聖經新譯本 (Simplified)

Swahili: New Testament

Revelation

19

1这些事以后,我听见天上好像有一大群人大声说:“哈利路亚!救恩、荣耀、权能都属于我们的 神,
1Baada ya hayo nikasikia kitu kama sauti kubwa ya umati wa watu wengi mbinguni ikisema, "Haleluya! Ukombozi, utukufu na nguvu ni mali yake Mungu wetu!
2因为他的审判是真实公义的。他审判了那大淫妇,那以淫乱败坏了世界的;并且为他的仆人向淫妇伸了流血的冤。”
2Maana hukumu yake ni ya kweli na ya haki. Amemhukumu yule mzinzi mkuu ambaye alikuwa ameipotosha dunia kwa uzinzi wake. Amemwadhibu kwa sababu ya kumwaga damu ya watumishi wake!"
3他们再一次说:“哈利路亚!烧淫妇的烟往上冒,直到永永远远!”
3Wakasema, "Asifiwe Mungu! Moshi wa moto unaoteketeza mji huo utapanda juu milele na milele!"
4那二十四位长老和四个活物,就俯伏敬拜那坐在宝座上的 神,说:“阿们!哈利路亚!”
4Na wale wazee ishirini na wanne, na vile viumbe hai vinne, wakajitupa chini, wakamwabudu Mungu aliyeketi juu ya kiti cha enzi wakisema, "Amina! Asifiwe Mungu!"
5羊羔的婚筵接着有声音从宝座发出来,说:“所有 神的仆人哪!凡是敬畏他的,无论大小,你们都应当赞美我们的 神!”
5Kisha kukatokea sauti kwenye kiti cha enzi: "Msifuni Mungu enyi watumishi wake wote, nyote mnaomcha, wadogo kwa wakubwa."
6我又听见一个声音,好像一大群人的声音,像众水的声音,又像大雷的声音,说:“哈利路亚!因为主、我们全能的 神作王了!
6Kisha nikasikia kitu kama sauti ya umati mkubwa wa watu na sauti ya maji mengi na ya ngurumo kubwa, ikisema, "Haleluya! Maana Bwana Mungu wetu Mwenye Uwezo ni Mfalme!
7我们要欢喜快乐,把荣耀归给他!因为羊羔的婚期到了;他的新娘也自己预备好了。
7Tufurahi na kushangilia; tumtukuze, kwani wakati wa arusi ya Mwanakondoo umefika, na bibi arusi yuko tayari.
8并且有光洁的细麻衣,赐给她穿上;这细麻衣就是圣徒的义行。”
8Amepewa uwezo wa kujivalia nguo ya kitani safi, iliyotakata na yenye kung'aa!" (Nguo hiyo ya kitani safi ni matendo mema ya watu wa Mungu.)
9天使对我说:“你要写下来:‘被邀请赴羊羔婚筵的人有福了!’”他又对我说:“这都是 神真实的话。”
9Kisha malaika akaniambia, "Andika haya: Heri wale walioalikwa kwenye karamu ya arusi ya Mwanakondoo!" Tena akaniambia, "Hayo ni maneno ya kweli ya Mungu."
10我就俯伏在天使脚前要拜他。但他对我说:“千万不可以这样!我和你,以及你那些为耶稣作见证的弟兄,都是同作仆人的。你应当敬拜 神!因为预言的精义,就是耶稣的见证。”
10Basi, mimi nikaanguka kifudifudi mbele ya miguu yake nikataka kumwabudu. Lakini yeye akaniambia, "Acha! Mimi ni mtumishi tu kama wewe na ndugu zako; sote tunauzingatia ukweli ule alioufunua Yesu. Mwabudu Mungu! Maana ukweli alioufunua Yesu ndio unaowaangazia manabii."
11骑白马的基督我观看,见天开了。有一匹白马,那骑马的称为“忠信”和“真实”;他按着公义审判和作战。
11Kisha nikaona mbingu zimefunguliwa; na huko alikuwako farasi mmoja mweupe, na mpanda farasi wake aliitwa "Mwaminifu" na "Kweli". Huyo huhukumu na kupigana kwa ajili ya haki.
12他的眼睛好像火焰,头上戴着许多皇冠,他身上写着一个名字,这名字除了他自己没有人认识。
12Macho yake ni kama mwali wa moto, na alikuwa amevaa taji nyingi kichwani. Alikuwa ameandikwa jina ambalo hakuna mtu alijuaye isipokuwa tu yeye mwenyewe.
13他身穿一件浸过血的衣服,他的名字称为“ 神的道”。
13Alikuwa amevaa vazi lililokuwa limelowekwa katika damu. Na jina lake huyo ni "Neno la Mungu."
14天上的众军,都骑着白马,穿着洁白的细麻衣,跟随着他。
14Majeshi ya mbinguni yalimfuata yakiwa yamepanda farasi weupe na walikuwa wamevaa mavazi ya kitani, meupe na safi.
15有一把利剑从他口中吐出来,他要用这剑击打列国,他必用铁杖治理他们;并且还要踹全能 神烈怒的压酒池。
15Upanga mkali hutoka kinywani mwake, na kwa upanga huo atawashinda mataifa. Yeye ndiye atakayetawala kwa fimbo ya chuma na kuikamua divai katika chombo cha kukamulia zabibu za ghadhabu kuu ya Mungu Mwenye Uwezo.
16在他的衣服和大腿上,写着“万王之王,万主之主”的名号。
16Juu ya vazi lake, na juu ya mguu wake, alikuwa ameandikwa jina: "Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana."
17我又看见一位天使站在太阳中,向高空所有的飞鸟大声呼喊说:“你们来吧!齐集起来赴 神的大筵席!
17Kisha nikamwona malaika mmoja amesimama katika jua. Akapaaza sauti na kuwaambia ndege wote waliokuwa wanaruka juu angani, "Njoni! Kusanyikeni pamoja kwa karamu kuu ya Mungu.
18可以吃君王的肉、将领的肉、壮士的肉,马和骑士的肉,以及自由的、作奴隶的、大的、小的,所有人的肉。”
18Njoni mkaitafune miili ya wafalme, ya majemadari, ya watu wenye nguvu, ya farasi na wapanda farasi wao; njoni mkaitafune miili ya watu wote: walio huru na watumwa, wadogo na wakubwa."
19我看见那兽和地上的众王,以及他们的众军,都集合起来,要跟那骑白马的和他的众军作战。
19Kisha nikaona yule mnyama pamoja na mfalme wa dunia na askari wao wamekusanyika pamoja kusudi wapigane na yule aliyekuwa ameketi juu ya farasi, pamoja na jeshi lake.
20那兽被捉住了;连同在兽面前用奇事迷惑人,使他们接受兽的记号,并且拜兽像的那假先知,也一起被捉住了。他们两个就活活地被拋在烧着硫磺的火湖里去。
20Lakini huyo mnyama akachukuliwa mateka, pamoja na nabii wa uongo aliyekuwa akifanya miujiza mbele yake. (Kwa miujiza hiyo, alikuwa amewapotosha wale waliokuwa na chapa ya huyo mnyama, na ambao walikuwa wameiabudu sanamu yake.) Huyo mnyama pamoja na huyo nabii walitupwa wote wawili, wakiwa wazimawazima, ndani ya ziwa linalowaka moto wa kiberiti.
21其余的人都被那位骑白马的口中所吐出来的剑杀了。所有飞鸟都吃饱了他们的肉。
21Majeshi yao yaliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa yule anayepanda farasi. Ndege wote wakajishibisha kwa nyama zao.