1耶稣基督降生(太1:18-25)
1Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote chini ya utawala wake wajiandikishe.
2这是第一次户口登记,是在居里纽作叙利亚总督的时候举行的。
2Kuandikishwa huku kulikuwa mara ya kwanza, wakati Kirenio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Siria.
3众人各归各城去登记户口。
3Basi, wote waliohusika walikwenda kujiandikisha, kila mtu katika mji wake.
4约瑟本是大卫家族的人,也从加利利的拿撒勒上犹太去,到了大卫的城伯利恒,
4Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya. Kwa kuwa alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yuda alikozaliwa Mfalme Daudi.
5与所聘之妻马利亚一同登记户口。那时马利亚的身孕已经重了。
5Alikwenda kujiandikisha pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mja mzito.
6他们在那里的时候,马利亚的产期到了,
6Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia,
7生了头胎儿子,用布包着,放在马槽里,因为客店里没有地方。
7akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni.
8天使向牧羊人报喜信在伯利恒的郊外,有一些牧人在夜间看守羊群。
8Katika sehemu hizo, walikuwako wachungaji wakikesha usiku mbugani kulinda mifugo yao.
9主的一位使者站在他们旁边,主的荣光四面照着他们,他们就非常害怕。
9Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, na utukufu wa Bwana ukawaangazia pande zote. Wakaogopa sana.
10天使说:“不要怕!看哪!我报给你们大喜的信息,是关于万民的:
10Malaika akawaambia, "Msiogope! Nimewaleteeni habari njema ya furaha kuu kwa watu wote.
11今天在大卫的城里,为你们生了救主,就是主基督。
11Kwa maana, leo hii katika mji wa Daudi, amezaliwa Mwokozi kwa ajili yenu, ndiye Kristo Bwana.
12你们要找到一个婴孩,包着布,卧在马槽里,那就是记号了。”
12Na hiki kitakuwa kitambulisho kwenu: mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelazwa horini."
13忽然有一大队天兵,同那天使一起赞美 神说:
13Mara kundi kubwa la jeshi la mbinguni likajiunga na huyo malaika, wakamsifu Mungu wakisema:
14“在至高之处,荣耀归与 神!在地上,平安归与他所喜悦的人!”
14"Utukufu kwa Mungu juu mbinguni, na amani duniani kwa watu aliopendezwa nao!"
15众天使离开他们升天去了,那些牧人彼此说:“我们往伯利恒去,看看主所指示我们已经成就的事。”
15Baada ya hao malaika kuondoka na kurudi mbinguni, wachungaji wakaambiana: "Twendeni moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukalione tukio hili Bwana alilotujulisha."
16他们急忙去了,找到马利亚、约瑟和那卧在马槽里的婴孩。
16Basi, wakaenda mbio, wakamkuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga amelazwa horini.
17他们见过以后,就把天使对他们论这孩子的话传开了。
17Hao wachungaji walipomwona mtoto huyo wakawajulisha wote habari waliyokuwa wamesikia juu yake.
18听见的人,都希奇牧人所说的事。
18Wote waliosikia hayo walishangaa juu ya habari walizoambiwa na wachungaji.
19马利亚把这一切放在心里,反复思想。
19Lakini Maria aliyaweka na kuyatafakari mambo hayo yote moyoni mwake.
20牧人因为听见的和看见的,正像天使对他们所说的一样,就回去了,把荣耀赞美归与 神。
20Wale wachungaji walirudi makwao huku wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa yote waliyokuwa wamesikia na kuona; yote yalikuwa kama walivyokuwa wameambiwa.
21满了八天,替孩子行割礼的时候,就给他起名叫耶稣,就是他成胎之前,天使所起的。
21Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina Yesu, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.
22在圣殿奉献耶稣满了洁净的日子,他们就按着摩西的律法,带孩子上耶路撒冷去,奉献给主。
22Siku zilipotimia za Yosefu na Maria kutakaswa kama walivyotakiwa na Sheria ya Mose, wazazi hao walimchukua mtoto, wakaenda naye Yerusalemu ili wamweke mbele ya Bwana.
23正如主的律法所记:“所有头生的男孩,都当称为圣归给主。”
23Katika Sheria ya Bwana imeandikwa: "Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atawekwa wakfu kwa Bwana."
