1YA anae esta manjijijot Jerusalem, yan Betfage, yan Betania, gui egso Olibo, jatago dos gui disipuluña,
1Walipokuwa wanakaribia Yerusalemu walifika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni. Hapo aliwatuma wawili wa wanafunzi wake,
2Ya ilegña nu sija: Janao fanmalag y sengsong gui menanmiyo: ya enseguidas qui manjalom jamyo, inseda un patgon bulico, na magogode, na taya nae matachonge; pila ya inquene mague.
2akawaambia, "Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia humo, mtakuta mwana punda amefungwa ambaye bado hajatumiwa na mtu. Mfungueni mkamlete.
3Ya yanguin jaye na taotao umalog nu jamyo; Jafa na infatinas este? Sangane: Señot janesesita: ya enseguidas umanajanao mague.
3Kama mtu akiwauliza, Mbona mnafanya hivyo? Mwambieni, Bwana anamhitaji na atamrudisha hapa mara."
4Ya manmapos, ya masoda nu patgon bulico gui caye na magogode gui jiyong potta ya mapula güe.
4Basi, wakaenda, wakamkuta mwana punda barabarani amefungwa mlangoni. Walipokuwa wakimfungua,
5Ya palo ni y mangaegue güije ilegñija nu sija: Jafa na inpila enao y patgon bulico?
5baadhi ya watu waliokuwa wamesimama hapo wakawauliza "Kwa nini mnamfungua huyo mwana punda?"
6Ya masangane jaftaemano y mansinangane as Jesus: ya japolo na ufanjanao.
6Wanafunzi wakajibu kama Yesu alivyokuwa amewaambia; nao wakawaacha waende zao.
7Ya macone guato y patgon bulico gui as Jesus, ya japolo magagoñija güi jiloña ya maudae si Jesus.
7Wakampelekea Yesu huyo mwana punda. Wakatandika mavazi yao juu ya huyo mwana punda, na Yesu akaketi juu yake.
8Ya megae jajuto magagoñija gui chalan: yan palo y ramas jayo na manmanuutot gui fangualuan.
8Watu wengi wakatandaza mavazi yao barabarani; wengine wakatandaza matawi ya miti waliyoyakata mashambani.
9Ya ayo sija y manmofona gui menaña, yan y madalalag gui tatteña, manaagang ilegñija: Hosana; Bendito ayo y mato pot y naan y Señot:
9Watu wote waliotangulia na wale waliofuata wakapaaza sauti zao wakisema, "Hosana! Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana!
10Bendito y raeno na mamamaela, y raenon y tatata as David, Hosana guiyajululu.
10Ubarikiwe Ufalme ujao wa baba yetu Daudi. Hosana juu mbinguni!"
11Ya si Jesus jumalom Jerusalem, ya jumalom gui templo; ya anae munjayan jalie todo y güinaja, ya y pupuenge, mapos yan y dose, manmalag Betania.
11Yesu aliingia mjini Yerusalemu akaenda moja kwa moja mpaka Hekaluni, akatazama kila kitu kwa makini. Lakini kwa vile ilikwisha kuwa jioni, akaenda Bethania pamoja na wale kumi na wawili.
12¶ Ya y inagpaña anae manmato guinen Betania, ñalang.
12Kesho yake, walipokuwa wanatoka Bethania, Yesu aliona njaa.
13Ya anae jalie mona un trongcon igos na gagaejagonja, malag ayo jinasoña na ufañoda jafa; lao anae mato guato, taya sinedaña na jagonja; sa ti tiempopoña y igos trabia.
13Basi, akaona kwa mbali mtini wenye majani mengi. Akauendea ili aone kama ulikuwa na tunda lolote. Alipoufikia, aliukuta bila tunda lolote ila majani matupu, kwa vile hayakuwa majira ya mtini kuzaa matunda.
14Ayonae manope ya ilegña nu güiya: Taya ni un taotao uquinano y tinegchamo para siempre. Ya majungog ni y disipuluña.
14Hapo akauambia mtini, "Tangu leo hata milele mtu yeyote asile matunda kwako." Nao wanafunzi wake walisikia maneno hayo.
15¶ Ya manmato Jerusalem; ya jumalom y templo, ya sigue di jayute juyong todo ayo sija y manmanbebende, yan y manmamamajan gui templo, yan janafanalinquin y lamasan salape y manmanulalaeca, yan y tachong y man manbebende paluma:
15Basi, wakafika Yerusalemu. Yesu akaingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza nje watu waliokuwa wanauza na kununua vitu humo ndani. Akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadilishana fedha na viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa.
16Ya taya ni uno jaconsiente na ufañule baso gui templo.
16Hakumruhusu mtu yeyote kupitia Hekaluni akichukua kitu.
17Ya mamanagüe, ilegña nu sija: Ada ti matugue na y guimajo umafanaan guma manaetae ni y todo nasion sija? lao jamyo fumatinas y liyang mañañaque.
17Kisha akawafundisha, "Imeandikwa: Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa ajili ya mataifa yote! Lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi!"
18Ya majungog ni y magas mamale yan y escriba sija, ya maaliligao jaftaemano para umapuno; sa mamaañao nu güiya, sa janafanmamanman y linajyan taotao ni y finanagüeña.
18Makuhani wakuu na walimu wa Sheria waliposikia hayo, walianza kutafuta njia ya kumwangamiza. Lakini walimwogopa kwa sababu umati wa watu ulishangazwa na mafundisho yake.
19Ya cada pupuenge, jumanao juyong gui siuda.
19Ilipokuwa jioni, Yesu na wanafunzi wake waliondoka mjini.
20Ya y egaan anae manmalolofan, malie y trongcon igos na anglo desde y jale.
20Asubuhi na mapema, walipokuwa wanapita, waliuona ule mtini umenyauka wote, hata mizizi.
21Ayonae jajaso si Pedro ya ilegña nu güiya: Rabi, estagüe y trongcon igos ni y unmatdise na anglo todo.
21Petro aliukumbuka, akamwambia Yesu, "Mwalimu, tazama! Ule mtini ulioulaani, umenyauka!"
22Ya manope si Jesus ilegña nu sija: Jenggue si Yuus.
22Yesu akawaambia, "Mwaminini Mungu.
23Sa magajet jusangane jamyo: Jayeja y umalog ni este y egso, janao ya unyutejao gui tase; ya ti bumuebuente gui corasonña, lao jajonggue na umafatinas ayo y sinanganña; uguaja.
23Nawaambieni kweli, mtu akiuambia mlima huu: Ng'oka ukajitose baharini bila kuona shaka moyoni mwake, ila akaamini kwamba mambo yote anayosema yanafanyika, atafanyiwa jambo hilo.
24Enaomina jusangane jamyo: Na todo sija ingagao, anae manmanaetae jamyo, jenggue na esta inresibe, ya infanmannae.
24Kwa hiyo nawaambieni, mnaposali na kuomba kitu, aminini kwamba mmekipokea, nanyi mtapewa.
25Ya an manojgue ya mananaetaejamyo, asie yanguin guajajao jafa contra jaye; sa y Tatanmiyo locue ni y gaegue gui langet, uninasie ni y isaomiyo.
25Mnaposimama kusali, sameheni kila mtu aliyewakosea chochote, ili Baba yenu aliye mbinguni awasamehe ninyi makosa yenu.
26Lao yanguin ti manasiijamyo, y Tatanmiyo ni y gaegue gui langet ti uninasie ni y isaomiyo.
26Lakini msipowasamehe wengine, hata Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu."
27¶ Ya manmato talo Jerusalem, ya anae mamomocat gui templo, manmato y magas mamale, yan y escriba, yan y manamco sija;
27Basi, wakafika tena Yerusalemu. Yesu alipokuwa akitembea Hekaluni, makuhani wakuu, walimu wa Sheria na wazee walimwendea,
28Ya ilegñija nu güiya: Pot jafa na ninasiña na unfatitinas estesija? yan jayejao numae ni este na ninasiña, para unfatinas estesija?
28wakamwuliza, "Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Nani aliyekupa mamlaka ya kufanya mambo haya?"
29Ya si Jesus ilegña nu sija: Bae jufaesen locue jamyo un finaesen ya inepeyo, ayonae jusangane jamyo pot jafa na ninasiña na jufatitinas este sija.
29Lakini Yesu akawaambia, "Nitawaulizeni swali moja; mkinijibu, na pia nitawaambieni ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.
30Y tinagpangen Juan, guinen y langet, pat guinen y taotao sija? epeyo.
30Je, mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka mbinguni ama kwa watu? Nijibuni."
31Ya jajajaso gui sumanjalomñija, ilegñija: Yanguin ilegmame, Guinen y langet; ualog: Jafanae na ti injenggue güe?
31Wakaanza kujadiliana, "Tukisema, Yalitoka mbinguni, atatuuliza, Basi, mbona hamkumsadiki?
32Yanguin ilegmame guinen y taotao sija--manmaañao ni y taotao, sa pineloñija todo na magajet na profeta si Juan.
32Na tukisema, Yalitoka kwa watu..." (Waliogopa umati wa watu maana wote waliamini kwamba Yohane alikuwa kweli nabii.)
33Ya manmanope, ilegñija as Jesus: Ti intingo. Ayonae si Jesus ilegña nu sija; ni guajo locue ti jusangane jamyo pot jafa naninasiña, na jufatitinas estesija.
33Basi, wakamjibu Yesu, "Sisi hatujui." Naye Yesu akawaambia, "Nami pia sitawaambieni ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani."