1YA estaba güije gui ilesia guiya Antioquia, profeta sija yan maestro, sija: Barnabé, yan si Simeon ni y mafanaan Niger, yan si Lucio, taotao Sirene, yan si Manaen, ni y chamapogsae yan Herodes tetrarca, yan si Saulo.
1Katika kanisa la Antiokia kulikuwa na watu wengine waliokuwa manabii na walimu; miongoni mwao akiwa Barnaba, Simoni aitwaye pia Mweusi, Lukio wa Kurene, Manaeni ambaye alikuwa amelelewa pamoja na mfalme Herode, na Saulo.
2Ya mientras sija sumesetbe y Señot, yan manayuyunat, y Espiritu Santo ilegña: Abatta guiya guajo Barnabé yan Saulo para y checho anae guinin juagange sija.
2Walipokuwa wanafanya ibada yao kwa Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema: "Niteulieni Barnaba na Saulo kwa ajili ya kazi niliyowaitia."
3Ayonae anae esta manayunat yan manmanayuyut yan japolo y canaeñija gui jilo ayo sija, jatago sija na ufanjanao.
3Basi, baada ya kusali na kufunga zaidi, wakawawekea mikono, wakawaacha waende zao.
4¶ Ya manmatago sija pot y Espiritu Santo, ya manunog para Seleusia; ya desde ayo mumamaya para Chipre.
4Basi, Barnaba na Saulo walipokwisha tumwa na Roho Mtakatifu, walishuka hadi Seleukia, na kutoka huko walipanda meli hadi kisiwa cha Kupro.
5Ya anae mangaegue gui Salamina, japredica y sinangan Yuus gui sinagogan y Judiosija: ya mañisijaja locue yan si Juan ni y sumesetbe sija.
5Walipofika Salami walihubiri neno la Mungu katika masunagogi ya Kiyahudi. Yohane (Marko) alikuwa msaidizi wao.
6Ya anae jajanagüe todo inanaco y isla asta Pafo, jasoda un taotao na cacana, fatso na profeta, Judio, na y naanña si Bar-Jesus:
6Walitembea toka upande mmoja wa kisiwa mpaka Pafo upande wa pili, na huko walimkuta mchawi mmoja Myahudi aitwaye Baryesu ambaye alijisingizia kuwa nabii.
7Ni y estaba yan y magalajen y tano, si Sergio Paulo, gaetiningo na taotao; ya jaaagang si Barnabé yan Saulo, sa malago na ujungog y sinangan Yuus.
7Huyu alikuwa pamoja na Sergio Paulo, mkuu wa kile kisiwa, ambaye alikuwa mtu mwelewa sana. Sergio Paulo aliwaita Barnaba na Saulo ili asikie neno la Mungu.
8Lao manquinentra as Elymas, taotao na cacana (taegüine nae comequilegña y naanña), jaaliligao na unamabira guinin jinenggue y magalaje.
8Lakini huyo mchawi Elima (kama alivyokuwa anaitwa kwa Kigiriki), alijaribu kuwapinga ili kumzuia huyo mkuu wa kisiwa asije akaigeukia imani ya Kikristo.
9Ayonae si Saulo ni y naanña locue Pablo, bula ni y Espiritu Santo, inaatanja güe,
9Basi, Saulo ambaye aliitwa pia Paulo, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alimkodolea macho huyo mchawi,
10Ya ilegña: O bula jao todo dinague, yan tinaelaye, jago lajin anite, jago enemigun todo y tininas, ada ti pumapara jao unnataelaye y tinas na chalan y Señot?
10akasema, "Mdanganyifu wa kupindukia na mlaghai wewe! Wewe ni mtoto wa Ibilisi! Wewe ni adui wa chochote kile kilicho cha kweli; hukomi hata mara moja kujaribu kuzipotosha njia za Bwana zilizonyoka.
11Ya pago estagüiya y canae y Señot gui jilomo, ya unbachet ya ti unlie y atdao pot un tiempo. Ya enseguidas podong gui jiloña y nublado ya jomjom, ya jumanao manaligao jaye uminantiene y canaeña para uinesgaejongüe.
11Sasa, mkono wa Bwana utakuadhibu: utakuwa kipofu na hutaweza kuuona mwanga wa jua kwa kitambo." Mara kila kitu kikawa kama ukungu na giza kwake, akaanza kwenda huku na huku akitafuta mtu wa kumshika mkono amwongoze.
12Ya anae jalie y magalaje jafa y mafatinas, jajonggue ya ninasenmanman ni y finanagüen y Señot.
12Yule mkuu wa kisiwa alipoona hayo, aliongoka akawa muumini; akastaajabia sana mafundisho aliyosikia juu ya Bwana.
