1葡萄园工人的比喻
1"Ufalme wa mbinguni unafanana na mtu mwenye shamba la mizabibu, ambaye alitoka asubuhi na mapema kuwaajiri wafanyakazi katika shamba lake.
2他和工人讲定了一天的工钱是一个银币,然后派他们到葡萄园去。
2Akapatana nao kuwalipa dinari moja kwa siku, kisha akawapeleka katika shamba lake la mizabibu.
3大约九点钟,他又出去,看见还有人闲站在街市上,
3Akatoka mnamo saa tatu asubuhi, akaona watu wengine wamesimama sokoni, hawana kazi.
4就对他们说:‘你们也到葡萄园来吧,我会给你们合理的工钱。’
4Akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu, nami nitawapeni haki yenu.
5他们就去了。约在正午和下午三点钟,他又出去,也是这样作。
5Basi, wakaenda. Huyo mwenye shamba akatoka tena mnamo saa sita na saa tisa, akafanya vivyo hivyo.
6下午五点钟左右,他再出去,看见还有人站着,就问他们:‘你们为什么整天站在这里不去作工?’
6Hata mnamo saa kumi na moja jioni, akatoka tena; akakuta watu wengine wamesimama pale sokoni. Basi, akawauliza, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
7他们回答:‘没有人用我们。’他说:‘你们也到葡萄园来吧。’
7Wakamjibu: Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Yeye akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu.
8到了黄昏,园主对管工说:‘把工人叫来,给他们工钱,从最后的开始,到最先来的。’
8"Kulipokuchwa, huyo mwenye shamba alimwambia mtunza hazina wake, Waite wafanyakazi ukawalipe mshahara wao, ukianzia na wale walioajiriwa mwisho, na kumalizia na wale wa kwanza.
9那些下午五点钟才开始作工的人来了,每个人都领到一个银币。
9Basi, wakaja wale walioajiriwa mnamo saa kumi na moja, wakapokea kila mmoja dinari moja.
10最先作工的人也来了,以为会多得一点,但每个人也是领到一个银币。
10Wale wa kwanza walipofika, walikuwa wanadhani watapewa zaidi; lakini hata wao wakapewa kila mmoja dinari moja.
11他们领到之后,就埋怨家主,说:
11Wakazipokea fedha zao, wakaanza kumnung'unikia yule bwana.
12‘我们整天在烈日之下劳苦,这些后来的人只工作了一个小时,你却给他们跟我们一样的工钱。’
12Wakasema, Watu hawa walioajiriwa mwisho walifanya kazi kwa muda wa saa moja tu, mbona umetutendea sawa na wao hali sisi tumevumilia kazi ngumu kutwa na jua kali?
13家主回答他们当中的一个,说:‘朋友,我并没有亏待你。你我不是讲定了一个银币吗?
13"Hapo yule bwana akamjibu mmoja wao, Rafiki, sikukupunja kitu! Je, hukupatana nami mshahara wa denari moja?
14拿你的工钱走吧!我给那后来的和给你的一样,是我的主意。
14Chukua haki yako, uende zako. Napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe.
15难道我不可以照自己的主意用我的财物吗?还是因为我仁慈你就嫉妒呢?’
15Je, sina haki ya kufanya na mali yangu nipendavyo? Je, unaona kijicho kwa kuwa mimi ni mwema?"
16因此,在后的将要在前,在前的将要在后。”
16Yesu akamaliza kwa kusema, "Hivyo, walio wa mwisho watakuwa wa kwanza na wa kwanza watakuwa wa mwisho."
17第三次预言受难及复活(可10:32-34;路18:31-34)耶稣上耶路撒冷去的时候,把十二门徒带到一边,对他们说:
17Yesu alipokuwa anakwenda Yerusalemu, aliwachukua wale wanafunzi kumi na wawili faraghani, na njiani akawaambia,
18“我们现在上耶路撒冷去,人子要被交给祭司长和经学家,他们要定他死罪,
18"Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe.
