1YA susede na manjalom gui sinagogan y Judios guiya Iconio, ya taegüenao manguentos na un dangculo na linajyan Judios yan Griegos manman jonggue.
1Kule Ikonio, mambo yalikuwa kama yalivyokuwa kule Antiokia; Paulo na Barnaba walikwenda katika sunagogi la Wayahudi wakaongea kwa uhodari hata Wayahudi wengi na Wagiriki wakawa waumini.
2Lao ayo sija na Judios y ti manmanosgue, jasuug y anten y Gentil sija, para ufanmanjaso taelaye contra y mañelo.
2Lakini Wayahudi wengine waliokataa kuwa waumini walichochea na kutia chuki katika mioyo ya watu wa mataifa mengine ili wawapinge hao ndugu.
3Lao mañagaja apmam, manguecuentos matatnga ni y Señot, ni y mannae testimonio ni y sinangan y grasiaña, yan mannae señat sija, yan mannamanman sija para ujafatinas ni y canaeñija.
3Paulo na Barnaba waliendelea kukaa huko kwa muda mrefu. Waliongea kwa uhodari juu ya Bwana, naye Bwana akathibitisha ukweli wa ujumbe walioutoa juu ya neema yake, kwa kuwawezesha kutenda miujiza na maajabu.
4Ya y linajyan taotao gui siuda manmadibide; y un banda mañija yan y Judios, ya y otro banda mañija yan y apostoles.
4Watu wa mji huo waligawanyika: wengine waliwaunga mkono Wayahudi, na wengine walikuwa upande wa mitume.
5Lao anae manmamatinas insulto y Judios yan y Gentiles, yan y magasñija, para ufanmacase sija, yan ufanmafagas ni y ocho,
5Mwishowe, baadhi ya watu wa mataifa mengine na Wayahudi, wakishirikiana na wakuu wao, waliazimu kuwatendea vibaya hao mitume na kuwapiga mawe.
6Esta matungo nu sija; ya manmalago guato Listra yan Derbe, siuda iya Licaonia, yan y tano gui oriya.
6Mitume walipogundua jambo hilo, walikimbilia Lustra na Derbe, miji ya Lukaonia, na katika sehemu za jirani,
7Ya güije japredica sija y ibangelio.
7wakawa wanahubiri Habari Njema huko.
8¶ Ya estaba güije guiya Listra un taotao na taeninasiña y adengña, sa cojo desde y jalom tuyan nanaña; ya taya nae mamocat:
8Kulikuwa na mtu mmoja huko Lustra ambaye alikuwa amelemaa miguu tangu kuzaliwa, na alikuwa hajapata kutembea kamwe.
9Ayo na taotao jajungog si Pablo na cumuentos: ya enseguidas na inatan, tiningo na guaja jinenggueña para umanajomlo,
9Mtu huyo alikuwa anamsikiliza Paulo alipokuwa anahubiri. Paulo alimtazama kwa makini, na alipoona kuwa alikuwa na imani ya kuweza kuponywa,
10Jaagang dangculo na inagang ilegña: Tojgue julo tunas ni y adengmo. Ya guiya mangope julo, ya mamocat.
10akasema kwa sauti kubwa, "Simama wima kwa miguu yako!" Huyo mtu aliyelemaa akainuka ghafla, akaanza kutembea.
11Ya anae malie ni y linajyan taotao sija y finatinas Pablo, jajatsa y inagangñija ilegñija gui cuentos Licaonia: Y yuus sija ni manparejo yan taotao, manunog guiya jita.
11Umati wa watu walipoona alichofanya Paulo, ulianza kupiga kelele kwa lugha ya Kilukaonia: "Miungu imetujia katika sura za binadamu!"
12Ya mafanaan si Barnabé Jupiter; ya si Pablo mafanaan Mercurio, sa güiya magas na cuecuentos.
12Barnaba akaitwa Zeu, na Paulo, kwa vile yeye ndiye aliyekuwa anaongea, akaitwa Herme.
13Ayonae y pale y Jupiter ni y temploña estaba gui menan y siuda, mangone toro sija, yan mañule coronan flores guato gui pettan y trangca, ya malago na ufanmamatinas inefrese, yan y linajyan taotao sija.
13Naye kuhani wa hekalu la Zeu lililokuwa nje ya mji akaleta fahali na shada za maua mbele ya mlango mkuu wa mji, na pamoja na ule umati wa watu akataka kuwatambikia mitume.
14Lao anae majungog ni y apostoles, si Barnabé yan si Pablo, jatiteg y magagoñija, ya manmalago gui entalo y linajyan taotao ya manaagang,
14Barnaba na Paulo walipopata habari hiyo waliyararua mavazi yao na kukimbilia katika lile kundi la watu wakisema kwa sauti kubwa:
15Ilegñija: Señot sija, jafa na infatinas este sija? Jame locue manaotaojam, manparejojajit, ya insangane jamyo na inbira jamyo güine gui este sija manaesetbe, ya infanmalag y lalâlâ na Yuus, ni y jafatinas y langet, yan y tano, yan y tase, yan todo y sinajguanña:
15"Ndugu, kwa nini mnafanya mambo hayo? Sisi pia ni binadamu kama ninyi. Na, tuko hapa kuwahubirieni Habari Njema, mpate kuziacha hizi sanamu tupu, mkamgeukie Mungu aliye hai, Mungu aliyeumba mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo.
16Ni y manmalofan na generasion sija, japolo todo y nasion na ufanjanao gui minalagoñija.
16Zamani Mungu aliruhusu kila taifa lifanye lilivyopenda.
17Masquesea güiya ti jadingo güe sin testigo, sa mauleg finatinasña, ya janaejit uchan guinin y langet, yan megae na tinegcha, janafanbula y corasonta nengcano yan minagof.
17Hata hivyo, Mungu hakuacha kujidhihirisha kwa mambo mema anayowatendea: huwanyeshea mvua toka angani, huwapa mavuno kwa wakati wake, huwapa chakula na kuijaza mioyo yenu furaha."
18Ya este sija na sinangan, canamapot jaafuetsas y linajyan taotao na chañija fumatitinas inefrese guiya sija.
18Ingawa walisema hivyo haikuwa rahisi kuwazuia wale watu wasiwatambikie.
19¶ Ya manmato güije Judios guinin Antioquia, yan Iconio, ni y manafanmañaña y linajyan; ya anae munjayan mafagas ni y acho si Pablo, mabatsala juyong gui siuda, jinasoñija na matae.
19Lakini Wayahudi kadhaa walikuja kutoka Antiokia na Ikonio, wakawafanya watu wajiunge nao, wakampiga mawe Paulo na kumburuta hadi nje ya mji wakidhani amekwisha kufa.
20Ya mientras manotojgue y disipulo sija gui oriyaña, cumajulo ya jumalom gui siuda; ya y inagpaña güije, jumanao yan si Barnabé manmalag Derbe.
20Lakini waumini walipokusanyika na kumzunguka, aliamka akarudi mjini. Kesho yake, yeye pamoja na Barnaba walikwenda Derbe.
21Ya anae munjayan japredica y ibangelio güije na siuda, yan mamadisipulo megae; tumalo guato Listra, yan Iconio, yan Antioquia,
21Baada ya Paulo na Barnabas kuhubiri Habari Njema huko Derbe na kupata wafuasi wengi, walifunga safari kwenda Antiokia kwa kupitia Lustra na Ikonio.
22Ya janafanfitme y anten y disipulo sija, ya jaaconseja na ujasigueja gui jinenggue; sa nesesita megae na pinite sija, ya ayonae siñajit manjalom gui raenon Yuus,
22Waliwaimarisha waumini wa miji hiyo na kuwatia moyo wabaki imara katika imani. Wakawaambia, "Ni lazima sisi sote tupitie katika taabu nyingi ili tuingie katika ufalme wa Mungu."
23Ya anae munjayan jatancho y manamco gui cada guimayuus, yan manaetae, yan umayunat, yan jatayuyute sija gui as Yuus ni manmanjonggue.
23Waliteua wazee katika kila kanisa kwa ajili ya waumini, na baada ya kusali na kufunga, wakawaweka chini ya ulinzi wa Bwana ambaye walikuwa wanamwamini.
24Ya manmalofan y inanaco Pisidia, ya manmato Pamfilia.
24Baada ya kupitia katika nchi ya Pisidia, walifika Pamfulia.
25Ya anae munjayan mapredica y sinangan guiya Petga, manunog guiya Atalia;
25Baada ya kuhubiri ule ujumbe huko Perga, walikwenda Atalia.
26Ya desde ayo mangagama asta Antioquia, anae manmanae ni y grasian Yuus, para y checho ni y mafatinas.
26Kutoka huko walisafiri kwa meli wakarudi Antiokia ambako hapo awali walikuwa wamewekwa chini ya ulinzi wa neema ya Mungu kwa ajili ya kazi ambayo sasa walikuwa wameitimiza.
27Ya anae manmato ya mandaña iglesia gui guimayuus, masangan todo sija y finatinas Yuus pot sija; yan jaftaemano jababaye y Gentiles ni y pettan y jinenggue.
27Walipofika huko Antiokia walifanya mkutano wa kanisa la mahali hapo, wakawapa taarifa juu ya mambo Mungu aliyofanya pamoja nao, na jinsi alivyowafungulia mlango watu wa mataifa mengine mlango wa kuingia katika imani.
28Ya mañaga güije yan y disipulo sija, apmam na tiempo.
28Wakakaa pamoja na wale waumini kwa muda mrefu.