1提防法利赛人的酵(太10:26-27)
1Wakati watu kwa maelfu walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu aliwaambia kwanza wanafunzi wake, "Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani unafiki.
2没有什么掩盖的事不被揭露,也没有什么隐藏的事不被人知道。
2Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, kila kilichofichika kitafichuliwa.
3所以,你们在暗处所说的,必在明处被人听见;在内室附耳所谈的,必在房顶上宣扬出来。
3Kwa hiyo, kila mliyosema gizani, watu watayasikia katika mwanga, na kila mliyonong'ona faraghani milango imefungwa, yatatangazwa juu ya nyumba.
4应该怕谁(太10:28-31)“我的朋友,我告诉你们,那杀身体以后不能再作什么的,不要怕他们。
4"Nawaambieni ninyi rafiki zangu: msiwaogope wale wanaoua mwili, wasiweze kufanya kitu kingine zaidi.
5我要指示你们当怕的是谁:当怕那杀身体以后,有权把人投入地狱里的;我告诉你们,应当怕他。
5Nitawaonyesheni yule ambaye ni lazima kumwogopa: mwogopeni yule ambaye baada ya kuua ana uwezo wa kumtupa mtu katika moto wa Jehanamu. Naam, ninawaambieni, mwogopeni huyo.
6五只麻雀,不是卖两个大钱吗?但在 神面前,一只也不被忘记。
6Inajulikana kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti kumi, au sivyo? Lakini mbele ya Mungu hasahauliki hata mmoja.
7甚至你们的头发都一一数过了。不要怕,你们比许多麻雀贵重得多呢。
7Lakini hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope, basi, ninyi mna thamani zaidi kuliko shomoro wengi!
8要在人面前承认主(太10:32-33)“我告诉你们,凡在人面前承认我的,人子在 神的使者面前也承认他;
8"Nawaambieni kweli, kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, Mwana wa Mtu naye atakiri mbele ya malaika wa Mungu kwamba mtu huyo ni wake.
9在人面前不认我的,我在 神的使者面前也不认他。
9Lakini, mtu yeyote anayenikana mbele ya watu, naye atakanwa mbele ya malaika wa Mungu.
10凡说话得罪人子的,还可以赦免;但亵渎圣灵的,必不得赦免。
10"Yeyote anayesema neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa; lakini anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
11人把你们拉到会堂、官长和当权者的面前,你们不要思虑怎样申辩或说什么话。
11"Watakapowapeleka ninyi mbele ya masunagogi na mbele ya wakuu na watawala msiwe na wasiwasi juu ya jinsi mtakavyojitetea au jinsi mtakavyosema.
12到了时候,圣灵必把当说的话教导你们。”
12Kwa maana wakati huo Roho Mtakatifu atawafundisheni kile mnachopaswa kusema."
13无知富翁的比喻群众中有一个人对耶稣说:“老师,请吩咐我的兄弟和我分家业。”
13Mtu mmoja katika ule umati wa watu akamwambia, "Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane urithi aliotuachia baba."
14耶稣说:“你这个人,谁立我作你们的审判官和分家业的人呢?”
14Yesu akamjibu, "Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi mwamuzi au msuluhishi kati yenu?"
15于是他对众人说:“你们要谨慎,远离一切贪心,因为人的生命并不在于家道丰富。”
15Basi, akawaambia wote, "Jihadharini na kila aina ya tamaa; maana uzima wa mtu hautegemei wingi wa vitu alivyo navyo."
16就对他们讲了一个比喻,说:“有一个富翁的田地丰收。
16Kisha akawaambia mfano: "Kulikuwa na tajiri mmoja ambaye shamba lake lilizaa mavuno mengi.
17他自己心里说:‘怎么办呢?因为我没有足够的地方收藏出产了!’
17Tajiri huyo akafikiri moyoni mwake: Nitafanyaje nami sina mahali pa kuhifadhia mavuno yangu?
18又说:‘我要这样办:我要拆掉这些仓房,建造更大的,好在那里收藏我的一切粮食和货物。
18Nitafanya hivi: nitabomoa ghala zangu na kujenga kubwa zaidi, na humo nitahifadhi mavuno yangu yote na mali yangu.
19然后,我要对我的灵魂说:灵魂啊,你拥有许多好东西,足够多年享用,只管安安逸逸地吃喝快乐吧!’
19Hapo nitaweza kuiambia roho yangu: sasa unayo akiba ya matumizi kwa miaka na miaka. Ponda mali, ule, unywe na kufurahi.
