Chamorro: Psalms, Gospels, Acts

Swahili: New Testament

Mark

14

1GUAJA dos na jaane antes di guipot y pascua yan y taelibadura na pan: ya y magas mamale sija, yan y escriba sija, maaliligao jaftaemano para umafababa, ya umacone, ya umapuno.
1Ilikuwa siku mbili tu kabla ya sikukuu ya Pasaka na ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria walikuwa wakitafuta njia ya kumtia Yesu nguvuni kwa hila wamuue.
2Lao ilegñija: Munga gui guipot na jaane, sa noseaja uguaja atboroto ni y taotao sija.
2Lakini walisema, "Tusimtie nguvuni wakati wa sikukuu, watu wasije wakafanya ghasia."
3¶ Ya anae estaba guiya Betania, gui guima Simon y ategtog, ya matachong gui lamasa para uchocho; mato un palaoan mañuñule un alabastro na boteyan inggüenten puro nardo, na gosguaguan; ya mafag y boteya, ya jachuda gui jilo y ilon Jesus.
3Yesu alikuwa Bethania, nyumbani kwa Simoni, Mkoma. Alipokuwa mezani kula chakula, mama mmoja aliyekuwa na chupa ya alabasta yenye marashi ya nardo safi ya thamani kubwa alikuja, akaivunja hiyo chupa, akammiminia Yesu marashi hayo kichwani.
4Ya guaja sija ninafanbubo sanjalomñija, ya ilegñija: Jafa este na inggüente na manalalastimaja?
4Baadhi ya watu waliokuwa hapo walikasirika wakajisemea, "Kwa nini kupoteza ovyo marashi haya?
5Maulegña umabende pot tresientos peseta, ya ufanmanae y mamobble: ya malalatde y palaoan.
5Yangaliweza kuuzwa kwa fedha kiasi cha denari mia tatu, wakapewa maskini!" Wakamkemea huyo mama.
6Lao si Jesus ilegña: Pologüe namaesa. Jafaja na inatbororota güe? Mauleg finatinasña nu guajo.
6Lakini Yesu akawaambia, "Mwacheni; kwa nini mnamsumbua? Amenitendea jambo jema.
7Sa manjajamyoja yan y mamobble siempre; ya ngaeanja nae manmalago jamyo, infatinasja mauleg guiya sija: lao guajo ti tafanjijitaja siempre.
7Maskini mnao daima pamoja nanyi; mnaweza kuwasaidia wakati wowote mnaopenda. Lakini mimi sitakuwapo pamoja nanyi daima.
8Güiya jafatinas taemanoja y ninasiñaña: güiya mato antes, para uinggüentiye y tataotaojo, para y naftan.
8Yeye amefanya alivyoweza; ameupaka mwili wangu marashi kuutayarisha kwa maziko.
9Magajet jusangane jamyo: Manoja este na ebangelio nae mapredica, gui todo y tano, este locue y finatinasña umasangan, para memoriasña.
9Nawaambieni kweli, popote ulimwenguni Habari Njema itakapohubiriwa, kitendo hiki alichofanya kitatajwa kwa ajili ya kumkumbuka."
10¶ Ya si Judas Iscariote, uno gui dose, mapos malag y magas mamale, para umentrega güe guiya sija.
10Kisha Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili, alienda kwa makuhani wakuu ili kumsaliti Yesu.
11Ya anae majungog, ninafansenmagof, ya mapromete manae güe salape. Ya jaaliligao jaftaemano para uinentrega.
11Makuhani wakuu waliposikia habari hiyo, walifurahi, wakaahidi kumpa fedha. Basi, Yuda akaanza kutafuta nafasi ya kumsaliti Yesu.
12¶ Ya y finenana na jaane y taelibadura na pan, anae maofrese y pascua, y disipuluña ilegñija nu güiya; Manojam malagomo guato ya infamauleg nae para unchocho gui pascua?
12Siku ya kwanza ya sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wakati ambapo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa, wanafunzi wake walimwuliza, "Wataka tukuandalie wapi karamu ya Pasaka?"
13Ya jatago y dos gui disipuluña, ya ilegña nu sija: Janao fanmalag y siuda, sa infanasoda güije yan un taotao na mangangatga un jarran janom: dalalag güe.
