1骑驴进耶路撒冷(可11:1-10;路19:28-38;约12:12-15)
1Yesu na wanafunzi wake walipokaribia Yerusalemu na kufika Bethfage katika mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
2对他们说:“你们往对面的村子里去,立刻就会看见一头驴拴在那里,还有小驴跟它在一起。把它们解开,牵来给我。
2akawaambia, "Nendeni hadi kijiji kilicho mbele yenu na mtamkuta punda amefungwa na mtoto wake. Wafungueni mkawalete kwangu.
3如果有人问你们,就要说:‘主需要它们。’他会立刻让你们牵走。”
3Kama mtu akiwauliza sababu, mwambieni, Bwana anawahitaji, naye atawaachieni mara."
4这件事应验了先知所说的:
4Jambo hili lilifanyika ili yale yaliyosemwa na nabii yatimie:
5“要对锡安的居民(“居民”原文作“女子”)说:‘看哪,你的王来到你这里了;他是温柔的,他骑着驴,骑的是小驴。’”
5"Uambieni mji wa Sioni: Tazama, Mfalme wako anakujia! Ni mpole na amepanda punda, mwana punda, mtoto wa punda."
6门徒照着耶稣的吩咐去作。
6Hivyo, wale wanafunzi walienda wakafanya kama Yesu alivyowaagiza.
7牵了驴和小驴来,把衣服搭在它们上面,耶稣就骑上。
7Wakamleta yule punda na mtoto wake, wakatandika nguo zao juu yao na Yesu akaketi juu yake.
8有一大群人把自己的衣服铺在路上,也有人从树上把树枝砍下来,铺在路上。
8Umati mkubwa wa watu ukatandaza nguo zao barabarani, na watu wengine wakakata matawi ya miti wakayatandaza barabarani.
9前呼后拥的群众喊叫着:“‘和散那’归于大卫的子孙,奉主名来的是应当称颂的,高天之上当唱‘和散那’。”
9Makundi ya watu waliomtangulia na wale waliomfuata wakapaaza sauti: "Hosana Mwana wa Daudi! Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana! Hosana Mungu juu mbinguni!"
10耶稣进了耶路撒冷,全城都震动起来,他们问:“这人是谁?”
10Yesu alipokuwa anaingia Yerusalemu, mji wote ukajaa ghasia. Watu wakawa wanauliza, "Huyu ni nani?"
11大家都说:“这就是那先知耶稣,是从加利利的拿撒勒来的。”
11Watu katika ule umati wakasema, "Huyu ni nabii Yesu, kutoka Nazareti katika mkoa wa Galilaya."
12洁净圣殿(可11:15-19;路19:45-47;约2:13-22)耶稣进了圣殿,把殿里所有作买卖的人赶走,并推倒找换银钱的人的桌子,和卖鸽子的人的凳子;
12Basi, Yesu akaingia Hekaluni, akawafukuza nje watu waliokuwa wanauza na kununua vitu ndani ya Hekalu; akazipindua meza za wale waliokuwa wanavunja fedha, na viti vya wale waliokuwa wanauza njiwa.
13又对他们说:“经上记着:‘我的殿要称为祷告的殿。’你们竟把它弄成贼窝了。”
13Akawaambia, "Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala. Lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi."
14殿里的瞎子和瘸腿的都走过来,耶稣就医好他们。
14Vipofu na vilema walimwendea huko Hekaluni, naye Yesu akawaponya.
15祭司长和经学家看见耶稣所行的奇事,又看见小孩子在殿中喊叫“‘和散那’归于大卫的子孙”,就很忿怒,
15Basi, makuhani wakuu na walimu wa Sheria walipoyaona maajabu aliyoyafanya Yesu, na pia watoto walipokuwa wanapaaza sauti zao Hekaluni wakisema: "Sifa kwa Mwana wa Daudi," wakakasirika.
16对耶稣说:“你听见他们说什么吗?”耶稣说:“我听见了。’你从小孩和婴儿的口中,得着了赞美。’这话你们没有念过吗?”
16Hivyo wakamwambia, "Je, husikii wanachosema?" Yesu akawajibu, "Naam, nasikia! Je hamjasoma Maandiko haya Matakatifu? Kwa vinywa vya watoto wadogo na wanyonyao unajipatia sifa kamilifu."
17于是离开他们,出了城,来到伯大尼,在那里过了一夜。
17Basi, akawaacha, akatoka nje ya mji na kwenda Bethania, akalala huko.
18咒诅无花果树(可11:12-14、20-24)耶稣清早回城的时候,觉得饿了。
18Yesu alipokuwa anarudi mjini asubuhi na mapema, aliona njaa.
19他看见路旁有一棵无花果树,就走过去;但他在树上什么也找不到,只有叶子,就对树说:“你永远不再结果子了。”那棵树就立刻枯萎。
19Akauona mtini mmoja kando ya njia, akauendea; lakini aliukuta hauma chochote ila majani matupu. Basi akauambia, "Usizae tena matunda milele!" Papo hapo huo mtini ukanyauka.
20门徒看见了,十分惊奇,说:“这棵无花果树是怎样立刻枯萎的呢?”
20Wanafunzi walipouona walishangaa wakisema, "Kwa nini mtini huu umenyauka ghafla?"
21耶稣回答他们:“我实在告诉你们,如果你们有信心,不怀疑,不但能作我对无花果树所作的,就是对这座山说‘移开,投到海里去’,也必成就。
21Yesu akawajibu, "Kweli nawaambieni, kama mkiwa na imani bila kuwa na mashaka, mnaweza si tu kufanya hivyo, bali hata mkiuambia mlima huu: Ng'oka ukajitose baharini, itafanyika hivyo.
22你们祷告,无论求什么,只要相信,都必得着。”
22Na mkiwa na imani, chochote mtakachoomba katika sala, mtapata."
23质问耶稣凭什么权柄作事(可11:27-33;路20:1-8)耶稣进了圣殿,正在教导人的时候,祭司长和民间的长老前来问他:“你凭什么权柄作这些事?谁给你这权柄?”
23Yesu aliingia Hekaluni, akawa anafundisha. Alipokuwa akifundisha, makuhani wakuu na wazee wa watu wakamwuliza, "Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Nani amekupa mamlaka haya?"
24耶稣回答他们:“我也要问你们一句话,如果你们告诉我,我就告诉你们我凭什么权柄作这些事。
24Yesu akawajibu, "Na mimi nitawaulizeni swali moja; mkinijibu, basi nami nitawaambieni ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.
25约翰的洗礼是从哪里来的呢?是从天上来的,还是从人来的呢?”他们就彼此议论:“如果我们说‘是从天上来的’,他会问我们’那你们为什么不信他呢?’
25Je, mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa nani? Je, yalitoka mbinguni ama kwa watu?" Lakini wakajadiliana wao kwa wao hivi: "Tukisema, Yalitoka mbinguni, atatuuliza, Basi, mbona hamkumsadiki?
26如果我们说‘是从人来的’,我们又怕群众,因为他们都认为约翰是先知。”
26Na tukisema, Yalitoka kwa watu, tunaogopa umati wa watu maana wote wanakubali kwamba Yohane ni nabii."
27于是回答耶稣:“我们不知道。”耶稣也对他们说:“我也不告诉你们,我凭什么权柄作这些事。
27Basi, wakamjibu, "Hatujui!" Naye Yesu akawaambia, "Nami pia sitawaambieni ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.
28两个儿子的比喻“你们认为怎样?有一个人,他有两个儿子。他去对大儿子说:‘孩子,你今天到葡萄园去工作吧。’
28"Ninyi mnaonaje; mtu mmoja alikuwa na wana wawili. Akamwambia yule wa kwanza, Mwanangu, leo nenda ukafanye kazi katika shamba la mizabibu.
29他说:‘我不想去。’但后来他改变主意,就去了。
29Yule kijana akamwambia, Sitaki! Lakini baadaye akabadili nia, akaenda kufanya kazi.
30父亲又照样去吩咐小儿子。小儿子说:‘父亲,我会去的。’后来却没有去。
30Yule baba akamwambia mtoto wake wa pili vivyo hivyo, naye akamjibu, Naam baba! Lakini hakwenda kazini.
31这两个儿子,哪一个听父亲的话呢?”他们说:“大儿子。”耶稣对他们说:“我实在告诉你们:税吏和娼妓比你们先进 神的国。
31Je, ni nani kati ya hawa wawili aliyetimiza matakwa ya baba yake?" Wakamjibu, "Yule mtoto wa kwanza." Basi, Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, watoza ushuru na waasherati wataingia katika Ufalme wa Mungu kabla yenu.
