1差遣十二使徒(太10:5-15;可6:7-13)
1Yesu aliwaita wale kumi na wawili, akawapa uwezo juu ya pepo wote, na uwezo wa kuponya wagonjwa.
2差遣他们去宣讲 神的国和医治病人,
2Halafu akawatuma waende kuhubiri Ufalme wa Mungu na kuponya wagonjwa.
3对他们说:“不要带着什么上路,不要带手杖,不要带口袋,不要带食物,不要带银钱,也不要带两件衣服。
3Akawaambia, "Mnaposafiri msichukue chochote: msichukue fimbo, wala mkoba, wala chakula, wala fedha, wala hata koti la ziada.
4无论进哪一家,就住在那里,直到离开。
4Nyumba yoyote mtakayoingia na kukaribishwa, kaeni humo mpaka mtakapoondoka katika kijiji hicho.
5凡不接待你们的,你们离开那城的时候,当把脚上的灰尘跺下去,作为反对他们的表示。”
5Watu wakikataa kuwakaribisha, tokeni katika mji huo, nanyi mnapotoka kung'uteni mavumbi miguuni mwenu kama onyo kwao."
6于是他们就出去,走遍各乡,传讲福音,到处医治病人。
6Basi, wakaanza safari, wakapitia vijijini wakihubiri Habari Njema na kuponya wagonjwa kila mahali.
7希律的困惑(太14:1-2;可6:14-16)分封王希律听见所发生的一切事,犹豫不定,因为有人说:“约翰从死人中复活了。”
7Sasa, mtawala Herode, alipata habari za mambo yote yaliyokuwa yanatendeka, akawa na wasiwasi kwa vile walikuwa wakisema: "Yohane amefufuka kutoka wafu!"
8又有人说:“以利亚显现了。”还有人说:“古时的一位先知复活了。”
8Wengine walisema kwamba Eliya ametokea, na wengine walisema kwamba mmojawapo wa manabii wa kale amerudi duniani.
9希律说:“约翰已经斩头了,但这是谁,我怎么会听到他这些事呢?”就设法要见他。
9Lakini Herode akasema, "Huyo Yohane nilimkata kichwa; sasa ni nani huyu ninayesikia habari zake?" Akawa na hamu ya kumwona.
10给五千人吃饱的神迹(太14:13-21;可6:30-44;约6:1-13)使徒们回来,把所作的事报告耶稣。他带着他们,悄悄地退往伯赛大城去。
10Wale mitume waliporudi, walimweleza yote waliyoyafanya. Yesu akawachukua, wakaenda peke yao mjini Bethsaida.
11群众知道了,也跟了去。他接待他们,向他们讲论 神的国,医好需要医治的人。
11Lakini wale watu walipojua alikokwenda, walimfuata. Yesu akawakaribisha akawazungumzia juu ya Ufalme wa Mungu, akawaponya wale waliohitaji kuponywa.
12天将晚的时候,十二门徒来到他跟前,说:“请解散众人,好让他们往周围的田舍村庄,去找地方住,找东西吃,因为我们这里是旷野。”
12Jua lilipokuwa linaanza kutua, wale kumi na wawili walimwendea wakamwambia, "Waage watu waende kwenye vijiji na mashamba ya karibu, wakajipatie chakula na mahali pa kulala, kwa maana hapa tulipo ni nyikani."
13他说:“你们给他们吃吧!”他们说:“我们所有的,不过是五个饼两条鱼,除非去为这些人另买食物。”
13Lakini Yesu akawaambia, "Wapeni ninyi chakula." Wakamjibu, "Hatuna chochote ila mikate mitano na samaki wawili. Labda twende wenyewe tukawanunulie chakula watu wote hawa!"
14原来男人就约有五千。他对门徒说:“叫他们一组一组地坐下,每组约五十人。”
14(Walikuwepo pale wanaume wapatao elfu tano.) Basi, Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Waambieni watu waketi katika makundi ya watu hamsinihamsini."
15门徒就照他的话,叫众人坐下。
15Wanafunzi wakafanya walivyoambiwa, wakawaketisha wote.
16耶稣拿起这五个饼,两条鱼,望着天,祝谢了,擘开递给门徒,摆在众人面前。
16Kisha Yesu akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu, akavimega, akawapa wanafunzi wake wawagawie watu.
