Chamorro: Psalms, Gospels, Acts

Swahili: New Testament

John

9

1ANAE malofan gui sanmenan, jalie un taotao na bachet desde y mafañagoña.
1Yesu alipokuwa akipita alimwona mtu mmoja, kipofu tangu kuzaliwa.
2Ya mafaesen güe ni y disipuloña ilegñija: Rabi, jaye umisao, este na taotao pat y mañaenaña, para que umafañago bachet?
2Basi, wanafunzi wakamwuliza, "Mwalimu! Ni nani aliyetenda dhambi: mtu huyu, ama wazazi wake, hata akazaliwa kipofu?"
3Manope si Jesus: Ti umisao este na taotao ni sija manaenaña lao para y finatinas Yuus ya ufafanue guiya güiya.
3Yesu akajibu, "Jambo hili halikutukia kwa sababu ya dhambi zake yeye, wala dhambi za wazazi wake; ila alizaliwa kipofu ili nguvu ya Mungu ionekane ikifanya kazi ndani yake.
4Tanesesita na infatitinas y checho ayo y tumago yo mientras y jaane; sa an mato y puenge, taya siña machocho.
4Kukiwa bado mchana yatupasa kuendelea kufanya kazi za yule aliyenituma; maana usiku unakuja ambapo mtu hawezi kufanya kazi.
5Anae gagaegue yo gui jilo y tano, y candet y tano guajoja.
5Wakati ningali ulimwenguni, mimi ni mwanga wa ulimwengu."
6Munjayan jasangan este, tumola gui tano, ya jafatinas fache nu y tela, ya y fache japalae y atadog y bachet,
6Baada ya kusema hayo, akatema mate chini, akafanyiza tope, akampaka yule kipofu machoni,
7Ya ilegña nu güiya: Janao fagase jao gui estanque Siloe (Ya cumequeilegña, tinago). Enao mina maposgüe ya fagase güe, ya anae tumalo guato este manlie.
7akamwambia, "Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu." (maana ya jina hili ni "aliyetumwa"). Basi, huyo kipofu akaenda, akanawa, kisha akarudi akiwa anaona.
8Pot este y tiguangña sija yan ayo y guinin manmalie antes, ya matungo na ampmam na mangagagao limosña, ilegñija: Ada ti este güiya ayo y matatachong ya gagao?
8Basi, jirani zake na wale waliokuwa wanajua kwamba hapo awali alikuwa maskini mwombaji, wakasema, "Je, huyu siye yule maskini aliyekuwa akiketi na kuomba?"
9Guaja sija sumangan: Güiya este; ya guaja palo sija sumangan: Ale, lao parejo yan güiya. Lao güiyaja ilegña: Guajo yo.
9Baadhi yao wakasema, "Ndiye." Wengine wakasema, "La! Ila anafanana naye." Lakini huyo aliyekuwa kipofu akasema, "Ni mimi!"
10Ya ilegñija nu güiya: Jaf taemano mababaña y atadogmo?
10Basi, wakamwuliza, "Sasa, macho yako yalipataje kufumbuliwa?"
11Manope ya ilegña: Ayo na taotao, naanña si Jesus, güiya fumatinas y fachae ya palae y atadogco, ya ilegña nu guajo: Janao falag y estanque Siloe ya unfagase jao! Mapos yo ya jufagase yo ya juresibe y liniijo.
11Naye akawajibu, "Yule mtu aitwaye Yesu alifanya tope, akanipaka machoni na kuniambia: Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu. Basi, mimi nikaenda, nikanawa, nikapata kuona."
12Ya ilegñija nu güiya: Manggue yuje? Ylegña: Ti jutungo.
12Wakamwuliza, "Yeye yuko wapi?" Naye akawajibu, "Mimi sijui!"
13¶ Macone guato gui Fariseo sija y guinin manbachet.
13Kisha wakampeleka huyo mtu aliyekuwa kipofu kwa Mafarisayo.
14Ya ayo na jaane sabado anae si Jesus jafatinas y fachae, ya jababa y atadogña sija.
14Siku hiyo Yesu alipofanya tope na kumfumbua macho mtu huyo, ilikuwa siku ya Sabato.
15Y Fariseo sija locue mafaesen güe talo: Jafa muna manlie güe. Ya ilegña nu sija: Janaye ni fachae y sanjilo gui atadogco, ya jufagase yo, ya manlie yo.
15Basi, Mafarisayo wakamwuliza mtu huyo, "Umepataje kuona?" Naye akawaambia, "Alinipaka tope machoni, nami nikanawa na sasa naona."
16Ya palo gui Fariseo sija ilegñija: Este na taotao ti güiya guinin as Yuus, sa ti jaadaje y sabado. Lao palo sija ilegñija: Jafa muna siña un taotao ni gaeisao, jafatitinas taemanoja y señat sija? Ya guaja dibision gui entaloñija.
16Baadhi ya Mafarisayo wakasema, "Mtu huyu hakutoka kwa Mungu, maana hashiki sheria ya Sabato." Lakini wengine wakasema, "Mtu mwenye dhambi awezaje kufanya ishara za namna hii?" Kukawa na mafarakano kati yao.
17Ylegñija talo ni bachet: Jago, jafa ilegmo nu güiya, ya esta mababa pot güiya y atadogmo sija? Ya ilegña: Profetagüe.
17Wakamwuliza tena huyo mtu aliyekuwa kipofu, "Maadam yeye amekufungua macho, wasemaje juu yake?" Naye akawaambia, "Yeye ni nabii!"
18Ayo nae y Judio sija, ti majonggue y esta masangan na güiya, y guinin bachet, ya esta jarisibe y liniiña, asta que nae maagange y mañaena y bachet ni esta jarisibe liniiña.
18Viongozi wa Wayahudi hawakusadiki kwamba mtu huyo alikuwa kipofu hapo awali na sasa anaona mpaka walipowaita wazazi wake.
19Ya manmafaesen ilegñija: Este patgonmiyo ni ilegmiyo bachet guinin y mafañagoña? Ya jafa pago ninamanlie?
19Basi, wakawauliza hao wazazi, "Je, huyu ndiye mtoto wenu ambaye ninyi mwasema alizaliwa kipofu? Sasa amepataje kuona?"
20Manope y tata ya, ilegñija: Yntingo na este patgonmame, ya bachet guinin y mafañagoña:
20Wazazi wake wakajibu, "Tunajua kwamba huyu ni mtoto wetu, na kwamba alizaliwa kipofu.
21Lao jaftaemano pago na manliigüe, ti intingo; pat jaye bumaba y atadogña, ti intingo; faesen güe; guaja sacanña: Güiya usangan pot güiyaja namaesa.
21Lakini amepataje kuona, hatujui; na wala hatumjui yule aliyemfumbua macho. Mwulizeni yeye mwenyewe; yeye ni mtu mzima, anaweza kujitetea mwenyewe."
22Este sija ilegñija si mañaenaña, sa manmaañao ni y Judio sija: sa unoja na jinaso gui entalo y Judio sija, na yaguin guaja sumangan na güiya si Cristo, umayute güe gui sanjiyong y sinagoga.
22Wazazi wake walisema hivyo kwa sababu waliwaogopa viongozi wa Wayahudi kwani viongozi hao walikuwa wamepatana ya kwamba mtu yeyote atakayekiri kwamba Yesu ni Kristo atafukuzwa nje ya sunagogi.
23Pot este ilegñija sija mañaenaña: Gauja sacaña; faesen güe.
23Ndiyo maana wazazi wake walisema: "Yeye ni mtu mzima, mwulizeni."
24Enao mina sija maagange talo y taotao ni y guinin bachet, ya ilegñija nu guiya: Nae minalag si Yuus: Jita tumungo na este na taotao güiya taotao isao güe.
24Basi, wakamwita tena aliyekuwa kipofu, wakamwambia, "Sema ukweli mbele ya Mungu! Sisi tunajua kwamba mtu huyu ni mwenye dhambi."
25Entonses manope yuje: Cao taotao isao güe, ti jutungo; unoja jugoftungo; na guajo, guinin bachet yo, ya pago manlie yo.
25Yeye akajibu, "Kama ni mwenye dhambi mimi sijui. Lakini kitu kimoja najua: Nilikuwa kipofu, na sasa naona."
26Entonses ilegñija talo: Jafa finatinasña nu jago? Jaftaemano jababa y atadogmo?
