Chamorro: Psalms, Gospels, Acts

Swahili: New Testament

Luke

22

1AYO nae estaba jijijot y jaanin y guipot y pan ni taelibadura, ni mafanaan pascua.
1Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
2Ya y magas mamale yan y escriba sija maaliligao jaftaemano para umapuno güe; lao manmaañao ni y taotaosija.
2Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
3¶ Ya jumalom si Satanas gui as Judas y apeyiduña Iscariote, uno gui numerou y dose.
3Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
4Ya maposgüe, ya manguentos yan y magas mamale, yan y manmagas, jafataemano para uinentrega guiya sija.
4Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
5Ya ninafanmagof, ya matratos na umanae salape.
5Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
6Ya manpromete ya jaaliligao lugat para uqueentrega guiya sija, yanguin manaegüe y linajyan taotao.
6Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
7¶ Ya mato y jaanin y taelibadura na pan, anae nesesita umaofrese y pascua.
7Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
8Ya jatago si Pedro yan Juan, ilegña: Janao ya innalisto y pascua para jita, para utafañocho.
8Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, "Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka."
9Ya sija ilegñija nu güiya: Mano malagomo nae innalisto?
9Nao wakamwuliza, "Unataka tuiandae wapi?"
10Ya ilegña nu sija: Estagüe, anae manjalom jamyo gui siuda, infanasoda güije yan un taotao, na mañuñule un jarran janom; dalalaque güe jalom mano na guma nae jumalom.
10Akawaambia, "Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
11Ya inalog ni y gaéguima: Y Maestro ilegña nu jago: Manggue y aposento anae para juchocho gui pascua yan y disipulujo sija?
11Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
12Ya infanfinanue ni y dangculo na aposento gui sanjilo todo cabales: ayonae innalisto.
12Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo."
13Ya manjanao ya masoda jaftaemano y mansinangane sija; ya manalisto para y pascua.
13Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
14¶ Ya anae mato y ora, matachong papa mañija yan y dose na apostoles.
14Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
15Ya ilegña nu sija: Jagasja juguefdesea na utafañocho guine na pascua antes di jufamadese:
15Akawaambia, "Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
16Sa jusangane jamyo: Ti juchocho mas, asta qui macumple gui raenon Yuus.
16Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu."
17Ya juresibe y copa ya janae grasia, ya ilegña: Chule este, ya infanafacae entre jamyo:
17Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, "Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
18Sa jusangane jamyo na ti juguimen otro biaje ni y tinegcha ubas, asta qui ufato y raenon Yuus.
18Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja."
19Ya jachule y pan, ya anae janae grasia, jaipe, ya janae sija, ilegña: Este y tataotaojo, ni y manmanae jamyo: fatitinas este para injajasoyo.
19Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, "Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka."
20Taegüijeja locue y copa, anae munjayan mañena ilegña: Este na copa y nuebo na trato gui jâgâjo, ni y machuda pot jamyo.
20Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, "Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
21Lao estagüeja y canae y umentregayo na jumajame gui lamasa.
21"Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
22Ya magajet na y Lajin taotao ujanao, ni y esta manfagpo, lao ay ay ayo na taotao uinentrega!
22Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti."
23Ya jatutujon manafaesen entre sija, jae guiya sija ufinatinas este.
23Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
24¶ Ya guaja locue inaguaguat guiya sija, jaye umasdangculo.
24Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
25Ya ilegña nu sija: Y ray y Gentiles, jafatitinas minagas gui jiloñija; ya ayo y fumatitinas ninasiña gui jiloñija, manmafanaan manmauleg na taotao.
25Yesu akawaambia, "Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
26Lao ti infanaegüenao: sa jaye y mas dangculo guiya jamyo, ufamataegüije y mas diquique; ya y magas, ufamataegüije y mañeñetbe.
26Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
27Sa cao dangculoña, ayo y matatachong chumocho, pat ayo y mañeñetbe? ti ayo y matachong chumocho; lao guajo gaegue gui entalonmiyo taegüije ayo y mañeñetbe.
27Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
28Jamyo ayo sija y sumisigueja mangachongjo gui tentasionjo.
28"Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
29Ya juaregla un raeno para jamyo, taegüije y as Tata ni y jaaregla y raeno para guajo.
29na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
30Para infañocho yan infanguimen, gui lamasajo gui raenoco; ya infanmatachong gui trono sija ya injisga y dose na tribo guiya Israel.
30Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
31Simon, Simon, estagüe, si Satanas, na malago nu jago para unquinila gui coladot taegüije y trigo;
31"Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
32Lao guajo tayuyute jao, para chaña fafatta y jinengguemo: ya yanguin umabira jao, nafanfitme y mañelumo.
32Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako."
33Ya ilegña nu güiya: Señot, estayo listo para judalalag jao para y catset yan para y finatae.
33Naye Petro akamjibu, "Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa."
34Ya ilegña: Jusangane jao Pedro, na ti uoo y gayo pago na jaane, antes di undagueyo tres biaje na guinin untungoyo.
34Yesu akamjibu, "Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu."
35¶ Ya ilegña nu sija: Anae jutago jamyo sin botsa, yan sin maleta, yan sin sapatos, guaja fattanmiyo? Ya ilegñija: Taya.
35Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, "Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?" Wakajibu, "La."
36Ayonae ilegña nu sija: Lao pago, y gaebotsa, uchuleja, yan taegüenaoja locue y maleta: ya jaye y taya espadaña, ubende y magaguña ya ufamajan uno.
36Naye akawaambia, "Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
37Sa jusangane jamyo, na este y esta matugue, nesesita na umacumple guiya guajo: Ya matufong gui entalo y manaelaye sija: sa y güinaja sija pot guajo, umanafanfagpo.
37Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake."
38Ya ilegñija: Señot, estagüeja dos na espada. Ya ilegña nu sija: Esta najong.
38Nao wakasema, "Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili." Naye akasema, "Basi!"
39Ya jumuyong, ya mapos, taegüijeja y costumbreña, para y egso Olibo; ya matatiye locue ni y disipuluña.
39Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
40Ya anae mato gui lugat, ilegña nu sija: Fanmanaetae, ya chamiyo fanjajalom gui tentasion.
40Alipofika huko akawaambia, "Salini, msije mkaingia katika kishawishi."
41Ya sumuja guiya sija, gui un inagüit acho; ya dumimo, ya manaetae,
41Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
42Ylegña: Tata, yanguin malago jao, nasuja guiya guajo este y copa: lao munga mafatinas y malagojo, lao y malagomo.
42"Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu."
43Ya finatoigüe güije un angjet guinin y langet, ya ninametgot.
43Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
44Ya anae estaba umagoninias, mas fejman manaetae: ya y masajalomña taegüije y mandangculo na gotan jâgâ, mamopodong papa gui eda.
44Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
45Ya anae cajulo guinin manaetae, ya mato gui disipuluña, jasoda na manmamaego sa mantriste,
45Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
46Ya ilegña nu sija: Jafa na manmamaego jamyo? fangajulo ya infanmanaetae, sa noseaja infanjalom gui tentasion.
46Akawaambia, "Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi."
47¶ Ya mientras cumuecuentos, estagüe un manadan taotao, yan ayo y mafanaan si Judas, uno gui dose, na mafona gui menanñija, ya jumijijot gui as Jesus para uchico.
47Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
48Lao si Jesus ilegña nu güiya: Judas, pot un chicoja na unentrega y Lajin taotao?
48Lakini Yesu akamwambia, "Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?"
49Ya anae malie, ni ayo sija y mangaegue gui oriyaña, jafa ujuyong, ilegñija: Señot, intaga ni y espada?
49Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, "Bwana, tutumie panga zetu?"
50Ya uno guiya sija jataga y tentago y magas mamale, ya jautut y agapa na talangaña.
50Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
51Ya manope si Jesus ilegña: Polo este esta. Ya japacha y talangaña, ya janamagong.
51Hapo, Yesu akasema, "Acha! Hii inatosha." Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
52Ayonae ilegña si Jesus ni y magas mamale, yan y capitan sija gui templo, yan y manamco sija ni y manmato guiya güiya: Manmato jamyo yan espada yan galute, taegüije y contra y saque?
52Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: "Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
53Anae estaba manjijitaja cada jaane gui templo, taya nae inestira y canaenmiyo contra guajo: lao este oranmiyo, yan y ninasiñan jinemjom.
53Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza."
54Ya maguot güe ya macone guato gui guima y magas mamale. Ya tinatitiyeja as Pedro lachago.
54Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
55Ya anae munjayan matotne y guafe gui talo gui patio, ya mandaña manmatachong, matachong si Pedro gui entaloñija.
55Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
56Ya linie ni un criada anae matachong gui ininan guafe, ya guinesatangüe, ya ilegña: Este locue na taotao manisija.
56Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, "Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu."
57Ya jadague, ilegña: Palaoan, ti jutungo güe.
57Lakini Petro akakana akisema, "Wee! simjui mimi."
58Ya anae na apmam linie ni otro ya ilegña: Mangachochongmo yuje sija? ya ilegña si Pedro: Taotao, ti guajo.
58Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, "Wewe ni mmoja wao." Lakini Petro akajibu "Bwana we; si mimi!"
59Ya anae malofan una ora, otro jagosasegura ilegña: Magajet na sumisija este yan ayo, sa taotao Galilea locue este.
59Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, "Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati."
60Ya si Pedro ilegña: Taotao, ti jutungo jafa ilelegmo. Ya mientras cumecuentos, enseguidas umoo y gayo.
60Lakini Petro akasema, "Bwana wee; sijui hata unachosema!" Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
61Ya jabira güe y Señot ya jaaatan si Pedro. Ayonae jajaso si Pedro y sinangan y Señot, ni y ilegña nu güiya: Antes que uoo y gayo pago na jaane, undagueyo tres biaje.
61Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: "Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu."
62Ya jumuyong si Pedro ya guefcumasao.
62Hapo akatoka nje, akalia sana.
63¶ Ya y taotao sija ni gumuguot si Jesus, mabotlelea ya manalalamen.
63Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
64Ya anae mabendas y atadogña, mafaesen ilelegñija: Sangan; jaye jao munalamen?
64Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, "Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!"
65Ya megae sija na chinatfino masasangan contra guiya, manamamajlao güe.
65Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
66¶ Ya anae manana mandaña sija y inetnon manamco na taotao sija y magas y mamale yan y escribas: ya macone guato gui tribunatñija, ilegñija:
66Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
67Yaguin jago si Jesucristo, sangane jam. Lao ilegña nu sija: Yaguin jusangane jamyo, ti injenggue yo;
67Nao wakamwambia, "Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?" Lakini Yesu akawaambia, "Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
68Ya yaguin guajo jamyo fumaesen, ti inepeyo.
68na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
69Lao desde pago para mona y Lajin taotao gaegue na matatachong gui agapa gui ninasiñan Yuus.
69Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi."
70Ya ilegña todos: Ayonae Lajin Yuus jao? Ya ilegña nu sija: Jamyo umalog na guajo yo.
70Hapo wote wakasema, "Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?" Naye akasema, "Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye."
71Ayonae ilegñija: Jafa mas na testimonio tanesesita? sa tajungogja esta gui pachotña.
71Nao wakasema, "Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe."