聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Revelation

16

1 神忿怒的七碗
1Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka Hekaluni ikiwaambia wale malaika saba, "Nendeni mkamwage mabakuli hayo saba ya ghadhabu ya Mungu duniani."
2第一位天使去了,把碗倒在地上,就有恶性的毒疮,生在那些有兽的记号和拜兽像的人身上。
2Basi, malaika wa kwanza akaenda akamwaga bakuli lake juu ya nchi. Mara madonda mabaya na ya kuumiza sana yakawapata wote waliokuwa na alama ya yule mnyama, na wale walioiabudu sanamu yake.
3第二位天使把碗倒在海里,海水就变成好像死人的血,海里的一切生物都死了。
3Kisha malaika wa pili akamwaga bakuli lake baharini. Nayo bahari ikawa damu tupu kama damu ya mtu aliyekufa, na viumbe vyote hai baharini vikafa.
4第三位天使把碗倒在江河和众水的泉源里,水就变成了血。
4Malaika wa tatu akamwaga bakuli lake katika mito na chemchemi za maji, navyo vikageuka damu.
5我听见掌管众水的天使说:“今在昔在的圣者啊!你这样审判是公义的,
5Nikamsikia malaika msimamizi wa maji akisema, "Ewe mtakatifu, Uliyeko na uliyekuwako! Wewe ni mwenye haki katika hukumu hii uliyotoa.
6因为他们曾流圣徒和先知的血,现在你给他们血喝,这是他们该受的。”
6Maana waliimwaga damu ya watu wako na ya manabii, nawe umewapa damu wainywe; wamestahili hivyo!"
7我又听见祭坛中有声音说:“是的,主啊!全能的 神,你的审判真实、公义!”
7Kisha nikasikia sauti madhabahuni ikisema, "Naam, Bwana Mungu Mwenye Uwezo! Hukumu zako ni za kweli na haki!"
8第四位天使把碗倒在太阳上,太阳就得了能力,可以用火烤人。
8Kisha malaika wa nne akamwaga bakuli lake juu ya jua. Jua likapewa nguvu ya kuwachoma watu kwa moto wake.
9人被高热烧烤,就亵渎那有权柄掌管这些灾难的 神的名,并不悔改,把荣耀归给他。
9Basi, watu wakaunguzwa vibaya sana; wakamtukana Mungu aliye na uwezo juu ya mabaa hayo makubwa. Lakini hawakuziacha dhambi zao na kumtukuza Mungu.
10第五位天使把碗倒在兽的座位上,兽的国就黑暗了。人因为痛苦就咬自己的舌头。
10Kisha malaika wa tano akamwaga bakuli lake juu ya makao makuu ya yule mnyama. Giza likauvamia utawala wake, watu wakauma ndimi zao kwa sababu za maumivu,
11他们又因为所受的痛苦和所生的疮,亵渎天上的 神,并不为自己所作的悔改。
11wakamtukana Mungu wa mbinguni kwa sababu ya maumivu yao na madonda yao. Lakini hawakuyaacha matendo yao mabaya.
12第六位天使把碗倒在幼发拉底大河上,河水就干了,为了要给那些从东方来的王预备道路。
12Kisha malaika wa sita akamwaga bakuli lake juu ya mto mkubwa uitwao Eufrate. Maji yake yakakauka, na hivyo njia ilitengenezwa kwa ajili ya wafalme wa mashariki.
13我看见三个污灵,好像青蛙从龙口、兽口和假先知的口中出来。
13Kisha nikaona pepo wabaya watatu walio kama vyura, wakitoka kinywani mwa yule joka, kinywani mwa yule mnyama, na kinywani mwa yule nabii wa uongo.
14他们原是鬼魔的灵,施行奇事;它们到普天下的众王那里去,叫他们在全能 神的大日聚集作战。
14Hawa ndio roho za pepo wafanyao miujiza. Ndio wanaokwenda kwa wafalme wa ulimwengu wote na kuwakusanya pamoja kwa ajili ya vita kuu Siku ile ya Mungu Mwenye Uwezo.
15(看哪,我来像贼一样!那警醒、看守自己衣服的是有福的!他就不至于赤身行走,让人看见他的羞耻。)
15"Sikiliza! Mimi naja kama mwizi! Heri mtu akeshaye na kuvaa nguo zake ili asije akaenda uchi huko na huko mbele ya watu."
16污灵就把众王聚集在一个地方,希伯来话叫哈米吉多顿。
16Basi, roho hao wakawakusanya hao wafalme mahali paitwapo kwa Kiebrania Harmagedoni.
17第七位天使把碗倒在空中,就有大声音从圣所的宝座上发出来,说:“成了!”
17Kisha malaika wa saba akamwaga bakuli lake hewani. Sauti kubwa ikasikika kutoka kwenye kiti cha enzi, Hekaluni, ikisema, "Mwisho umefika!"
18于是有闪电、响声、雷轰和大地震,自从地上有人以来,没发生过这么大的地震,
18Kukatokea umeme, kelele, ngurumo na tetemeko kubwa la ardhi ambalo halijapata kutokea tangu Mungu alipomuumba mtu.
19那大城裂为三段,列国的城也都倒塌了。 神也想起巴比伦大城来,要把自己烈怒的酒杯递给它。
19Mji ule mkuu ukapasuliwa sehemu tatu, nayo miji ya mataifa ikateketea. Babuloni, mji mkuu, haukusahauliwa na Mungu. Aliunywesha kikombe cha divai ya ghadhabu yake kuu.
20各海岛都逃避了,众山也不见了。
20Visiwa vyote vikatoweka, nayo milima haikuonekena tena.
21有大冰雹从天上落在人的身上,每块重约四十公斤。由于这冰雹的灾,人就亵渎 神,因为这灾太严重了。
21Mvua ya mawe makubwa yenye uzito wa kama kilo hamsini kila moja, ikawanyeshea watu. Nao wakamtukana Mungu kwa sababu ya mapigo ya mvua hiyo ya mawe. Naam, pigo la mvua hiyo ya mawe lilikuwa kubwa mno.