19把他交给外族人凌辱、鞭打,并且钉在十字架上。然而第三天他要复活。”
19Watamkabidhi kwa watu wa mataifa mengine ili adhihakiwe, apigwe viboko na kusulubiwa; lakini siku ya tatu atafufuliwa."
20不是要人服事而是要服事人(可10:35-45)那时,西庇太的儿子的母亲,带着她的两个儿子前来见耶稣。她跪在耶稣面前求他。
20Hapo mama yao wana wa Zebedayo alimjia Yesu pamoja na wanawe, akapiga magoti mbele yake na kumwomba kitu.
21耶稣问她:“你想要什么?”她说:“求你下令,使我这两个儿子在你的国里,一个坐在你的右边,一个坐在你的左边。”
21Yesu akamwuliza, "Unataka nini?" Huyo mama akamwambia, "Ahidi kwamba katika Ufalme wako, hawa wanangu wawili watakaa mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto."
22耶稣回答:“你们不知道你们求的是什么。我将要喝的杯,你们能喝吗?”他们说:“能。”
22Yesu akajibu, "Hamjui mnaomba nini. Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa mimi?" Wakamjibu, "Tunaweza."
23他对他们说:“我的杯你们固然要喝,只是坐在我的左右,不是我可以赐的;我父预备赐给谁,就赐给谁。”
23Yesu akawaambia, "Kweli mtakunywa kikombe changu, lakini kuketi kulia au kushoto kwangu si kazi yangu kupanga; jambo hilo watapewa wale waliowekewa tayari na Baba yangu."
24其他十个门徒听见了,就向他们兄弟二人生气。
24Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakawakasirikia hao ndugu wawili.
25耶稣把他们叫过来,说:“你们知道各国都有元首统治他们,也有官长管辖他们。
25Hivyo Yesu akawaita, akawaambia, "Mnajua kwamba watawala wa mataifa hutawala watu wao kwa mabavu na wakuu hao huwamiliki watu wao.
26但你们中间却不要这样;谁想在你们中间成为大的,就要作你们的仆役;
26Lakini kwenu isiwe hivyo, ila yeyote anayetaka kuwa mkuu kati yenu sharti awe mtumishi wa wote;
27谁想在你们中间为首的,就要作你们的奴仆。
27na anayetaka kuwa wa kwanza kati yenu sharti awe mtumishi wenu.
28正如人子来,不是要受人的服事,而是要服事人,并且要舍命,作许多人的赎价。”
28Jinsi hiyohiyo, Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, bali kutumikia na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi."
29治好瞎眼的人(可10:46-52;路18:35-43)他们从耶利哥出来的时候,有许多人跟着耶稣。
29Yesu alipokuwa anaondoka mjini Yeriko, umati wa watu ulimfuata.
30有两个瞎眼的人坐在路旁,听说耶稣经过,就喊叫:“主啊,大卫的子孙,可怜我们吧!”
30Basi, kulikuwa na vipofu wawili wameketi kando ya njia, na waliposikia kwamba Yesu alikuwa anapitia hapo, walipaaza sauti: "Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!"
31群众责备他们,叫他们不要出声,他们却更加放声喊叫:“主啊,大卫的子孙,可怜我们吧!”
31Ule umati wa watu ukawakemea na kuwaambia wanyamaze. Lakini wao wakazidi kupaaza sauti: "Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!"
32耶稣就站住,叫他们过来,说:“要我为你们作什么呢?”
32Yesu akasimama, akawaita na kuwauliza, "Mnataka niwafanyie nini?"
33他们说:“主啊,求你开我们的眼睛。”
33Wakamjibu, "Mheshimiwa, tunaomba macho yetu yafumbuliwe."
34耶稣就怜悯他们,摸他们的眼睛。他们立刻能看见,就跟从了耶稣。
34Basi, Yesu akawaonea huruma, akawagusa macho yao, na papo hapo wakaweza kuona, wakamfuata.