13Basi Yesu akawatuma wawili wa wanafunzi wake akiwaambia, "Nendeni mjini, nanyi mtakutana na mtu anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni
14Ya amanoja nae jumalom, alog ni y taotao guma: Y Maestro, ilegña: Mangue y aposento ni y anae para infañocho gui pascua yan y disipulujo?
14mpaka katika nyumba atakayoingia, mkamwambie mwenye nyumba, Mwalimu anasema: wapi chumba changu ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
15Ya güiya infanfinanue un dangculo na cuatto; esta mafamauleg yan listo; ayo nae famauleg para jita.
15Naye atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani kilichotayarishwa na kupambwa. Tuandalieni humo."
16Ya y disipuluña sija manmapos, ya manmato gui siuda, ya jasoda jaftaemano y mansinangane sija: ya mafamauleg para y pascua.
16Wanafunzi wakaondoka, wakaenda mjini, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia. Wakaandaa karamu ya Pasaka.
17¶ Ya y pupuenge mato yan y dose.
17Ilipokuwa jioni, Yesu alifika pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili.
18Ya anae manmatatachong ya mañochocho, si Jesus ilegña: Magajet jusangane jamyo: Uno guiya jamyo umentregayo; güiyaja uchumocho yan guajo.
18Walipokuwa mezani wakila, Yesu alisema, "Kweli nawaambieni, mmoja wenu anayekula pamoja nami, atanisaliti."
19Ayo nae ninafangostriste, ya ilegñija nu güiya uno yan otro: Guajo? y otro ilegña: Guajo?
19Hapo wanafunzi wake wakaanza kuhuzunika, wakamwuliza mmojammoja, "Je, ni mimi?"
20Ayo nae manope ilegña nu sija: Uno gui dose ni y jumajame manotche gui tason.
20Yesu akawaambia, "Ni mmoja wenu ninyi kumi na wawili, anayechovya mkate pamoja nami katika bakuli.
21Y Lajin taotao magajet na mapos, ni y esta matugue pot güiya: lao namaase ayo na taotao ni y jaentrega y Lajin taotao. Maulegña ayo na taotao na ti umafañago.
21Kweli Mwana wa Mtu anakwenda zake kama Maandiko Matakatifu yanavyosema juu yake; lakini, ole wake mtu yule anayemsaliti Mwana wa Mtu! Ingalikuwa afadhali kwa mtu huyo kama hangalizaliwa!"
22¶ Ya anae mañochocho, jachule si Jesus y pan, ya jabendise, ya jaipe, ya janae sija, ilegña: Chile ya incano, sa este y tataotaojo.
22Walipokuwa wanakula, Yesu alitwaa mkate, akashukuru, akaumega na kuwapa wanafunzi wake akisema, "Twaeni; huu ni mwili wangu."
23Ya jachule y posuelo, ya anae munjayan janae grasia, janae sija: ya todos manguimen.
23Kisha akatwaa kikombe, akamshukuru Mungu, akawapa; nao wote wakanywa katika kikombe hicho.
24Ya ilegña nu sija: Este y jâgâjo, gui nuebo na testamento, ni machuda pot y megae.
24Akawaambia, "Hii ni damu yangu inayothibitisha agano la Mungu, damu inayomwagwa kwa ajili ya watu wengi.
25Magajet jusangane jamyo, na ti juguimen talo ni y tinegcha ubas, asta ayo na jaane, na juguimen nuebo gui raenon Yuus.
25Kweli nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka siku ile nitakapoinywa upya katika Ufalme wa Mungu."
26Ya anae munjayan macanta un himno, manmapos manmalag y finabeca Olibo.
26Kisha wakaimba wimbo, wakaondoka, wakaenda katika mlima wa Mizeituni.
27¶ Ya si Jesus ilegña nu sija: Todos jamyo infaninefende pot guajo; sa esta matugue: Bae jupanag y pastot, ya y quinilo sija ufanmachalapon.
27Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Ninyi nyote mtakuwa na mashaka nami; maana Maandiko Matakatifu yasema: Nitampiga mchungaji nao kondoo watatawanyika.
28Lao despues di lâlâyo talo, ya cumajuloyo, jujanao esta y menanmiyo guiya Galilea.
