1DESPUES di manmalofan estesija, mapos si Jesus malag y otro banda y tasen Galilea, na ayo y tasen Tiberias.
1Baada ya hayo, Yesu alivuka ziwa Galilaya (au Ziwa Tiberia).
2Ya madalalag güe ni y dangculo na linajyan taotao sa jalie sija y megaegae na señat ni jafatinas gui manmalango.
2Umati mkubwa wa watu ulimfuata kwa sababu watu hao walikuwa wameona ishara alizokuwa akifanya kwa kuwaponya wagonjwa.
3Ya cajulo si Jesus gui un ogso, ya matachong güije yan y disipuluña sija.
3Yesu alipanda mlimani, akaketi pamoja na wanafunzi wake.
4Ya jijot y guipot pascua, guipot y Judio sija.
4Sikukuu ya Wayahudi iitwayo Pasaka ilikuwa imekaribia.
5Ya anae tumalag jilo si Jesus, jalie na guaja mamamaela para iya güiya, un linajyan na taotao, ilegña as Felipe: Manu nae tafanmamajan pan para ufañocho este sija?
5Basi, Yesu na alipotazama na kuona umati wa watu ukija kwake, alimwambia Filipo, "Tununue wapi mikate ili watu hawa wapate kula?"
6Jasangan este para uchague güe; sa güiya tumungo jafa ufatinas.
6(Alisema hivyo kwa kumjaribu Filipo, kwani alijua mwenyewe atakalofanya.)
7Manope si Felipe: Dosiento na denario na pan, ti ufannajong para cada uno guiya sija ufañule didide.
7Filipo akamjibu, "Mikate ya denari mia mbili za fedha haiwatoshi watu hawa hata kama ila mmoja atapata kipande kidogo tu!"
8Ylegña nu güiya, uno gui disipuluña sija, Andres, chelun Simon Pedro:
8Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, nduguye Simoni Petro, akamwambia,
9Un patgon gaegue güine na guaja sinco pan sebada yan dos güijan na diquique: Lao jafa na estesija, gui entalo y este na minegae?
9"Yupo hapa mtoto mmoja aliye na mikate mitano ya shayiri na samaki wawili; lakini hivi vyatosha nini kwa watu wengi kama hawa?"
10Ylegña si Jesus: Nafanason y taotao. Ya megae na chaguan gaegue güije na lugat, ya manason y taotao, cana sinco mil na lalaje.
10Yesu akasema, "Waketisheni watu." Palikuwa na nyasi tele mahali hapo. Basi, watu wakaketi, jumla yapata wanaume elfu tano.
11Ya jachule si Jesus ayo sija na pan ya anae janae si Yuus grasias, jaipie todo ayo y manaason; taegüijija locue ni y güijan sija, jaf taemanoja y minalagoñija.
11Yesu akaitwaa ile mikate, akamshukuru Mungu, akawagawia watu waliokuwa wameketi; akafanya vivyo hivyo na wale samaki, kila mtu akapata kadiri alivyotaka.
12Ya anae manjaspog ilegña ni disipuluña sija: Joca todo y dinidide ni y tetenjan, sa munga guaja malingo.
12Watu waliposhiba Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Kusanyeni vipande vilivyobaki visipotee."
13Ya jajoca todo, ya janabula dose na canastran dangculo ni y dinidide, dinididin y sincoja na pan sebada, y tejnan ayo sija y mañocho.
13Basi, wakakusanya vipande vya mikate ya shayiri walivyobakiza wale watu waliokula, wakajaza vikapu kumi na viwili.
14Ayo sija na taotao, anae jalie y señat ni jafatinas si Jesus, ilegñija: Este senmagajet na güiya y profeta ni para umamaela gui tano.
14Watu walipoiona ishara hiyo aliyoifanya Yesu, wakasema, "Hakika huyu ndiye nabii anayekuja ulimwenguni."
