Chamorro: Psalms, Gospels, Acts

Swahili: New Testament

Mark

15

1YA enseguidas y egaan güije, y magas mamale yan y manamco, yan y escriba sija, yan todo y inetnon ofisiat manaconseja entaloñija, ya magode si Jesus, ya macone, ya maentrega si Pilato.
1Kulipopambazuka, makuhani wakuu walifanya shauri pamoja na wazee, walimu wa Sheria na Baraza lote, wakamfunga Yesu pingu, wakampeleka na kumkabidhi kwa Pilato.
2Ya finaesen as Pilato, ilegña nu güiya: Jago y Ray Judios? Ya manope ilegña: Jago sumangan.
2Pilato akamwuliza Yesu, "Je, wewe ni mfalme wa Wayahudi?" Yesu akajibu, "Wewe umesema."
3Ya mafaaela ni y magas mamale, megae sija na güinaja.
3Makuhani wakuu wakamshtaki Yesu mambo mengi.
4Ya finaesen güe talo as Pilato, ilegña: Ti unfanope ni jafa? liija na minegae finaela contra jago.
4Pilato akamwuliza tena Yesu, "Je, hujibu neno? Tazama wanavyotoa mashtaka mengi juu yako."
5Lao si Jesus ti manope ni jafa; ayo mina ninamanman si Pilato.
5Lakini Yesu hakujibu neno, hata pilato akashangaa.
6¶ Ya ayo na gupot, y costumbre masosotta un preso, yanguin jagagao jaye y malagoñija.
6Kila wakati wa sikukuu ya Pasaka, Pilato alikuwa na desturi ya kuwafungulia mfungwa mmoja waliyemtaka.
7Ya guaja güije uno, y naanña si Barabas, na mapreso yan y mangachongña gui un jatsamiento; sija manmamuno anae mangajulo gui jatsamiento.
7Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Baraba, ambaye alikuwa amefungwa pamoja na waasi wengine kwa kusababisha uasi na mauaji.
8Ya y linajyan taotao manmato jijot, ya jatutujon manmangaogao na ufatinas taegüije y guinen jafatinas guiya sija,
8Watu wengi wakamwendea Pilato wakamwomba awafanyie kama kawaida yake.
9Lao si Pilato manope sija, ilegña: Manmalago jamyo na jusottaye jamyo y Ray Judios?
9Pilato akawauliza, "Je, mwataka niwafungulieni Mfalme wa Wayahudi?"
10Sa jatungo, na ayo na maentrega ni y magas mamale, pot y embidia.
10Alisema hivyo kwa sababu alijua wazi kwamba makuhani wakuu walimkabidhi Yesu kwake kwa sababu ya wivu.
11Lao y magas mamale jatago y taotao sija, na ujagagao na si Barabas umasotta.
11Lakini makuhani wakuu wakawachochea watu wamwombe Pilato awafungulie Baraba.
12Ya si Pilato manope ilegña talo nu sija: Jafanae malagomiyo jufatinas ayo y infananaan Ray Judios?
12Pilato akawauliza tena, "Basi, sasa mwataka nifanye nini na mtu huyu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?"
13Ya managang talo ilegñija: Atane gui quiluus.
13Watu wote wakapaaza sauti tena: "Msulubishe!"
14Ayonae si Pilato, ilegña nu sija: Jafa na taelaye finatinasña? Ya mas managang, ilegñija: Atane gui quiluus.
14Lakini Pilato akawauliza, "Kwa nini! Amefanya kosa gani?" Lakini wao wakazidi kupaaza sauti, "Msulubishe!"
15Ya si Pilato, malago na ufanmagof y taotao sija, jasottaye sija si Barabas, ya maentrega si Jesus, anae munjayan masaulag, para umaatane gui quiluus.
15Pilato alitaka kuuridhisha huo umati wa watu; basi, akamwachilia Baraba kutoka gerezani. Akaamuru Yesu apigwe viboko, kisha akamtoa asulubiwe.
16¶ Ya maosgaejon ni y sendalo sija, guato gui patio mafanaan Pretorio; ya madaña todo y mangachong.
16Kisha askari walimpeleka Yesu ndani ukumbini, katika ikulu, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
17Ya manaminagago púrpura, ya matufog un coronan tituca.
17Wakamvika vazi la rangi ya zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamwekea kichwani.
18Ya matutujon masaluda, ilegñija: Jafa tatatmanojao Ray Judios!
18Wakaanza kumsalimu, "Shikamoo Mfalme wa Wayahudi!"
19Ya mapanag y iluña ni y piao, ya matolae güe, yan mandidimo, ya maadodora güe.
19Wakampiga kichwani kwa mwanzi, wakamtemea mate; wakampigia magoti na kumsujudia.
20Ya anae munjayan mamofeagüe, manajanao y púrpura, ya manaminagago ni y magaguñaja. Ya macone güe para umaatane gui quiluus.
20Baada ya kumdhihaki, walimvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
21¶ Ya manacatga uno ni y malolofan para ufañija, si Simon Sirineo, tatan Alejandro yan Rufo, na mato guinen y fangualuan, para uquinatgaye ni y quiluus Jesus.
21Walipokuwa njiani, walikutana na mtu mmoja aitwaye Simoni, mwenyeji wa Kurene. Yeye alikuwa baba wa Aleksanda na Rufo, na wakati huo alikuwa akitoka shambani. Basi, wakamlazimisha auchukue msalaba wa Yesu.
22Ya macone guato gui un lugat na y naanña Golgota: cumequeilegña, Sagan calabera.
22Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha, maana yake, "Mahali pa Fuvu la Kichwa."
23Ya manae guimenña, bino manadaña yan mira, lao ti jaresibe.
23Wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini yeye akaikataa.
24Ya maatane güe gui quiluus, manafacae ni magaguña; ya manrifa jaye uchinile cada uno.
24Basi, wakamsulubisha, wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura waamue nani angepata nini.
25Ya y mina tres na ora, anae maatane güe gui quiluus.
25Ilikuwa saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
26Ya y tinigue y fumaaelagüe, matugue gui sanjilo. Y RAY JUDIOS.
26Na mshtaka wake ulikuwa umeandikwa: "Mfalme wa Wayahudi."
27Ya maatane dos na saque yan güiya: y uno gui agapaña, ya y otro gui acagüeña.
27Pamoja naye waliwasulubisha wanyang'anyi wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
28(Ya macumple y tinigue ni y ilegña: Güiya, usaouao matufong yan y manisao.)
28Hapo yakatimia Maandiko Matakatifu yanayosema, "Aliwekwa kundi moja na waovu."
29Ya macacase todo ni y manmalolofan, ya jayeyengyong y ilonñija, ya ilegñija: Ay! jago ni y unyulang y templo, ya unjatsa talo gui mina tres na jaane;
29Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana, wakitikisa vichwa vyao na kusema, "Aha! Wewe mwenye kuvunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu!
30Satba maesajao, ya maela tunog papa güenao gui quiluus.
30Sasa, shuka msalabani ujiokoe mwenyewe!"
31Taegüenaoja locue y magas mamale, manmanbotlelea gui entaloñija, ya ilegñija yan y escriba sija: Jasatba y palo, ya güiya na maesa ti siña güe jasatba.
31Nao makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria walimdhihaki wakisema, "Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi!
32Si Cristo y Ray Israel, polo ya utunog pago gui quiluus, para utafanlie, ya utafanjonggue güe. Yan ayo y mangachochongña manmaatane gui quiluus madespresia güe.
32Eti yeye ni Kristo, Mfalme wa Israeli! Basi, na ashuke msalabani ili tuone na kuamini." Hata watu wale waliosulubiwa pamoja naye walimtukana.
33¶ Ya anae mato y mina saes na ora, jomjom todo y tano asta y mina nuebe na ora.
33Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa kulikuwa giza nchini kote.
34Ya y mina nuebe na ora, janagosagang si Jesus ilegña: Eli, Eli, lama sabactani? cumequeilegña: Yuusso, Yuusso, jafa muna undingoyo?