13¶ Ya anae si Pablo yan y mangachongña jadingo Pafo, ya mumamaya ya manmato Petga guiya Pamfilia, ya si Juan jumanao guiya sija ya tumalo guato Jerusalem.
13Kutoka Pafo, Paulo na wenzake walipanda meli wakaenda hadi Perga katika Pamfulia; lakini Yohane (Marko) aliwaacha, akarudi Yerusalemu.
14Lao sija manmalofan inanaco guinin Petga, manmato Antioquia guiya Pisidia; ya manjalom gui sinagoga gui sabado na jaane ya manmatachong.
14Lakini wao waliendelea na safari toka Pisga hadi mjini Antiokia Pisidia. Siku ya Sabato waliingia ndani ya Sunagogi, wakakaa.
15Ya anae munjayan jataetae y lay yan y profeta sija, y magas y sinagoga ninafamnaagange sija ilegñija: Jamyo mañelo, yaguin guaja jafa na finijo para insangane y taotao sija, sangan.
15Baada ya masomo katika kitabu cha Sheria ya Mose na katika maandiko ya manabii, wakuu wa lile sunagogi waliwapelekea ujumbe huu: "Ndugu, kama mnalo jambo la kuwaambia watu ili kuwapa moyo, semeni."
16Ayonae si Pablo tumojgue julo ya mañeñas ni y canaeña, ilegña: Taotao Israel, yan jamyo ni y manmaañao as Yuus, ecungog.
16Basi, Paulo alisimama, akatoa ishara kwa mkono, akaanza kuongea: "Wananchi wa Israeli na wengine wote mnaomcha Mungu, sikilizeni!
17Y Yuus este na taotao iya Israel, jaayeg y mañaenata, yan jajatsa y taotao sija anae mañasaga taegüije y taotao juyong guiya Egipto, ya ni y taquilo na canaeña jacone sija juyong güije.
17Mungu wa taifa hili la Israeli aliwateua babu zetu na kuwafanya wawe taifa kubwa walipokuwa ugenini kule Misri. Mungu aliwatoa huko kwa uwezo wake mkuu.
18Ya y cuarenta años ni tiempo, jasungon ni y costumbreñija gui jalomtano.
18Aliwavumilia kwa muda wa miaka arobaini kule jangwani.
19Ya guinin mujayan jayulang siete na nasion gui tano Cananea, ya japatte y tanoñija guiya sija para y erensiañija nae mañasaga, como cuatro siento y sincuenta años;
19Aliyaangamiza mataifa ya nchi ya Kanaani akawapa hao watu wake ile nchi kuwa mali yao.
20Ya despues di ayo sija, manninae sija jues sija asta qui mato y profeta Samuel.
20Miaka mia nne na hamsini ilipita, halafu akawapatia waamuzi wawaongoze mpaka wakati wa nabii Samweli.
21Ya despues manmalago ray: ya manninae as Yuus as Saulo lajin Sis, un taotao gui tribon Benjamin para cuarenta años.
21Hapo wakapendelea kuwa na mfalme, na Mungu akawapa Saulo, mtoto wa Kishi wa kabila la Benyamini, awe mfalme wao kwa muda wa miaka arobaini.
22Yaanae jarechasa si Saulo, janacajulo guiya sija si David para rayñija. Sa si Yuus numae güe locue testimonio, ilegña: Guajo jusoda si David lajin Isai, un taotao na parejoja yan y corasonjo, ya güiya ucumple todo y malagojo.
22Baada ya kumwondoa Saulo, Mungu alimteua Daudi kuwa mfalme wao. Mungu alionyesha kibali chake kwake akisema: Nimemwona Daudi mtoto wa Yese; ni mtu anayepatana na moyo wangu; mtu ambaye atatimiza yale yote ninayotaka kuyatenda.
23Ya y semiyan este na taotao nae, unacajulo si Yuus guiya Israel y Satbadot Jesus jaftaemanoja y promesa:
23Kutokana na ukoo wake mtu huyu, Mungu, kama alivyoahidi, amewapelekea watu wa Israeli Mwokozi, ndiye Yesu.
24Ya si Juan finena prumedica, antes di y finatoña, y tinagpangen sinetsot para todo y taotao guiya Israel.
24Kabla ya kuja kwake Yesu, Yohane alimtangulia akiwahubiria watu wote wa Israeli kwamba ni lazima watubu na kubatizwa.
25Ya anae jacumple si Juan y chechoña, ilegña: Jayeyo jinasonmimiyo? Ti guajo güe. Lao estagüe na mamamaela uno gui tateco, na ni y sapatos gui adengña ti dignoyo na jupula.
