聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

John

3

1人必须重生
1Kulikuwa na kiongozi mmoja Myahudi, wa kikundi cha Mafarisayo, jina lake Nikodemo.
2他夜间来到耶稣那里,对他说:“拉比,我们知道你是从 神那里来的教师,因为如果没有 神同在,你所行的这些神迹,就没有人能行。”
2Siku moja alimwendea Yesu usiku, akamwambia, "Rabi, tunajua kwamba wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, maana hakuna mtu awezaye kufanya ishara unazozifanya Mungu asipokuwa pamoja naye."
3耶稣回答:“我实实在在告诉你,人若不重生,就不能见 神的国。”
3Yesu akamwambia, "Kweli nakwambia, mtu asipozaliwa upya hataweza kuuona ufalme wa Mungu."
4尼哥德慕说:“人老了,怎能重生呢?难道他能再进母腹生出来吗?”
4Nikodemo akamwuliza, "Mtu mzima awezaje kuzaliwa tena? Hawezi kuingia tumboni mwa mama yake na kuzaliwa mara ya pili!"
5耶稣回答:“我实实在在告诉你,人若不是从水和圣灵生的,就不能进 神的国。
5Yesu akamjibu, "Kweli nakwambia, mtu asipozaliwa kwa maji na Roho, hawezi kamwe kuingia katika ufalme wa Mungu.
6从肉身生的就是肉身,从灵生的就是灵。
6Mtu huzaliwa kimwili kwa baba na mama, lakini huzaliwa kiroho kwa Roho.
7你不要因为我对你说‘你们必须重生’而感到希奇。
7Usistaajabu kwamba nimekwambia kuwa ni lazima kuzaliwa upya.
8风随意而吹,你听见它的响声,却不知道它从哪里来,往哪里去;凡从圣灵生的,也是这样。”
8Upepo huvuma kuelekea upendako; waisikia sauti yake, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda. Ndivyo ilivyo kwa mtu aliyezaliwa kwa Roho."
9尼哥德慕说:“怎能有这事呢?”
9Nikodemo akamwuliza, "Mambo haya yanawezekanaje?"
10耶稣说:“你是以色列人的教师,还不明白这事吗?
10Yesu akamjibu, "Je, wewe ni mwalimu katika Israel na huyajui mambo haya?
11我实实在在告诉你,我们知道的,才讲论;见过的,就作证,然而你们却不接受我们的见证。
11Kweli nakwambia, sisi twasema tunayoyajua na kushuhudia tuliyoyaona, lakini ninyi hamkubali ujumbe wetu.
12我对你们讲地上的事,你们尚且不信,如果讲天上的事,怎能相信呢?
12Ikiwa nimewaambieni mambo ya kidunia nanyi hamniamini, mtawezaje kuamini nikiwaambieni mambo ya mbinguni?
13除了那从天上降下来的人子(有些抄本作“除了那从天上降下来仍旧在天上的人子”),没有人升过天。
13Hakuna mtu aliyepata kwenda juu mbinguni isipokuwa Mwana wa Mtu ambaye ameshuka kutoka mbinguni.
14摩西在旷野怎样把铜蛇举起,人子也必照样被举起来,
14"Kama vile Mose alivyomwinua juu nyoka wa shaba kule jangwani, naye Mwana wa Mtu atainuliwa juu vivyo hivyo,
15使所有信他的人都得永生。
15ili kila anayemwamini awe na uzima wa milele.
16“ 神爱世人,甚至把他的独生子赐给他们,叫一切信他的,不至灭亡,反得永生。
16Maana Mungu aliupenda ulimwengu hivi hata akamtoa Mwana wake wa pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
17因为 神差他的儿子到世上来,不是要定世人的罪,而是要使世人借着他得救。
17Maana Mungu hakumtuma Mwanae ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali aukomboe ulimwengu.
18信他的,不被定罪;不信的,罪已经定了,因为他不信 神独生子的名。
18"Anayemwamini Mwana hahukumiwi; asiyemwamini amekwisha hukumiwa kwa sababu hakumwamini Mwana wa pekee wa Mungu.
19光来到世上,世人因为自己的行为邪恶,不爱光倒爱黑暗,定他们罪的原因,就在这里。