24又照着主的律法所说的献上祭物,就是一对斑鸠或两只雏鸽。
24Pia walikwenda ili watoe sadaka: hua wawili au makinda wawili ya njiwa, kama ilivyotakiwa katika Sheria ya Bwana.
25在耶路撒冷有一个人,名叫西面,这人公义虔诚,一向期待以色列的安慰者来到,又有圣灵在他身上。
25Wakati huo huko Yerusalemu kulikuwa na mtu mmoja, mwema na mcha Mungu, jina lake Simeoni. Yeye alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa Israeli. Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye.
26圣灵启示他,在死前必得见主所应许的基督,
26Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Masiha wa Bwana.
27他又受圣灵感动进了圣殿。那时,耶稣的父母抱着孩子进来,要按着律法的规矩为他行礼。
27Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia Hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta Hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na Sheria,
28西面就把他接到手上,称颂 神说:
28Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu na kusema:
29“主啊,现在照你的话,释放仆人平平安安地去吧!
29"Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako, waweza kumruhusu mtumishi wako aende kwa amani.
30因我的眼睛已经看见你的救恩,
30Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu utokao kwako,
31就是你在万民面前所预备的,
31ambao umeutayarisha mbele ya watu wote:
32为要作外族人启示的光,和你民以色列的荣耀。”
32Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa, na utukufu kwa watu wako Israeli."
33他父母因论到他的这些话而希奇。
33Baba na mama yake Yesu walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto.
34西面给他们祝福,对他母亲马利亚说:“看哪!这孩子被立,要叫以色列中许多人跌倒,许多人兴起,又要成为反对的目标,
34Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, "Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu;
35(你自己的心也会被刀刺透,)这样,许多人心中的意念就要被揭露出来。”
35na hivyo mawazo ya watu wengi yataonekana wazi. Nawe mwenyewe, uchungu ulio kama upanga mkali utauchoma moyo wako."
36又有一个女先知,就是亚拿,是亚设支派法内利的女儿。她已经上了年纪,从童女出嫁,和丈夫住了七年,
36Palikuwa na nabii mmoja mwanamke, mzee sana, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa ameishi na mumewe kwa miaka saba tangu alipoolewa.
37就寡居了,直到八十四岁(“就寡居了,直到八十四岁”或译:“就寡居了八十四年”)。她没有离开过圣殿,以禁食和祷告昼夜事奉主。
37Halafu alibaki mjane hadi wakati huo akiwa mzee wa miaka themanini na minne. Wakati huo wote alikaa Hekaluni akifunga na kusali usiku na mchana.
38就在那时候,她前来称谢 神,并且向期待耶路撒冷蒙救赎的众人,讲论孩子的事。
38Saa hiyohiyo alijitokeza mbele, akamshukuru Mungu, na akaeleza habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wanatazamia ukombozi wa Yerusalemu.
39他们按着主的律法办完一切,就回加利利,到自己的城拿撒勒去了。
39Hao wazazi walipokwisha fanya yote yaliyoamriwa na Sheria ya Bwana, walirudi makwao Nazareti, mkoani Galilaya.
40孩子渐渐长大,强壮起来,充满智慧,有 神的恩典在他身上。
40Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa pamoja naye.
41孩童耶稣上耶路撒冷过节每年逾越节,他父母都上耶路撒冷去。
41Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka.
42当他十二岁时,他们按着节期的惯例,照常上去。
42Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
43过完了节,他们回去的时候,孩童耶稣仍留在耶路撒冷,他父母却不知道,
43Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari.
44还以为他在同行的人中间。走了一天,就在亲戚和熟人中找他,
44Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki.
45没有找到,就转回耶路撒冷找他。
45Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta.
46过了三天,才发现他在圣殿里,坐在教师中间,一面听,一面问。
46Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
47所有听见他的人,都希奇他的聪明和应对。
47Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima.
48他父母见了,非常惊奇,他母亲说:“孩子,为什么这样对待我们呢?你看,你父亲和我都很担心地在找你呢!”
48Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, "Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni."
49他说:“为什么找我呢?你们不知道我必须在我父的家里吗?(“在我父的家里吗?”或译:“以我父的事为念吗?”)”
49Yeye akawajibu, "Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?"
50但他们不明白他所说的话。
50Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia.
51他就同他们下去,回到拿撒勒,并且顺从他们。他母亲把这一切事,都存在心里。
51Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake.
52耶稣的智慧和身量,以及 神和人对他的喜爱,都不断增长。
52Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu.