ule tunaoongea habari zake.
6但是有人在圣经上某一处证实说:“人算什么,你竟记念他?世人算什么,你竟眷顾他?
6Tena yasemwa mahali fulani katika Maandiko: "Mtu ni nini ee Mungu, hata umfikirie; mwanaadamu ni nini hata umjali?
7你使他比天使稍低微一点,却赐给他荣耀尊贵作冠冕,(有些古卷在此有“并立他统管你手所造的一切”一句)
7Ulimfanya kwa kitambo kidogo kuwa chini zaidi kuliko malaika; ukamvika taji ya utukufu na heshima,
8使万物都服在他的脚下。”既然万有都服了他,就没有剩下一样不服他的了。但是现在我们还没有看见万有都服他。
8ukaweka kila kitu chini ya miguu yake, avitawale." Yasemwa kwamba Mungu alimweka mtu kuwa mtawala wa vitu vyote yaani bila kuacha hata kimoja. Hata hivyo, hatuoni bado mtu akivitawala vitu vyote sasa.
9不过,我们看见那位暂时成了比天使卑微的耶稣,因为受了死的痛苦,就得了荣耀尊贵作冠冕,好叫他因着 神的恩典,为万人尝了死味。
9Lakini twamwona Yesu ambaye alifanywa kwa kitambo kidogo kuwa chini zaidi kuliko malaika, ili kwa neema ya Mungu afe kwa ajili ya watu wote. Sasa tunamwona ametawazwa kwa utukufu na heshima kwa sababu ya kifo alichoteseka.
10救恩的元首耶稣万有因他而有、借他而造的那位,为了要带领许多儿子进入荣耀里去,使救他们的元首借着受苦而得到成全,本是合适的。
10Ilikuwa haki tupu kwamba Mungu, ambaye huumba na kutegemeza vitu vyote, alimfanya Yesu kuwa mkamilifu kabisa kwa njia ya mateso, ili awalete watoto wengi waushiriki utukufu wake. Maana Yesu ndiye anayewaongoza kwenye wokovu.
11因为那位使人成圣的,和那些得到成圣的,同是出于一个源头;所以他称他们为弟兄也不以为耻。
11Yeye anawatakasa watu dhambi zao, naye pamoja na wale waliotakaswa, wote wanaye Baba mmoja. Ndiyo maana Yesu haoni aibu kuwaita hao ndugu zake;
12他说:“我要向我的弟兄宣扬你的名,我要在聚会中歌颂你。”
12kama asemavyo: "Ee Mungu, nitawatangazia ndugu zangu matendo yako. Nitakusifu katika kusanyiko lao."
13又说:“我要信靠他。”又说:“看哪,我和 神所赐给我的孩子们。”
13Tena asema: "Nitamwekea Mungu tumaini langu." Na tena: "Mimi niko hapa pamoja na watoto alionipa Mungu."
14孩子们既然同有血肉之体,他自己也照样成为血肉之体,为要借着死,消灭那掌握死权的魔鬼,
14Basi, kwa vile watoto hao, kama awaitavyo, ni watu wenye mwili na damu, Yesu mwenyewe akawa kama wao na kushiriki ubinadamu wao. Alifanya hivyo ili kwa njia ya kifo chake amwangamize Ibilisi, ambaye ana mamlaka juu ya kifo,
15并且要释放那些因为怕死而终身作奴仆的人。
15na hivyo awaokoe wale waliokuwa watumwa maisha yao yote kwa sababu ya hofu yao ya kifo.
16其实,他并没有救援天使,只救援亚伯拉罕的后裔。
16Maana ni wazi kwamba yeye hakuja kwa ajili ya kuwasaidia malaika, bali kama yasemavyo Maandiko; "Anawasaidia wazawa wa Abrahamu."
17所以,他必须在各方面和他的弟兄们相同,为了要在 神的事上,成为仁慈忠信的大祭司,好为人民赎罪。
17Ndiyo maana ilimbidi awe kama ndugu zake kwa kila namna, ili awe Kuhani Mkuu wao aliye mwaminifu na mwenye huruma katika kumtumikia Mungu, ili dhambi za watu ziondolewe.
18因为他自己既然经过试探,受了苦,就能够帮助那些被试探的人。
18Na, anaweza sasa kuwasaidia wale wanaojaribiwa na kuteswa.