Chamorro: Psalms, Gospels, Acts

Swahili: New Testament

Acts

1

1Y finenana na sinangan, jutugue, O Teofilo, pot todo ayo sija, na si Jesus jatutujon fumatinas, yan mamanagüe.
1Ndugu Theofilo, Katika kitabu cha kwanza niliandika juu ya mambo yote Yesu aliyotenda na kufundisha tangu mwanzo wa kazi yake
2Asta y jaane anae maresibe gui sanjilo, despues di munjayan jatago pot y Espiritu Santo y apostoles sija ni y inayegña:
2mpaka siku ile alipochukuliwa mbinguni. Kabla ya kuchukuliwa mbinguni aliwapa maagizo kwa njia ya Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua.
3Ni ayo locue y jafanue nu güiya lalâlâ, anae munjayan mapinito pot y megae na señat, liniiñija cuarenta na jaane yan manguecuentos güinaja sija ni y mangaegue gui raenon Yuus:
3Kwa muda wa siku arobaini baada ya kifo chake aliwatokea mara nyingi kwa namna ambazo zilithibitisha kabisa kwamba alikuwa hai. Walimwona, naye aliongea nao juu ya ufalme wa Mungu.
4Ya mandaña yan sija, ya jatago sija na chañija fanjajanao Jerusalem, lao ujanangga y promesan y Tata ni y, ilegña, injingog guiya guajo:
4Wakati walipokutana pamoja aliwaamuru hivi: "Msiondoke Yerusalemu, bali ngojeeni ile zawadi aliyoahidi Baba, zawadi ambayo mlikwisha nisikia nikiongea juu yake.
5Sa si Juan magajet na managpapange ni y janom: lao jamyo infanmatagpange ni y Espiritu Santo ti megae na jaane desde pago.
5Kwani Yohane alibatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache, ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu."
6¶ Enao mina, ayo sija y mandaña, finaesen güe, ilegñija: Señot, malago jao unnatalo guato y raeno guiya Israel?
6Basi, mitume walipokutana pamoja na Yesu, walimwuliza, "Je Bwana, wakati huu ndipo utakaporudisha ule ufalme kwa Israeli?"
7Ya güiya ilegña nu sija: Ti para jamyo intingo y jaane yan y tiempo sija, ni y pinelon y Tata gui ninasiñañaja.
7Lakini Yesu akawaambia, "Nyakati na majira ya mambo hayo viko chini ya mamlaka ya Baba yangu, wala si shauri lenu kujua yatakuwa lini.
8Lao jamyo infanmanresibe y ninasiña anae si Espiritu Santo ufato gui jilo miyo: yan jamyo utestigojo sija, iya Jerusalem yan todo iya Judea yan Samaria, yan asta y uttimon y tano.
8Lakini wakati Roho Mtakatifu atakapowashukieni ninyi, mtajazwa nguvu na mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika nchi yote ya Yudea na Samaria, na hata miisho ya dunia."
9Ya anae munjayan jasangan este na güinaja, mientras maaatan güe, machule güe gui sanjilo; ya y mapagajes rinesibe güe, guinen liniiñija.
9Baada ya kusema hayo, wote wakiwa wanamtazama, alichukuliwa mbinguni; wingu likamficha wasimwone tena.
10Ya anae maaatan fitme y langet, anae mapos güe, estagüe dos taotao na minagagon ápaca, manotojgue jijot guiya sija.
10Walipokuwa bado wanatazama juu angani, akiwa anakwenda zake, mara watu wawili waliokuwa wamevaa nguo nyeupe walisimama karibu nao,
11Ni y ilegñija locue: Jamyo taotao Galilea, jafa na manotojgue jamyo ya inaatan julo y langet? este mismo si Jesus ni y maresibe gui sanjilo guinen iya jamyo para y langet, umamaela talo taegüijeja anae inlie güe jumanao para y langet.
11wakasema, "Enyi wananchi wa Galilaya! Mbona mnasimama mkitazama angani? Yesu huyu ambaye amechukuliwa kutoka kwenu kwenda mbinguni atakuja tena namna hiyohiyo mliivyomwona akienda mbinguni."
12¶ Ayo nae sija manalo guato Jerusalem guinen y egso Olibo, ni y jijot Jerusalem, gui sabado na jaana na jinanao.
12Kisha mitume wakarudi Yerusalemu kutoka mlima wa Mizeituni ulioko karibu kilomita moja kutoka mjini.
13Ya anae sija manjalom, manjanao julo gui sanjilo na cuarto anae mañasaga todos, si Pedro yan si Juan yan si Santiago yan si Andres yan si Felipe yan si Tomas yan si Bartolome yan si Mateo yan si Santiago lajin Alfeo yan si Simon Selote yan si Judas chelun Santiago.