15¶ Ayo na tiempo jatungo si Jesus, na ufanmamaela para umacone pot minetgot, ya jafatinas y ray, tumalo guato gui un jalomtano güigüiyaja namaesa.
15Yesu akajua ya kuwa watu walitaka kumchukua wamfanye mfalme, akaondoka tena, akaenda mlimani peke yake.
16Anae esta pupuenge manunog y disipuluña sija gui tase.
16Ilipokuwa jioni wanafunzi wake waliteremka hadi ziwani,
17Ya manjalom gui un sajyan, ya manchinichile ni tase para Capernaum. Ya pago jomjom, ya si Jesus ti manfinatotoe sija.
17wakapanda mashua ili wavuke kwenda Kafarnaumu. Giza lilikuwa limeingia, na Yesu alikuwa hajawafikia bado.
18Ya cajulo dangculo na napon pot rason un dangculo na manglo na manguaefe.
18Ziwa likaanza kuchafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma.
19Ya anae esta manmamogsae gui tase calang bente sinco pot trenta estadio, malie si Jesus na mamomocat gui jilo y tase ya lumalajijot guato gui sajyan: ya manmaañao sija.
19Wanafunzi walipokuwa wamekwenda umbali wa kilomita tano au sita, walimwona Yesu akitembea juu ya maji, anakaribia mashua; wakaogopa sana.
20Lao güiya ilegña nu sija: Guajoyo; chamiyo fanmaañao!
20Yesu akawaambia, "Ni mimi, msiogope!"
21Manmagof anae maresibe gui sajyan; ya ensiguidas mato y sajyan gui tano ni y jajananao güe.
21Walifurahi kumchukua Yesu katika mashua; na mara mashua ikawasili nchi kavu walipokuwa wanakwenda.
22¶ Y inagpaña na jaane, y linajyan taotao ni gaegue gui otro bandan tase, jalilie na taya güije mas na unoja na sajyan diquique, ya jatungo na si Jesus ti jumalom gui sajyan yan y disipuloña sija, lao y disipuloña sija esta manmapos sijaja;
22Kesho yake umati wa watu wale waliobaki upande wa pili wa ziwa walitambua kwamba kulikuwa na mashua moja tu pale, na Yesu hakuingia katika mashua pamoja na wanafunzi wake, ila wanafunzi hao walikuwa wamekwenda zao peke yao.
23(Ya manmato sija y sajyan diquique guine Tiberias, jijot güije na lugat anae mañocho ni pan, despues di y Señot janae si Yuus grasias.)
23Mashua nyingine kutoka Tiberia zilifika mahali hapo watu walipokula ile mikate, Bwana alipokwisha mshukuru Mungu.
24Ya anae jalie y linajyan taotao sija na si Jesus taegüe güije, ni y disipuluña sija; manjalom sija locue gui sajyan diquique, ya manmapos para Capernaum, maaliligao si Jesus.
24Basi, hao watu walipogundua kwamba Yesu na wanafunzi wake hawakuwapo mahali hapo, walipanda mashua, wakaenda Kafarnaumu wakimtafuta.
25Ya anae masoda gui otro bandan tase, ilegñija nu güiya: Rabi Ngaean nae mato jao güine?
25Wale watu walipomkuta Yesu ng'ambo ya pili wa ziwa walimwuliza, "Mwalimu, ulifika lini hapa?"
26Maninepe as Jesus ilegña: Magajet ya magajet jusangane jamyo; na inaliligao yo, ti pot y liniimiyo ni señat sija; lao pot y quinanomiyo ni pan, y ninafanjaspog jamyo.
26Yesu akawajibu, "Kweli nawaambieni, mnanitafuta si kwa kuwa mmeona ishara, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba.
27Fanmachocho, munga para ayo y fafalingo na nengcano, lao ayo na nengcano y sumaga taejinecog na linâlâ, ni y Lajin taotao numae jamyo; sa güiya sineyo ni Tata, si Yuus.
