1YA otro biaje güiya jumalom guiya Capernaum, despues di malofan ti megae na jaane sija; ya majungog na gaegue güe gui jalom guma.
1Baada ya siku kadhaa, Yesu alirudi Kafarnaumu, watu wakapata habari kwamba alikuwa nyumbani.
2Ya mandaña megae, ya ti manulag, ni gui oriyan y petta; ya jasetmon y sinangan guiya sija.
2Basi, wakaja watu wengi sana hata nafasi yoyote ikakosekana mlangoni. Yesu alikuwa akiwahubiria ujumbe wake,
3Ayo nae manmato guiya güiya manmangongone un paralitico, na macocone ni cuatro.
3wakati mtu mmoja aliyepooza alipoletwa kwake akiwa amechukuliwa na watu wanne.
4Ya anae ti siña manmato guiya güiya pot y linajyan taotao, manajanao y atof anae estaba güe, ya anae munjayan mababa, manatunog y cama anae mapopolo y paralitico.
4Kwa sababu ya huo umati wa watu, hawakuweza kumpeleka karibu na Yesu. Basi, wakatoboa sehemu ya dari iliyokuwa juu ya mahali alipokuwa Yesu. Walipokwisha pata nafasi, wakamteremsha huyo mtu akiwa amelala juu ya mkeka.
5Ya anae jalie si Jesus y jinenggueñija, ilegña ni paralitico: Lajijo, y isaomo unmaasie.
5Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Mwanangu, umesamehewa dhambi zako."
6Ya estaba güije manmatatachong palo escriba sija, ya manmanjajaso gui corasonñija, ilegñija:
6Baadhi ya walimu wa Sheria waliokuwa wameketi hapo wakawaza mioyoni mwao,
7Jafa na cumuecuentos este na taotao chatfino contra si Yuus? Jaye siña manasie isao, solo si Yuusja?
7"Anathubutuje kusema hivyo? Anamkufuru Mungu! Hakuna mtu awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake."
8Ya jatungo si Jesus enseguidas gui espirituña na manmanjajaso gui sumanjalomñija, ya ilegña nu sija: Jafa muna injajaso este sija gui corasonmiyo?
8Yesu alitambua mara mawazo yao, akawaambia, "Mbona mnawaza hivyo mioyoni mwenu?
9Jafa mas guse taalog y paralitico: Y isaomo unmaasie; pat taalog: Cajulo, chule y camamo, ya unjanao?
9Ni lipi lililo rahisi zaidi: kumwambia mtu huyu aliyepooza, Umesamehewa dhambi zako, au kumwambia, Inuka! Chukua mkeka wako utembee?
10Lao para intingo na y Lajin taotao guaja ninasiñaña gui jilo tano manasie isao (ilegña ni paralitico),
10Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anayo mamlaka ya kuwasamehe watu dhambi duniani." Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza,
11Jualog nu jago: Cajulo, ya unchule y camamo ya janao falag iyajamyo.
11"Nakwambia simama, chukua mkeka wako uende nyumbani!"
12Ayo nae cajulo güe enseguidas, ya jachule y camaña, ya mapos gui menan todo; enao muna todo ninafanmanman, ya manamalag si Yuus, ilegñija: Taya nae inlie ayo.
12Mara, watu wote wakiwa wanamtazama, huyo mtu akainuka, akauchukua mkeka wake, akaenda zake. Watu wote wakashangaa na kumtukuza Mungu wakisema, "Hatujapata kamwe kuona jambo kama hili."
13¶ Ya jumanao talo gui oriyan tase, ya todo y linajyan taotao manmato guiya güiya, ya jafanagüe sija.
13Yesu alikwenda tena kando ya ziwa. Umati wa watu ukamwendea, naye akaanza kuwafundisha.
14Ya anae malofan jalie si Levi, lajin Alfeo, na matatachong gui bancon y tributo sija, ya ilegña nu güiya: Dalalagyo. Ya cajulo ya dinalalag güe.
14Alipokuwa akipita, akamwona Lawi mwana wa Alfayo, ameketi katika ofisi ya ushuru. Yesu akamwambia, "Nifuate!" Lawi akasimama, akamfuata.
15Ya susede na estaba güe matachong para uchocho gui lamasa gui guima ayo, ya megae sija na publicano yan manisao sija manmatatachong mañisija locue yan si Jesus, yan y disipoluña sija; sa guaja megae dumadalalag güe.
15Baadaye, Yesu alikuwa amekaa mezani, nyumbani kwa Lawi, kula chakula. Watoza ushuru wengi na wenye dhambi walikuwa wamemfuata Yesu na wengi wao wakawa wamekaa mezani pamoja naye na wanafunzi wake.
