1YA todo y linajyanñija mangajulo, ya macone asta as Pilatos.
1Kisha, wote kwa jumla, wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
2Ya matutujon mafaaela ilegñija: Inseda este na taotao na janaquequelache y nasionta, yan mañoñoma na umanae tributo si Sesat, ya ilelegña na güiya si Cristo un ray.
2Wakaanza kumshtaki wakisema: "Tulimkuta mtu huyu akiwapotosha watu wetu, akipinga kulipa kodi kwa Kaisari na kujiita ati yeye ni Kristo, Mfalme."
3Ayonae si Pilatos finaesen ilegña: Jago y Ray y Judio sija? ya inepe ya ilegña: Jago umalog.
3Pilato akamwuliza Yesu, "Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?" Yesu akamjibu, "Wewe umesema."
4Ya si Pilatos ilegña ni y magas y mamale, yan y linajyan taotao sija: Taya isao jusoda güine na taotao.
4Pilato akawaambia makuhani wakuu na umati wa watu, "Sioni kosa lolote katika mtu huyu."
5Lao sija japotfia, ilegñija: Jaatbororota y taotao sija, mamananagüe guiya Judea todo, jatutujon desde Galilea asta esteja na lugat.
5Lakini wao wakasisitiza wakisema: "Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika nchi yote ya Yudea; alianza Galilaya, na sasa yuko hapa."
6Ya anae jajungog este si Pilatos, mamaesen cao taotao Galilea.
6Pilato aliposikia hayo, akauliza, "Je, mtu huyu ni mwenyeji wa Galilaya?"
7Ya anae jatungo na gaegue gui sisiñan Herodes, janamanajanao asta as Herodes, sa estaba güe locue guiya Jerusalem güije sija na jaane.
7Alipojua kwamba Yesu alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa Yerusalemu.
8¶ Ya si Herodes anae jalie si Jesus, ninasenmagof: sa jagasja jadesea na ulie, sa jajujungog guinin güiya, megae na güinaja: ya jananangga na ufanlie guinin güiya y milagro.
8Herode alifurahi sana alipomwona Yesu. Alikuwa amekwisha sikia habari zake, na hivyo alikuwa anatazamia kwa muda mrefu kumwona kwa macho yake mwenyewe. Zaidi ya hayo, alikuwa anatumaini kumwona Yesu akitenda mwujiza.
9Ya jafaesen megae na sinangan: lao taya inepe güe.
9Basi, akamwuliza maswali mengi kwa muda mrefu, lakini Yesu hakumjibu neno.
10Yan mangaegue y magas y mamale yan y escribas na manmatatachong ya mafaaela güe fijom.
10Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakajitokeza mbele, wakatoa mashtaka yao kwa nguvu sana.
11Lao si Herodes yan y sendaluña, madespresia yan mabotlea, yan manaminagago ni lamlam na magago, ya manatalo guato as Pilatos.
11Basi, herode pamoja na maaskari wake, wakamwaibisha Yesu na kumfanyia mzaha; kisha wakamvika vazi la kifalme, wakamrudisha kwa Pilato.
12Ya umamigo si Pilatos yan Herodes güijeja na jaane: sa guinin umachatlie y dos.
12Herode na Pilato, ambao hapo awali walikuwa maadui, tangu siku hiyo wakawa marafiki.
13Ya si Pilatos janaetnon y magas y mamale, yan y magalaje yan y taotao sija,
13Basi, Pilato akaitisha mkutano wa makuhani wakuu, viongozi na watu,
14Ya ilegña nu sija: Inquene mague guiya guajo este na taotao na janaquequelache y taotao sija; ya, estagüe, na jufaesen gui menanmiyo, ya taya jusoda ni jafa na isao güine na taotao pot y finaaelamimiyo sija.