27Msikishughulikie chakula kiharibikacho; kishugulikieni chakula kidumucho kwa ajili ya uzima wa milele. Mwana wa Mtu ambaye Baba amemthibitisha atawapeni chakula hicho."
28Enao mina ilegñija nu güiya: Jafa tafatinas, para utafatinas y checho Yuus?
28Wao wakamwuliza, "Tufanye nini ili tuweze kuzitenda kazi za Mungu?"
29Si Jesus manope ilegña nu sija: Este y checho Yuus, na injenggue ayo y jatago.
29Yesu akawajibu, "Hii ndiyo kazi anayotaka Mungu muifanye: kumwamini yule aliyemtuma."
30Entonses ilegñija nu güiya: Jafa na señat unfatinas para inlie, ya injenggue jao? Jafa chechomo?
30Hapo wakamwambia, "Utafanya ishara gani ili tuione tupate kukuamini? Utafanya kitu gani?
31Si tatanmame jacano y mana gui desierto, taemanoja y munjayan matugue; pan guine y langet manmanae para u jacano.
31Wazee wetu walikula mana kule jangwani, kama yasemavyo Maandiko: Aliwalisha mkate kutoka mbinguni."
32Ya ilegña si Jesus nu sija: Magajet ya magajet jusangane jamyo, na ti si Moises numae jamyo ni pan guine y langet, si Tatajo janae jamyo ni magajet na pan guine y langet.
32Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, Mose hakuwapeni mkate kutoka mbinguni; Baba yangu ndiye awapaye ninyi mkate halisi kutoka mbinguni.
33Sa y pan Yuus ayo y tumunog guine y langet, ya jananae linâlâ y tano.
33Maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na aupaye ulimwengu uzima."
34Ayo nae ilegñija nu güiya: Señot naejam siempre ni este na pan!
34Basi, wakamwambia, "Mheshimiwa, tupe daima mkate huo."
35Si Jesus ilegña nu sija: Guajo y pan lalâlâ; y mato guiya guajo, ti uñalang; ya y jumonggue yo, ti umajo para taejinecog.
35Yesu akawaambia, "Mimi ndimi mkate wa uzima. Anayekuja kwangu hataona njaa; anayeniamini hataona kiu kamwe.
36Lao jusangane jamyo; na este inlie yo ya ti injenggue.
36Lakini niliwaambieni kwamba ingawa mmeniona hamniamini.
37Todo y janae yo si Tata, ufato guiya guajo; ya ayo y ufanmato guiya guajo, gosmagajet na guajo ti siña juyute güe juyong.
37Wote anaonipa Baba watakuja kwangu; nami sitamtupa nje yeyote anayekuja kwangu,
38Sa tumunog yo guine y langet ti para jufatinas y minalagojo, lao y minalagoña ayo y tumago yo.
38kwani nimeshuka kutoka mbinguni si kwa ajili ya kufanya matakwa yangu, ila kutimiza matakwa ya yule aliyenituma.
39Ya este y minalagoña ayo y tumago yo, na todo y janae yo ti siña junafalingo taya, lao junacajulo güe gui uttimo na jaane.
39Na matakwa ya yule aliyenituma ndiyo haya: nisimpoteze hata mmoja kati ya wale alionipa, ila niwafufue wote Siku ya mwisho.
40Ya este y minalagon Tata, na todo ayo y jalie y Lajiña ya jinenggue guiya güiya, uguaja linâlâña taejinecog; ya junacajulo güe gui uttimo na jaane.
40Maana anachotaka Baba yangu ndicho hiki: kila amwonaye Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele; nami nitamfufua Siku ya mwisho."
41¶ Enaomina y Judio sija mamofea güe anae jasangan: Guajo y pan ni tumunog guine y langet.
41Basi, Wayahudi wakaanza kunung'unika kwa kuwa alisema: "Mimi ni mkate ulioshuka kutoka mbinguni."