17他们都吃饱了,把剩下的零碎拾起来,装满了十二个篮子。
17Wakala wote, wakashiba; wakakusanya makombo ya chakula, wakajaza vikapu kumi na viwili.
18彼得承认耶稣是基督(太16:13-19;可8:27-29)有一次耶稣独自祈祷的时候,只有门徒和他在一起。他问他们:“人说我是谁?”
18Siku moja, Yesu alikuwa anasali peke yake, na wanafunzi wake walikuwa karibu. Basi, akawauliza, "Eti watu wanasema mimi ni nani?"
19他们回答:“有人说是施洗的约翰,有人说是以利亚,还有人说是古时的一位先知复活了。”
19Nao wakamjibu, "Wengine wanasema kuwa wewe ni Yohane mbatizaji, wengine wanasema wewe ni Eliya, hali wengine wanasema kuwa wewe ni mmoja wa manabii wa kale ambaye amefufuka."
20他又问他们:“你们说我是谁?”彼得回答:“是 神的基督!”
20Hapo akawauliza, "Na ninyi je, mwasema mimi ni nani?" Petro akajibu, "Wewe ndiwe Kristo wa Mungu."
21耶稣预言受难及复活(太16:20-28;可8:30-9:1)耶稣郑重地嘱咐他们,不要把这事告诉人。
21Halafu Yesu akawaamuru wasimwambie mtu yeyote habari hiyo.
22又说:“人子必须受许多苦,被长老、祭司长,和经学家弃绝、杀害,第三日复活。”
22Akaendelea kusema: "Ni lazima Mwana wa Mtu apate mateso mengi na kukataliwa na wazee na makuhani wakuu na walimu wa Sheria; atauawa, lakini siku ya tatu atafufuliwa."
23耶稣又对众人说:“如果有人愿意跟从我,就当舍己,天天背起他的十字架来跟从我。
23Kisha akawaambia watu wote, "Mtu yeyote akitaka kuwa mfuasi wangu, ni lazima ajikane nafsi yake, auchukue msalaba wake kila siku, anifuate.
24凡是想救自己生命的,必丧掉生命;但为我牺牲自己生命的,必救了生命。
24Maana, mtu anayetaka kuyaokoa maisha yake mwenyewe, atayapoteza; lakini atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu, atayaokoa.
25人若赚得全世界,却丧失自己,或赔上自己,有什么好处呢?
25Je, kuna faida gani mtu kuupata utajiri wote wa dunia kwa kujipoteza au kujiangamiza yeye mwenyewe?
26凡是把我和我的道当作可耻的,人子在他与父并圣天使的荣耀里降临的时候,也必把他当作可耻的。
26Mtu akinionea aibu mimi na mafundisho yangu, Mwana wa Mtu atamwonea aibu mtu huyo wakati atakapokuja katika utukufu wake na wa Baba na wa malaika watakatifu.
27我实在告诉你们,站在这里的,有人在没有尝过死味以前必定要看见 神的国。”
27Nawaambieni kweli, kuna wengine papa hapa ambao hawatakufa kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu."
28在山上改变形象(太17:1-13;可9:2-8)说了这些话以后约有八天,耶稣带着彼得、约翰和雅各,上山去祷告。
28Yapata siku nane baada ya kusema hayo, Yesu aliwachukua Petro, Yohane na Yakobo, akaenda nao mlimani kusali.
29正祷告的时候,他的面貌就改变了,衣服洁白发光。
29Alipokuwa akisali, sura yake ilibadilika, mavazi yake yakawa meupe na kung'aa sana.
30忽然有两个人和他谈话,就是摩西和以利亚。
30Na watu wawili wakaonekana wakizungumza naye, nao ni Mose na Eliya,
31他们在荣光里显现,谈论他去世的事,就是他在耶路撒冷将要完成的。
31ambao walitokea wakiwa wenye utukufu, wakazungumza naye juu ya kifo chake ambacho angekikamilisha huko Yerusalemu.
32彼得和同伴都在打盹。醒过来之后,就看见他的荣光,并与他站在一起的那两个人。
32Petro na wenzake walikuwa wamelemewa na usingizi mzito, hata hivyo waliamka, wakauona utukufu wake, wakawaona na wale watu wawili waliokuwa wamesimama pamoja naye.