14akawaambia, "Mmemleta mtu huyu kwangu mkisema kwamba alikuwa anawapotosha watu. Sasa sikilizeni! Baada ya kuchunguza jambo hilo mbele yenu, sikumpata na kosa lolote kuhusu mashtaka yenu juu yake.
15Aje, ni si Herodes: sa junafalag iya güiya, ya, estagüe, ni jafa na ufanmerese na finatae pot y guinin finatinasña.
15Wala si mimi tu, bali hata Herode hakuona kosa lolote, kwa maana amemrudisha kwangu. Ni dhahiri kwamba mtu huyu hakufanya chochote kinachostahili adhabu ya kifo.
16Enao mina bae jucastiga ya jusotta.
16Hivyo, nitaamuru apigwe viboko, halafu nitamwachilia."
17Ya manesesita na umasotta uno gui guipot.
17Kila sikukuu ya Pasaka, ilimlazimu Pilato kuwafungulia mfungwa mmoja.
18Ya managang cada uno, ilegñija: Nasuja juyong enao na taotao ya umasotta si Barabas:
18Lakini wote wakapiga kelele pamoja: "Mwondoe huyo, utufungulie Baraba!"
19Sa mapreso pot un jatsamiento yan mamuno ni y jafatinas gui siuda.
19(Baraba alikuwa ametiwa ndani kwa kusababisha uasi katika mji na pia kwa sababu ya kuua.)
20Ya si Pilatos ilegña talo nu sija, Malagomiyo na umasotta si Jesus.
20Pilato alitaka kumwachilia Yesu, hivyo akasema nao tena;
21Lao managang ilegñija: Atane gui quiluus, atane gui quiluus.
21lakini wao wakapiga kelele: "Msulubishe, msulubishe!"
22Ya ilegña nu sija gui mina tres biaje: Sa jafa? jafa na taelaye finatinasña este na taotao? Taya ni jafa na causa para umapuno jusoda guiya güiya. Pot este na rason bae jucastigaja ya jusotta.
22Pilato akawaambia mara ya tatu, "Amefanya kosa gani? Sioni kosa lolote kwake linalomstahili auawe; kwa hiyo nitampiga viboko, halafu nimwachilie."
23Lao sija enseguidas janadangculo inagangñija, ya magagao na umaatane gui quiluus. Ya y inagangñija mangana.
23Lakini wao wakazidi kupiga kelele kwa nguvu sana, kwamba Yesu ni lazima asulubiwe. Mwishowe, sauti zao zikashinda.
24Ayonae si Pilatos janae sentensia na ufatinas taemano y guinagaoñiñija.
24Basi, Pilato akaamua kwamba matakwa yao yatimizwe.
25Ya masotta ayo y guinin mapreso pot jatsamiento yan mamuno, ayo y guinin magagagao: ya manmaentrega as Jesus gui minalagoñija.
25Akamfungua kutoka gerezani yule waliyemtaka, ambaye alikuwa ametiwa gerezani kwa sababu ya uasi na kuua; akamtoa Yesu kwao, wamfanyie walivyotaka.
26¶ Ya anae macocone güe maguot si Simon, taotao Sirene, ni guinin y fangualuan, ya manae ni quiluus na uapagaye gui taten Jesus.
26Walipokuwa wakimpeleka, walikutana na mtu mmoja, aitwaye Simoni wa Kurene, aliyekuwa anatoka shambani. Basi, walimkamata, wakamtwika ule msalaba auchukue nyuma ya Yesu.
27¶ Ya matatitiye ni y dangculon linajyan taotao yan famalaoan sija ni mangacasao yan manatangis pot güiya.
27Watu, umati kwa umati, walimfuata; miongoni mwao wakiwemo wanawake waliokuwa wanaomboleza na kumlilia.
28Lao si Jesus jabira güe tate guiya sija ilegña; Famalaoan Jerusalem, chamiyo fangacasao pot guajo, lao fangacasao pot jamyoja yan pot y famaguonmiyo.
28Yesu akawageukia, akasema, "Enyi kina mama wa Yerusalemu! Msinililie mimi, ila lieni kwa ajili yenu wenyewe na kwa ajili ya watoto wenu.
29Sa, estagüe, na ufato sija jaane nae umaalog: Mandichoso sa y manmachora, yan y tiyan sija ni ti manmamañago, yan y pecho sija ni ti manmamómogsae.
29Maana, hakika siku zitakuja ambapo watasema: Heri yao wale walio tasa, ambao hawakupata kuzaa wala kunyonyesha watoto!
30Ayonae matutujon maalog ni egso sija: Famodong gui jilonmame; ya y sabana sija: Tampe jam.
30Wakati huo, ndipo watu wataanza kuiambia milima: Tuangukieni! na vilima, Tufunikeni!
31Sa yaguin y betde na jayo jafatinas estesija, y anglo, jafa uchogüe?
31Kwa maana, kama watu wanautendea mti mbichi namna hiyo, itakuwaje kwa mti mkavu?"
32¶ Ya macone locue dos palo na taelaye finatinasñija para ufanmapuno yan güiya.
32Waliwachukua pia watu wengine wawili, wahalifu, wauawe pamoja naye.
33Ya anae manmato güije na lugat ni mafanaan Calabera, maatane gui quiluus güije yan ayo y dos ni y taelaye finatinasñija, uno gui agapa ya y otro gui acagüe.
33Walipofika mahali paitwapo, "Fuvu la Kichwa," ndipo wakamsulubisha Yesu pamoja na wale wahalifu wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
34Ya si Jesus ilegña: Tata, asie estesija; sa ti jatungo jafa jachochogüe. Ya manafacae entre sija y magaguña, ya marifa.
34Yesu akasema, "Baba, uwasamehe kwa maana hawajui wanalofanya." Kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
35Ya y taotao sija manotojgue ya maaatanja. Ya mabotlelea ni y magas sija locue, ya ilelegñija: Ufañatba otrosija: palo ya usatban maesagüe, yaguin este si Cristo, ni guine as Yuus.
35Watu wakawa wamesimama pale wakitazama. Nao viongozi wakamdhihaki wakisema: "Amewaokoa wengine; sasa na ajiokoe mwenyewe, kama yeye ndiye Kristo, mteule wa Mungu!"
36Ya mamofefea ni y sendalo sija, manmato guiya güiya, ya mafanunue ni y binagle.
36Askari nao walimdhihaki pia; walimwendea wakampa siki
37Ya ilegñija: Yaguin jago Ray y Judio sija, satban maesa jao.
37wakisema: "Kama kweli wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe."
38Ya guaja locue un tinigue gui jiloña: ESTE GUIYA Y RAY Y JUDIO SIJA.
38Vilevile maandishi haya yalikuwa yameandikwa na kuwekwa juu yake: "Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi."
39Ya uno gui ayo y taelaye finatinasñija ilegna: Yaguin jago si Cristojao? Satban maesajao yan jame.
39Mmoja wa wale wahalifu waliotundikwa msalabani, alimtukana akisema: "Je, si kweli kwamba wewe ndiwe Kristo? Basi, jiokoe mwenyewe, utuokoe na sisi pia."
40Lao inepe ni otro, ya linalatde ilegña: Ti maañao jao as Yuus, sa gaegue jao gui mismo sinentensia?
40Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake akisema: "Wewe humwogopi Mungu hata kidogo? Wewe umepata adhabu hiyohiyo.
41Lao jita magajet na tunas; sa utafanresibe pot y finatinasta: lao este na taotao, taya taelaye finatinasña.
41Wewe na mimi tunastahili, maana haya ni malipo ya yale tuliyotenda. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya."
42Ya ilegña: Jesus, jajaso yo yaguin matojao gui raenomo.
42Kisha akasema, "Ee Yesu! Unikumbuke wakati utakapoingia katika ufalme wako."
43Ayonae ilegña nu güiya: Magajet jusangane jao: Pago mismo na jaane utajita na dos guiya Paraiso.
43Yesu akamwambia, "Nakwambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi."
44Ya anae buente y oran a las sais, jumuyong jomjom todo y jilo y tano asta y oran a las nuebe,
44Ilikuwa yapata saa sita mchana; jua likaacha kuangaza, giza likafunika nchi yote mpaka saa tisa,
45Ya y atdao jomjom, ya y cottinan templo maipe gui talo.
45na pazia lililokuwa limetundikwa Hekaluni likapasuka vipande viwili.
46Ya anae umagang si Jesus, ni dangculo na inagang, ilegña: Tata, y canaemo nae jupolo y espiritujo; ya anae munjayan jasangan este, jaentrega y espiritu.
46Yesu akalia kwa sauti kubwa: "Baba, naiweka roho yangu mikononi mwako." Alipokwisha sema hayo, akakata roho.
47¶ Ya anae jalie y senturion estesija y manmalofan, janamalag si Yuus, ilegña: Sen magajet este na taotao na tunas.
47Hapo, yule jemadari alipoona yaliyotukia akamsifu Mungu akisema: "Hakika huyu alikuwa mtu mwema."
48Ya todo y linajyan taotao ni mandaña anae manmalofan este sija, anae malie y jagas sinesede, natumalo guato ya jaseco pechonñija.
48Watu wale wote waliokuwa wamekusanyika hapo kwa ajili ya tukio hilo, walipoona hayo yaliyotukia, walirudi makwao wakijipiga vifua kwa huzuni.
49Lao todo y atungoña yan y famalaoan ni tumatitiye güe desde Galilea, manestaba manlachago maatanja este sija.
49Marafiki zake wote pamoja na wale wanawake walioandamana naye kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali kutazama tukio hilo.
50¶ Ya estagüe, un taotao na y naanña si José, un taotao na pápagat, mauleg na taotao yan tunas:
50Kulikuwa na mtu mmoja jina lake Yosefu, mwenyeji wa kijiji kimoja cha Wayahudi kiitwacho Armathaya. Alikuwa mtu mwema anayeheshimika;
51(Ti jaconsiente y pinagatñija ni y finatinasñija:) Taotao Arimatea, gui Siuda y Judiosija, ya güiya locue jananangga y raenon Yuus.
51Alikuwa akitazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Ingawa alikuwa mmoja wa Baraza kuu la Wayahudi, hakuwa amekubaliana nao katika kitendo chao.
52Este mato gui as Pilatos, ya jagagao y tataotao Jesus.
52Basi, yeye alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
53Ya janatunog gui quiluus, ya jabalutan gui un sabanas, ya japolo gui un naftan ni maguadog gui acho, ya taya ni uno mapolo güije antes.
53Kisha, akaushusha mwili huo kutoka msalabani, akauzungushia sanda ya kitani, akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limetumika.
54Ya ayo na jaane y inaregla y pascua, ya pago manana gui sabado.
54Siku hiyo ilikuwa Ijumaa, na maandalio ya siku ya Sabato yalikuwa yanaanza.
55Ya manmato locue y famalaoan ni y tumatitiye desde Galilea, ya malie y naftan yan jaftaemano mapoloña y tataotaoña.
55Wale wanawake walioandamana na Yesu kutoka Galilaya walimfuata Yosefu, wakaliona lile kaburi na jinsi mwili wake Yesu ulivyowekwa
56Ya tumalo guato sija, ya manmamamauleg paopao yan inggüente sija: ya mandescansa gui sabado na jaane jaftaemanoja y tinago.
56Halafu, walirudi nyumbani, wakatayarisha manukato na marashi kuyapaka mwili wa Yesu. Siku ya Sabato walipumzika kama ilivyoamriwa na sheria.