Chamorro: Psalms, Gospels, Acts

Swahili: New Testament

Acts

11

1YA y apostoles yan y mañelo ni y manestaba Judea, jajungog na y Gentiles jaresibe locue y sinangan Yuus.
1Mitume na ndugu kule Yudea walisikia kwamba watu wa mataifa mengine pia walikuwa wamelipokea neno la Mungu.
2Ya anae mato si Pedro Jerusalem, managuaguat yan ayo sija y manmansirconsisida,
2Basi, Petro aliporudi Yerusalemu, wale Wayahudi waumini waliopendelea watu wa mataifa mengine watahiriwe, walimlaumu wakisema:
3Ilegñija: Jago jumajalom jao gui ti manmasirconsida, yan manjajamyo mañocho.
3"Wewe umekwenda kukaa na watu wasiotahiriwa na hata umekula pamoja nao!
4Lao si Pedro jasigue sumangane sija claro y sinesede, ilegña:
4Hapo Petro akawaeleza kinaganaga juu ya yale yaliyotendeka tangu mwanzo:
5Estabayo gui siuda guiya Joppe na mananaetae; ya anae lalangoyo, julie y vision, un nayan tumunog, taegüije y dangculo na sabanas, ni mapolo pot cuatro punta ni y tumunog guinin y langet; ya mato guiya guajo:
5"Siku moja nikiwa nasali mjini Yopa, niliona maono; niliona kitu kama shuka kubwa likishushwa chini kutoka mbinguni likiwa limeshikwa pembe zake nne, likawekwa kando yangu.
6Ya anae juatan ayo, ya jujaso, julie y cuatro patasña na gâgâ gui tano, yan manmachaleg sija na gâgâ, yan y mangucunanaf na gâgâ, yan y pajaro sija gui aire.
6Nilichungulia ndani kwa makini nikaona wanyama wenye miguu minne, wanyama wa mwituni, wanyama watambaao na ndege wa angani.
7Ya jujungog locue y inagang na ilegña nu guajo: Cajulo Pedro; puno ya uncano.
7Kisha nikasikia sauti ikiniambia: Petro amka, chinja, ule.
8Lao ilegco: Aje, Señot: sa taya comun, pat áplacha guinin jumalom gui jalom pachotjo.
8Lakini mimi nikasema: La, Bwana; maana chochote kilicho najisi au kichafu hakijapata kamwe kuingia kinywani mwangu.
9Lao jaopeyo talo y inagang guinin y langet, ilegña: Jafa y janagasgas si Yuus, chamo fumatitinas comun.
9Ile sauti ikasikika tena kutoka mbinguni: Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa.
10Ya este mafatinas tres biaje: ya todo manmachule talo guato gui langet.
10Jambo hilo lilifanyika mara tatu, na mwishowe vyote vilirudishwa juu mbinguni.
11Ya estagüe enseguidas manotojgue güije gui menan guma anae sumasagayo, tres na taotao, manmatago guinin Sesarea para iya guajo.
11Ghafla, watu watatu waliokuwa wametumwa kwangu kutoka Kaisarea waliwasili kwenye nyumba niliyokuwa nakaa.
12Ya jatagoyo na judalalag sija ya chajo fumatitinas dinesparejo. Ya manjame yan este sija y saes na mañelo, ya manjalomjam gui guima y taotao:
12Roho aliniambia niende pamoja nao bila kusita. Hawa ndugu sita waliandamana nami pia kwenda Kaisarea na huko tuliingia nyumbani mwa Kornelio.
13Ya jasanganejam ni y liniiña ni y angjet ni y tumotojgue gui jalom gumaña, ya jaftaemano ilegña nu güiya: Fanago taotao para Joppe, ya uncone si Simon ni y apiyiduña Pedro;
13Yeye alitueleza jinsi alivyokuwa amemwona malaika amesimama nyumbani mwake na kumwambia: Mtume mtu Yopa akamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petro.
14Ya unsinangane sinangan sija anae unsatbo; jago, yan todo y guimamo.
14Yeye atakuambia maneno ambayo kwayo wewe na jamaa yako yote mtaokolewa.
15Ya anae sigue di cumuentosyo, podong y Espiritu Santo gui jiloñija, taegüijeja gui jilota gui tutujonña.
15Na nilipoanza tu kuongea, Roho Mtakatifu aliwashukia kama alivyotushukia sisi pale awali.
16Ayonae jujaso y sinangan y Señot, ni y ilegña: Si Juan, magajet na managpapange ni y janom; lao jamyo infanmatagpange ni y Espiritu Santo.
16Hapo nilikumbuka yale maneno Bwana aliyosema: Yohane alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.
17Sa yaguin manninae sija locue as Yuus y ninae, taegüije y janaejit anae jumongguejit y Señot Jesucristo, ya jayeyo na siña jucontra si Yuus?
17Basi, kama Mungu amewapa pia watu wa mataifa mengine zawadi ileile aliyotupa sisi tulipomwamini Bwana Yesu Kristo, je, mimi ni nani hata nijaribu kumpinga Mungu?"
18Ya anae jajungog sija estesija, manmamatquilo, ya manamalag si Yuus, ilegñija: Magajet na janae locue si Yuus y Gentiles sinetsot para linâlâ.
18Waliposikia hayo, waliacha ubishi, wakamtukuza Mungu wakisema, "Mungu amewapa watu wa mataifa mengine nafasi ya kutubu na kuwa na uzima!"
19¶ Ya ayo sija y manmachalapon pot y mapetsiguen ni y Esteban, manjanao asta Finesia, yan Chipre, yan Antioquia, ya taya nae japredica y sinangan na ayoja sija y Judios.
19Kutokana na mateso yaliyotokea wakati Stefano alipouawa, waumini walitawanyika. Wengine walikwenda mpaka Foinike, Kupro na Antiokia wakihubiri ule ujumbe kwa Wayahudi tu.
20Ya palo guiya sija taotao Chipre, yan Sirene, ya anae manmato Antioquia, manguentos yan y Griegosija, ya japredica y Señot Jesus.
20Lakini baadhi ya waumini waliotoka Kupro na Kurene, walikwenda Antiokia wakautangaza huo ujumbe kwa watu wa mataifa mengine wakiwahubiria ile Habari Njema juu ya Bwana Yesu.
21Ya mañisijaja yan y canae y Señot; ya megae manmanjonggue ya jabira sija para y Señot.
21Bwana aliwasaidia na idadi kubwa ya watu iliamini na kumgeukia Bwana.
22Ya mato este sija na notisia gui iglesia ni y estaba Jerusalem: ya matago si Barnabé, na ujanao asta Antioquia;
22Habari ya jambo hilo ikasikika kwa lile kanisa la Yerusalemu. Hivyo wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
23Ya anae mato, ya jalie y grasian Yuus, magof güe; ya jasangane sija todo, na nu sinasuyen y corasonñija, unafanmeton sija gui Señot:
23Alipofika huko na kuona jinsi Mungu alivyowaneemesha wale watu, alifurahi na kuwahimiza wote wadumu katika uaminifu wao kwa Bwana.
24Sa güiya mauleg na taotao, ya bula ni y Espiritu Santo, yan jinenggue: ya megae na taotao manmafato gui Señot.
24Barnaba alikuwa mtu mwema na mwenye kujaa Roho Mtakatifu na imani. Kundi kubwa la watu lilivutwa kwa Bwana.
25Ayonae mapos güe para Tarso, para ualigao si Saulo:
25Kisha, Barnaba alikwenda Tarso kumtafuta Saulo
26Ya anae jasoda, jacone guato Antioquia. Ya un año di mandadañaja güije yan iglesia, ya manmamananagüe megae na taotao; ya y disipulo sija manmafanaan finena mangilisyano guiya Antioquia.
26Alipompata, alimleta Antiokia. Nao wote wawili walikaa na lile kanisa kwa mwaka wote mzima wakifundisha kundi kubwa la watu. Huko Antiokia, ndiko, kwa mara ya kwanza, wafuasi waliitwa Wakristo.
27¶ Ya este sija na jaane, manmato profeta sija guinin Jerusalem para Antioquia,
27Wakati huohuo, manabii kadhaa walikuja Antiokia kutoka Yerusalemu.
28Ya tumojgue julo uno guiya sija, na y naanña Agabo, ya janamatungo pot y Espiritu na uguaja un dangculon niñalang gui todo y tano: ya umasusede gui tiempon Claudio Sesat.
28Basi, mmoja wao aitwaye Agabo alisimama, na kwa uwezo wa Roho akabashiri kwamba kutakuwa na njaa kubwa katika nchi yote (Njaa hiyo ilitokea wakati Klaudio alipokuwa akitawala).
29Ayonae y disipulo sija, cada uno jaftaemano y güinajaña, jadetetmina para umanamamaela inayuda para y mañelo ni y mañasaga Judea:
29Wale wanafunzi waliamua kila mmoja kwa kadiri ya uwezo wake apeleke chochote ili kuwasaidia wale ndugu waliokuwa wanaishi Yudea.
30Ya sija locue jafatinas, janamaela para y manamco pot y canae Barnabé yan Saulo.
30Basi, wakafanya hivyo na kupeleka mchango wao kwa wazee wa kanisa kwa mikono ya Barnaba na Saulo.