28Lakini nikisha fufuka, nitawatangulieni kule Galilaya."
29Ayo nae si Pedro ilegña: Achogja todos maninefende; lao guajo aje.
29Petro akamwambia "Hata kama wote watakuwa na mashaka nawe na kukuacha, mimi sitakukana kamwe!"
30Ya sinangane as Jesus ilegña: Magajet jusanganejao na jago pagoja na puenge, antes qui uoo dos biaje y gayo, unpuneyo tres biaje.
30Yesu akamwambia, "Kweli nakwambia, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu."
31Lao guiya janaguefchadeg y cuentosña, ilegña: Yanguin jumitamatae, ti jupunejao ni jaftaemano. Taegüineja locue sinanganñija todos.
31Lakini Petro akasisitiza, "Hata kama ni lazima nife pamoja nawe, sitakuacha kamwe." Wanafunzi wote pia wakasema vivyo hivyo.
32¶ Ya manmato un lugat na y naaña Gethsemane: ya ilegña ni y disipuluña sija: Fanmatatachong güine, mientras mananaetaeyo.
32Basi, wakafika katika bustani iitwayo Gethsemane. Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Kaeni hapa wakati mimi nasali."
33Ya jacone gachongña si Pedro, yan si Santiago, yan si Juan, ya jatutujon manmajalang, yan mangostriste,
33Kisha akawachukua Petro, Yakobo na Yohane; akaanza kufadhaika sana na kuhangaika.
34Ya ilegña nu sija: Y antijo sentriste asta qui jumatae; fañaga güine, ya iafanmamulan.
34Akawaambia, "Nina huzuni kubwa moyoni hata karibu kufa. Kaeni hapa mkeshe."
35Ya jumanao mona didide, dumimo papa gui jilo oda, ya manaetae, na yanguin siña, ufalofan y ora guiya güiya.
35Akaenda mbele kidogo, akajitupa chini kifudifudi, akasali kwamba, kama ingewezekana, asiipitie saa hiyo ya mateso.
36Ya ilegña: Abba, Tata: todo y güinaja mansiña para jago; nasuja este y posuelo guiya guajo: lao ti taemanoja minalagojo, na y minalagomo.
36Akasema, "Baba yangu, kwako mambo yote yanawezekana. Uniondolee kikombe hiki; lakini isiwe kama nitakavyo mimi, bali utakavyo wewe."
37Ya mato talo guato ya jasoda sija manmaego, ya ilegña as Pedro: Simon mamaegojao? ti siñajao bumela un oraja?
37Kisha akarudi kwa wanafunzi wale watatu, akawakuta wamelala. Basi, akamwuliza Petro, "Simoni, je umelala? Hukuweza kukesha hata saa moja?"
38Fanbela, yan infanmanaetae; para chamiyo fanjajalom gui tentasion: Y Espiritu magajet na malago; lao y catne echecho.
38Kisha akawaambia, "Kesheni na kusali ili msije mkaingia katika majaribu. Roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu."
39Ya jumanao talo ya manaetae ya ayoja mismo na sinangan.
39Akaenda kusali tena akirudia maneno yaleyale.
40Ya anae tumalo guato jasoda talo sija na manmamaego: sa y atadogñija mangosmacat, ya ti ujatungo jafa umaope güe.
40Kisha akarudi tena, akawakuta wamelala. Macho yao yalikuwa yamebanwa na usingizi. Hawakujua la kumjibu.
41Ya mato talo gui mina tres biaje, ya ilegña nu sija: Fanmaego pago, ya infandescansa: esta najong; y ora esta mato; lie y Lajin taotao na maentrega gui canae y manisao sija.
41Alipowajia mara ya tatu aliwaambia, "Mnalala bado na kupumzika? Sasa imetosha! Saa imefika! Mwana wa Mtu anakabidhiwa kwa watu waovu.
42Fangajulo ya nije tafanjanao; sa esta y umentregayo jijot.
42Amkeni, twendeni zetu. Tazameni, yule atakayenisaliti amekaribia."
43Ya enseguidas, mientras cumuecuentos, mato si Judas, uno gui dose, ya mañisija yan un linajyan taotao, manmañuñule espada, yan galute guinen y magas mamale, yan y escriba, yan y manamco sija.