16Ya y escriba sija gui entalo y Fariseo sija, anae jalie na mañochocho yan y manisao yan y publicano sija, ilegñija ni disipoluña sija: Jafa este na güiya chomocho yan gumiguimen, yan y publicano sija yan y manisao?
16Basi, baadhi ya walimu wa Sheria ambao walikuwa Mafarisayo walipomwona Yesu akila pamoja na watu wenye dhambi na watoza ushuru, wakawauliza wanafunzi wake, "Kwa nini anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?"
17Ya anae jajungog si Jesus, ilegña nu sija: Y manjomlo ti janesesita medico, na y manmalango. Ti matoyo para juagang y manunas, na y manisao sija.
17Yesu alipowasikia, akawaambia, "Watu wenye afya hawahitaji daktari; wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa. Sikuja kuwaita watu wema, ila wenye dhambi."
18¶ Ya y disipulon Juan, yan y disipulon Fariseo sija manayunat: ya manmato, ya ilegñija nu güiya: Jafa muna y disipulon Juan yan y disipulon Fariseo sija manayuyunat; ya y disipulumo ti manayuyunat?
18Wakati mmoja wanafunzi wa Yohane na wanafunzi wa Mafarisayo walikuwa wanafunga. Basi, watu wakaja, wakamwuliza Yesu, "Kwa nini wanafunzi wa Yohane na wa Mafarisayo wanafunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?"
19Si Jesus ilegña nu sija: Siña manayunat y mangaegue gui guipot umasagua, yaguin mañisija yan y nobio? Y tiempo nae mañisijaja yan y nobio, ti siña manayunat.
19Yesu akajibu, "Walioalikwa harusini wanawezaje kufunga kama bwana harusi yupo pamoja nao? Wakati wote wawapo pamoja na bwana harusi hawawezi kufunga.
20Lao ufato y jaane sija, na y nobio umanajanao guiya sija; ya ayo sija na jaane nae ufanayunat.
20Lakini wakati utafika ambapo bwana harusi ataondolewa kati yao; wakati huo ndipo watakapofunga.
21Taya ni uno lumimendanñañaejon y nuebo na magago gui bijo na bestido; sa ayo y nuebo na limenda ujanao gui bijo, ya mas taelaye y matiteg.
21"Hakuna mtu anayekata kiraka kutoka katika nguo mpya na kukishonea katika nguo kuukuu. Kama akifanya hivyo, hicho kiraka kipya kitararuka kutoka hilo vazi kuukuu, nalo litaharibika zaidi.
22Ya taya ni uno umasajguane y nuebo na bino gui bijo na boteyan cuero: sa y nuebo na bino uyamag y boteyan cuero sija, ya umachuda y bino, ya y boteyan cuero manmalingo; lao y nuebo na bino, y nuebo na boteyan cuero nae umasajguane.
22Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu. Kama akifanya hivyo, divai itavipasua hivyo viriba, nayo divai pamoja na hivyo viriba vitaharibika. Divai mpya hutiwa katika viriba vipya!"
23¶ Ya manmapos este, malolofan güe gui jalom fangualuan trigo gui sabado na jaane; ya y disipoluña sijas igue di manmanjala ni espiga sija.
23Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano. Walipokuwa wanatembea, wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano.
24Ya y Fariseo sija, ilegñija: Atanja, jafa na jafatitinas gui sabado na jaane y ti mauleg para umafatinas?
24Mafarisayo wakawaambia, "Tazama! Kwa nini wanafanya jambo ambalo si halali kufanya wakati wa Sabato?"
25Ya güiya ilegña nu sija: Taya nae intaetae jafa checho David anae janesesita, ya ñalang yan y mangachongña?
25Yesu akawajibu, "Je, hamjapata kusoma juu ya kile alichofanya Daudi wakati alipohitaji chakula? Yeye pamoja na wenzake waliona njaa,
26Jafa taemano jalomña gui guimayuus anae si Abiatar magas na pale, ya jacano y pan ni inefrese, ni ti para macano, na para y pale sija; ya janae locue y mangachongña sija?
26naye akaingia ndani ya Nyumba ya Mungu, akala ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu. Jambo hili lilifanyika wakati Abiathari alikuwa Kuhani Mkuu. Na ni makuhani tu peke yao waliokuwa wameruhusiwa kula mikate hiyo. Lakini Daudi aliila, tena akawapa na wenzake."
27Ylegña talo nu sija: Y sabado pot y taotao na mafatinas: ti y taotao pot y sabado.
27Basi, Yesu akawaambia, "Sabato iliwekwa kwa ajili ya binadamu na si binadamu kwa ajili ya Sabato!
28Enaomina y Lajin taotao Señot locue gui sabado.
28Kwa hiyo, Mwana wa Mtu ni Bwana hata wa Sabato."