Chamorro: Psalms, Gospels, Acts

Swahili: New Testament

John

13

1YA antes di y guipot pascua, jatungo si Jesus na y oraña esta mato para ujanao güine na tano para y Tata, esta jaguaeya y iyoña sija ni mangaegue güine gui tano, ya jaguaeya sija asta y jinecog.
1Ilikuwa kabla ya sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kuondoka ulimwenguni na kwenda kwa Baba ilikuwa imefika. Alikuwa amewapenda daima watu wake walioko duniani; naam, aliwapenda mpaka mwisho!
2Y sena munjayan ya y anite esta jumalom gui corason Judas Iscariote, lajin Simon, ni umentrega güe;
2Basi, Yesu na wanafunzi wake walikuwa mezani kwa chakula cha jioni. Ibilisi alikwisha mtia Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti, nia ya kumsaliti Yesu.
3Ya jatungo si Jesus na y Tata jagasja janae todo ni güinaja gui canaeña, ya mato güe guinin as Yuus, ya as Yuus guaguato;
3Yesu alijua kwamba Baba alikuwa amemkabidhi kila kitu, na kwamba alikuwa ametoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.
4Cajulo gui sena ya janajanao y magagoña, ya jachule un toaya, ya jaafuyut güiya namaesa.
4Basi, Yesu aliondoka mezani, akaweka kando vazi lake, akachukua kitambaa na kujifunga kiunoni.
5Anae esta munjayan este, janaye y janom gui palangana diquique, ya jatutujon fumagase y adeng y disipulo sija, ya jasaosao nu y toaya na jaafuyut güe.
5Kisha akatia maji katika bakuli, akaanza kuwaosha wanafunzi wake miguu na kuipangusa kwa kile kitambaa alichojifungia.
6Ayo nae malag as Simon Pedro; ya este ilegña nu güiya: Señot jago fumagase y adengjo?
6Basi, akamfikia Simoni Petro; naye Petro akasema, "Bwana, wewe utaniosha miguu mimi?"
7Manope si Jesus ya ilegña nu güiya: Y jufatitinas ti untungo pago; lao ti ampmam untungo.
7Yesu akamjibu, "Huelewi sasa ninachofanya lakini utaelewa baadaye."
8Si Pedro ilegña nu güiya: Ti unfagase y adengjo ni ngaean! Ynepe as Jesus: Yaguin ti jufagase jao taepattemo guiya guajo.
8Petro akamwambia, "Wewe hutaniosha miguu kamwe!" Yesu akamjibu, "Nisipokuosha hutakuwa na uhusiano nami tena."
9Ylegña nu güiya si Simon Pedro: Señot, ti adengjoja, lao locue asta y canaejo yan y ilujo.
9Simoni Petro akamwambia, "Bwana, nioshe, si miguu tu, bali na mikono yangu na kichwa pia."
10Si Jesus ilegña nu güiya: Y esta mafagase, ti guaelaye yaguin adengña esta mafagase, lao esta gasgas todo. Ya jamyo mangasgas pago, achogja ti todos.
10Yesu akamwambia, "Aliyekwisha oga hana lazima ya kunawa isipokuwa miguu, maana amekwisha takata mwili wote. Ninyi mmetakata, lakini si nyote."
11Sa esta matungo jaye uje y umentrega güe; pot enao ilegña: Ti mangasgas jamyo todos.
11(Yesu alimjua yule ambaye atamsaliti, ndiyo maana alisema: "Ninyi mmetakata, lakini si nyote.")
12¶ Anae munjayan manfinagase y adengñija, jachule y magagoña ya tumalo matachong otro biaje, ya mansinangane: Yntingo y finatinasjo?
12Alipokwisha waosha miguu na kuvaa tena vazi lake, aliketi mezani, akawaambia, "Je, mmeelewa hayo niliyowatendeeni?
13Jamyo infanaan yo Maestro yan Señot: ya y sinanganmiyo mauleg; sa guajo yo.
13Ninyi mwaniita Mwalimu na Bwana, nanyi mwasema vyema, kwa kuwa ndimi.
14Yaguin guajo Señotmiyo yan Maestronmiyo, guinin jufagase y adengmiyo, debe jamyo locue infanafagase y adengmiyo uno yan otro.
14Basi, ikiwa mimi niliye Bwana na Mwalimu, nimewaosha ninyi miguu, nanyi pia mnapaswa kuoshana miguu.
15Sa un ejemplo junae jamyo, sa taemanoja guajo jufatinase jamyo, jamyo locue infatitinas.
15Nimewapeni mfano, ili nanyi pia mfanye kama nilivyowafanyieni.
16Magajet ya magajet jusangane jamyo: Y tintago ti güiya magasña na y senotña; ni y matago, ti güiya magasña na y tumago güe.
16Kweli nawaambieni, mtumishi si mkuu zaidi kuliko bwana wake, wala mtume si mkuu zaidi kuliko yule aliyemtuma.
17Yaguin intingo este sija na güinaja, mandichoso jamyo yaguin infatitinas,
17Basi, ikiwa mwayajua hayo, mtakuwa na heri mkiyatekeleza.
18¶ Ti umadingan yo nu jamyo todo: guajo tumungo sija y inayigco; lao para umacumple y tinigue sija: Y chumocho pan yan guajo, güiya cumajulo contra guajo y dedegoña.
18"Haya nisemayo hayawahusu ninyi nyote. Mimi nawajua wale niliowachagua. Lakini lazima yatimie Maandiko Matakatifu yasemayo: Yule aliyeshiriki chakula changu amegeuka kunishambulia.
19Desde pago jusangane jamyo antes di ujuyong, para yaguin jumujuyong, injenggue na guajo yo.
19Mimi nimewaambieni mambo haya sasa kabla hayajatokea, ili yatakapotokea mpate kuamini kuwa mimi ndimi.
20Magajet ya magajet jusangane jamyo, na y rumesibe y tinagojo, jaresibe yo; ya y rumesibe yo, jaresibe y tumago yo.
20Kweli nawaambieni anayempokea yule ninayemtuma anaponipokea mimi; na anayenipokea mimi, anampokea yule aliyenituma."
21Anae munjayan jasangan si Jesus este, inigongña si Jesus jinalomña, ya janae testimonio ya ilegña: Magajet ya magajet jusangane jamyo, na uno guiya jamyo unintrega yo.
21Alipokwisha sema hayo, Yesu alifadhaika sana rohoni, akasema wazi, "Kweli nawaambieni, mmoja wenu atanisaliti!"
22Y disipulo sija manaatan entre sija uno yan otro ya ti matungo jaye umadingan.
22Wanafunzi wakatazama wasiweze kabisa kujua anasema nani.
23Y uno gui disipuluña na guiniflie as Jesus, estaba umaason gui pechon Jesus.
23Mmoja wa wanafunzi, ambaye Yesu alikuwa anampenda sana, alikuwa ameketi karibu na Yesu.
24Ayo nae si Simon Pedro fumatinas señat nu este, para umafaesen jaye uje na umadingan.
24Basi, Simoni Petro akamwashiria na kusema: "Mwulize anasema juu ya nani."
25Ayo nae, y umaason gui jilo pechon Jesus ilegña nu güiya: Señot jaye uje?
25Mwanafunzi huyo akasogea karibu zaidi na Yesu, akamwuliza, "Bwana, ni nani?"
26Enaomina manope si Jesus: Ayo uje ni junafotgue ni pan ya junae güe. Ya janafotgon y pan, ya janae si Judas Iscariote, lajin Simon.
26Yesu akajibu, "Yule nitakayempa kipande cha mkate nilichochovya katika sahani, ndiye." Basi, akatwaa kipande cha mkate, akakichovya katika sahani, akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti.
27Anae munjayan y quinanoña ni y pan fotgon, si Satanas jumalom guiya güiya. Entonses si Jesus sinangane: Fatinas guse y finatinasmo.
27Yuda alipokwisha pokea kipande hicho, Shetani akamwingia. Basi Yesu akamwambia, "Unachotaka kufanya, kifanye haraka!"
28Ni uno, guiya sija na mangaegue gui lamasa, tumungo pot jafa na umasangane.
28Lakini hakuna hata mmoja wa wale waliokaa pale mezani aliyefahamu kwa nini alikuwa amemwambia hivyo.
29Pineloñija y palo guiya sija, sa si Judas na gaebetsa, na si Jesus sumangane: Fajan y güinaja na mannesesitajit para y guipot; pat ufanmanae y mamobble.
29Kwa kuwa Yuda alikuwa na wajibu wa kuutunza mfuko wa fedha, baadhi yao walidhani kwamba Yesu alikuwa amemwambia anunue vilivyohitajiwa kwa sikukuu, au kwamba alikuwa amemwambia akatoe chochote kwa maskini.
30Ya güiya, guinin mañule y pan fotgon, enseguidas mapos; ya esta puenge.
30Basi, Yuda alipokwisha twaa kile kipande cha mkate, akatoka nje mara. Na ilikuwa usiku.
31¶ Pot enao, anae esta mapos güe, ilegña si Jesus: Pago y Lajin taotao rumesisibe y minalagña, ya si Yuus rumesibe y minalagña guiya güiya.
31Baada ya Yuda kuondoka, Yesu akasema, "Sasa Mwana wa Mtu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
32Ya si Yuus minamalag güe guiya güiya; ya enseguidas unamalag güe.
32Na kama utukufu wa Mungu umefunuliwa ndani ya Mwana, basi, naye Mungu ataudhihirisha utukufu wa Mwana ndani yake mwenyewe, na atafanya hivyo mara.
33Mandiquique na fumaguon, ti juapmam guiya jamyo; ya inaligao yo; ya taegüenoja jusangane y Judio sija: Mano yo guato, jamyo ti siña manmamaela; taemanoja pago jusangane jamyo.
33"Watoto wangu, bado niko nanyi kwa muda mfupi tu. Mtanitafuta, lakini sasa nawaambieni yale niliyowaambia viongozi wa Wayahudi: Niendako ninyi hamwezi kwenda!
34Un tinago nuebo junae jamyo, na infanguaeya uno yan otro entre jamyo; taegüije yan guajo juguaeya jamyo, ya jamyo locue infanguaeya uno yan otro entre jamyo.
34Nawapeni amri mpya: pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda ninyi.
35Ya pot este todo y taotao ufanmatungo na jamyo disipulujo, yaguin infanguaeya uno yan otro entre jamyo.
35Mkipendana, watu wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu."
36Si Simon Pedro ilegña nu güiya: Señot, para mano jao? Ynepe as Jesus: Mano yo guato, ti siña jao pago undalalag yo, lao ti apmam undalalag yo.
36Simoni Petro akamwuliza, "Bwana, unakwenda wapi?" Yesu akajibu, "Niendako huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye."
37Ylegña nu güiya si Pedro: Señot, sa jafa na ti siña judalalag jao pago? jupolo y linâlâjo guiya jago.
37Petro akamwambia "Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Niko tayari kufa kwa ajili yako!"
38Ynepe as Jesus: Unpolo y linâlâmo guiya guajo? Magajet ya magajet jusangane jao, na ti uoo y gayo asta tiempo na undague yo tres biaje!
38Yesu akajibu, "Je, uko tayari kweli kufa kwa ajili yangu? Kweli nakwambia, kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu!"