43Yesu alipokuwa bado anasema, Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili, akafika pamoja na umati wa watu wenye mapanga na marungu. Watu hao walikuwa wametumwa na makuhani wakuu, walimu wa Sheria na wazee.
44Ya ayo y umentrega güe, mannae señat, ilegña: Jaye y juchico, güiya ayo: guiot ya inquene na seguro.
44Msaliti Yuda alikuwa amewapa ishara: "Yule nitakayembusu ndiye; mkamateni, mkampeleke chini ya ulinzi."
45Ya enseguidas nae matogüe, jumajanaoja guato guiya güiya, ya ilegña: Maestro; ya jachico.
45Yuda alipofika tu, alimwendea Yesu moja kwa moja, akasema, "Mwalimu!" Kisha akambusu.
46Ya ayonae mapolo canae sija gui jiloña ya macone.
46Basi, hao watu wakamkamata Yesu, wakamtia nguvuni.
47Ya uno guiya sija ni y tumotojgue gui oriya, jalagnos y espadaña, ya jataga y tentago y magas mamale, ya jautut talangaña.
47Mmoja wa wale waliokuwa wamesimama hapo pamoja na Yesu akauchomoa upanga wake, akampiga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
48Ya manope si Jesus ilegña nu sija: Ada manmato jamyo calang contra y saque, na manmañuñule jamyo espada, yan galute para inguiotyo?
48Yesu akawaambia, "Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
49Guinen manjijitaja todo y jaane gui templo manmamananagüe, ya ti inquequeneyo? lao mafatinas este para umacumple y tinigue.
49Kila siku nilikuwa pamoja nanyi nikifundisha Hekaluni, wala hamkunikamata. Lakini sasa lazima Maandiko Matakatifu yatimie."
50Ya madingo, ya manmalago todos.
50Hapo wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.
51¶ Ya dinalalaggüe un patgon na taotao, na jatatampe güe un sábanas, sa taya magagago: ya y mamatgon sija na taotao, maguot güe.
51Kulikuwa na kijana mmoja aliyekuwa anamfuata Yesu akiwa amevaa shuka. Nao wakajaribu kumkamata.
52Lao güiya japolo y sábanas, ya malago sin magago.
52Lakini yeye akaponyoka, akaiachilia ile shuka, akakimbia uchi.
53¶ Ya macone si Jesus para y magas na pale: ya mandaña y manmagas mamale yan y manamco, yan y escriba sija.
53Basi, wakampeleka Yesu kwa Kuhani Mkuu ambapo makuhani wakuu wote, wazee na walimu wa Sheria walikuwa wamekutanika.
54Ya si Pedro dinalalag güe, lao chago, asta gui sanjalom, sanjalom y palasyon y magas na pale: ya matachong yan y tentago sija, ya janama maope güe gui guafe.
54Petro alimfuata Yesu kwa mbali, akaingia ndani ya ya wa Kuhani Mkuu, akaketi pamoja na walinzi akiota moto.
55Ya y magas mamale, yan todo y inetnon ofisiat, manmanaliligao testimonio contra si Jesus para umapuno; lao taya masoda.
55Makuhani wakuu na Baraza lote wakatafuta ushahidi wa kumshtaki Yesu wapate kumwua, lakini hawakupata.
56Sa megae manmannae ti manmagajet na testimonio contra güiya: lao y testimonioñija ti manparejo.
56Watu wengi walitoa ushahidi wa uongo juu ya Yesu, lakini ushahidi wao haukupatana.
57Ya mangajulo palo ni manmannae contra güiya y testimonio na ti manmagajet, ilegñija:
57Kisha wengine walisimama, wakatoa ushahidi wa uongo wakisema:
58Injingog y ilegña: Juyulang este na templo, ni y mafatinas nu canae, ya y tres na jaane, janacajulo talo otro na ti finatinas canae.
58"Tulimsikia mtu huyu akisema, Nitaliharibu Hekalu hili lililojengwa kwa mikono, na kwa siku tatu nitajenga lingine lisilojengwa kwa mikono."
59Lao este na testimonioñija, locue ti manparejo.
59Lakini hata hivyo, ushahidi wao haukupatana.
