聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Luke

14

1治好水臌病的人
1Siku moja ya Sabato, Yesu alikwenda kula chakula nyumbani kwa mmoja wa viongozi wa Mafarisayo; watu waliokuwapo hapo wakawa wanamchunguza.
2正好在他面前有一个患水臌病的人;
2Mbele yake Yesu palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa na ugonjwa wa kuvimba mwili.
3耶稣对律法师和法利赛人说:“在安息日治病,可以不可以呢?”
3Yesu akawauliza walimu wa Sheria na Mafarisayo, "Je, ni halali au la kumponya mtu siku ya sabato?"
4他们却不出声。耶稣扶着病人,治好他,叫他走了,
4Lakini wao wakakaa kimya. Yesu akamshika huyo mgonjwa, akamponya, akamwacha aende zake.
5就对他们说:“你们中间谁的儿子或牛在安息日掉在井里,不立刻把他拉上来呢?”
5Halafu akawaambia, "Ni nani kati yenu ambaye mtoto wake au ng'ombe wake akitumbukia shimoni, hangemtoa hata kama ni siku ya Sabato?"
6他们不能回答这些话。
6Nao hawakuweza kumjibu swali hilo.
7耶稣教训筵席的主人(参箴25:6-7)耶稣看见被邀请的客人选择高位,就用比喻对他们说:
7Yesu aliona jinsi wale walioalikwa walivyokuwa wanajichagulia nafasi za heshima, akawaambia mfano:
8“你被邀请参加婚筵的时候,不要自己坐在高位上,恐怕有比你更尊贵的客人也被请来;
8"Kama mtu akikualika arusini, usiketi mahali pa heshima isije ikawa amealikwa mwingine mheshimiwa kuliko wewe;
9那请你又请他的人过来对你说:‘请你让位给这个人。’那时你就惭愧地退居末位了。
9na mwenyeji wenu ninyi wawili atakuja na kukwambia: Mwachie huyu nafasi. Hapo utaaibika mbele ya wote na kulazimika kwenda kuchukua nafasi ya mwisho.
10你被邀请的时候,要坐在末位上,等请你的人过来对你说:‘朋友,请上座。’那时你在同席的人面前才有光彩。
10Bali ukialikwa kwenye karamu, keti mahali pa mwisho, ili mwenyeji wako atakapokuja akwambie: Rafiki, njoo hapa mbele, mahali pazuri zaidi. Hapo utakuwa umeheshimika mbele ya wote wanaoketi pamoja nawe.
11因为凡高抬自己的,必要降卑;自己谦卑的,必要升高。”
11Kwa maana yeyote anayejikweza atashushwa, na anayejishusha, atakwezwa."
12耶稣又对邀请他的人说:“你设午餐或晚宴,不要请你的朋友、弟兄、亲戚或富裕的邻舍,恐怕他又回请你,你就得了报答。
12Halafu akamwambia na yule aliyemwalika, "Kama ukiwaandalia watu karamu mchana au jioni, usiwaalike rafiki zako au jamaa zako au jirani zako walio matajiri, wasije nao wakakualika nawe ukawa umelipwa kile ulichowatendea.
13你摆筵席的时候,总要邀请那贫穷的、残废的、瘸腿的、瞎眼的,
13Badala yake, unapofanya karamu, waalike maskini, vilema viwete na vipofu,
14那你就有福了。因为他们没有什么可以报答你,义人复活的时候,你必定得着报答。”
14nawe utakuwa umepata baraka, kwa kuwa hao hawana cha kukulipa. Maana Mungu atakupa tuzo lako wakati watu wema watakapofufuka."
15婚筵的比喻(参太22:1-10)一起吃饭的人中有一个,听了这些话,就对耶稣说:“在 神的国里吃饭的人有福了。”
15Mmoja wa wale waliokuwa wameketi pamoja na Yesu akasema, "Ana heri mtu yule atakayekula chakula katika Ufalme wa Mungu."
16耶稣对他说:“有一个人大摆筵席,请了许多客人。
16Yesu akamjibu, "Mtu mmoja alifanya karamu kubwa, akaalika watu wengi.
17到了开席的时候,他打发仆人去对所请的人说:‘请来吧!样样都准备好了。’
17Wakati wa karamu ulipofika alimtuma mtumishi wake awaambie walioalikwa, Njoni, kila kitu ni tayari.