32约翰来到你们那里,指示你们行义路(或译:“约翰在义路中,来到你们这里”),你们不信他;税吏和娼妓却信了他。你们看见了之后,还是没有改变心意去信他。
32Maana Yohane alikuja kwenu akawaonyesha njia njema ya kuishi, nanyi hamkumwamini; lakini watoza ushuru na waasherati walimwamini. Hata baada ya kuona hayo yote ninyi hamkubadili mioyo yenu, na hamkusadiki."
33佃户的比喻(可12:1-12;路20:9-19)“你们再听一个比喻:有一个家主,栽种了一个葡萄园,四面围上篱笆,在园子里挖了一个压酒池,盖了一座瞭望台,然后把园子租给佃户,就远行去了。
33Yesu akasema, "Sikilizeni mfano mwingine. Mtu mmoja mwenye nyumba alilima shamba la mizabibu; akalizungushia ukuta, akachimba kisima cha kusindikia divai, akajenga humo mnara pia. Kisha akalikodisha kwa wakulima, akasafiri kwenda nchi ya mbali.
34到了收成的时候,园主派了仆人到佃户那里,收取应该纳给他的果子。
34Wakati wa mavuno ulipofika, aliwatuma watumishi wake kwa wale wakulima, ili wakachukue sehemu ya mavuno yake.
35佃户却抓住他的仆人,打伤一个,杀了一个,又用石头打死一个。
35Wale wakulima wakawakamata hao watumishi; mmoja wakampiga, mwingine wakamwua na mwingine wakampiga mawe.
36于是园主再派其他的仆人去,人数比前一次更多,但佃户也是同样对付他们。
36Huyo mtu akawatuma tena watumishi wengine, wengi kuliko wa safari ya kwanza. Wale wakulima wakawatendea namna ileile.
37最后,他派了自己的儿子去,说:‘他们必尊敬我的儿子。’
37Mwishowe akamtuma mwanawe huku akifikiri: Watamheshimu mwanangu.
38佃户看见他的儿子,就彼此说:‘这是继承产业的;来,我们杀了他,占有他的产业吧!’
38Lakini wale wakulima walipomwona mwanawe wakasemezana wao kwa wao: Huyu ndiye mrithi; na tumuue ili tuuchukue urithi wake!
39于是他们抓住他,把他推出葡萄园外杀了。
39Basi, wakamkamata, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamwua.
40那么,葡萄园的主人来到的时候,会怎样对待那些佃户呢?”
40"Sasa, huyo mwenye shamba la mizabibu atakapokuja, atawafanyaje hao wakulima?"
41他们回答:“他会毫不留情地除掉那些恶人,把葡萄园租给按时缴纳果子的佃户。”
41Wao wakamjibu, "Atawaangamiza vibaya hao waovu, na lile shamba atawapa wakulima wengine ambao watampa sehemu ya mavuno wakati wa mavuno."
42耶稣对他们说:“经上记着:‘建筑工人所弃的石头,成了房角的主要石头;这是主所作的,在我们眼中看为希奇。’这话你们没有念过吗?
42Hapo Yesu akawaambia, "Je, hamkusoma jambo hili katika Maandiko Matakatifu? Jiwe walilokataa waashi sasa limekuwa jiwe kuu la msingi. Bwana ndiye aliyefanya jambo hili, nalo ni la ajabu sana kwetu!
43因此我告诉你们, 神的国要从你们那里取去,赐给那结果子的外族人。
43"Kwa hiyo nawaambieni, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu na kupewa watu wa mataifa mengine wenye kutoa matunda yake."
44谁跌在这石头上,就必摔碎;这石头掉在谁的身上,就必把他压得粉碎。”
44"Atakayeanguka juu ya jiwe hilo atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamponda."
45祭司长和法利赛人听了耶稣这些比喻,知道是指着他们说的。
45Makuhani wakuu na Mafarisayo waliposikia hiyo mifano yake walitambua kwamba alikuwa anawasema wao.
46他们想要逮捕他,但又怕群众,因为他们都认为耶稣是先知。
46Kwa hiyo wakawa wanatafuta njia ya kumtia nguvuni, lakini waliwaogopa watu kwa sababu wao walimtambua yeye kuwa nabii.