1施洗约翰(太3:1-12;可1:3-5、7-8;约1:19-28)
1Mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alikuwa anatawala mkoa wa Yudea. Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo, ndugu yake, alikuwa mkuu wa mikoa ya Iturea na Trakoniti. Lusania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
2亚那和该亚法作大祭司的时候, 神的话临到撒迦利亚的儿子,在旷野的约翰。
2na Anasi na Kayafa walikuwa makuhani wakuu mjini Yerusalem. Wakati huo ndipo neno la Mungu lilipomjia Yohane, mwana wa Zakariya, kule jangwani.
3他就来到约旦河一带地方,宣讲悔改的洗礼,使罪得赦。
3Basi, Yohane akaenda katika sehemu zote zilizopakana na mto Yordani, akihubiri watu watubu na kubatizwa ili Mungu awaondolee dhambi.
4正如以赛亚先知的书上写着:“在旷野有呼喊者的声音:‘预备主的道,修直他的路!
4Ndivyo ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: "Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake; nyosheni mapito yake.
5一切洼谷都当填满,大小山冈都要削平!弯弯曲曲的改为正直,高高低低的修成平坦!
5Kila bonde litafukiwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa; palipopindika patanyooshwa, njia mbaya zitatengenezwa.
6所有的人都要看见 神的救恩。’”
6Na, watu wote watauona wokovu utokao kwa Mungu."
7约翰对那出来要受他洗礼的群众说:“毒蛇所生的啊,谁指示你们逃避那将要来的忿怒呢?
7Basi, Yohane akawa anawaambia watu wengi waliofika ili awabatize: "Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mngeweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?
8应当结出果子来,与悔改的心相称;你们心里不要说:‘我们有亚伯拉罕作我们的祖宗。’我告诉你们, 神能从这些石头中给亚伯拉罕兴起后裔来。
8Basi, onyesheni kwa matendo kwamba mmetubu. Msianze sasa kusema: Sisi ni watoto wa Abrahamu. Nawaambieni hakika, Mungu anaweza kuyageuza mawe haya yawe watoto wa Abrahamu!
9现在斧头已经放在树根上,所有不结好果子的树,就砍下来,丢在火里。”
9Lakini, sasa hivi shoka limewekwa tayari kukata mizizi ya miti. Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni."
10群众问他:“那么,我们该作什么呢?”
10Umati wa watu ukamwuliza, "Tufanye nini basi?"
11他回答:“有两件衣服的,当分给那没有的,有食物的也当照样作。”
11Akawajibu, "Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo."
12又有税吏来要受洗,问他:“老师,我们当作什么呢?”
12Nao watoza ushuru wakaja pia ili wabatizwe, wakamwuliza, "Mwalimu, tufanye nini?"
13他说:“除了规定的以外,不可多收。”
13Naye akawaambia, "Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa."
14兵丁也问他:“至于我们,我们又应当作什么呢?”他说:“不要恐吓,不要敲诈,当以自己的粮饷为满足。”
14Nao askari wakamwuliza, "Na sisi tufanye nini?" Naye akawajibu, "Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu."
15那时众人正在期待,人人心里都在猜想会不会约翰就是基督。
15Wote walikuwa wanatazamia kitu fulani; basi, wakaanza kujiuliza mioyoni mwao kuhusu Yohane: kuwa labda yeye ndiye Kristo.
16约翰对众人说:“我用水给你们施洗,但那能力比我更大的要来,我就是给他解鞋带都没有资格。他要用圣灵与火给你们施洗。
16Hapo Yohane akawaambia wote, "Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi ambaye sistahili hata kumfungulia kamba za viatu vyake. Yeye atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17他手里拿着簸箕,要扬净麦场,把麦子收进仓里,却用不灭的火把糠秕烧尽。”
17Yeye ni kama mtu anayeshika mikononi mwake chombo cha kupuria nafaka, aipure nafaka yake, akusanye ngano ghalani mwake, na makapi ayachome kwa moto usiozimika."
18他还用许多别的话劝勉众人,向他们传福音。
18Hivyo, pamoja na mawaidha mengine mengi, Yohane aliwahimiza watu akiwahubiria Habari Njema.
19分封王希律,因他弟弟的妻子希罗底,并因他自己所行的一切恶事,受到约翰的责备。
19Lakini Yohane alimgombeza Herode, mkuu wa mkoa, kwa sababu alikuwa amemchukua Herodia, mke wa ndugu yake, na kumfanya mke wake; na pia kwa ajili ya mabaya yote aliyokuwa amefanya.
20他在这一切事以外,再加上一件,就是把约翰关在监里。
20Kisha Herode akazidisha ubaya wake kwa kumtia Yohane gerezani.
21耶稣受洗(太3:13-17;可1:9-11)众人受了洗,耶稣也受了洗。他正在祷告,天就开了,
21Watu wote walipokuwa wamekwisha batizwa, Yesu naye alibatizwa. Na alipokuwa akisali, mbingu zilifunguka,
22圣灵仿佛鸽子,有形体地降在他身上;有声音从天上来,说:“你是我的爱子,我喜悦你。”
22na Roho Mtakatifu akamshukia akiwa na umbo kama la njiwa. Sauti ikasikika kutoka mbinguni: "Wewe ndiwe Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe."
23耶稣的家谱(太1:1-17)耶稣开始传道,年约三十岁,人以为他是约瑟的儿子,约瑟是希里的儿子,
23Yesu alipoanza kazi yake hadharani, alikuwa na umri upatao miaka thelathini, na watu walidhani yeye ni mwana wa Yosefu, mwana wa Heli.
24依次往上推,是玛塔、利未、麦基、雅拿、约瑟、
24Heli alikuwa mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yanai, mwana wa Yosefu,
25玛他提亚、亚摩斯、拿鸿、以斯利、拿该、
25mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Hesli, mwana wa Nagai,
26玛押、玛他提亚、西美、约瑟、约大、
26mwana wa Maathi, mwana wa Matathia, mwana wa Shemeni, mwana wa Yoseki, mwana wa Yuda,
27约哈难、利撒、所罗巴伯、撒拉铁、尼利、
27mwana wa Yohanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
28麦基、亚底、哥桑、以摩当、珥、
28mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
29耶书、以利以谢、约令、玛塔、利未、
29mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Mathati, mwana wa Lawi,
30西缅、犹大、约瑟、约南、以利亚敬、
30mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yosefu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliakimu,
31米利亚、买拿、马达他、拿单、大卫、
31mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
32耶西、俄备得、波阿斯、撒门(“撒门”有些抄本作“撒拉”)、拿顺、
32mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
33亚米拿达、亚当民(有些抄本无“亚当民”一词)、亚兰(“亚兰”有些抄本作“亚珥尼”)、希斯仑、法勒斯、犹大、
33mwana wa Aminadabu, mwana wa Admini, mwana wa Arni, mwana wa Hesroni, mwana wa Feresi, mwana wa Yuda,
34雅各、以撒、亚伯拉罕、他拉、拿鹤、
34mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Abrahamu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
35西鹿、拉吴、法勒、希伯、沙拉、
35mwana wa Serugi, mwana wa Reu, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
36该南、亚法撒、闪、挪亚、拉麦、
36mwana wa Kainani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Noa, mwana wa Lameki,
37玛土撒拉、以诺、雅列、玛勒列、该南、
37mwana wa Mathusala, mwana wa Henoki, mwana wa Yaredi, mwana wa Mahalaleli, mwana wa Kenani,
38以挪士、塞特、亚当,亚当是 神的儿子。
38mwana wa Enosi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, aliyekuwa wa Mungu.