18众人一致推辞,头一个说:‘我买了一块地,不得不去看一看,请原谅我。’
18Lakini wote, kwa namna moja, wakaanza kuomba radhi. Wa kwanza akamwambia mtumishi: Nimenunua shamba, kwa hiyo sina budi kwenda kuliangalia; nakuomba uniwie radhi.
19另一个说:‘我买了五对牛,要去试一试,请原谅我。’
19Mwingine akasema: Nimenunua ng'ombe jozi tano wa kulima; sasa nimo njiani kwenda kuwajaribu; nakuomba uniwie radhi.
20又一个说:‘我刚结了婚,不能去。’
20Na mwingine akasema: Nimeoa mke, kwa hiyo siwezi kuja.
21仆人回来把这些事告诉他主人,家主就发怒,对仆人说:‘快到城里大街小巷去,把贫穷的、残废的、瞎眼的、瘸腿的,都领到这里来。’
21Mtumishi huyo akarudi na kumwarifu bwana wake jambo hilo. Yule mwenye nyumba alikasirika, akamwambia mtumishi wake: Nenda upesi kwenye barabara na vichochoro vya mji, uwalete hapa ndani maskini, viwete, vipofu na waliolemaa.
22仆人说:‘主啊,你所吩咐的已经办了,还有空位。’
22Baadaye, mtumishi huyo akasema: Bwana mambo yamefanyika kama ulivyoamuru, lakini bado iko nafasi.
23主人就对仆人说:‘你出去到路边篱畔,勉强人进来,好把我的屋子坐满。
23Yule bwana akamwambia mtumishi: Nenda katika barabara na vichochoro vya mji uwashurutishe watu kuingia ili nyumba yangu ijae.
24我告诉你们,先前请的那些人,一个也不得尝我的筵席。’”
24Kwa maana, nawaambieni, hakuna hata mmoja wa wale walioalikwa atakayeonja karamu yangu."
25作门徒的代价(参太10:37-38)有许多人与耶稣同行,他转身对他们说:
25Hapo, makundi mengi yakawa yanaandamana pamoja na Yesu. Basi, akawageukia akawaambia,
26“如果有人到我这里来,爱我不超过爱(“爱我不超过爱”原文作“不恨”)自己的父母、妻子、儿女、兄弟、姊妹,甚至自己的性命,就不能作我的门徒。
26"Mtu yeyote akija kwangu, asipowachukia baba na mama yake, mke wake, watoto, ndugu na dada zake, naam, hata na nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
27凡不背着自己的十字架跟随我的,也不能作我的门徒。
27Mtu asipochukua msalaba wake na kunifuata hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
28你们当中有谁要盖一座楼,不先坐下计算费用,能不能盖成呢?
28Kwa maana, ni nani miongoni mwenu ambaye akitaka kujenga mnara hataketi kwanza akadirie gharama zake ili ajue kama ana kiasi cha kutosha cha kumalizia?
29恐怕安了地基,而不能完成,所有看见的人都讥笑他,
29La sivyo, baada ya kuweka msingi na kushindwa kumaliza, watu watamcheka
30说:‘这个人开了工,却不能完工。’
30wakisema: Mtu huyu alianza kujenga, lakini hakumalizia.
31或者一个王去和别的王打仗,哪有不先坐下想想,能否用一万兵去抵抗那领两万来攻打他的呢?
31"Au, ni mfalme gani ambaye, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, hataketi kwanza chini na kufikiri kama ataweza, kwa askari wake elfu ishirini?
32如果不能,就该趁对方还远的时候,派使者去谈判和平的条件。
32Kama anaona hataweza, atawatuma wajumbe kutaka masharti ya amani wakati mfalme huyo mwingine angali mbali.
33这样,你们中间不论谁,如果不撇下一切所有的,就不能作我的门徒。
33Vivyo hivyo, basi, hakuna hata mmoja wenu atakayekuwa mwanafunzi wangu kama asipoachilia kila kitu alicho nacho.
34“盐本来是好的,但如果失了味,怎能使它再咸呢?
34"Chumvi ni nzuri; lakini ikipoteza ladha yake, itakolezwa na nini?
35或用在田里,或放在粪里,都不合适;只好扔在外面。有耳可听的,就应当听。”
35Haifai kitu wala kwa udongo wala kwa mbolea. Watu huitupilia mbali. Sikieni basi, kama mna masikio!"