42Ya ilegñija: Ada ti güiya este as Jesus lajin José? si tataña, yan nanaña tatungoja? Jafa pues muna ilegña: Guajo tumunog guine y langet?
42Wakasema, "Je, huyu si mwana wa Yosefu? Tunawajua baba yake na mama yake! Basi, anawezaje kusema kwamba ameshuka kutoka mbinguni?"
43Si Jesus manope ya ilegña nu sija: Chamiyo fanmanmofefea entre jamyo.
43Yesu akawaambia, "Acheni kunung'unika ninyi kwa ninyi.
44Taya siña mato guiya guajo yaguin si Tata, ni tumago yo, ti quinene güe; ya guajo junacajulo güe gui uttimo na jaane.
44Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, Baba aliyenituma asipomvuta kwangu; nami nitamfufua mtu huyo Siku ya mwisho.
45Matugue esta gui profeta sija: Ya todo ayo sija ufanmafanagüe finanagüen Yuus. Enaomina cada uno ni jumungog y Tata ya jatungo y mafanagüeña, ufato guiya guajo.
45Manabii wameandika: Watu wote watafundishwa na Mungu. Kila mtu anayemsikia Baba na kujifunza kutoka kwake, huja kwangu.
46Munga yo na jusangan na guaja na taotao y esta jalie si Tata, lao ayo y mamaela guinin as Yuus, güiyaja jalie si Tata.
46Hii haina maana kwamba yupo mtu aliyemwona Baba, isipokuwa yule aliyetoka kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba.
47Magajet ya magajet jusangane jamyo: Ayo y jumonggue yo guaja linâlâña na taejinecog,
47Kweli, nawaambieni, anayeamini anao uzima wa milele.
48Guajo y pan y linâlâ.
48Mimi ni mkate wa uzima.
49Si tatanmiyo, jacano y mana gui jalomtano ya manmatae.
49Wazee wenu walikula mana kule jangwani, lakini walikufa.
50Estagüiya y pan ni tumunog guine y langet, para jaye y cumano güe, ti umatae.
50Huu ndio mkate kutoka mbinguni; mkate ambao anayekula hatakufa.
51Guajo y lalâlâ na pan ni tumunog guine y langet: yaguin guaja cumano este na pan, ulâlâ para todo y tiempo; junggan ya y pan ni guajo mannae, guiya mismo catneco, na junae para linâlâ y tano.
51Mimi ni mkate hai ulioshuka kutoka mbinguni. Mtu yeyote akila mkate huu ataishi milele. Na mkate nitakaompa ni mwili wangu ninaoutoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu."
52¶ Managuaguat entre sija y Judio sija, ilegñija: Jafa muna usiña este na taotao unaejit ni catneña para utacano?
52Ndipo Wayahudi wakaanza kubishana kati yao:
53Si Jesus pot anão ilegña nu sija: Magajet ya magajet jusangane jamyo: Yaguin ti incano y catnen y Lajin taotao, ya ti inguimen y jâgâña, taya linâlâ guiya jamyo.
53Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, msipokula mwili wa Mwana wa Mtu na kunywa damu yake, hamtakuwa na uzima ndani yenu.
54Y cumano y catneco, ya jaguimen y jâgâjo, guaja linâlâña taejinecog, ya junacajulo güe gui uttimo na jaane.
54Anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu anao uzima wa milele nami nitamfufua siku ya mwisho.
55Sa y catneco, güiya y magajet na nengcano; ya y jâgâjo, güiya y magajet na guimen.
55Maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
56Ayo y cumano y catneco, y jaguimen y jâgâjo, sumaga guiya guajo, ya guajo guiya güiya.
56Aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, akaa ndani yangu, nami nakaa ndani yake.
57Taegüine y Tata, ni lalâlâ, janamamaela yo, ya guajo lalâlâ pot si Tata; taegüineja locue y cumano yo, güiya locue ulâlâ pot guajo.