26Basi, wakamwuliza, "Alikufanyia nini? Alikufumbuaje macho yako?"
27Maninepe sija: Jusangane jamyo esta, ya ti injingog: Jafa muna manmalago jamyo injingog talo? Ada manmalago jamyo buente locue disipuluña?
27Huyo mtu akawajibu, "Nimekwisha waambieni, nanyi hamkusikiliza; kwa nini mwataka kusikia tena? Je, ninyi pia mnataka kuwa wafuasi wake?"
28Entonses janafanmamajlao ya ilegñija: Jago disipuluña; ya jame disipulon Moises!
28Lakini wao wakamtukana wakisema, "Wewe ni mfuasi wake; sisi ni wafuasi wa Mose.
29Jame intingo na si Yuus guinin jasangan pot si Moises; lao este na taotao ti intingo taotao mano güe.
29Sisi tunajua kwamba Mungu alisema na Mose, lakini mtu huyu hatujui ametoka wapi!"
30Manope y taotao ya ilegña nu sija: Jafa na namanman este, ya ti intingo jamyo taotao mano; ya güiya bumaba y atadogco!
30Naye akawajibu, "Hili ni jambo la kushangaza! Ninyi hamjui ametoka wapi, lakini amenifumbua macho yangu!
31Jame intingo na si Yuus ti jajungog y manisao; yaguin guaja maañao as Yuus ya jaosgue y minalagoña, este jiningog.
31Tunajua kwamba Mungu hawasikilizi watu wenye dhambi, ila humsikiliza yeyote mwenye kumcha na kutimiza mapenzi yake.
32Guinin y tutujon y tano, taya nae majungog, ni uno mababa atadogña ni mafañago bachet.
32Tangu mwanzo wa ulimwengu haijasikika kwamba mtu ameyafumbua macho ya mtu aliyezaliwa kipofu.
33Yaguin este ti guine as Yuus, ti siña jafatinas jafa.
33Kama mtu huyu hakutoka kwa Mungu, hangeweza kufanya chochote!"
34Sija manmanope ilegñija nu güiya: Jago mafañago jao gui isao sija! Ada jago fumanagüe jam? Ya mayute juyong.
34Wao wakamjibu, "Wewe ulizaliwa na kulelewa katika dhambi; unawezaje kutufundisha sisi?" Basi, wakamfukuzia mbali.
35¶ Jajungog si Jesus na mayute juyong, ya anae jasoda, ilegña: Unjonggue y Lagin Yuus?
35Yesu alisikia kwamba walikuwa wamemfukuzia mbali, naye alipomkuta akamwuliza, "Je, wewe unamwamini Mwana wa Mtu?"
36Manope güe ya ilegña: Jaye enao Señot, para guajo umajonggue güe?
36Huyo mtu akajibu, "Mheshimiwa, niambie yeye ni nani, ili nipate kumwamini."
37Ylegña nu güiya si Jesus: Esta unlie güe ya ayo y umadingangange jao, güiya güe.
37Yesu akamwambia, "Umekwisha mwona, naye ndiye anayesema nawe sasa."
38Ya ilegña: Jujonggue, Señot. Ya jaadora güe.
38Basi, huyo mtu akasema, "Ninaamini Bwana!" Akamsujudia.
39Ylegña si Jesus: Guajo pot juisio mamaela yo güine gui jilo y tano, para y ti manmanlilie, ufanmanlie; ya y manmanlie, ayo sija ufanbachet.
39Yesu akasema, "Mimi nimekuja ulimwenguni kutoa hukumu, kusudi wasioona wapate kuona, na wale wanaoona wawe vipofu."
40Ya manmanjungog y ayo na Fariseo sija ni y mangaegue guiya güiya ya ilegñija nu güiya: Jame locue, manbachet jam?
40Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa pamoja naye walisikia maneno hayo, wakamwuliza, "Je, sisi pia ni vipofu?"
41Ylegña nu sija si Jesus: An mojon manbachet jamyo, taya isaomiyo; pago nae insasangan, talie; enao mina isaomiyo gagaegue.
41Yesu akawajibu, "Kama mngekuwa vipofu, hamngekuwa na hatia; lakini sasa ninyi mwasema: Sisi tunaona, na hiyo yaonyesha kwamba mna hatia bado.