20 神却对他说:‘无知的人哪,今天晚上,你拥有的就要取去你的灵魂,你所预备的要归给谁呢?’
20Lakini Mungu akamwambia: Mpumbavu wewe; leo usiku roho yako itachukuliwa. Na vitu vile vyote ulivyojilundikia vitakuwa vya nani?"
21凡为自己积财,在 神面前却不富足的,也是这样。”
21Yesu akamaliza kwa kusema "Ndivyo ilivyo kwa mtu anayejilundikia mali kwa ajili yake mwenyewe, lakini si tajiri mbele ya Mungu."
22不要忧虑,积财于天(太6:19-21、25-33)耶稣又对门徒说:“所以我告诉你们,不要为生命忧虑吃什么,也不要为身体忧虑穿什么。
22Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Kwa sababu hiyo nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula mnachohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu.
23因为生命比饮食重要,身体比衣服重要。
23Kwa sababu uzima ni bora kuliko chakula, na mwili ni bora kuliko mavazi.
24你们想想乌鸦:它们不种也不收,无仓又无库, 神尚且养活它们;你们比飞鸟贵重得多了。
24Chukueni kwa mfano, kunguru: hawapandi, hawavuni wala hawana ghala yoyote. Hata hivyo, Mungu huwalisha. Ninyi mna thamani zaidi kuliko ndege!
25你们中间谁能用忧虑使自己的寿命延长一刻呢?
25Ni nani kati yenu kwa kuwa na wasiwasi anaweza kuongeza urefu wa maisha yake?
26既然连这极小的事都不能作,为什么还忧虑其他的事呢?
26Basi, kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini kuwa na wasiwasi juu ya yale mengine?
27你们想想百合花,怎样不劳苦,也不纺织。但我告诉你们,就是所罗门最荣华的时候所穿的,也比不上这花中的一朵呢。
27Angalieni maua jinsi yanavyomea. Hayafanyi kazi wala hayafumi. Hata hivyo, nawahakikishieni kwamba hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
28小信的人哪,田野的草,今天还在,明天就投进炉里, 神尚且这样给它装饰,何况你们呢?
28Lakini, kama Mungu hulivika vizuri jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatawafanyia ninyi zaidi? Enyi watu wenye imani haba!
29你们不要求吃什么,喝什么,也不要忧虑,
29"Basi, msivurugike akili, mkihangaika daima juu ya mtakachokula au mtakachokunywa.
30因为这一切都是世上不信的人所寻求的。你们的父原知道你们需要这一切。
30Kwa maana hayo yote ndiyo yanayohangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo.
31你们只管求他的国,这些东西都必加给你们。
31Shughulikieni kwanza Ufalme wa Mungu, na hayo yote mtapewa kwa ziada.
32你们这小群,不要怕,因为你们的父乐意把国赐给你们。
32"Msiogope, enyi kundi dogo! Maana Baba yenu amependa kuwapeni Ufalme.
33当变卖你们所有的施舍给人,为自己制造不朽坏的钱囊,积蓄用不尽的财宝在天上,就是贼不能近、虫不能蛀的地方。
33Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu.
34因为你们的财宝在哪里,你们的心也在哪里。
34Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
35忠心的仆人有福了(太24:45-51;可13:33-37)“你们的腰当束起来,灯也该点着,
35"Muwe tayari! Jifungeni mkanda kiunoni, na taa zenu ziwe zinawaka;
36像等候自己的主人从婚筵回来一样,好叫你们在主人回来敲门时,立刻给他开门。
36muwe kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka arusini, ili wamfungulie mara atakapobisha hodi.
37主人来到了,看见仆人警醒,这些仆人就有福了。我实在告诉你们,主人必亲自束腰,招待他们吃饭,进前来侍候他们。
37Heri yao watumishi wale ambao bwana wao atakaporudi atawakuta wanakesha! Nawaambieni hakika, huyo bwana atajifunga mkanda kiunoni, atawaketisha mezani na kuwahudumia.
38主人也许半夜之前,或天亮之前回来,看见他们这样,这些仆人就有福了。
38Heri yao watumishi hao ikiwa bwana wao atawakuta wanakesha hata ikiwa atarudi usiku wa manane au alfajiri.
39你们都知道,家主若晓得窃贼什么时候来,就不会让他摸进屋里。
39Jueni kwamba, kama mwenye nyumba angejua saa ambayo mwizi atakuja, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
40你们也要准备妥当,因为在想不到的时候,人子就来了。”
40Nanyi, kadhalika muwe tayari, maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia."
41彼得说:“主啊,你说这比喻,是为我们还是为众人呢?”
41Petro akamwambia, "Bwana, mfano huo ni kwa ajili yetu tu, au ni kwa ajili ya watu wote?"
42主说:“谁是那忠心精明的管家,被主人指派管理家里的仆人,按时分粮呢?
42Bwana akajibu, "Ni nani basi, mtumishi aliye mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watumishi wake ili awape chakula wakati ufaao?
43主人来到的时候,看见他这样作,那仆人就有福了。
43Heri yake mtumishi huyo ikiwa bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
44我实在告诉你们,主人要指派他管理主人的一切财产。
44Hakika atampa madaraka juu ya mali yake yote.
45如果那仆人心里说:‘我的主人不会那么快回来’,就动手打其他的仆人使女,并且吃喝醉酒;
45Lakini, kama mtumishi huyo atafikiri moyoni mwake: na kusema: Bwana wangu amekawia sana kurudi halafu aanze kuwapiga watumishi wenzake, wa kiume au wa kike, na kula, kunywa na kulewa,
46在他想不到的日子、不知道的时间,那仆人的主人要来,严厉地处罚他,使他和不信的人同在一起。
46bwana wake atarudi siku asiyoitazamia na saa asiyoijua; atamkatilia mbali na kumweka fungu moja na wasioamini.
47那仆人知道主人的意思,却不预备,也不照他的意思行,必多受责打;
47Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana.
48但那不知道的,虽然作了该受责打的事,也必少受责打。多给谁就向谁多取,多托谁就向谁多要。
48Lakini yule afanyaye yanayostahili adhabu bila kujua, atapigwa kidogo. Aliyepewa vingi atatakiwa vingi; aliyekabidhiwa vingi zaidi atatakiwa kutoa vingi zaidi.
49将引起纷争(太10:34-36)“我来要把火投在地上,如果烧了起来,那是我所愿意的。
49"Nimekuja kuwasha moto duniani, laiti ungekuwa umewaka tayari!
50我有应当受的洗,我是多么迫切地期待这事完成。
50Ninao ubatizo ambao inanipasa niupokee; jinsi gani ninavyohangaika mpaka ukamilike!
51你们以为我来是要地上有和平吗?不是的,我告诉你们,是要有纷争。
51Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? Hata kidogo; si amani bali utengano.
52从今以后,一家五口将起纷争,三个反对两个,两个反对三个。
52Na tangu sasa, jamaa ya watu watano itagawanyika; watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
53他们将起纷争:父亲反对儿子,儿子反对父亲,母亲反对女儿,女儿反对母亲,婆婆反对媳妇,媳妇反对婆婆。”
53Baba atakuwa dhidi ya mwanawe, mwana dhidi ya baba yake; mama dhidi ya bintiye, binti dhidi ya mama yake; mama mkwe dhidi ya mke wa mwanawe na huyo dhidi ya mama mkwe wake."
54当晓得分辨和判断(太16:2-3)耶稣又对众人说:“你们一看见西边有云彩升起来,就说:‘要下大雨’,果然这样;
54Yesu akayaambia tena makundi ya watu, "Mnapoona mawingu yakitokea upande wa magharibi, mara mwasema: Mvua itanyesha, na kweli hunyesha.
55起了南风,就说:‘天要热了’,也果然这样。
55Mnapoona upepo wa kusi unavuma, mwasema Kutakuwa na hali ya joto na ndivyo inavyokuwa.
56伪君子啊!你们知道分辨天地的气象,怎么不知道分辨这个时代呢?
56Enyi wanafiki! Mnajua kutabiri hali ya hewa kwa kuangalia dunia na anga; kwa nini basi, hamwezi kujua maana ya nyakati hizi?
57“你们为什么自己不能判断什么是对的呢?
57"Na kwa nini hamwezi kujiamulia wenyewe jambo jema la kufanya?
58你和你的对头去见官长,还在路上的时候,应当尽力向他求和,免得他把你拉到法官面前,法官把你交给差役,差役把你关在监里。
58Maana kama mshtaki wako anakupeleka mahakamani, ingekuwa afadhali kwako kupatana naye mkiwa bado njiani, ili asije akakupeleka mbele ya hakimu, naye hakimu akakutoa kwa polisi, nao wakakutia ndani.
59我告诉你,除非你还清最后的一个小钱,否则决不能从那里出来。”
59Hakika hutatoka huko nakwambia, mpaka utakapomaliza kulipa senti ya mwisho."