1天使与小书卷
1Kisha nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa amevikwa wingu, na upinde wa mvua kichwani mwake. Uso wake ulikuwa kama jua, na miguu yake ilikuwa kama moto.
2手里拿着展开的小书卷。他的右脚踏在海上,左脚踏在地上,
2Mikononi mwake alishika kitabu kidogo kimefunguliwa. Aliweka mguu wake wa kulia juu ya bahari, na wa kushoto juu ya nchi kavu,
3大声呼喊,好像狮子吼叫。他呼喊的时候,就有七雷发声说话。
3na kuita kwa sauti kubwa kama ya mngurumo wa simba. Alipopaaza sauti, ngurumo saba ziliitikia kwa kishindo.
4七雷说话的时候,我正要写下来,就听见有声音从天上出来,说:“七雷所说的你要封住,不可写出来!”
4Na hizo ngurumo saba ziliposema, mimi nikataka kuandika. Lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni: "Maneno ya ngurumo hizo saba ni siri; usiyaandike!"
5我看见那站在海上和地上的天使,向天举起右手来,
5Kisha yule malaika niliyemwona akisimama juu ya bahari na juu ya nchi kavu akainua mkono wake wa kulia juu mbinguni,
6指着那活到永永远远,创造天和天上之物、地和地上之物、海和海中之物的 神起誓,说:“必不再延迟了!
6akaapa kwa jina la Mungu aishiye milele na milele, Mungu aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, bahari na vyote vilivyomo, dunia na vyote vilivyomo. Akasema, "Wakati wa kusubiri zaidi umekwisha!
7到第七位天使吹号的时候, 神向他的仆人众先知所宣告的奥秘,就要实现了。”
7Lakini wakati ule malaika wa saba atakapotoa sauti yake, wakati atakapopiga tarumbeta yake, Mungu atakamilisha mpango wake wa siri kama alivyowatangazia watumishi wake manabii."
8我先前听见那从天上来的声音又对我说:“你去,把那站在海上和地上的天使手中展开的书卷拿过来。”
8Kisha ile sauti niliyokuwa nimeisikia kutoka mbinguni pale awali ikasema nami tena: "Nenda ukakichukue kile kitabu kilichofunguliwa, kilicho mkononi mwa malaika asimamaye juu ya bahari na juu ya nchi kavu."
9我就走到天使那里,请他把小书卷给我。他对我说:“你拿着,吃下去。它必使你肚子苦涩,但是口里却好像蜜一样甘甜。”
9Basi, nikamwendea huyo malaika, nikamwambia anipe hicho kitabu kidogo. Naye akaniambia, "Kichukue, ukile; kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali, lakini tumboni kitakuwa kichungu!"
10我把小书卷从天使手中拿过来,吃了,在口里果然甘甜如蜜;但是吃完之后,我肚子就觉得苦涩。
10Basi, nikakichukua kitabu hicho kidogo kutoka mkononi mwa huyo malaika, nikakila; nacho kilikuwa kitamu kinywani mwangu kama asali, lakini nilipokimeza kikawa kichungu tumboni mwangu.
11他们又对我说:“论到许多民族、邦国、方言和君王,你必须再说预言。”
11Kisha nikaambiwa, "Inakubidi tena kutangaza ujumbe wa Mungu kuhusu watu wengi, mataifa, watu wa lugha nyingi na wafalme!"