25Yohane alipokuwa anamaliza ujumbe wake aliwaambia watu: Mnadhani mimi ni nani? Mimi si yule mnayemtazamia. Huyo anakuja baada yangu na mimi sistahili hata kuzifungua kamba za viatu vyake.
26Mañelo lalaje, fumaguon y rasan Abraham, yan jayeja guiya jamyo y maañao as Yuus, sa para jamyo na matago y sinangan este na satbasion.
26"Ndugu, ninyi mlio watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wengine wote mnaomcha Mungu! Ujumbe huu wa wokovu umeletwa kwetu.
27Pot ayo sija y mañasaga Jerusalem, yan y magasñija sa ti matungo si Yuus, ni y sinangan y profeta ni y jatataetaeja cada sabado, anae masentensia güe jacumple sija.
27Kwa maana wenyeji wa Yerusalemu na wakuu wao hawakumtambua yeye kuwa Mwokozi. Wala hawakuelewa maneno ya manabii yanayosomwa kila Sabato. Hata hivyo, waliyafanya maneno ya manabii yatimie kwa kumhukumu Yesu adhabu ya kifo.
28Ya achogja ti jasoda sija jafa na causa guiya güiya na umapuno, lao magagao si Pilatos na umapuno.
28Ingawa hawakumpata na hatia inayostahili auawe, walimwomba Pilato amhukumu auawe.
29Ya anae macumple todo ayo y esta matugue pot güiya, machule papa guinin y jayo, ya mapolo gui jalom y naftan.
29Na baada ya kutekeleza yote yaliyokuwa yameandikwa kumhusu yeye, walimshusha kutoka msalabani, wakamweka kaburini.
30Lao si Yuus munacajulo guinen y manmatae:
30Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu.
31Ya malie megae na jaane ni ayo sija y mangachochongña mangajulo guinin Galilea para Jerusalem, ni y pago testiguña sija gui taotao.
31Naye, kwa siku nyingi aliwatokea wale waliofuatana naye kutoka Galilaya mpaka Yerusalemu. Hao ndio walio sasa mashahidi wake kwa watu wa Israeli.
32Ya jame chumule guiya jamyo y mauleg na notisia, ni ayo na promesa y mafatinas gui mañaena,
32Sisi tumekuja hapa kuwaleteeni Habari Njema: jambo lile Mungu alilowaahidia babu zetu amelitimiza sasa kwa ajili yetu sisi tulio wajukuu wao kwa kumfufua Yesu kutoka wafu.
33Jaftaemano si Yuus cumunple guiya jita, ni y famaguonñija, sa ayonae janacajulo si Jesus talo; taegüije locue y esta matugue gui mina dos gui Salmos: Jago y Lajijo ya pago na jaane nae julilis jao.
33Kama ilivyoandikwa katika zaburi ya pili: Wewe ni Mwanangu, mimi leo nimekuwa baba yako.
34Ya ninacajulo guinin y manmatae, ya pago ti utalo guato gui minitong guinin jasangan taegüine: Guajo junae jao ni y santos yan magajet na bendisjon David.
34Na juu ya kumfufua kutoka wafu, asipate tena kurudi huko na kuoza, Mungu alisema hivi: Nitakupa baraka takatifu na za kweli nilizomwahidia Daudi.
35Enaomina ilegña locue y otro Salmo: Na chamo pumopolo y Santosmo na ulie y minitong.
35Naam, na katika sehemu nyingine za zaburi asema: Hutamwacha Mtakatifu wako aoze.
36Sa si David anae munjayan jasetbe y generasionña pot y pinagat Yuus, maego ya mapolo manafandaña yan y mañaenaña, ya jalie y minitong.
36Sasa, Daudi mwenyewe alitimiza mapenzi ya Mungu wakati wake; kisha akafa na kuzikwa karibu na wazee wake, na mwili wake ukaoza.
37Lao ayo y ninacajulo as Yuus talo ti jalie minitong.
37Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu hakupata kuoza.
38Ya umatungo guiya jamyo mañelo lalaje, na pot este na taotao na mapredidica guiya jamyo y inasiin y isao:
38Jueni wazi, ndugu zangu, kwamba ujumbe kuhusu kusamehewa dhambi unahubiriwa kwenu kwa njia ya Yesu Kristo;
39Ya pot güiya na todo ayo y jumonggue manunas ni todo y güinaja, sa ti siña jamyo manunas, pot y lay Moises.
39na ya kwamba kila mmoja anayemwamini Yesu anasamehewa dhambi zote, jambo ambalo halingewezekana kwa njia ya Sheria ya Mose.
40Adaje na nosea ufato guiya jamyo, y masangan gui profeta sija;
40Jihadharini basi, msije mkapatwa na yale yaliyosemwa na manabii:
41Estagüe, jamyo ni y manmañatlilie, yan infanmanman, yan infanmalingo. Sa machochochoyo ni y checho y jaanemniyo, ayo na chocho y ti injengue, ni jaye na taotao unaclaro guiya jamyo.
41Sikilizeni enyi wenye madharau, shangaeni mpotee! Kwa maana kitu ninachofanya sasa, nyakati zenu, ni kitu ambacho hamtakiamini hata kama mtu akiwaelezeni."
42Ya anae manjuyong gui sinagoga, jagagao na umapredica este na sinangan guiya sija gui siguiente sabado.
42Paulo na Barnaba walipokuwa wanatoka katika ile sunagogi, wale watu waliwaalika waje tena siku ya Sabato iliyofuata, waongee zaidi juu ya mambo hayo.
43Ya anae manadingo y inetnon gui sinagoga, megae na Judios yan y deboto na proselito sija dumalalag si Pablo yan Barnabé; ni y sumangangane siga yan jaeepogna ufañaga gui grasian Yuus.
43Mkutano huo ulipomalizika, Wayahudi wengi na watu wa mataifa mengine waliokuwa wameongokea dini ya Kiyahudi waliwafuata Paulo na Barnaba. Hao mitume waliongea nao, wakawatia moyo waendelee kuishi wakitegemea neema ya Mungu.
44¶ Ya y siguiente sabado canaja todo y taotao y siuda mandaña para ujajungog y sinangan Yuus.
44Siku ya Sabato iliyofuata, karibu kila mtu katika ule mji alikuja kusikiliza neno la Bwana.
45Lao anae jalie y Judios y linajyan taotao, manbula linatga, ya manguentos contra ayo y sinangan Pablo ya jachatfino contra si Yuus.
45Lakini Wayahudi walipoliona hilo kundi la watu walijaa wivu, wakapinga alichokuwa anasema Paulo na kumtukana.
46Ayonae si Pablo yan Barnabé jausa y minatatngañija, ilegñija: Nesesita ayo y sinangan Yuus ni y esta manmasangane jamyo finena, lao pot innasuja guiya jamyo, injisganmaesa jamyo na ti dignojamyo y taejinecog na linâlâ, ya estagüe na tabirajit para y Gentiles.
46Hata hivyo, Paulo na Barnaba waliongea kwa uhodari zaidi, wakasema, "Ilikuwa ni lazima neno la Mungu liwafikieni ninyi kwanza; lakini kwa kuwa mmelikataa na kujiona hamstahili uzima wa milele, basi, tunawaacheni na kuwaendea watu wa mataifa mengine.
47Sa taegüenao tinagoña si Yuus nu jita, ilegña: Jupolo jamyo para candet y Gentiles, na jamyo siña para satbasion asta y uttimon patte y tano.
47Maana Bwana alituagiza hivi: Nimekuteua wewe uwe mwanga kwa mataifa, uwe njia ya wokovu kwa ulimwengu wote."
48Ya anae jajungog este y Gentiles, ninafansenmagof, ya maalaba y sinangan Yuus: ya megae manmanjonggue ni ayo sija y manmatancho para y taejinecog na linâlâ.
48Watu wa mataifa mengine waliposikia jambo hilo walifurahi, wakausifu ujumbe wa Mungu; na wale waliokuwa wamechaguliwa kupata uzima wa milele, wakawa waumini.
49Ya machalapon y sinangan Yuus todo güije na tano.
49Neno la Bwana likaenea kila mahali katika sehemu ile.
50¶ Lao y Judio sija, janafangalamten y mandebota yan y manonra na famalaoan, yan y manmagas na taotao sija gui siuda, ya janafangajulo pinetsigue contra si Pablo yan Barnabé, ya janafanmayute juyong gui tanoñija.
50Lakini Wayahudi waliwachochea wanawake wa tabaka ya juu wa mataifa mengine ambao walikuwa wacha Mungu, na wanaume maarufu wa mji huo. Wakaanza kuwatesa Paulo na Barnaba, wakawafukuza kutoka katika eneo lao.
51Lao sija, jasacude y petbos gui adengñija contra sija, ya manjanao para Iconio.
51Basi, mitume wakayakung'uta mavumbi yaliyokuwa katika miguu yao kama onyo, kisha wakaenda Ikonio.
52Ya y disipulo sija, manbula minagof yan y Espiritu Santo.
52Lakini hao wafuasi walikuwa wamejaa furaha na Roho Mtakatifu.