60Ya y magas na pale tumojgue julo gui talolo, ya jafaesen si Jesus ilegña: Ti unfanope ni jafa? Jafa este sija na testimonioñija contra jago?
60Basi, Kuhani Mkuu akasimama katikati yao, akamwuliza Yesu, "Je, hujibu neno? Watu hawa wanashuhudia nini dhidi yako?"
61Lao mamatquiquiloja, taya inepeña. Tumalo y magas na pale finaesen ilegña: Jago si Jesucristo Lajin y Bendito?
61Lakini yeye akakaa kimya; hakusema hata neno moja. Kuhani Mkuu akamwuliza tena, "Je, wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu Mtukufu?"
62Ya si Jesus ilegña: Guajo; ya umamaela y tiempo anae inlie y Lajin taotao matatachong gui agapa y gaeninasiña na canae, ya umamaela gui jalom y mapagajes y langet.
62Yesu akajibu, "Naam, mimi ndiye. Tena, mtamwona Mwana wa Mtu amekaa upande wa kulia wa Mwenyezi, akija katika mawingu ya mbinguni."
63Ayonae y magas na pale, jatiteg y magaguña, ya ilegña: Para jafajit palo testigo sija?
63Hapo Kuhani Mkuu akararua joho lake, akasema, "Tuna haja gani tena ya mashahidi?
64Injingogja y chinatfinoña contra si Yuus: Jafa jinasonmimiyo? Ya todos manmañentensia para umapuno.
64Mmesikia kufuru yake! Ninyi mwaonaje?" Wote wakaamua kwamba anastahili kuuawa.
65Ya y palo matutujon matolae, yan matatampe mataña, yan mapatmada, ya ilegñija nu güiya: Profetisa: ya y ofisiat sija rumesibe güe ya japatmada ni y canaeñija.
65Basi, baadhi yao wakaanza kumtemea mate, wakamfunika uso, wakampiga na kumwambia, "Bashiri ni nani aliyekupiga!" Hata watumishi wakamchukua, wakampiga makofi.
66¶ Ya anae si Pedro gaegue gue sanpapa gui palasyo, mato un palaoan tentago y magas na pale:
66Petro alipokuwa bado chini ukumbini, mmoja wa wajakazi wa kuhani Mkuu alikuja.
67Ya anae jalie si Pedro na janamamaepe güe, jaatan ya ilegña: Jago locue manjajamyo yan si Jesus Nasareno?
67Alipomwona Petro akiota moto, alimtazama, akamwambia, "Hata wewe ulikuwa pamoja na Yesu Mnazareti."
68Lao jadague ilegña: Ti jutungo, ni jutungo jafa ilelegmo. Ya mapos juyong gui cajida; ya umoo y gayo.
68Lakini Petro akakana, "Sijui, wala sielewi unayosema!" Kisha Petro akaondoka, akaenda nje uani. Hapo jogoo akawika.
69Ya linie talo ni y palaoan, ya jatutujon sumangane ayo sija y manotojgue gui oriyaña: Este uno guiya sija.
69Yule mjakazi alipomwona tena Petro, akaanza tena kuwaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, "Mtu huyu ni mmoja wao."
70Ya jadague talo. Ti apmam ayo y manotojgue gui oriya ilegñija as Pedro: Magajet na jago uno guiya sija? sa jago taotao Galileajao.
70Petro akakana tena. Baadaye kidogo, watu waliokuwa wamesimama hapo wakamwambia Petro, "Hakika wewe ni mmoja wao, maana wewe ni Mgalilaya."
71Lao jatutujon mamatdise yan manjula ya ilegña: Ti jutungo este na taotao y insasangan.
71Lakini Petro akaanza kulaani na kuapa akisema, "Mimi simjui mtu huyu mnayesema habari zake."
72Ya enseguidas y mina dos biaje umoo y gayo. Jajaso si Pedro y sinangan, jaftaemano si Jesus nu güiya ilegña: Antes que uoo y gayo dos biaje, undagueyo tres biaje. Ya anae jajaso, tumanges.
72Hapo jogoo akawika mara ya pili. Basi, Petro akakumbuka jinsi Yesu alivyokuwa amemwambia: "Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu." Petro akabubujika machozi.