33二人正要离开他的时候,彼得对耶稣说:“主啊,我们在这里真好!我们可以搭三个帐棚,一个为你,一个为摩西,一个为以利亚。”他根本不知道自己在说什么。
33Basi, watu hao wawili walipokuwa wakiondoka, Petro alimwambia Yesu, "Bwana, ni vizuri kwamba tupo hapa: basi, tujenge vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Eliya." --Kwa kweli hakujua anasema nini.
34他说这话的时候,有一片云彩笼罩他们,他们入了云彩,门徒就害怕起来。
34Petro alipokuwa akisema hayo, mara wingu likatokea na kuwafunika; na wingu hilo lilipowajia, wale wanafunzi waliogopa sana.
35有声音从云彩里出来,说:“这是我的儿子,我所拣选的(“这是我的儿子,我所拣选的”有些抄本作“这是我的爱子”),你们要听从他!”
35Sauti ikasikika kutoka katika hilo wingu: "Huyu ndiye Mwanangu niliyemchagua, msikilizeni."
36声音过了,只见耶稣独自在那里。在那些日子,门徒保持缄默,不把所看见的告诉任何人。
36Baada ya hiyo sauti kusikika, Yesu alionekana akiwa peke yake. Wanafunzi walikaa kimya juu ya tukio hilo, na wakati ule hawakumwambia mtu yeyote mambo hayo waliyoyaona.
37治好癫痫病的小孩(太17:14-18;可9:14-27)第二天,他们下了山,有一大群人迎面而来。
37Kesho yake walipokuwa wakishuka kutoka kule mlimani, kundi kubwa la watu lilikutana na Yesu.
38在人群中有一个人喊叫说:“老师,求你怜悯我的儿子,因为他是我的独生子。
38Hapo, mtu mmoja katika lile kundi akapaaza sauti, akasema, "Mwalimu! Ninakusihi umwangalie mwanangu--mwanangu wa pekee!
39你看,污灵一抓住他,他就忽然喊叫,并且抽疯,口吐白沫;污灵又折磨糟践他,不肯放过他。
39Pepo huwa anamshambulia, na mara humfanya apige kelele; humtia kifafa, na povu likamtoka kinywani. Huendelea kumtesa sana, asimwache upesi.
40我求过你的门徒,把他赶出去,他们却办不到。”
40Niliwaomba wanafunzi wako wamfukuze, lakini hawakuweza."
41耶稣说:“唉!这不信又乖谬的世代啊!我跟你们在一起,忍受你们,要到几时呢?把你儿子带到这里来吧!”
41Yesu akasema, "Enyi kizazi kisicho na imani, kilichopotoka! Nitakaa nanyi na kuwavumilia mpaka lini?" Kisha akamwambia huyo mtu, "Mlete mtoto wako hapa."
42那孩子正走过来的时候,污鬼把他摔倒,使他重重地抽疯。耶稣斥责那污灵,把孩子医好,交给他父亲。
42Wakati mtoto huyo alipokuwa anamjia Yesu, yule pepo alimwangusha chini na kumtia kifafa. Lakini Yesu akamkemea yule pepo mchafu akamponya mtoto na kumkabidhi kwa baba yake.
43众人都惊奇 神的大能。众人还在希奇耶稣所作的这一切时,他对门徒说:
43Watu wote wakashangazwa na uwezo mkuu wa Mungu. Wale watu walipokuwa bado wanashangaa juu ya mambo yote aliyofanya, Yesu aliwaambia wanafunzi wake,
44第二次预言受难及复活(太17:22-23;可9:30-32)“你们要把这些话存在心里:人子将要被交在人的手里。”
44"Tegeni masikio, myasikie mambo haya: Mwana wa Mtu anakwenda kutiwa mikononi mwa watu."
45门徒不明白这话,因为这话的意思是隐藏的,不让他们明白,他们也不敢问。
45Lakini wao hawakuelewa maana ya usemi huo. Jambo hilo lilikuwa limefichwa kwao ili wasitambue; nao wakaogopa kumwuliza juu ya msemo huo.
46门徒争论谁最大(太18:1-5;可9:33-40)后来,门徒起了意见,争论谁是最大的。
46Kukatokea majadiliano kati ya wale wanafunzi kuhusu nani kati yao aliyekuwa mkuu zaidi.
47耶稣看出他们的心意,就领了一个小孩子来,叫他站在自己旁边,
47Yesu aliyajua mawazo yaliyokuwa mioyoni mwao; basi akamchukua mtoto mdogo akamweka karibu naye,
48对他们说:“凡因我的名接待这小孩子的,就是接待我;凡接待我的,就是接待那差我来的。谁是你们中间最小的,那人就是最大的。”
48akawaambia, "Mtu yeyote anayempokea mtoto huyu mdogo kwa jina langu, ananipokea mimi; na yeyote anayenipokea mimi, anampokea yule aliyenituma. Maana yule aliye mdogo kuliko wote kati yenu ndiye aliye mkubwa kuliko wote."
49约翰说:“主,我们看见有一个人奉你的名赶鬼,就禁止他,因为他不和我们一起跟从你。”
49Yohane alidakia na kusema, "Bwana, tumemwona mtu mmoja akitoa pepo kwa kulitumia jina lako nasi tukajaribu kumkataza kwa kuwa yeye si mmoja wetu."
50耶稣说:“不要禁止他,因为不反对你们的,就是赞成你们的。”
50Lakini Yesu akamwambia, "Msimkataze; kwani asiyepingana nanyi yuko upande wenu."
51撒玛利亚人不接待主耶稣被接上升的日子快到了,他就决意向耶路撒冷去,
51Wakati ulipokaribia ambapo Yesu angechukuliwa juu mbinguni, yeye alikata shauri kwenda Yerusalemu.
52并且差遣使者走在前头;他们去了,进入撒玛利亚的一个村庄,要为他预备。
52Basi, akawatuma wajumbe wamtangulie, nao wakaenda wakaingia kijiji kimoja cha Wasamaria ili wamtayarishie mahali.
53那里的人不接待他,因为他面向着耶路撒冷走。
53Lakini wenyeji wa hapo hawakutaka kumpokea kwa sababu alikuwa anaelekea Yerusalemu.
54他的门徒雅各、约翰看见了,就说:“主啊,你要我们吩咐火从天降下来,烧灭他们吗?”
54Basi, wanafunzi wake, kina Yohane na Yakobo, walipoona hayo, wakasema, "Bwana, wataka tuamuru moto ushuke kutoka mbinguni uwateketeze?"
55耶稣就转过身来,责备他们,
55Lakini yeye akawageukia, akawakemea akasema, "Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo;
56然后他们就往别的村庄去了。
56kwa maana Mwana wa Mtu hakuja kuyaangamiza maisha ya watu, bali kuyaokoa." Wakatoka, wakaenda kijiji kingine.
57要求跟从耶稣(太8:19-22)他们走路的时候,有一个人对他说:“你无论往哪里去,我都要跟从你!”
57Walipokuwa wakisafiri njiani, mtu mmoja akamwambia Yesu, "Nitakufuata kokote utakakokwenda."
58耶稣说:“狐狸有洞,天空的飞鸟有窝,人子却没有栖身的地方。”
58Yesu akasema, "Mbweha wana mapango, na ndege wana viota; lakini Mwana wa Mtu hana mahali pa kupumzikia."
59他对另一个人说:“你跟从我吧!”那人说:“主啊,请准我先回去安葬我的父亲吧。”
59Kisha akamwambia mtu mwingine, "Nifuate." Lakini huyo akasema, "Bwana, niruhusu kwanza niende kumzika baba yangu."
60耶稣说:“让死人去埋葬他们的死人,你应该去传扬 神的国。”
60Yesu akamwambia, "Waache wafu wazike wafu wao; bali wewe nenda ukatangaze Ufalme wa Mungu."
61又有一个人说:“主,我要跟从你,但容我先回去,向家人道别。”
61Na mtu mwingine akamwambia, "Nitakufuata, lakini niruhusu kwanza nikawaage wale walio nyumbani kwangu."
62耶稣说:“手扶着犁向后看的,不适合进 神的国。”
62Yesu akamwambia, "Yeyote anayeshika jembe tayari kulima na huku anaangalia nyuma, hafai kwa Ufalme wa Mungu."