聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Luke

5

1呼召四个门徒(太4:18-22;可1:16-20;约1:40-42)
1Siku moja Yesu alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti, na watu wengi walikuwa wamemzunguka wakisongana wanalisikiliza neno la Mungu.
2他看见两只船停在湖边,渔夫离开船洗网去了。
2Akaona mashua mbili ukingoni mwa ziwa; wavuvi wenyewe walikuwa wametoka, wanaosha nyavu zao.
3他上了西门的那一只船,请他撑开,离岸不远,就坐下,从船上教导众人。
3Baada ya Yesu kuingia katika mashua moja, iliyokuwa ya Simoni, alimtaka Simoni aisogeze majini, mbali kidogo na ukingo wa ziwa. Akaketi, akafundisha umati wa watu akiwa ndani ya mashua.
4讲完了,就对西门说:“把船开到水深的地方,下网打鱼!”
4Alipomaliza kufundisha, akamwambia Simoni, "Peleka mashua mpaka kilindini, mkatupe nyavu zenu mpate kuvua samaki."
5西门说:“主啊,我们整夜劳苦,毫无所得,不过,我愿照你的话下网。”
5Simoni akamjibu, "Bwana, tumejitahidi kuvua samaki usiku kucha bila kupata kitu, lakini kwa kuwa umesema, nitatupa nyavu."
6他们下了网,就圈住很多鱼,网几乎裂开,
6Baada ya kufanya hivyo, wakavua samaki wengi, hata nyavu zao zikaanza kukatika.
7就招呼另外那只船上的同伴来帮助,他们就来把两只船装满,甚至船要下沉。
7Wakawaita wenzao waliokuwa katika mashua nyingine waje kuwasaidia. Wakaja, wakazijaza mashua zote mbili samaki, hata karibu zingezama.
8西门.彼得看见这种情景,就俯伏在耶稣膝前,说:“主啊,离开我,因为我是个罪人。”
8Simoni Petro alipoona hayo, akapiga magoti mbele ya Yesu akisema, "Ondoka mbele yangu, ee Bwana, kwa kuwa mimi ni mwenye dhambi!"
9他和跟他在一起的人,因这网所打的鱼,都十分惊骇。
9Simoni pamoja na wenzake wote walishangaa kwa kupata samaki wengi vile.
10西门的伙伴,西庇太的儿子雅各、约翰也是这样。耶稣对西门说:“不要怕!从今以后,你要作得人的渔夫了。”
10Hali kadhalika Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, waliokuwa wavuvi wenzake Simoni. Yesu akamwambia Simoni, "Usiogope; tangu sasa utakuwa ukivua watu."
11他们把两只船拢了岸,撇下一切,跟从了耶稣。
11Basi, baada ya kuzileta zile mashua ukingoni mwa ziwa, wakaacha yote, wakamfuata.
12治好痲风病人(太8:2-4;可1:40-45)有一次,耶稣在一个城里,突然有一个满身痲风的人看见他,就把脸伏在地上,求他说:“主啊!如果你肯,必能使我洁净。”
12Ikawa, Yesu alipokuwa katika mmojawapo wa miji ya huko, mtu mmoja mwenye ukoma mwili mzima akamwona. Basi, mtu huyo akaanguka kifudifudi akamwomba Yesu: "Mheshimiwa, ukitaka, waweza kunitakasa."
13耶稣伸手摸他,说:“我肯,你洁净了吧!”痲风立刻离开了他。
13Yesu akaunyosha mkono wake, akamgusa na kusema, "Nataka, takasika!" Mara ule ukoma ukamwacha.
14耶稣嘱咐他不可告诉任何人,“你只要去给祭司检查,并且照着摩西所规定的,为你得洁净献祭,好向大家作证。”
14Yesu akamwamuru: "Usimwambie mtu yeyote; bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, ukatoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama inavyotakiwa na Sheria ya Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona."
15但他的名声却越发传扬出去,成群的人来聚集,要听道,并且要使他们的疾病痊愈。
15Lakini habari za Yesu zilizidi kuenea kila mahali. Watu makundi mengi wakakusanyika ili kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao.
16耶稣却退到旷野去祷告。
16Lakini yeye alikwenda zake mahali pasipo na watu, akawa anasali huko.
17治好瘫子(太9:2-8;可2:3-12)有一天,耶稣正在教导人,法利赛人和律法教师也坐在那里,他们是从加利利和犹太各乡村,并耶路撒冷来的;主的能力与他同在,叫他能医病。
17Siku moja Yesu alikuwa akifundisha. Mafarisayo na walimu wa Sheria kutoka katika kila kijiji cha Galilaya, Yudea na Yerusalemu, walikuwa wameketi hapo. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kwa ajili ya kuponyea wagonjwa.
18有人用床抬着一个瘫子,想送进去,放在耶稣跟前。
18Mara watu wakaja wamemchukua mtu mmoja aliyepooza maungo, amelala kitandani; wakajaribu kumwingiza ndani wamweke mbele ya Yesu.
19因为人多,没有办法进去,就上了房顶,从瓦间把瘫子和床往当中缒下去,正在耶稣跟前。
19Lakini kwa sababu ya wingi wa watu, hawakuweza kuingia ndani. Basi, wakapanda juu ya dari, wakaondoa vigae, wakamshusha huyo aliyepooza pamoja na kitanda chake, wakamweka mbele ya Yesu.
20他看见他们的信心,就说:“朋友(“朋友”原文作“人”),你的罪赦了。”
20Yesu alipoona jinsi walivyokuwa na imani kubwa, akamwambia huyo mtu, "Rafiki, umesamehewa dhambi zako."
21经学家和法利赛人就议论起来,说:“这人是谁,竟然说僭妄的话?除 神一位以外,谁能赦罪呢?”
21Walimu wa Sheria na Mafarisayo wakaanza kujiuliza: "Nani huyu anayemkufuru Mungu kwa maneno yake? Hakuna mtu awezaye kusamehe dhambi ila Mungu peke yake!"
22耶稣知道他们的议论,就对他们说:“你们心里为什么议论呢?
22Yesu alitambua mawazo yao, akawauliza, "Mnawaza nini mioyoni mwenu?
23说:‘你的罪赦了’,或说:‘起来行走’,哪一样容易呢?
23Ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, Umesamehewa dhambi, au kusema, Simama utembee?
24然而为了要你们知道,人子在地上有赦罪的权柄,(他就对瘫子说:)我吩咐你,起来,拿起你的床,回家去吧。”
24Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anao uwezo wa kusamehe dhambi duniani." Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Simama, chukua kitanda chako uende zako nyumbani."
25那人立刻当众起来,拿着他躺过的床,颂赞 神,回家去了。
25Mara, huyo mtu aliyepooza akasimama mbele yao wote, akachukua kitanda chake akaenda zake nyumbani huku akimtukuza Mungu.
26众人都惊奇,颂赞 神,并且十分惧怕,说:“我们今天看见了不平常的事。”
26Wote wakashangaa na kushikwa na hofu; wakamtukuza Mungu wakisema: "Tumeona maajabu leo."
27呼召利未(太9:9-13;可2:14-17)事后,耶稣出去,看见一个税吏,名叫利未,坐在税关那里,就对他说:“来跟从我!”
27Baada ya hayo, Yesu akatoka nje, akamwona mtoza ushuru mmoja aitwaye Lawi, ameketi ofisini. Yesu akamwambia, "Nifuate!"
28他就撇下一切,起来跟从了耶稣。
28Lawi akaacha yote, akamfuata.
29利未在自己家里,为他大摆筵席,有许多税吏和别的人一起吃饭。
29Kisha Lawi akamwandalia Yesu karamu kubwa nyumbani mwake; na kundi kubwa la watoza ushuru na watu wengine walikuwa wameketi pamoja nao.
30法利赛人和经学家埋怨他的门徒,说:“你们为什么跟税吏和罪人一起吃喝呢?”
30Mafarisayo na walimu wa Sheria wakawanung'unikia wafuasi wake wakisema: "Mbona mnakula na kunywa pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?"
31耶稣回答:“健康的人不需要医生,有病的人才需要。
31Yesu akawajibu, "Wenye afya hawahitaji daktari, lakini wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa.
32我来不是要召义人,而是要召罪人悔改。”
32Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi, ili wapate kutubu."
33新旧的比喻(太9:14-17;可2:18-22)他们说:“约翰的门徒常常禁食、祈祷,法利赛人的门徒也是这样,而你的门徒却又吃又喝。”
33Watu wengine wakamwambia Yesu, "Wafuasi wa Yohane mbatizaji hufunga mara nyingi na kusali; hata wafuasi wa Mafarisayo hufanya vivyo hivyo. Lakini wafuasi wako hula na kunywa."
34耶稣说:“新郎跟宾客在一起的时候,你们怎么可以叫宾客禁食呢?
34Yesu akawajibu, "Je, mnaweza kuwataka wale walioalikwa arusini wafunge hali bwana arusi yuko pamoja nao?
35但日子到了,新郎要被取去,离开他们,那一天他们就要禁食了。”
35Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kati yao, na wakati huo ndipo watakapofunga."
36他又对他们设个比喻说:“没有人会从新衣服撕下一块布,补在旧衣服上,如果这样,不但新衣服撕破了,而且新撕下的布,也和旧的不调和。
36Yesu akawaambia mfano huu: "Hakuna mtu akataye kiraka cha nguo mpya na kukitia katika vazi kuukuu; kama akifanya hivyo, atakuwa amelikata hilo vazi jipya, na hicho kiraka hakitachukuana na hilo vazi kuukuu.
37也没有人会把新酒装在旧皮袋里;如果这样,新酒就会把皮袋胀破,不但酒漏掉,皮袋也损坏了;
37Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu; kwani hiyo divai mpya itavipasua hivyo viriba, divai itamwagika, na viriba vitaharibika.
38人总是把新酒装在新皮袋里。
38Divai mpya hutiwa katika viriba vipya!
39喝惯陈酒的人,就不想喝新酒,他总说陈的好。”
39Wala hakuna mtu ambaye hutamani kunywa divai mpya baada ya kunywa ya zamani, kwani husema: Ile ya zamani ni nzuri zaidi."