1DESPUES di manmalofan estesija, jafanue gue si Jesus otro biaje y disipulo sija gui oriyan tasen Tiberias; ya taegüine jafanue güe namaesa.
1Baada ya hayo Yesu aliwatokea tena wanafunzi wake kando ya ziwa Tiberia. Aliwatokea hivi:
2Mangaegue mandadaña si Simon Pedro yan si Tomas, na mafananaan si Didimo, yan si Nataniel, taotao Cana guiya Galilea, yan y famaguon Sebedeo, yan otro dos disipuluña.
2Simoni Petro, Thoma (aitwaye Pacha), na Nathanieli mwenyeji wa Kana Galilaya, wana wawili wa Zebedayo na wanafunzi wake wengine wawili, walikuwa wote pamoja.
3Ylegña nu sija si Simon Pedro: Jujanao para jucone y güijan. Ylegñija nu güiya: Jame indalalag jao. Manmapos ya manjalom gui un sajyan; ya ayo na puenge, taya quineneñija.
3Simoni Petro aliwaambia, "Nakwenda kuvua samaki." Nao wakamwambia, "Nasi tutafuatana nawe." Basi, wakaenda, wakapanda mashua, lakini usiku huo hawakupata chochote.
4Anae manana gui egaan si Jesus sumaga tomotojgue gui oriyan tase; ya y disipulo ti matungo cao güiya si Jesus.
4Kulipoanza kupambazuka, Yesu alisimama kando ya ziwa, lakini wanafunzi hawakujua kwamba alikuwa yeye.
5Ayo nae ilegña nu sija si Jesus: Famaguon, guaja jamyo jafa para incano? Manope güe: Taya.
5Basi, Yesu akawauliza, "Vijana, hamjapata samaki wowote sio?" Wao wakamjibu, "La! Hatujapata kitu."
6Ya ilegña nu sija: Yute y lagua gui agapan y sajyan, ya inseda. Mayute ya ti manasiña machule gui tase pot y minegae y güijan.
6Yesu akawaambia, "Tupeni wavu upande wa kulia wa mashua nanyi mtapata samaki." Basi, wakatupa wavu lakini sasa hawakuweza kuuvuta tena kwa wingi wa samaki.
7Ayo na disipulo y güinaeya as Jesus, umadingane si Pedro: Güiya y Señot. Entonses si Simon Pedro anae jajungog na güiya y Señot jadudog güe nu y magagon pescadot (sa taemagago güe), ya tumayog gui tase.
7Hapo yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akamwambia Petro, "Ni Bwana!" Simoni Petro aliposikia ya kuwa ni Bwana, akajifunga vazi lake (maana hakuwa amelivaa), akarukia majini.
8Ya y palo disipulo sija manmato yan y sajyan (sa ti chago gui tano, lao guaja dosientos codo) machule y lagua, na bula ni güijan.
8Lakini wale wanafunzi wengine walikuja pwani kwa mashua huku wanauvuta wavu uliojaa samaki; hawakuwa mbali na nchi kavu, ila walikuwa yapata mita mia moja kutoka ukingoni.
9Ya anae manmato gui tano manmanlie guafe y pinigan na mapolo esta y güijan gui jiloña, yan pan.
9Walipofika nchi kavu waliona moto wa makaa umewashwa na juu yake pamewekwa samaki na mkate.
10Ylegña si Jesus nu sija: Chule mague y güijan ni inquene pago.
10Yesu akawaambia, "Leteni hapa baadhi ya samaki mliovua."
11Ayo anae cajulo si Simon Pedro ya jajala y lagua para y tano, bula dangculon güijan sija, siento y sincuenta y tres; ya achogja taegüenao y minegaeña, y lagua ti matitig.
11Basi, Simoni Petro akapanda mashuani, akavuta hadi nchi kavu ule wavu uliokuwa umejaa samaki wakubwa mia moja na hamsini na watatu. Na ingawa walikuwa wengi hivyo wavu haukukatika.
12Ylegña nu sija si Jesus: Fanmamaela ya infañocho. Ya ni uno gui disipulo sija fumaesen güe: Jago, jaye jao? matungo na güiya y Señot.
12Yesu akawaambia, "Njoni mkafungue kinywa." Hakuna hata mmoja wao aliyethubutu kumwuliza: "Wewe ni nani?" Maana walijua alikuwa Bwana.
13Entonses mamaela si Jesus, ya jachule y pan ya manninae, ya y güijan taegüenao.
13Yesu akaja, akatwaa mkate akawapa; akafanya vivyo hivyo na wale samaki.
14Esta güiya y mina tres na biaje na si Jesus jafanue güe y disipuluña desde tiempo nae cajulo güe guine entalo manmatae.
14Hii ilikuwa mara ya tatu Yesu kuwatokea wanafunzi wake baada ya kufufuka kutoka wafu.
15¶ Anae munjayan mañocho, si Jesus ilegña as Simon Pedro: Simon lajin Juan, unguaeya yo mas qui este sija? Sinangane güe: Si Señot, jago tumungo na juguaeya jao. Ylegña nu güiya: Pasto y gajo patgon quinilo.
15Walipokwisha kula, Yesu alimwuliza Simoni Petro, "Simoni, mwana wa Yohane! Je, wanipenda mimi zaidi kuliko hawa?" Naye akajibu, "Naam, Bwana; wajua kwamba mimi nakupenda." Yesu akamwambia, "Tunza wana kondoo wangu."
16Tumalo ilegña nu güiya y mina dos biaje: Simon, lajin Juan, unguaeya yo? Ylegña nu güiya: Si Señot, untungoja na juguflie jao. Ylegña nu güiya: Adaje y gajo quinilo.
16Kisha akamwambia mara ya pili, "Simoni mwana wa Yohane! Je, wanipenda?" Petro akamjibu, "Naam, Bwana; wajua kwamba nakupenda." Yesu akamwambia, "Tunza kondoo wangu."
17Ylegña nu güiya y mina tres na biaje: Simon, lajin Juan, unguflie yo? Ninatriste si Pedro na sinangane güe asta tres biaje: Unguflie yo? ya ilegña nu güiya: Señot, jago tumungo todosija: jago tumungo na juguflie jao. Ylegña nu güiya si Jesus: Pasto y gajo quinilo.
17Akamwuliza mara ya tatu, "Simoni mwana wa Yohane! Je, wanipenda?" Hapo Petro akahuzunika kwa sababu alimwuliza mara ya tatu: "Wanipenda?" akamwambia, "Bwana, wewe wajua yote; wewe wajua kwamba mimi nakupenda." Yesu akamwambia, "Tunza kondoo wangu!
18Magajet ya magajet jusangane jao, anae patgon jao, undudog jao nu y sentura ya malag y malagomoja: ya anae bijo jao unjuto y canaemo, ya guinede jao ni y otro, ya unquinene guato gui ti malagomo.
18Kweli nakwambia, ulipokuwa kijana ulizoea kujifunga mshipi na kwenda kokote ulikotaka. Lakini utakapokuwa mzee utanyosha mikono yako, na mtu mwingine atakufunga na kukupeleka usikopenda kwenda."
19Ya este ilegña, janatungo jafa na finatae nae siña namalag si Yuus. Ya anae jasangan este, ilegña nu güiya: Dalalag yo.
19(Kwa kusema hivyo, alionyesha jinsi Petro atakavyokufa na kumtukuza Mungu.) Kisha akamwambia, "Nifuate."
20Entonses jabira güe si Pedro ya jalie ayo na disipulo na güinaeya as Jesus dinalalag güe; ya locue umason gui pichon gui sena, ya sinangane, Señot jaye uje y umentregao?
20Hapo Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda, anafuata (Huyu mwanafunzi ndiye yule ambaye wakati wa chakula cha jioni, alikaa karibu sana na Yesu na kumwuliza: "Bwana ni nani atakayekusaliti?")
21Anae si Pedro jalie este, ilegña as Jesus: Señot, jafa jumuyong para este?
21Basi, Petro alipomwona huyo akamwuliza Yesu, "Bwana, na huyu je?"
22Yegña nu güiya si Jesus: Yaguin malagojo na güiya ugagaegue asta qui mato yo, jafa y uguaja guiya jago? Dalalag yo.
22Yesu akamjibu, "Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, yakuhusu nini? Wewe nifuate mimi."
23Jumuyong este na sinangan entre y mañelo na ayo na disipulo ti umatae: lao si Jesus sinangane, na ti umatae; lao yaguin malagoyo na güiya ugagaegue asta qui mato yo, jafa y uguaja guiya jago?
23Basi, habari hiyo ikaenea miongoni mwa wale ndugu kwamba mwanafunzi huyo hafi. Lakini Yesu hakumwambia kwamba mwanafunzi huyo hafi, ila, "Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, yakuhusu nini?"
24¶ Este güiya y disipulo ni manae testimonio nu este sija na güinaja, ya jatugue este sija na güinaja: ya tatungo na y testimonioña, güiya magajet.
24Huyo ndiye yule aliyeshuhudia mambo haya na kuyaandika. Nasi twajua kwamba aliyoyasema ni kweli.
25¶ Ya guaja locue palo megae na güinaja na jafatinas si Jesus, yaguin ufanmangue cada uno, jujaso na todo y tano ti omlat y leblo sija y ufanmatugue. Amen.
25Kuna mambo mengine mengi aliyofanya Yesu, ambayo kama yangeandikwa yote, moja baada ya lingine, nadhani hata ulimwengu wenyewe usingetosha kuviweka vitabu ambavyo vingeandikwa.