57Baba aliye hai alinituma, nami naishi kwa sababu yake; vivyo hivyo anilaye mimi ataishi pia kwa sababu yangu.
58Estagüiya y pan ni tumunog guine y langet; ti parejo yan y tatanmiyo ni cumano y mana ya manmatae: y cumano este na pan ulâlâ para taejinecog.
58Basi, huu ndio mkate ulioshuka kutoka mbinguni; si kama mana waliyokula babu zetu, wakafa. Aulaye mkate huu ataishi milele."
59Este sija jasangan guiya sunagoga, parejoja yan anae mamanagüe guiya Capernaum.
59Yesu alisema hayo alipokuwa akifundisha katika sunagogi kule Kafarnaumu.
60¶ Enaomina megae gui disipuluña sija anae majungog este, ilegñija: Majetog na sinangan este; jaye siña umecungog?
60Basi, wengi wa wafuasi wake waliposikia hayo, wakasema, "Haya ni mambo magumu! Nani awezaye kuyasikiliza?"
61Si Jesus jatungo pot güiyaja namaesa, na y disipuluña sija mangogonggong pot este, ya ilegña nu sija: Ninafañatsaga jamyo nu este?
61Yesu alijua bila kuambiwa na mtu kwamba wanafunzi wake walikuwa wananung'unika juu ya jambo hilo, akawauliza, "Je, jambo hili linawafanya muwe na mashaka?
62Jafa yaguin inlie y Lajin taotao cajulo anae gaegue antes?
62Itakuwaje basi, mtakapomwona Mwana wa Mtu akipanda kwenda kule alikokuwa kwanza?
63Y espiritu mannanae linâlâ; y catne taya probechoña: y sinangan sija ni jusangane jamyo, ayo espiritu, yan ayo linâlâ.
63Roho ndiye atiaye uzima; binadamu peke yake hawezi. Maneno niliyowaambieni ni Roho, ni uzima.
64Lao guajo palo guiya jamyo na ti manmanjonggue. Sa si Jesus desde y finenana jatungoja jaye sija y ti ufanmanjonggue, yan jaye y uinentrega güe.
64Hata hivyo, wako baadhi yenu wasioamini." (Yesu alisema hivyo kwani alijua tangu mwanzo ni kina nani wasioamini, na pia ni nani atakayemsaliti.)
65Ya ilegña: Pot este na rason jusangane jamyo: na taya siña mato guiya guajo, yaguin ti ninae ni Tatajo.
65Kisha akasema, "Ndiyo maana niliwaambieni kwamba hakuna awezaye kuja kwangu asipowezeshwa na Baba yangu."
66¶ Ayo nae, megae gui disipoluña sija manalo tate, ya ti mañija talo manjanao yan güiya.
66Kutokana na hayo, wengi wa wafuasi wake walirudi nyuma wasiandamane naye tena.
67Ayo nae ilegña si Jesus ni dose: Manmalago jamyo manjanao locue?
67Basi, Yesu akawauliza wale kumi na wawili, "Je, nanyi pia mwataka kwenda zenu?"
68Ynepe as Simon Pedro: Señot, jayejam injanao güe? Jago nae guaja sija y sinangan ni taejinecog na linâlâ.
68Simoni Petro akamjibu, "Bwana, tutakwenda kwa nani? Wewe unayo maneno yaletayo uzima wa milele.
69Ya jame injenggue, ya intingo na jago Ayo na Santos na guine as Yuus.
69Sisi tunaamini, na tunajua kwamba wewe ndiwe yule Mtakatifu wa Mungu."
70Si Jesus jaope sija: Ti juayig jamyo dose, ya y uno guiya jamyo anite?
70Yesu akawaambia, "Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Hata hivyo, mmoja wenu ni Ibilisi!"
71Ya jasangan pot si Judas Iscariote, lajin Simon: sa este y para uinentrega gae, uno gui dose.
71Yesu alisema hayo juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti; maana huyu alikuwa ndiye atakayemsaliti, ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili.