1YA anae jumuyong gui templo; ilegña nu güiya uno gui disipuluña: Maestro, liija na jechuran acho, yan guma sija.
1Yesu alipokuwa anatoka Hekaluni, mmoja wa wanafunzi wake alimwambia, "Mwalimu, tazama jinsi mawe haya na majengo haya yalivyo ya ajabu!"
2Ya si Jesus manope ilegña nu sija: Unlie este sija na mandangculon guma? taya usobbla ni un acho gui jilo y otro, na ti umayute papa.
2Yesu akamwambia, "Je, unayaona majengo haya makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitabomolewa."
3¶ Ya anae matachong gui jilo y finabeca na y naanña Olibo, gui menan y templo, finaesen gui secreto as Pedro, yan Santiago, yan si Juan, yan si Andres,
3Yesu alipokuwa ameketi juu ya mlima wa Mizeituni akielekea Hekalu, Petro, Yakobo, Yohane na Andrea wakamwuliza kwa faragha,
4Ilegñija: Sanganejam, ngaean estesija ufanmato? yan jafa na señat yanguin para todo estesija nae ufanmacumple?
4"Twambie mambo haya yatatukia lini? Ni ishara gani itakayoonyesha kwamba mambo haya karibu yatimizwe?"
5Si Jesus jatutujon ilegña nu sija: Adaje jamyo, ya chamiyo fanmafabababa.
5Yesu akaanza kuwaambia, "Jihadharini msije mkadanganywa na mtu.
6Sa megae ufanmato pot y naanjo, ya ualog: Guajo güiya Jesucristo, ya ufababa megae.
6Maana wengi watakuja wakilitumia jina langu, wakisema, Mimi ndiye! nao watawapotosha watu wengi.
7Yanguin injingog y guera, yan y masangan y guera: chamiyo ninafañachatsaga: sa nesesita estesija jumuyong: lao trabia ti y jinecog.
7Mtakaposikia juu ya vita na fununu za vita, msifadhaike. Mambo hayo lazima yatokee, lakini mwisho wenyewe ungali bado.
8Sa y nasion sija ufangajulo contra y nasion, yan y raeno contra raeno: ya uguaja linao gui megae na lugat ya uguaja ñinalang: estesija tutujon y pinite.
8Taifa moja litapigana na taifa lingine; utawala mmoja utapigana na utawala mwingine; kila mahali kutakuwa na mitetemeko ya ardhi na njaa. Mambo haya ni kama tu maumivu ya kwanza ya kujifungua mtoto.
9¶ Lao adaje jamyo: sa infanmaentrega gui tribunal sija; ya infanmasaulag gui sinagoga: yan infanojgue gui menan y manmagas sija yan y ray sija, pot causa de guajo para un testimonio contra sija.
9"Lakini ninyi jihadharini. Maana watu watawapelekeni mahakamani, na kuwapigeni katika masunagogi. Mtapelekwa mbele ya watawala na wafalme kwa sababu yangu ili mpate kunishuhudia kwao.
10Ya y ibangelio nesesita umapredica finenana gui entre todo y nasion.
10Lakini lazima kwanza Habari Njema ihubiriwe kwa mataifa yote.
11Lao anae maconejamyo, ya maentregajamyo, chamiyo jumajaso jafa para insangan, ni injasuye jafa: sa jafaja y manaejamyo güije na ora, ayoja insangan: sa ti jamyo infangcuentos, na y Espiritu Santo.
11Nao watakapowatieni nguvuni na kuwapeleka mahakamani, msiwe na wasiwasi juu ya yale mtakayosema; saa ile itakapofika, semeni chochote mtakachopewa, maana si ninyi mtakaosema, bali Roho Mtakatifu.
12Pago y laje uentrega y cheluña laje, para umapuno; ya y tata y lajiña: ya y famaguon ufangajulo contra y mañaenanñija: ya uuafanmapuno.
12Ndugu atamsaliti ndugu yake auawe; baba atamsaliti mwanae; watoto watawashambulia wazazi wao na kuwaua.
13Ya jamyo infanmachatlie ni todo y taotao sija, pot y naanjo: lao jaye y sumungon asta y uttimo, umasatba.
13Watu wote watawachukieni ninyi kwa sababu ya jina langu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa.
14Lao anae inlie y chinatlie y inginon na yinilang tumotojgue gui anae ti para utojgue, (y mananaetae utungo) ayo sija y mangaegue guiya Judea ufanmalago para y jalomtano:
14"Mtakapoona Chukizo Haribifu limesimama mahali ambapo si pake, (msomaji na atambue maana yake!) Hapo watu walioko Yudea wakimbilie milimani.
15Ya y gaegue gui jilo guma, chaña tumutunog ni ujalom ya ufañule jafa na güinaja gui jalom gumaña.
15Mtu aliye juu ya paa la nyumba asishuke kuingia nyumbani mwake kuchukua kitu.
16Ya y gaegue gui fangualuan, chaña tumatalo tate para uchule y magaguña.
16Aliye shambani asirudi nyuma kuchukua vazi lake.
17Lao mannamaase ayo sija y manmapotgue yan y mannanasusu, güije sija na jaane!
17Ole wao waja wazito na wanaonyonyesha siku hizo!
18Fanmanaetae, ya munga y jinanaomiyo gui tiempon y manenggeng.
18Ombeni ili mambo hayo yasitukie nyakati za baridi.
19Sa ayo sija na jaane, uguaja pininite, ni y taya nae guaja desde y matutujon y tano, anae jafatinas si Yuus, asta pago; ni uguaja asta jinecog.
19Maana wakati huo kutakuwa na dhiki ambayo haijatokea tangu Mungu alipoumba ulimwengu mpaka leo, wala haitatokea tena.
20Lao yaguin ti janacadada y Señot ayo sija na jaane, taya catne usatba: lao pot y rason y manmaayigja, ni y inayigña, janacadada ayo sija na jaane.
20Kama Bwana asingepunguza siku hizo, hakuna binadamu ambaye angeokolewa. Lakini kwa ajili ya wateule wake, Bwana amezipunguza siku hizo.
21Ya yanguin guaja umalog nu jago: Estagüe si Cristo: pat ayogüe guato; chamiyo jumojonggue.
21"Basi mtu akiwaambieni, Tazama, Kristo yupo hapa! au Yupo pale! msimsadiki.
22Sa ufangajulo sija ti manmagajet na Cristo sija, yan ti manmagajet na profeta sija, ya ufanmamanue sija señat yan mannamanman, para ufanmamababa, yanguin janasiña, asta y manmaayig.
22Maana watatokea kina Kristo wa uongo na manabii wa uongo, watafanya ishara na maajabu, ili kuwapotosha wateule wa Mungu, kama ikiwezekana.
23Lao adaje jamyo: Sa estagüeja, na jusangane jamyo todos antes.
23Lakini ninyi jihadharini. Mimi nimewaambieni mambo yote kabla hayajatokea.
24¶ Lao ayo sija na jaane an munjayan y pininite sija; ujomjom y atdao, ya y pilan ti ufanina,
24"Basi, siku hizo baada ya dhiki hiyo, jua litatiwa giza na mwezi hautaangaza.
25Ya y pution sija gui langet ufamodong, ya y ninasifia sija gui langet ufanmayengyong.
25Nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za mbingu zitatikiswa.
26Ya ayo nae ujalie y Lajin taotao na mamamaela gui sanjalom mapagajes, yan y dangculon ninasiñaña yan y minalagña.
26Hapo watamwona Mwana wa Mtu akija katika mawingu kwa nguvu nyingi na utukufu.
27Ya ayonae utago y angjetña sija na ujarecoje y inayigña sija, guinen y cuatro na manglo, guinen y uttimon y tano asta y uttimon y langet.
27Kisha atawatuma malaika wake; atawakusanya wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka mwisho wa dunia mpaka mwisho wa mbingu.
28¶ Tingo y acomparasion y trongcon igos; Anae mamaulegja trabia y ramasña, ya manjajagonja, intingoja na esta jijijot y tiempon maepe.
28"Kwa mtini jifunzeni mfano huu: Mara tu matawi yake yanapoanza kuwa laini na kuchanua majani, mnajua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
29Jamyo locue anae inlie estesija, na manmato, tingoja na güiya esta jijijot, parejoja yan esta gaegue gui petta.
29Hali kadhalika nanyi mtakapoona mambo hayo yakitendeka, jueni kwamba Mwana wa Mtu yuko karibu sana.
30Magajet jusangane jamyo: Este na generasion ti ufanmalofan, asta que todo estesija munjayan manmachogüe.
30Nawaambieni kweli, kizazi hiki hakitapita kabla ya mambo hayo yote kutukia.
31Y langet yan y tano, ufanmalofan, lao y sinanganjo ti ufalofan.
31Mbingu na dunia zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
32Lao ayo na jaane pat ayo na ora, taya ni un taotao tumungo; ni y angjet sija ni mangaegue gui langet, ni y Laje; na y Tata güiyaja.
32"Lakini hakuna mtu ajuaye siku au saa hiyo itakuja lini; wala malaika wa mbinguni, wala Mwana; Baba peke yake ndiye ajuaye.
33Adaje jamyo: fanbela, ya infanmanaetae: sa ti intingo ngaean y tiempo.
33Muwe waangalifu na kesheni, maana hamjui wakati huo utafika lini.
34Say y Lajin taotao, parejoja yan un taotao ni y jumajanao chago ya jadingo y gumaña; ya janae y tentagoña ninasiñañija yan cada uno y chechoña, ya jatago y pottero na ufanbela.
34Itakuwa kama mtu anayeondoka nyumbani kwenda safari akiwaachia watumishi wake madaraka, kila mmoja na kazi yake; akamwambia mlinzi wa mlango awe macho.
35Fanbela, sa ti intingo ngaean nae ufato y magas y guima; cao y pupuenge, pat y tatalopuenge, pat y oogayo, pat y egaan;
35Kesheni, basi, kwa maana hamjui mwenye nyumba atarudi lini; huenda ikawa jioni, usiku wa manane, alfajiri au asubuhi.
36Na, noseaja derepente ufato, ya infansineda manmamaego.
36Kesheni ili akija ghafla asije akawakuta mmelala.
37Ya jafa y jusangane jamyo, jusanganeja todos: Fanbela.
37Ninayowaambieni ninyi, nawaambia wote: Kesheni!"