聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Luke

4

1耶稣受试探(太4:1-11;可1:12-13)
1Yesu alitoka katika mto Yordani akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akaongozwa na Roho mpaka jangwani.
2那些日子他什么也没有吃,日子满了他就饿了。
2Huko alijaribiwa na Ibilisi kwa muda wa siku arubaini. Wakati huo wote hakula chochote, na baada ya siku hizo akasikia njaa.
3魔鬼对他说:“你若是 神的儿子,就吩咐这块石头变成食物吧!”
3Ndipo Ibilisi akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate."
4耶稣回答:“经上记着:‘人活着不是单靠食物。’”
4Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Mtu haishi kwa mkate tu."
5魔鬼引他上到高处,霎时间把天下万国指给他看,
5Kisha Ibilisi akamchukua hadi mahali pa juu, akamwonyesha kwa mara moja falme zote za ulimwengu. Huyo Shetani akamwambia,
6对他说:“这一切权柄、荣华,我都可以给你;因为这些都交给了我,我愿意给谁就给谁。
6"Nitakupa uwezo juu ya falme zote hizi na fahari zake, kwa maana nimepewa hivi vyote; nikitaka kumpa mtu ninaweza.
7所以,只要你在我面前拜一拜,这一切就全是你的了。”
7Hivi vyote vitakuwa mali yako wewe, kama ukiniabudu."
8耶稣回答:“经上记着:‘当拜主你的 神,单要事奉他。’”
8Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Utamwabudu Bwana Mungu wako, na utamtumikia yeye peke yake."
9魔鬼又引他到耶路撒冷,叫他站在殿顶上,对他说:“你若是 神的儿子,就从这里跳下去吧!
9Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, kwenye mnara wa Hekalu, akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu,
10因为经上记着:‘他为了你,会吩咐自己的使者保护你。’
10kwa maana imeandikwa: Atawaamuru malaika wake wakulinde,
11又记着:‘用手托住你,免得你的脚碰到石头。’”
11na tena, Watakuchukua mikononi mwao usije ukajikwaa mguu wako kwenye jiwe."
12耶稣回答:“经上说:‘不可试探主你的 神。’”
12Lakini Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Usimjaribu Bwana Mungu wako."
13魔鬼用尽了各种试探,就暂时离开了耶稣。
13Ibilisi alipokwishamjaribu kwa kila njia, akamwacha kwa muda.
14在加利利传道(太4:12-17;可1:14-15)耶稣带着圣灵的能力,回到加利利。他的名声传遍了周围各地。
14Yesu alirudi Galilaya akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, na habari zake zikaenea katika sehemu zote za jirani.
15他在各会堂里教导人,很受众人的尊崇。
15Naye akawa anawafundisha watu katika masunagogi yao, akasifiwa na wote.
16在本乡遭人厌弃(太13:53-58;可6:1-6)耶稣来到拿撒勒自己长大的地方,照着习惯在安息日进入会堂,站起来要读经。
16Basi, Yesu alikwenda Nazareti, mahali alipolelewa, na siku ya Sabato, aliingia katika sunagogi, kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome Maandiko Matakatifu kwa sauti.
17有人把以赛亚先知的书递给他,他展开书卷找到一处,上面写着:
17Akapokea kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na akakuta mahali palipoandikwa:
18“主的灵在我身上,因为他膏我去传福音给贫穷的人,差遣我去宣告被掳的得释放,瞎眼的得看见,受压制的得自由,
18"Roho wa Bwana yu juu yangu, kwani amenipaka mafuta niwahubirie maskini Habari Njema. Amenituma niwatangazie mateka watapata uhuru, vipofu watapata kuona tena; amenituma niwakomboe wanaoonewa,
19又宣告主悦纳人的禧年。”
19na kutangaza mwaka wa neema ya Bwana."
20他把书卷卷好,交还侍役,就坐下。会堂里众人都注视他。
20Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.
21他就对他们说:“这段经文今天应验在你们中间(“中间”原文作“耳中”)了。”
21Naye akaanza kuwaambia, "Andiko hili mlilosikia likisomwa, limetimia leo."
22众人称赞他,希奇他口中所出的恩言,并且说:“这不是约瑟的儿子吗?”
22Wote wakavutiwa sana naye, wakastaajabia maneno mazuri aliyosema. Wakanena, "Je, huyu si mwana wa Yosefu?"
23他说:“你们必向我说这俗语:‘医生,治好你自己吧!’也必说:‘我们听见你在迦百农所行的一切事,也该在你本乡这里行啊!’”
23Naye akawaambia, "Bila shaka mtaniambia msemo huu: Mganga jiponye mwenyewe, na pia mtasema: Yote tuliyosikia umeyafanya kule Kafarnaumu, yafanye hapa pia katika kijiji chako."
24他又说:“我实在告诉你们,没有先知在他本乡是受欢迎的。
24Akaendelea kusema, "Hakika nawaambieni, nabii hatambuliwi katika kijiji chake.
25我对你们说实话,当以利亚的时候,三年六个月不下雨(“不下雨”原文作“天闭塞”),遍地大起饥荒,那时以色列中有许多寡妇,
25Lakini, sikilizeni! Kweli kulikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli nyakati za Eliya. Wakati huo mvua iliacha kunyesha kwa muda wa miaka mitatu na nusu; kukawa na njaa kubwa katika nchi yote.
26以利亚没有奉差遣往他们中间任何一个那里去,只到西顿撒勒法的一个寡妇那里。
26Hata hivyo, Eliya hakutumwa kwa mjane yeyote ila kwa mwanamke mjane wa Sarepta, Sidoni.
27以利沙先知的时候,以色列中有许多患痲风的人,其中除了叙利亚的乃缦,没有一个得洁净的。”
27Tena, katika nchi ya Israeli nyakati za Elisha kulikuwa na wenye ukoma wengi. Hata hivyo, hakuna yeyote aliyetakaswa ila tu Naamani, mwenyeji wa Siria."
28会堂里的众人听见这话,都怒气填胸,
28Wote waliokuwa katika lile sunagogi waliposikia hayo walikasirika sana.
29起来赶他出城(这城原来建在山上),他们拉他到山崖,要把他推下去。
29Wakasimama, wakamtoa nje ya mji wao uliokuwa umejengwa juu ya kilima, wakampeleka mpaka kwenye ukingo wa kilima hicho ili wamtupe chini.
30耶稣却从他们中间走过,就离去了。
30Lakini Yesu akapita katikati yao, akaenda zake.
31在迦百农赶出污灵(可1:21-28)耶稣下到加利利的迦百农城,在安息日教导人。
31Kisha Yesu akashuka mpaka Kafarnaumu katika mkoa wa Galilaya, akawa anawafundisha watu siku ya Sabato.
32他们对他的教训都很惊奇,因为他的话带着权柄。
32Wakastaajabia uwezo aliokuwa nao katika kufundisha.
33会堂里有一个被污鬼附着的人,大声喊叫:
33Na katika lile sunagogi kulikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na roho ya pepo mchafu; akapiga ukelele wa kuziba masikio:
34“哎!拿撒勒人耶稣,我们跟你有什么关系呢?你来毁灭我们吗?我知道你是谁,你是 神的圣者。”
34"We! Yesu wa Nazareti! Kwa nini unatuingilia? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakufahamu wewe ni nani. Wewe ni mjumbe Mtakatifu wa Mungu!"
35耶稣斥责他说:“住口!从他身上出来!”鬼把那人摔倒在众人中间,就从他身上出来了,没有伤害他。
35Lakini Yesu akamkemea huyo pepo akisema: "Nyamaza! Mtoke mtu huyu!" Basi, huyo pepo baada ya kumwangusha yule mtu chini, akamtoka bila kumdhuru hata kidogo.
36众人都惊骇,彼此谈论说:“这是怎么回事?他用权柄能力吩咐污灵,污灵竟出来了。”
36Watu wote wakashangaa, wakawa wanaambiana, "Hili ni jambo la ajabu, maana kwa uwezo na nguvu anawaamuru pepo wachafu watoke, nao wanatoka!"
37耶稣的名声,传遍了周围各地。
37Habari zake zikaenea mahali pote katika mkoa ule.
38治病赶鬼(太8:14-17;可1:29-34)他起身离开会堂,进入西门的家。西门的岳母正在发高热,他们为她求耶稣。
38Yesu alitoka katika lile sunagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa na homa kali; wakamwomba amponye.
39耶稣站在她旁边,斥责那热病,热就退了;她立刻起身服事他们。
39Yesu akaenda akasimama karibu naye, akaikemea ile homa, nayo ikamwacha. Mara yule mama akainuka, akawatumikia.
40日落的时候,不论害什么病的人,都被带到耶稣那里;他一一为他们按手,医好他们。
40Jua lilipokuwa linatua, wote waliokuwa na wagonjwa wao mbalimbali waliwaleta kwake; naye akaweka mikono yake juu ya kila mmoja wao, akawaponya wote.
41又有鬼从好些人身上出来,喊着说:“你是 神的儿子。”耶稣斥责他们,不许他们说话,因为他们知道他是基督。
41Pepo waliwatoka watu wengi, wakapiga kelele wakisema: "Wewe u Mwana wa Mungu!" Lakini Yesu akawakemea, wala hakuwaruhusu kusema, maana walimfahamu kwamba yeye ndiye Kristo.
42往别的城传道(可1:35-39)天一亮,耶稣出来,到旷野地方去。众人寻找他,一直找到他那里,要留住他,不要他离开他们。
42Kesho yake asubuhi Yesu aliondoka akaenda mahali pa faragha. Watu wakawa wanamtafuta, na walipofika mahali alipokuwa, wakajaribu kumzuia ili asiondoke kwao.
43他却说:“我也必须到别的城去传 神国的福音,因为我是为了这缘故奉差遣的。”
43Lakini yeye akawaambia, "Ninapaswa kuhubiri Habari Njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, maana nilitumwa kwa ajili hiyo."
44于是他往犹太的各会堂去传道。
44Akawa anahubiri katika masunagogi ya Yudea.