19Na hukumu yenyewe ndiyo hii: Mwanga umekuja ulimwenguni lakini watu wakapenda giza kuliko mwanga, kwani matendo yao ni maovu.
20凡作恶的都恨光,不来接近光,免得他的恶行暴露出来。
20Kila mtu atendaye maovu anauchukia mwanga, wala haji kwenye mwanga, maana hapendi matendo yake maovu yamulikwe.
21凡行真理的,就来接近光,好显明他所作的都是靠着 神而作的。”
21Lakini mwenye kuuzingatia ukweli huja kwenye mwanga, ili matendo yake yaonekane yametendwa kwa kumtii Mungu."
22他必兴旺,我必衰微这事以后,耶稣和门徒来到犹太地,他和他们住在那里,并且施洗。
22Baada ya hayo, Yesu alifika mkoani Yudea pamoja na wanafunzi wake. Alikaa huko pamoja nao kwa muda, akibatiza watu.
23约翰也在靠近撒冷的艾嫩施洗,因为那里水多;众人都去受洗。
23Yohane pia alikuwa akibatiza watu huko Ainoni, karibu na Salemu, maana huko kulikuwa na maji mengi. Watu walimwendea, naye akawabatiza.
24那时约翰还没有入狱。
24(Wakati huo Yohane alikuwa bado hajafungwa gerezani.)
25约翰的门徒和一个犹太人为洁净礼发生辩论。
25Ubishi ulitokea kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yohane na Myahudi mmoja kuhusu desturi za kutawadha.
26他们来到约翰那里,对他说:“拉比,你看,从前和你在约旦河东,你为他作见证的那一位,他也在施洗,众人都到他那里去了。”
26Basi, wanafunzi hao wakamwendea Yohane na kumwambia, "Mwalimu, yule mtu aliyekuwa pamoja nawe ng'ambo ya Yordani na ambaye wewe ulimshuhudia, sasa naye anabatiza, na watu wote wanamwendea."
27约翰回答:“除了从天上赐下来给他的,人就不能得到什么。
27Yohane akawaambia, "Mtu hawezi kuwa na kitu asipopewa na Mungu.
28你们自己可以为我作证:我曾说,我不是基督,不过是奉差遣作他的先锋的。
28Nanyi wenyewe mwaweza kushuhudia kuwa nilisema: Mimi siye Kristo, lakini nimetumwa ili nimtangulie!
29娶新娘的是新郎。新郎的好友站在那里听着,听见新郎的声音就非常喜乐。因此,我这喜乐满溢了!
29Bibiarusi ni wake bwanaarusi, lakini rafiki yake bwana arusi, anayesimama na kusikiliza, hufurahi sana anapomsikia bwana arusi akisema. Ndivyo furaha yangu ilivyokamilishwa.
30他必兴旺,我必衰微。
30Ni lazima yeye azidi kuwa maarufu, na mimi nipungue.
31从天上来的“那从天上来的,是在万有之上;从地上来的,是属于地,所讲的也是属于地。那从天上来的,是超越万有之上。
31"Anayekuja kutoka juu ni mkuu kuliko wote; atokaye duniani ni wa dunia, na huongea mambo ya kidunia. Lakini anayekuja kutoka mbinguni ni mkuu kuliko wote.
32他把所见所闻的见证出来,可是没有人接受他的见证。
32Yeye husema yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna mtu anayekubali ujumbe wake.
33那接受他的见证的,就确认 神是真的。
33Lakini mtu yeyote anayekubali ujumbe wake anathibitisha kwamba Mungu ni kweli.
34 神所差来的那一位讲 神的话,因为 神把圣灵无限地赐给他。
34Yule aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, maana Mungu humjalia mtu huyo Roho wake bila kipimo.
35父爱子,已经把万有交在他手里。
35Baba anampenda Mwana na amemkabidhi vitu vyote.
36信子的,有永生;不信从子的,必不得见永生, 神的震怒却常在他身上。”
36Anayemwamini Mwana anao uzima wa milele; asiyemtii Mwana hatakuwa na uzima wa milele, bali ghadhabu ya Mungu hubaki juu yake."