1差遣七十二人
1Baada ya hayo, Bwana aliwachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawiliwawili, wamtangulie katika kila kijiji na mahali ambapo yeye mwenyewe alitaka kwenda.
2耶稣对他们说:“庄稼多,工人少,所以你们应当求庄稼的主,派工人出去收他的庄稼。
2Akawaambia, "Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache. Kwa hivyo, mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake.
3你们去吧!我差你们去,如同羊羔进入狼群。
3Sasa nendeni; fahamuni kwamba ninawatuma ninyi kama kondoo wanaokwenda kati ya mbwa mwitu.
4不要带钱囊,不要带口袋,不要带鞋,不要在路上问候人。
4Msichukue mfuko wa fedha, mkoba, wala viatu; msimsalimu mtu yeyote njiani.
5无论进哪一家,先说:‘愿平安归与这家!’
5Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza wasalimuni hivi: Amani iwe katika nyumba hii!
6那里若有配得平安的人(“配得平安的人”原文作“平安之子”),你们的平安就必临到他,不然,就归给你们。
6Kama akiwako mwenye kupenda amani, amani yenu itakaa naye, la sivyo, itawarudieni.
7你们要住在那家,吃喝他们所供给的,因为作工的理当得工资;不必从这家搬到那家。
7Kaeni katika nyumba hiyo mkila na kunywa wanavyowapeni, maana mfanyakazi anastahili mshahara wake. Msiende mara nyumba hii mara nyumba ile.
8无论进哪一城,人若接待你们,摆上什么,就吃什么。
8Kama mkifika mji fulani na watu wakiwakaribisha, kuleni wanavyowapeni.
9要医治城中的病人,对他们宣讲:‘ 神的国临近你们了。’
9Ponyeni wagonjwa walioko huko, waambieni watu: Ufalme wa Mungu umekaribia kwenu.
10无论进哪一城,人若不接待你们,你们就出来到街上,说:
10Lakini mkiingia katika mji wowote, wasipowakaribisheni, tokeni; nanyi mpitapo katika barabara zao semeni:
11‘连你们城里那粘在我们脚上的尘土,我们也要当着你们擦去。虽然这样,你们应该知道: 神的国临近了!’
11Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu tunawakung'utieni. Lakini, jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
12我告诉你们,当那日,所多玛所受的,比那城所受的还轻呢。
12Hakika nawaambieni, siku ile mji huo utapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Sodoma.
13责备不肯悔改的城(太11:21-23)“哥拉逊啊,你有祸了!伯赛大啊,你有祸了!因为在你们那里行过的神迹,如果行在推罗和西顿,他们早已披麻蒙灰,坐在地上悔改了。
13"Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Maana, kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika kule Tiro na Sidoni, watu wake wangalikwishavaa mavazi ya gunia kitambo, na kukaa katika majivu kuonyesha kwamba wametubu.
14在审判的时候,推罗和西顿所受的,比你们所受的还轻呢。
14Hata hivyo, Siku ya Hukumu ninyi mtapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Tiro na Sidoni.
15还有你,迦百农啊!你会被高举到天上吗?你必降到阴间。
15Na wewe Kafarnaumu, unataka kujikweza mpaka mbinguni? La; utaporomoshwa mpaka Kuzimu."
16听从你们的,就是听从我;弃绝你们的,就是弃绝我;弃绝我的,就是弃绝那差我来的。”
16Halafu akasema, "Anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; na anayekataa kuwapokea ninyi, anakataa kunipokea mimi. Yeyote anayekataa kunipokea, anakataa kumpokea yule aliyenituma."
17七十二人回来那七十二个人欢欢喜喜地回来,说:“主啊,因你的名,连鬼也服了我们。”
17Baadaye, wale sabini na wawili walirudi wamejaa furaha, wakisema, "Bwana, hata pepo wametutii tulipolitaja jina lako."
18耶稣说:“我看见撒但,像闪电一样从天坠落。
18Yeye akawaambia, "Nilimwona Shetani jinsi alivyokuwa anaporomoka kama umeme kutoka mbinguni.
19我已经给你们权柄,去践踏蛇和蝎子,胜过仇敌的一切能力。绝对没有什么能伤害你们了。
19Naam, nimewapeni uwezo wa kukanyaga nyoka na ng'e, na uwezo juu ya nguvu zote za yule adui; hakuna chochote kitakachowadhuru.
20然而不要因为鬼服了你们就欢喜,却要因为你们的名字记录在天上而欢喜。”
20Hata hivyo, msifurahi kwa sababu pepo wamewatii, bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni."
21耶稣欢乐赞美天父(太11:25-27,13:16-17)就在这时候,耶稣因圣灵而欢乐,说:“父啊,天地的主,我赞美你,因为你把这些事向智慧和聪明的人隐藏起来,却向婴孩显明。父啊,是的,这就是你的美意。
21Saa ileile, Yesu akafurahi kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akasema, "Nakushukuru ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa kuwa umewaficha wenye hekima na elimu mambo haya, ukawafumbulia wadogo. Naam, Baba, ndivyo ilivyokupendeza."
22我父已经把一切交给我;除了父没有人知道子是谁,除了子和子所愿意启示的人,也没有人知道父是谁。”
22Kisha akasema, "Baba yangu ameweka yote mikononi mwangu. Hakuna amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala amjuaye Baba ni nani ila Mwana, na yeyote yule ambaye Mwana anataka kumfunulia hayo."
23耶稣转过身来,悄悄地对门徒说:“看见你们所看见的,那眼睛有福了!
23Halafu akawaelekea wafuasi wake akawaambia, "Heri wanaoona yale mnayoyaona ninyi!
24我告诉你们,曾经有许多先知和君王,想看你们所看见的,却没有看到;想听你们所听见的,却没有听到。”
24Hakika, manabii na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona ninyi wasiyaone, na kusikia yale mnayoyasikia wasiyasikie."
25好撒玛利亚人的比喻(太22:34-40;可12:28-31)有一个律法师起来试探耶稣,说:“老师,我应该作什么,才可以承受永生呢?”
25Baadaye mwalimu mmoja wa Sheria alisimama akamwuliza akitaka kumtega, "Mwalimu, nifanye nini ili nipate uzima wa milele?"
26耶稣对他说:“律法上写的是什么?你怎么念的呢?”
26Yesu akamwuliza, "Imeandikwa nini katika Sheria? Unaelewaje?"
27他回答:“你要全心、全性、全力、全意爱主你的 神,并且要爱邻舍如同自己。”
27Akamjibu, "Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote. Na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe."
28耶稣说:“你答得对,你这样行,就必得生命。”
28Yesu akawaambia, "Vema! Fanya hivyo, nawe utaishi."
29那人想证明自己有理,就对耶稣说:“谁是我的邻舍呢?”
29Lakini yeye akitaka kujihakikishia kuwa mwema akamwuliza Yesu, "Na jirani yangu ni nani?"
30耶稣回答:“有一个人从耶路撒冷下耶利哥去,落在强盗手中。他们剥去他的衣服,把他打得半死,撇下他一个人就走了。
30Yesu akamjibu, "Mtu mmoja alikuwa anashuka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko. Alipokuwa njiani, alivamiwa na majambazi, wakamnyang'anya mali yake na kumpiga, wakamwacha amelala pale nusu mfu.
31正好有一个祭司,从那条路下来,看见他,就从旁边走过去了。
31Kumbe, kuhani mmoja akawa anapita barabara ileile, akamwona, akapita kando.
32又有一个利未人,来到那里,看见他,也照样从旁边走过去了。
32Hali kadhalika na Mlawi mmoja, alipofika mahali akamwona, akapita kando.
33只有一个撒玛利亚人,旅行来到他那里,看见了,就动了怜悯的心,
33Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa anasafiri, alifika pale yule mtu alipokuwa, naye alipomwona, alimwonea huruma.
34上前用油和酒倒在他的伤处,包裹好了,把他扶上自己的牲口,带他到客店里照顾他。
34Akamwendea, akamtibu majeraha yake kwa kumtia mafuta na divai; na kuyafunga halafu akampandisha juu ya punda wake akampeleka katika nyumba moja ya wageni akamuuguza.
35第二天,他拿出两个银币交给店主,说:‘请你照顾他,额外的开支,我回来的时候必还给你。’
35Kesho yake akatoa fedha dinari mbili akampa yule mwenye nyumba, akamwambia, Muuguze mtu huyu; na chochote utakachotumia zaidi, nitakulipa nitakaporudi."
36你想,这三个人,谁是那个落在强盗手中的人的邻舍呢?”
36Kisha Yesu akauliza, "Kati ya hao watatu, ni yupi aliyeonyesha kuwa jirani yake yule aliyevamiwa na majambazi?"
37他说:“是那怜悯他的。”耶稣说:“你去,照样作吧。”
37Yule mwalimu wa Sheria akamjibu, "Ni yule aliyemwonea huruma." Yesu akamwambia, "Nenda ukafanye vivyo hivyo."
38马大和马利亚他们走路的时候,耶稣进了一个村庄。有一个名叫马大的女人,接他到家里。
38Walipokuwa safarini, waliingia katika kijiji kimoja na mwanamke mmoja, aitwaye Martha, alimkaribisha nyumbani kwake.
39她有一个妹妹,名叫马利亚,坐在主的脚前听道。
39Martha alikuwa na dada yake aitwaye Maria; huyu aliketi karibu na Yesu akisikiliza mafundisho yake.
40马大被许多要作的事,弄得心烦意乱,就上前来,说:“主啊,我妹妹让我一个人侍候,你不理吗?请吩咐她来帮助我。”
40Lakini Martha alikuwa anashughulika na mambo mengi. Basi, akamwendea Yesu, akamwambia, "Bwana, hivi hujali kwamba dada yangu ameniacha nishughulike peke yangu? Mwambie basi, anisaidie."
41主回答她:“马大,马大,你为许多事操心忙碌,
41Lakini Bwana akamjibu, "Martha, Martha, unahangaika na kusumbuka kwa mambo mengi.
42但是最需要的只有一件,马利亚已经选择了那上好的分,是不能从她夺去的。”
42Kitu kimoja tu ni muhimu. Maria amechagua kitu bora zaidi ambacho hakuna mtu atakayemnyag'anya."