13Walipofika mjini waliingia katika chumba ghorofani ambamo walikuwa wanakaa; nao walikuwa Petro, Yohane, Yakobo, Andrea, Filipo na Thoma, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda mwana wa Yakobo.
14Estesija todo mañasagaja gui un jinasoja na tinaetae, yan manmangagagao fitme, yan y palo famalaoan sija yan si Maria nanan Jesus, yan y mañeluña lalaje sija.
14Hawa wote walikusanyika pamoja kusali, pamoja na wanawake kadha wa kadha, na Maria mama yake Yesu, na ndugu zake.
15¶ Ya ayo sija na jaane, si Pedro tumojgue julo gui entalo y mañelo, ya y numeron y mandaña guaja siento y bente. Ya ilegña:
15Siku chache baadaye, kulikuwa na mkutano wa waumini, karibu watu mia moja na ishirini. Petro alisimama mbele yao,
16Lalaje an mañelo, nesesita umacumple este na tinigue ni y jasangan antes y Espiritu Santo gui pachot David pot si Judas ni umesgaejon ayo sija y cumone si Jesus.
16akasema, "Ndugu zangu, ilikuwa lazima ile sehemu ya Maandiko Matakatifu itimie, sehemu ambayo Roho Mtakatifu, kwa maneno ya Daudi, alibashiri habari za Yuda ambaye aliwaongoza wale waliomtia Yesu nguvuni.
17Sa güiya estaba matufong guiya jita, yan guaja patteña güine na sinetbe.
17Yuda alikuwa mmoja wa kikundi chetu maana alichaguliwa ashiriki huduma yetu.
18Este na taotao, mamajan un fangualuan ni y apas y tinaelayeña; ya japodong papa y mapta tiyanña, ya malagnos todo tilipasña.
18("Mnajua kwamba yeye alinunua shamba kwa zile fedha alizopata kutokana na kitendo chake kiovu. Akaanguka chini, akapasuka na matumbo yake yakamwagika nje.
19Ya este matungo todo ni y mañasaga guiya Jerusalem; ya pot enao na mafanaan ayo na fangualuan ni y finoñija: Aqueldama, comequeilegña, Fangualuan jâgâ.
19Kila mtu katika Yerusalemu alisikia habari za tukio hilo na hivyo, kwa lugha yao, wakaliita lile shamba Hekeli Dama, maana yake, Shamba la Damu.)
20Sa esta matugue gui leblon y Salmos: Polo ya y sagaña umayulang ya taya taotao sumagaye: ya y ofisioña otro chumule.
20Basi, imeandikwa katika kitabu cha Zaburi: Nyumba yake ibaki mahame; mtu yeyote asiishi ndani yake. Tena imeandikwa: Mtu mwingine achukue nafasi yake katika huduma hiyo.
21Gui entalo estesija na taotao y mangachochongta todo y tiempo anae y Señot Jesus jumalom yan jumuyong guiya jita,
21Kwa hiyo, ni lazima mtu mwingine ajiunge nasi kama shahidi wa ufufuo wake Bwana Yesu.
22Matutujon guinen y tinagpangen Juan asta ayo na jaane anae maresibe gui sanjilo guinen iya jita, nesesita uno gui entalo sija umatancho testigo yan jita ni y quinajuluña.
22Anapaswa kuwa mmoja wa wale waliokuwa katika kundi letu wakati wote Bwana alipokuwa anasafiri pamoja nasi, tangu wakati Yohane alipokuwa anabatiza mpaka siku ile Yesu alipochukuliwa kutoka kwetu kwenda mbinguni."
23Ya matancho dos, si José ni y mafanaan Barsabas ni y apiyiduña Justo, yan si Matias.
23Basi, wakataja majina ya watu wawili; wa kwanza Yosefu aliyeitwa Barsaba (au pia Yusto), na wa pili Mathia.
24Ya manmanaetae ilegñija: Jago Señot ni y tumungo y corason y taotao todo, famanue jaye güine gui dos unayeg.
24Kisha wakasali: "Bwana, wewe unajua mioyo ya watu wote. Hivyo, utuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua
25Para usaouao güine na sinetbe, yan y chechon apostoles anae si Judas ni y podong pot y tinaelayeña, ya güiya ujanao para y sagaña.
25ili achukue nafasi hii ya huduma ya kitume aliyoacha Yuda akaenda mahali pake mwenyewe."
26Ya manmanae ni y suertenñija; ya y suerte podong gui as Matias; ya güiya matufong gui onse na apostoles.
26Hapo, wakapiga kura; kura ikampata Mathia, naye akaongezwa katika idadi ya wale mitume wengine kumi na mmoja.