34Saa tisa alasiri Yesu akalia kwa sauti kubwa, "Eloi, Eloi, lema sabakthani?" Maana yake, "Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?"
35Ya palo ni y manotojgue gui oriyaña, anae majungog güe, ilegñija: Estagüe na jaaagang si Elias.
35Baadhi ya watu waliosimama pale waliposikia hivyo, walisema, "Sikiliza! Anamwita Eliya!"
36Ya malago uno, ya jasupog y espongja gui binagle, ya japolo gui puntan y piao, ya janae para uguimen, ya ilegña: Poloja güe namaesa; ya utafanlie cao ufato si Elias, ya uninatunog.
36Mtu mmoja akakimbia, akachovya sifongo katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe akisema, "Hebu tuone kama Eliya atakuja kumteremsha msalabani!"
37Ya si Jesus umagang goságang, ya jaentrega y espiritu.
37Yesu akapaaza sauti kubwa, akakata roho.
38Ya y cottinan y templo, masisen dos pedaso, y sanjilo asta y sanpapa.
38Basi, pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini.
39Ya anae y senturion ni y tumotojgue gui menaña, linie, na taegüenao jaentrega y espiritu, ilegña: Magajet na este na taotao Lajin Yuus.
39Jemadari mmoja aliyekuwa amesimama mbele yake aliona jinsi Yesu alivyolia kwa sauti na kukata roho, akasema, "Kweli mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!"
40Ya mangaegue locue sija famalaoan, na maaatan gui chago, ya entre sija estaba si Maria Magdalena, yan si Maria nanan Santiago y patgon, yan si José, yan si Salome;
40Walikuwako pia wanawake waliotazama kwa mbali, miongoni mwao akiwa Maria toka mji wa Magdala, Salome, na Maria mama wa kina Yakobo mdogo na Yose.
41Ni y anae estaba güe guiya Galilea, madalalag güe, ya masetbe güe; yan megae sija na famalaoan mangachochongña julo guiya Jerusalem.
41Hawa walimfuata Yesu alipokuwa Galilaya na kumtumikia. Kulikuwa na wanawake wengine wengi waliokuja Yerusalemu pamoja naye.
42¶ Ya anae estaba pupuenge, sa ayo na jaane y Preparasion, cumequeilegña y jaane antes di y sábado,
42Wakati wa jioni ulikuwa umekwisha fika. Hiyo ilikuwa siku ya Maandalio, yaani siku inayotangulia Sabato.
43Mato si José, taotao Arimatea, mauleg na taotao na pápagat, ni y jananangga locue y raenon Yuus; ya mapos yan atrebe malag as Pilato, ya jagagao y tataotao Jesus.
43Hapo akaja Yosefu mwenyeji wa Armathaya, mjumbe wa Baraza Kuu, aliyeheshimika sana. Yeye pia alikuwa anatazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Basi, alimwendea Pilato bila uoga, akaomba apewe mwili wa Yesu.
44Ya ninamanman si Pilato, cao esta matae; ya jaagang y senturion, ya jafaesen cao esta matae algun tiempo.
44Pilato alishangaa kusikia kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa. Basi, akamwita jemadari, akamwuliza kama Yesu alikuwa amekufa kitambo.
45Ya anae jatungo gui senturion; janae si José ni y tataotao.
45Pilato alipoarifiwa na huyo jemadari kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa, akamruhusu Yosefu auchukue mwili wake.
46Ya güiya mamajan fino na magagao; ya janatunog y tataotaoña ya jabalutan ni y fino na magago, ya japolo gui un naftan ni maguadog gui acho, ya janagaliligue guato un acho, gui pettan y naftan.
46Hapo Yosefu akanunua sanda ya kitani, akauteremsha chini huo mwili, akauzungushia sanda. Akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa mwambani, kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango.
47Ya si Maria Magdalena, yan si Maria nanan José, jalie amano nae mapolo.
47Nao Maria Magdalene na Maria mama yake Yose walipaona hapo alipolazwa.